Mkuu wangu maneno yako ni hekima sana. Maelfu ya wananchi wa Meru walioshiriki uchaguzi jana na kumchagua Nasari na kuhakikisha hakuna hila wa hujuma inafanyika kuwakosesha ushindi ni wananchi masikini kama familia ya Joshua Nasari ilivyo! Naomba usisahau ulipotoka,watumikie wananchi wa Meru kwa nguvu zako zote! Hongera CDM na Watanzania wapenda haki wote.Hongera kijana mwenzetu Nassari kwa kuwa nauthubutu na kumtanguliza mungu mbele hakika ushindi wako unamaana sana kwa watanzania na vijana. Tunakuomba ukawe sauti ya vijana na masikini wote wa nchi ili tunapokuona wewe tujione cc.
Bravo chadema
Dogo Nasari furahia ushindi lakini ujue kwamba ubunge si lelemama.
Hatutarajii uige ya kule Arusha Mjini ya kujipeleka gereza la Kisongo na kupoteza muda wetu.
Pia upuuzi wa maandamano Arumeru mwiko, tuko bize na shughuli zetu za maendeleo. Usijaribu kutuvugua.
Tunadai ututatulie kero zetu fasta kama ulivyoahidi, vinginevyo 2015 inakula kwako kwani tutakupiga chini bila huruma.
Hao maelfu ni akina nani na walikuwa wapi? Kwa nini mambo yasiwe shwari? Mbona nahisi kama ulikuwa na kitu kizuri cha kusema lakini umeshindwa kujieleza? hebu fafanua mawazo yako basi!Ni vizuri kuwa kijana mwenzetu kuchaguliwa kuwa mbunge. Lakini jamani naomba niwakumbushe kuwa this does not mean everything is ok kwa vijana na wanamageuzi wengine. Lazima tujue kwa kila kijana na mwanamageuzi kama nasari ambaye amepata nafasi ya kutuwakilisha bungeni, maelfu wamekosa hiyo nafasi hata kama walisitahili. Kwa hiyo mambo yasichukuliwe kama yako shwari. Nawasilisha
anza na mafisadi wenzako wanaojambia viti vya bunge kwa kulala lala hovyo na kudai posho. idiot
mungu akiwa upande wetu nani atakae tuzuia?nawasiisha mkuul