Hotuba ya Kikwete haina jipya kwa watuhumiwa wa Escrow. Muhongo ziarani Mara kesho

kik.jpg
 
Leo tarehe 22 Desemba, 2014 Mhe. Zuma atakutana kwa mazungumzo rasmi na Mhe. Rais Kikwete Ikulu kabla ya kuondoka nchini mchana wa leo kurejea nchini kwake. Nahisi hayo mazungumzo ndo yamefanya waandishi wa Habari waitwe. Kutakua kuna msaada Tanzania inaahidiwa.

Kwahiyo mkuu unataka kusema fisadi la sauzi limekuja kuwapa maujanja mafisadi ya bongo? Hapa lazima kitanuka bunge lijalo!
 
Yericko,
Mbona CHADEMA mmeiteka nyara hoja ya Escrow? Eti hata Mzee Ntagazwa anatumia ushushushu wake wa zamani kujua Rais wetu ataongea nini leo!
 
Mkuu Feedback, ujue kiukwewli mimi sio Team Lowassa, bali ni team ukweli!, kiukweli Lowassa ndie the best CCM has so far!. Tatizo la CCM ni ule mtindo wake wa kuwaacha the best na kukumbatia makapi!, reference ni 2005!.

Siku zote ninachopigania humu ni ukweli usemwe!.

Pasco

salim was the right one...
 
Yericko, na mimi nataka iwe hivyo. Asifanye chochote kuhusika na Escrow scandal wala asigusie kabisa suala hilo kwenye hotuba zake.

Kwa nini kumlazimisha mtu mzima atazame anga kana kwamba ni kitu kidogo kilichofichika??? NOOOO.

Attitude yake iko bayana, msimamo wako uko wazi sana.....ni hivi yeye na Escrow thugs lao moja. So asishinikizwe kufanya asilo taka wala kuliamini.

Na ni vizuriii asipofanya lolote ndio anakimaliza chama chake unajua hela alishachukua na watazitumia kwenye kampeni sasa unadhani watarudi nyuma? No Way ila sasa sijui Hao wahisani na misaada inakuwaje
 
Zuma naye kwao ni mwizi mkubwa c mtu mzuri hotuba ya Rais itabaki nchi vipande vipande kama atashindwa kuwawajibisha Maswi Muhongo Tibaijuka athari zake utendaji kazi utashuka maofisini pia wizi utaongezeka maoficn naungana na Ole Sendeka wasipowajibishwa Mwakyembe na Tume yake imuombe radhi Lowasa pia Bunge kamati ya James Lembeli iwaombe Radhi Maige Vuai Nchimbi Kagasheki ili jamii ya watanzania ijue hawana makosa walionewa tu hawa jamaa Kura yangu 2015 ni kwa Lowasa.
 
Aliita wazee was dini wachungaji name masheikh akusitakutetea mpakawqnaondoka viongozi waroman wanamsifia kabisauamuzi was kutowaondoa wakaishia kuelewana kutoelewana so something anasema
Leo
 
Amkuelewa kilaini alivyosema chaguo LA Mungu huyu kaletwa kUIONDOA CCm name hiliindilio chaguo MUNGU ANATAKA KULETA MABADILIKO KUPITIA JK
 
Kama mnasubiri hotuba ya rais Kikwete mkitegemea maamuzi chanya kwenye suala la Escrow basi mnapoteza muda wenu tu.

Kesho mwizi wa escrow na dalali mhimu katika wizi huo ndugu Prof Muongo anaanza ziara rasmi ya kiserikali mkoani mara.

Hii inatafsiriwa kuwa ktk hotuba ya mwenye jamhuri, watuhumiwa wa escrow sio sehemu ya agenda zake na wala hatambui uwepo wa agizo la Bunge.

Maandalizi yote kwaajili ya ziara hiyo ya le prof Muongo yamekamilika.

Atatembelea wachimbaji wadogo wilaya ya butiama, mgodi wa nyamongo na kueleza mafanikio ya wizara kuhusu umeme vijijini.

Atatoa mitaji kwa wachimbaji wadogo wadogo na kueleza fursa zilizopo katika Mkoa wa Mara, pia atatembelea wilaya zote na kuzungumza na wananchi.


Hata sipati picha na uwezo wa huyu jamaa. Wazee wenyewe anaoenda kuongea nao ni wazee wa CCM. Kwani mpaka sasa taarifa tulizo nazo ni kwamba amewaita na washindi wote wa uchaguzi kupitia chama chake. Swali ni hili: Je, nikikao cha kuongelea Masuala ya Taifa au ni kikao cha Chama????
Kazi kweli kweli. Heri Mangungo wa Msovero kuliko huyu jamaa
 
Basi watatnzania tujue kwamba wezi wamehalalishwa kufanya walitakalo...tusilipe kodi mpka tujue hatima ya hili sakata kwani hatuwezi kulipa kodi kwa mafisadi huku maospitalini hakuna dawa.
 
Nidhambi kubakumuhukumu mtu pasipokuwa na ushahidi wa kujiridhisha tusiwe wachoyo na wabnafsi wa fikra je kila mmoja wetu ajiulize kama yeye ndio angekuwa mhanga wa kitu kama hicho angefanya jambo kama ambavyo anavyo mlazimisha mwenzie kufanya?sivzur pia uwajibikaji hutokea endapo kuna ushahidi bora na sio hisia za mtu au si kwa ajili mtu kaamua kuhoji kinyume na uadilifu wa mtu.
 
Yericko nyerere acha ujuha kalulu wewe. Usiwe wa kumpangia mheshimiwa rais aseme nini au afanye nini. Una chaguzi mbili tu. Moja ni kuisikiliza na pili ni kuacha kuisikiliza. Kama kwako haina jipya kwetu imejaa nasaha. Na profesa muhongo yuko kikazi zaidi hayuko kisiasa kama unavyotarajia..mwache afanye kazi kwani wenye macho tunaona.
kama mnasubiri hotuba ya rais kikwete mkitegemea maamuzi chanya kwenye suala la escrow basi mnapoteza muda wenu tu.

Kesho mwizi wa escrow na dalali mhimu katika wizi huo ndugu prof muongo anaanza ziara rasmi ya kiserikali mkoani mara.

Hii inatafsiriwa kuwa ktk hotuba ya mwenye jamhuri, watuhumiwa wa escrow sio sehemu ya agenda zake na wala hatambui uwepo wa agizo la bunge.

Maandalizi yote kwaajili ya ziara hiyo ya le prof muongo yamekamilika.

Atatembelea wachimbaji wadogo wilaya ya butiama, mgodi wa nyamongo na kueleza mafanikio ya wizara kuhusu umeme vijijini.

Atatoa mitaji kwa wachimbaji wadogo wadogo na kueleza fursa zilizopo katika mkoa wa mara, pia atatembelea wilaya zote na kuzungumza na wananchi.
 
Amini....duh..unakauli kali.....huoni watanzania wanateseka au. Au ndo umepata mgao huo jaman. Safisha kinywa hicho. Watu wamechoka
 
Back
Top Bottom