Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,180
- 10,903
Meli inayoitwa Mt/Stindra inaendelea kuwaka moto na karibu ya kuzama baada ya makombora ya Houth kuishambulia katikati ya meli kadhaa za kivita za Marekani na Ufaransa.
Kwa mujibu wa wasemaji wa jeshi la Marekani ambao hawakutaka kutajwa majina yao meli hiyo ilishambuliwa kwa kombora moja tu ambalo halikukosea shabaha yake kutoka meli 60 ndani ya mamlaka ya Houth wa Yemen.
Meli ya kivita ya Mason iliyokuwa eneo hilo japo ilipokea muito wa shida za shambulio lakini haikuweza kutoa msaada wowote na ipo eneo la tukio ikishuhudia na kuangalia namna ya kutoa msaada mwengine,
Zaidi ya wiki moja iliyopita meli tatu za kibiashara zilishambuliwa eneo hilo hilo na meli ya kivita ya USS corney kupambana na makombora kadhaa ya Houth na mwishowe nayo ikarushiwa kombora na kulengwa kwa droni.
Kwenye shambulio hili jipya la leo meli hiyo USS CORNEY haijatajwa kushiriki kwenze zoezi la kupambana na makombora ya Houth wanaopigana kulenga maslahi ya Israel kutokana na vita vinavyoendelea Gaza.
Kwa mujibu wa wasemaji wa jeshi la Marekani ambao hawakutaka kutajwa majina yao meli hiyo ilishambuliwa kwa kombora moja tu ambalo halikukosea shabaha yake kutoka meli 60 ndani ya mamlaka ya Houth wa Yemen.
Meli ya kivita ya Mason iliyokuwa eneo hilo japo ilipokea muito wa shida za shambulio lakini haikuweza kutoa msaada wowote na ipo eneo la tukio ikishuhudia na kuangalia namna ya kutoa msaada mwengine,
Zaidi ya wiki moja iliyopita meli tatu za kibiashara zilishambuliwa eneo hilo hilo na meli ya kivita ya USS corney kupambana na makombora kadhaa ya Houth na mwishowe nayo ikarushiwa kombora na kulengwa kwa droni.
Kwenye shambulio hili jipya la leo meli hiyo USS CORNEY haijatajwa kushiriki kwenze zoezi la kupambana na makombora ya Houth wanaopigana kulenga maslahi ya Israel kutokana na vita vinavyoendelea Gaza.