JK ana sehemu yake na taratibu zake, vyombo vya dola, taasisi zoote zina taratibu zake, Bunge ambapo ndipo kwenye uwakilishi wetu kuna taratibu zake, na bado serikali kupitia mwanasheria mkuu wana taratibu zao. Hawa wote ni mihimili ya mchakato mzima wa uundwaji wa katiba.
La Mnyika litaendelea bungeni na la rais litaendelea au yatakutana mahali. Ila ikumbukwe la msingi sote na hao wengine angalau tunatambua na kukubaliana juu ya umuhimu wa katiba mpya. Mikakati itaainishwa, itachanganuliwa, itaratibiwa na kufikia kinachohitajika. Mungu ibariki Tanzania HASA WATU WAKE
Mungu Ibariki Tanzania!
Kuna vyombo vingine vya mihimili mathalani mahakama, Jambo likisha fika mahakamani,halipaswi kujadiliwa (kimaamuzi) na chombo kingine chochote. Na huo ndio msingi wa swali langu! Tuendelee kuelimishana.