Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,325
- 11,193
Tamko kwamba Marekani haina tena pesa kuisaidia Ukraine limekuwa ni la wazi na hata taifa hilo limesema jukumu la kuendelea kuisaidia Ukraine kupigana na Urusi imewaachia wenzake 50 wafanye hivyo.
Pamoja na tamko hilo kutokana na uchofu katika vita hivyo, Marekani pia imesema haina mpango wa kwenda kutengeneza silaha za kivita ambazo zimeharibika.
Mbinu za kivita zinazotumiwa na wanamgambo wa Houth katika kuendelea kuzuia safari za meli za mataifa yanayoisaidia Israel kuleta janga Gaza zinazopita bahari nyekundu, nazo zimetajwa huenda zikapelekea kuchoka kwa Marekanini kwa mara nyengine kupambana na wanamgambo hao.
Mpaka juzi Marekani ilikuwa imeshafanya mashambulizi dhidi ya maeneo ya wanamgambo hao kwa siku 8 tofauti.Katika kila siku ya mashambulia Marekani ilitoa takwimu za mafanikio ya mashambulio hayo na kusema ilikuwa imeharibu rada za kufuatilia safari za meli na za kuongozea mashambulizi ya kundi hilo.
Pamoja na matangazo ya mafanikio hayo mashambulio ya Houth bado hayajasita ambapo juzi hiyo hiyo walifanikiwa kuzilenga na kuzipiga bila madhara makubwa meli mbili za mizigo zilizokuwa zikipeperusha bendera ya Marekani.
Wanamgambo hao wa Yemen wameelezwa kuwa kutokana na vita vyao na Saudi Arabia vya miaka kadhaa kabla ya kusitishwa mwaka 2022 wamepata uzoefu mkubwa wa kuficha silaha zao.
Sehemu kubwa ya wapiganaji wa jeshi hilo huwa wanapata mafunzo na kusambaa maeneo mbali mbali bila kuwa na kambi maalumu. Teknolojia za kivita wamekuwa wakipata kwa msaada kutoka wataalamu wa Hizbullaha na wale wa Marekani.
Rada na silaha zao muhimu huwa wanaziweka kwenye gari ndogo ndogo ambapo mara baada ya kufanya shambulio moja huondoka eneo hilo na kuelekea kituo kingine. Marekani tayari ina droni za upelelezi aina ya Reaper juu ya anga la Yemen kufuatilia mienendo ya kundi hilo. Hata hivyo kutokana na mfumo wa kupiga na kuhama imetajwa kuwa droni hizo hazitoweza kuleta tija kubwa katika kuzuia mashambulio ya Houth.
Kuhusu silaha wanazotumia Houth ni uhakika kuwa nyingi zinatokea au kupitia Iran baadae kusafirishwa kwa meli ndogo ndogo kupelekwa Yemen. Kutokana na wingi wa meli hizo na pamoja na ujasusi mkubwa inaofanya Marekani kufuatilia silaha hizo nako kumeelezwa haitokuwa rahisi kuzipekua meli zote hizo kuzuia silaha hizo zisiwafikie Houth.
Wiki mbili zilizopita jaribio la kuzuia silaha kutowafikia wanamgambo wa Yemen zilipelekea askari wawili wa Marekani kuzama na kupoteza maisha. Haikuwekwa wazi mazingira yaliyopelekea askari hao kuzama na hatimae kupotea moja kwa moja
Mwisho wa yote matarajio ni kuwa katika vita baina ya Marekani na wanamgambo wa Houth kutapelekea hasara kubwa kwa Marekani na hatimae kuchoka bila kufanikiwa kuwazuia wanamgambo hao kuendelea kuzichagiza meli za mizigo zinazopita kwenye lango la bab Mandeb kuelekea au kutoka mfereji wa Suez.
Pamoja na tamko hilo kutokana na uchofu katika vita hivyo, Marekani pia imesema haina mpango wa kwenda kutengeneza silaha za kivita ambazo zimeharibika.
Mbinu za kivita zinazotumiwa na wanamgambo wa Houth katika kuendelea kuzuia safari za meli za mataifa yanayoisaidia Israel kuleta janga Gaza zinazopita bahari nyekundu, nazo zimetajwa huenda zikapelekea kuchoka kwa Marekanini kwa mara nyengine kupambana na wanamgambo hao.
Mpaka juzi Marekani ilikuwa imeshafanya mashambulizi dhidi ya maeneo ya wanamgambo hao kwa siku 8 tofauti.Katika kila siku ya mashambulia Marekani ilitoa takwimu za mafanikio ya mashambulio hayo na kusema ilikuwa imeharibu rada za kufuatilia safari za meli na za kuongozea mashambulizi ya kundi hilo.
Pamoja na matangazo ya mafanikio hayo mashambulio ya Houth bado hayajasita ambapo juzi hiyo hiyo walifanikiwa kuzilenga na kuzipiga bila madhara makubwa meli mbili za mizigo zilizokuwa zikipeperusha bendera ya Marekani.
Wanamgambo hao wa Yemen wameelezwa kuwa kutokana na vita vyao na Saudi Arabia vya miaka kadhaa kabla ya kusitishwa mwaka 2022 wamepata uzoefu mkubwa wa kuficha silaha zao.
Sehemu kubwa ya wapiganaji wa jeshi hilo huwa wanapata mafunzo na kusambaa maeneo mbali mbali bila kuwa na kambi maalumu. Teknolojia za kivita wamekuwa wakipata kwa msaada kutoka wataalamu wa Hizbullaha na wale wa Marekani.
Rada na silaha zao muhimu huwa wanaziweka kwenye gari ndogo ndogo ambapo mara baada ya kufanya shambulio moja huondoka eneo hilo na kuelekea kituo kingine. Marekani tayari ina droni za upelelezi aina ya Reaper juu ya anga la Yemen kufuatilia mienendo ya kundi hilo. Hata hivyo kutokana na mfumo wa kupiga na kuhama imetajwa kuwa droni hizo hazitoweza kuleta tija kubwa katika kuzuia mashambulio ya Houth.
Kuhusu silaha wanazotumia Houth ni uhakika kuwa nyingi zinatokea au kupitia Iran baadae kusafirishwa kwa meli ndogo ndogo kupelekwa Yemen. Kutokana na wingi wa meli hizo na pamoja na ujasusi mkubwa inaofanya Marekani kufuatilia silaha hizo nako kumeelezwa haitokuwa rahisi kuzipekua meli zote hizo kuzuia silaha hizo zisiwafikie Houth.
Wiki mbili zilizopita jaribio la kuzuia silaha kutowafikia wanamgambo wa Yemen zilipelekea askari wawili wa Marekani kuzama na kupoteza maisha. Haikuwekwa wazi mazingira yaliyopelekea askari hao kuzama na hatimae kupotea moja kwa moja
Mwisho wa yote matarajio ni kuwa katika vita baina ya Marekani na wanamgambo wa Houth kutapelekea hasara kubwa kwa Marekani na hatimae kuchoka bila kufanikiwa kuwazuia wanamgambo hao kuendelea kuzichagiza meli za mizigo zinazopita kwenye lango la bab Mandeb kuelekea au kutoka mfereji wa Suez.