Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,194
- 10,929
Marekani kwa nafsi yake imepiga maeneo ya Yemen yanayotawaliwa na Houth mara 8 na kila mara husema wamepiga rada zao na pia kuyawahi makombora ya kuripulia meli yakitayarishwa kurushwa hewani.
Mafanikio hayo kiuhalisia yalikuwa ni madogo sana kuliko uwezo wa kujificha wa Houth. Hatimae katika wiki hii wameweza kurusha makombora yao kwa kasi zaidi na kwanza kuzilenga meli za US zilizokuwa na bidhaa kwa ajili ya vikosi vya Pentagon. Meli hizo kwa maelezo ya vikosi vya ulinzi wa Red Sea hazikupata madhara makubwa lakini ilibidi zipindishe na kurudi kufuata ile njia ndefu ya kuzunguka Afrika Kusini.
Katika kuilinda bahari nyekundu tayari Pentagon imepata hasara ya dola 1.84 bln ambalo ni deni walilosema hawawezi kulilipa kwa sasa.
Kwa upande mwengine bunge la Marekani limemtaka raisi Biden asichukue tena maamuzi ya kipekee kuishambulia Houth kama alivyofanya siku ya mwanzo.
Kama ilivyoripotiwa leo katika taarifa inayotatanisha kutokana na kupewa kipaumbele kidogo na vyombo vya habari vya magharibi, lakini meli ya mafuta ya Uiengereza iittwayo Martin Luanda iliyopeperusha bendera ya visiwa vya Marshal imepigwa na kombora ambalo halikupata kizuizi. Utata ni jee ni kweli inawaka moto kulelekea kuzama au hakuna madhara makubwa kama wanavyoripoti wenye meli hiyo.
Yote hayo yanaweza kutajwa kuwa ni ushindi mkubwa wa Houth katika kuwatetea wapalestina na ushujaa ambao ungepaswa kufanywa na mataifa mengine tajiri katika ukanda huo wa mashariki ya kati.
Mafanikio hayo kiuhalisia yalikuwa ni madogo sana kuliko uwezo wa kujificha wa Houth. Hatimae katika wiki hii wameweza kurusha makombora yao kwa kasi zaidi na kwanza kuzilenga meli za US zilizokuwa na bidhaa kwa ajili ya vikosi vya Pentagon. Meli hizo kwa maelezo ya vikosi vya ulinzi wa Red Sea hazikupata madhara makubwa lakini ilibidi zipindishe na kurudi kufuata ile njia ndefu ya kuzunguka Afrika Kusini.
Katika kuilinda bahari nyekundu tayari Pentagon imepata hasara ya dola 1.84 bln ambalo ni deni walilosema hawawezi kulilipa kwa sasa.
Kwa upande mwengine bunge la Marekani limemtaka raisi Biden asichukue tena maamuzi ya kipekee kuishambulia Houth kama alivyofanya siku ya mwanzo.
Kama ilivyoripotiwa leo katika taarifa inayotatanisha kutokana na kupewa kipaumbele kidogo na vyombo vya habari vya magharibi, lakini meli ya mafuta ya Uiengereza iittwayo Martin Luanda iliyopeperusha bendera ya visiwa vya Marshal imepigwa na kombora ambalo halikupata kizuizi. Utata ni jee ni kweli inawaka moto kulelekea kuzama au hakuna madhara makubwa kama wanavyoripoti wenye meli hiyo.
Yote hayo yanaweza kutajwa kuwa ni ushindi mkubwa wa Houth katika kuwatetea wapalestina na ushujaa ambao ungepaswa kufanywa na mataifa mengine tajiri katika ukanda huo wa mashariki ya kati.