Hosea ameathiri maisha yangu na familia yangu!

Ndugu zangu tutofautishe kati ya sheria na haki. Watu wanaweza kutumia vifungu vya sheria halali za nchi mtu akapatikana na hatia au kuachiliwa huru, lakini bado ikawa haki haijatendeka kwa mhusika. Hivi ndivyo majambazi wanavyoachiliwa huru na waliobambikiziwa kesi wanavyofungwa. Wanasheria wanatumia vipengele vya kiufundi vya sheria na jinsi ya kucheza na maneno. Unaweza kushuhudia kabisa kwa macho yako mtu akitenda uhalifu, lakini unapoutoa ushahidi huo mahakamani unashangaa wanasheria wanaugeuzageuza hadi inaonekana kuwa ushahidi huo hauna nguvu, hakimu anautupilia mbali! Vivyo hivyo mtu anapobambikiwa kesi, kama mbambikaji ana utaalamu wa kutosha, ataubambika kiufundi kiasi kwamba mahitaji yote ya kisheria ya kumtia mtu hatiani yanakuwapo. Kwa nafasi kubwa aliyokuwa nayo Bw Hosea kipindi hicho na utaalam wa sheria alionao, sishangai hata kidogo kuwa alifanikisha kumfunga huyu Mzee Zephania, kwa hakika inasikitisha sana.

Ningependa kujua pia kama Mzee huyu alikata rufaa na majibu yake yalikuwaje. Na kama hakukata rufaa, nini kilimzuia kufanya hivyo? Nakumbuka mwandishi mmoja kwa jina Adam Mwaibabile aliwahi kubambikiwa kesi huko Songea na mkuu wa mkoa Nicodemus Banduka, akafungwa jela mwaka mmoja. Waandishi wenzie waliishikilia bango kesi ile na kukata rufaa, akaachiwa baada ya muda mfupi tu. Sasa sijui kwa huyu mzee Musendo waandishi wenzie na wanaharakati wa haki za binadamu walimsusa au ilikuwaje?
 
Alitaka kuvuta asituyeyushe. Iweje akaonane na Hosea mara mbili wakati ni yeye ndie alikuwa ana story ya rushwa inayowahusu?
 
Last edited:
Darwin,

Kuna kitu hapo hakielezeki. Nimesoma sana alivyoingiziwa hela..... Cha ajabu hapo hapo akaambiwa atoe....Je muda gani alijua kama ana hela mfukoni?

Kuna ka kitu hapo ndugu yangu. Huko kukutana na HOSEA kila mara mbili.... ina maana alidai rushwa mara ya kwanza ya pili akapewa!!!

FP

Kaka uliondoka Bongo lini?Watu wanabambikiwa kesi kila siku.Sema tu si wote wanapata fursa kama mwandishi huyu wa habari kuelezea kilichowasibu.
 
Kama ni kweli alichukua rushwa hana mtu wa kumlaumu zaidi ya yeye mwenyewe. Hosea alitumia njia mbaya lakini mwenye makosa ni mwandishi mwenyewe. Ni vizuri akubali makosa yake na kusonga mbele. Wengi tunajifunza kwa makosa.

Kama Hosea alitumia njia mbaya basi huwezi sema na yeye hana makosa.

Lakini kama ni kweli Mwandishi alichukua rushwa, sasa Hosea alitumia njia mbaya kivipi?
 
This is definetely one of the contenders of my sadest story of the year! I think kuna umuhimu wa kuwa na kamera kwenye all public buildings, kungekuwa na CCCTV hapa huu mchezo ungekuwa ni wa kitoto. Hainiingii akilini kabisa kwa mtu yoyote kumuomba rushwa Mkurugenzi wa Operesheni wa taasisi ya kuzuia rushwa, you will have to be insane to attempt anything near this!
Pia kuna umuhimu wa watu wa human rights kuanza kutupia macho magereza yetu, the level of abuse huko is horrifying and shocking.

Ninafahamu mtu mmoja aliyekwenda kwa Hosea kumuomba rushwa. Nadhani alionewa huruma maana huyo yangemkuta mabaya zaidi ya Musendo, lakini aliondoka salama na bado akafanya mambo ambayo ni kinyume kabisa cha maadili ya uandishi wa habari. Hii ndio Tanzania yetu, kila mahali pameoza
 
Kama Hosea alitumia njia mbaya basi huwezi sema na yeye hana makosa.

Lakini kama ni kweli Mwandishi alichukua rushwa, sasa Hosea alitumia njia mbaya kivipi?

Ni ngumu kumuomba polisi RUSHWA ila ni rahisi kumpa polisi rushwa.

kwa mantiki hiyo ni KICHAA tu ambaye anaweza muomba RUSHWA macho kwa macho na kuipokea hiyo rushwa macho kwa macho kutoka kwa bosi wa kuzuia rushwa.


Na hata hivyo bado naamini huyo mwandishi asingekubali pokea rushwa mkono kwa mkono kutoka kwa HOSEA ni logic ya kawaida tu jamani.Hivi ni nani anaweza kukubali kupokea rushwa kutoka kwa polisi tena yule sungeti tu?
 
Ni ngumu kumuomba polisi RUSHWA ila ni rahisi kumpa polisi rushwa.

kwa mantiki hiyo ni KICHAA tu ambaye anaweza muomba RUSHWA macho kwa macho na kuipokea hiyo rushwa macho kwa macho kutoka kwa bosi wa kuzuia rushwa.

Na hata hivyo bado naamini huyo mwandishi asingekubali pokea rushwa mkono kwa mkono kutoka kwa HOSEA ni logic ya kawaida tu jamani.Hivi ni nani anaweza kukubali kupokea rushwa kutoka kwa polisi tena yule sungeti tu?

Na unajuaje ex-Mhariri hakufanya UKICHAA?

Mimi na wewe hapa hatuna details, na tunafanya uchambuzi wa juu juu mno. Mahakamani watakua walipitia yooooote hayo. Mzee akaonekana guilty. Na vigezo vya polisi kukuingizia mikono yake mfukoni, na rules of evidence, na search warrant, na yoooote haya ex-Mhariri atakuwa aliyasema Mahakamani kupitia lawyer.

Kama mimi na wewe tunaona hiyo "logic" kwamba huwezi kuomba rushwa kwa mzuia rushwa, hudhani kwamba lawyer wake hakuyaona hayo? Unless nae ni KICHAA. Jaji hakuyaona hayo? Unless nae ni KICHAA. Jurists (kama walikuwepo) hawakuyaona hayo. Unless nao ni VICHAA. Sijui kama wote hao VICHAA.

Nitakwambia nani ameleta UKICHAA.

Mwandishi wa hii stori (aliyemu interview huyu ex-Mhariri) ndio kafanya kazi KI-KICHAA KICHAA.

Ingekuwa ni nchi za watu zenye press ya maana, mmoja wao kakumbwa na controversial case ya rushwa, tena mhariri wa gazeti, tena kuhusu investigative story iliyoandikwa kuhusiana na rushwa, tena rushwa inayoshutumiwa kufanywa na Ofisa wa Kuzuia rushwa, tena Mhariri anasema walimuingizia mikono mfukoni, hii ingekuwa bonge la issue kwenye Tanzania press. Lakini angalia ilivyo andikwa kidaku.

Hawajasema yaliyojiri mahakamani. Serikali ilitumia mashahidi wale wale, lile trupu lililokuja la Hosea ? Kwa nini alishindwa kesi ? Ex-Mhariri alijitetea nini? Ile original story ya Daily Mirror kuhusu original allegations dhidi ya Hosea iliishia wapi? Hili lilikuwa introduced kwenye kesi ya ex-Mhariri? Alifikiria kukata rufaa? Nini kilikuwa kinampeleka peleka mahotelini kukutana na mtu ambae mnamwandikia investigative story? We mtu umetangualia hotelini saa nzima, kwa nini aje mtu nyuma ndio akununulie wewe vinywaji? Ulipopigwa "telo" ulionyeshwa search warrant? Search Warrant ilitolewa kwa wewe kushukiwa unafanya nini? I mean kabla ya hapo, wewe ulikuwa under suspicion gani? Daily Mirror msimamo wao kwenye hili ni upi, maana inaoneka hawakutaki tena.

I mean, ni vizuri kujua shuruba za wafungwa, lakini stori za prayer times au meal schedule za vyakula vya jela na daily regimen za lupango ni zile zile. Bondo na Ndondo. Kulima na Wanyampara. Funza na Uji. Kuhesabiwa na Kulala. Jumapili Nyama. Sigara ni dili. Kwishne. Wamarekani wanasema, same ol' shit!

Kwa hiyo Mwandishi cut that extraneous stuff, tuambie kesi ya Hosea mwenyewe iliishaje, na muulize ex-Mhariri atueleze vizuri alikamatwa kamatwaje?

Ex-Mhariri atuandikie kwanza kitabu kuhusu soo lake la kusingiziwa. Tukishawishika na uaminifu wake ndio tutasoma kitabu chake cha pili kuhusu hali ya maisha ya jela. Na alivyo dili na lile tatizo sugu kubwa zaidi jela. Forget sigara, japo matatizo yote inasemekana yanaanzia kwenye tamaa ya sigara.
 
Na unajuaje ex-Mhariri hakufanya UKICHAA?

Mimi na wewe hapa hatuna details, na tunafanya uchambuzi wa juu juu mno. Mahakamani watakua walipitia yooooote hayo. Mzee akaonekana guilty. Na vigezo vya polisi kukuingizia mikono yake mfukoni, na rules of evidence, na search warrant, na yoooote haya ex-Mhariri atakuwa aliyasema Mahakamani kupitia lawyer.

Kama mimi na wewe tunaona hiyo "logic" kwamba huwezi kuomba rushwa kwa mzuia rushwa, hudhani kwamba lawyer wake hakuyaona hayo? Unless nae ni KICHAA. Jaji hakuyaona hayo? Unless nae ni KICHAA. Jurists (kama walikuwepo) hawakuyaona hayo. Unless nao ni VICHAA. Sijui kama wote hao VICHAA.

Nitakwambia nani ameleta UKICHAA.

Mwandishi wa hii stori (aliyemu interview huyu ex-Mhariri) ndio kafanya kazi KI-KICHAA KICHAA.

Ingekuwa ni nchi za watu zenye press ya maana, mmoja wao kakumbwa na controversial case ya rushwa, tena mhariri wa gazeti, tena kuhusu investigative story iliyoandikwa kuhusiana na rushwa, tena rushwa inayoshutumiwa kufanywa na Ofisa wa Kuzuia rushwa, tena Mhariri anasema walimuingizia mikono mfukoni, hii ingekuwa bonge la issue kwenye Tanzania press. Lakini angalia ilivyo andikwa kidaku.

Hawajasema yaliyojiri mahakamani. Serikali ilitumia mashahidi wale wale, lile trupu lililokuja la Hosea ? Kwa nini alishindwa kesi ? Ex-Mhariri alijitetea nini? Ile original story ya Daily Mirror kuhusu original allegations dhidi ya Hosea iliishia wapi? Hili lilikuwa introduced kwenye kesi ya ex-Mhariri? Alifikiria kukata rufaa? Nini kilikuwa kinampeleka peleka mahotelini kukutana na mtu ambae mnamwandikia investigative story? We mtu umetangualia hotelini saa nzima, kwa nini aje mtu nyuma ndio akununulie wewe vinywaji? Ulipopigwa "telo" ulionyeshwa search warrant? Search Warrant ilitolewa kwa wewe kushukiwa unafanya nini? I mean kabla ya hapo, wewe ulikuwa under suspicion gani? Daily Mirror msimamo wao kwenye hili ni upi, maana inaoneka hawakutaki tena.

I mean, ni vizuri kujua shuruba za wafungwa, lakini stori za prayer times au meal schedule za vyakula vya jela na daily regimen za lupango ni zile zile. Bondo na Ndondo. Kulima na Wanyampara. Funza na Uji. Kuhesabiwa na Kulala. Jumapili Nyama. Sigara ni dili. Kwishne. Wamarekani wanasema, same ol' shit!

Kwa hiyo Mwandishi cut that extraneous stuff, tuambie kesi ya Hosea mwenyewe iliishaje, na muulize ex-Mhariri atueleze vizuri alikamatwa kamatwaje?

Ex-Mhariri atuandikie kwanza kitabu kuhusu soo lake la kusingiziwa. Tukishawishika na uaminifu wake ndio tutasoma kitabu chake cha pili kuhusu hali ya maisha ya jela. Na alivyo dili na lile tatizo sugu kubwa zaidi jela. Forget sigara, japo matatizo yote inasemekana yanaanzia kwenye sigara.

Vipi investigation yako ya dokta Masau?
 
inashangaza mtu aliyeshitakiwa na kukutwa na hatia ya kupokea rushwa anageuzwa shujaa. Utawala wa sheria unasema ni guilty na kama ni kweli alionewa au la haijalishi, nikuwa mahakamani ushahidi uliwekwa akaonekana mwenye hatia. Kama alionekana ameoonewa ni kwa sababu aidha yeye mwenyewe alijiseti up kwa kutofuata maadili ya kazi na hivyo kuwekwa mtegoni kirahisi. Kama alionewa inasikitisha lakini ni vizuri akubali kuwajibika kwa makosa yake yeye mwenyewe.

a. Unapoenda kumhoji mtu hasa kwenye mazingira ya namna hiyo, hakikisha unajilinda vizuri kucover your back. Kwa mfano, mahojiano usifanyie chumba cha hoteli, lazima iwe public place, pili usikubali mtu akupe zawadi yoyote ya kificho pasipo yeye mwenyewe kutia sahihi au kuonesha kuwa anachokupa si rushwa (mnakumbuka ya Mtikila na Rostam?, Rostam hakuweza kudai Mtikila alichukua rushwa!).

b. Pili alikuwa na nafasi ya kukata rufaa kama aliona ameonewa lakini kama baada ya ushauri wa wanasheria wake ni kuwa hakuwa na chance ya kushinda, the record will remain kuwa yeye alikuwa ni mla mrushwa na akubali kuwa aliifanya makosa, na amejifunza na yuko tayari kuanza kujenga upya maisha yako. Tunapowakatalia wananchi kuwaimbia sifa mafisadi na kuwashangilia waliojiuzulu kwa kashfa tusigeuke na kuanza kuwaimbia sifa za kuonewa mwandishi aliyekutwa na hatia ya kula rushwa na ambaye ametumikia kifungo chake.
 
inashangaza mtu aliyeshitakiwa na kukutwa na hatia ya kupokea rushwa anageuzwa shujaa. Utawala wa sheria unasema ni guilty na kama ni kweli alionewa au la haijalishi, nikuwa mahakamani ushahidi uliwekwa akaonekana mwenye hatia. Kama alionekana ameoonewa ni kwa sababu aidha yeye mwenyewe alijiseti up kwa kutofuata maadili ya kazi na hivyo kuwekwa mtegoni kirahisi. Kama alionewa inasikitisha lakini ni vizuri akubali kuwajibika kwa makosa yake yeye mwenyewe.

a. Unapoenda kumhoji mtu hasa kwenye mazingira ya namna hiyo, hakikisha unajilinda vizuri kucover your back. Kwa mfano, mahojiano usifanyie chumba cha hoteli, lazima iwe public place, pili usikubali mtu akupe zawadi yoyote ya kificho pasipo yeye mwenyewe kutia sahihi au kuonesha kuwa anachokupa si rushwa (mnakumbuka ya Mtikila na Rostam?, Rostam hakuweza kudai Mtikila alichukua rushwa!).

b. Pili alikuwa na nafasi ya kukata rufaa kama aliona ameonewa lakini kama baada ya ushauri wa wanasheria wake ni kuwa hakuwa na chance ya kushinda, the record will remain kuwa yeye alikuwa ni mla mrushwa na akubali kuwa aliifanya makosa, na amejifunza na yuko tayari kuanza kujenga upya maisha yako. Tunapowakatalia wananchi kuwaimbia sifa mafisadi na kuwashangilia waliojiuzulu kwa kashfa tusigeuke na kuanza kuwaimbia sifa za kuonewa mwandishi aliyekutwa na hatia ya kula rushwa na ambaye ametumikia kifungo chake.

Duh umemkoma nyani mbaya mazee!
 
Alitaka kuvuta situyeyusha. Iweje akaonane na Hosea wakati ni yeye ndie alikuwa ana story ya rushwa inayowahusu?

Nina wasi wasi sana na hii Story Mzee Musonde alichukua rushwa kama ilivyo waandishi wengi wa habari Tanzania njaa sana!!! Musonde was amoung those, aliingia mtego akalamba hiyo miaka jela....asitafute mchawi, ndo wanavyoishi. Nikiwa Tanzania tuliisha ita waandishi wa vyombo mbali mbali kwa kuwalipia kila kitu, siku ya siku kuna mwandishi mmoja mwandamizi wa gazeti la serikali alinifata kuniomba ubani ili story itoike TVT na gazeti ila nimpe ubani, nilimwambia usiandike na ubani hupati. Ndahani Musendo aliisha kula sana rushwa sababu ya njaa na hii ilimnasa asitafute mchawi hapa
I might be wrong ila kwa rushwa na media Tanzania ni tatizo

Ushi
 
Kama kweli alionewa nafikiri ana option ya kufungua kesi tena na kutafuta haki yake, nafikiri wanaojua sheria vizuri wanaweza mshauri nini cha kufanya.

Tanzania wanyonge hawana sheria, hata akifungua mashtaka sidhani kama yatafika popote.
 
Kwanza nitoe pole wa mzee, lakini I am sorry kwamba reading between the lines kwangu binafsi haijakaa sawa sana hii habari,

Lakini namuombea mzee aweze kurudi haraka kazini ili kuiongoza familia yake, sio kila neno baya linalorushwa kwa serikali yetu huwa tunalikubali tu hapa JF kirashisi rahisi tu, hii habari haijkaa sawa!

Ni kweli kama binadam kuna ajira umesimama kwa muda mrefu na uongozi wa kifamilia pia amabao ndio hasa uti wa mgongo wa taifa wa uongozi wa taifa letu.
 
Hivi wewe Musendo (Mhariri) ulienda kukutana na Hosea hotelini ukitegemea nini hasa?........kazi?....acha hizo zako bana....weee shukur Mungu umetoka.....nenda ukajenge familia yako....usitafute sympath na story za jela hapa....story yako haina mantiki kabisaaa
 
Na unajuaje ex-Mhariri hakufanya UKICHAA?

Mimi na wewe hapa hatuna details, na tunafanya uchambuzi wa juu juu mno. Mahakamani watakua walipitia yooooote hayo. Mzee akaonekana guilty. Na vigezo vya polisi kukuingizia mikono yake mfukoni, na rules of evidence, na search warrant, na yoooote haya ex-Mhariri atakuwa aliyasema Mahakamani kupitia lawyer.

Kama mimi na wewe tunaona hiyo "logic" kwamba huwezi kuomba rushwa kwa mzuia rushwa, hudhani kwamba lawyer wake hakuyaona hayo? Unless nae ni KICHAA. Jaji hakuyaona hayo? Unless nae ni KICHAA. Jurists (kama walikuwepo) hawakuyaona hayo. Unless nao ni VICHAA. Sijui kama wote hao VICHAA.

Nitakwambia nani ameleta UKICHAA.

Mwandishi wa hii stori (aliyemu interview huyu ex-Mhariri) ndio kafanya kazi KI-KICHAA KICHAA.

Ingekuwa ni nchi za watu zenye press ya maana, mmoja wao kakumbwa na controversial case ya rushwa, tena mhariri wa gazeti, tena kuhusu investigative story iliyoandikwa kuhusiana na rushwa, tena rushwa inayoshutumiwa kufanywa na Ofisa wa Kuzuia rushwa, tena Mhariri anasema walimuingizia mikono mfukoni, hii ingekuwa bonge la issue kwenye Tanzania press. Lakini angalia ilivyo andikwa kidaku.

Hawajasema yaliyojiri mahakamani. Serikali ilitumia mashahidi wale wale, lile trupu lililokuja la Hosea ? Kwa nini alishindwa kesi ? Ex-Mhariri alijitetea nini? Ile original story ya Daily Mirror kuhusu original allegations dhidi ya Hosea iliishia wapi? Hili lilikuwa introduced kwenye kesi ya ex-Mhariri? Alifikiria kukata rufaa? Nini kilikuwa kinampeleka peleka mahotelini kukutana na mtu ambae mnamwandikia investigative story? We mtu umetangualia hotelini saa nzima, kwa nini aje mtu nyuma ndio akununulie wewe vinywaji? Ulipopigwa "telo" ulionyeshwa search warrant? Search Warrant ilitolewa kwa wewe kushukiwa unafanya nini? I mean kabla ya hapo, wewe ulikuwa under suspicion gani? Daily Mirror msimamo wao kwenye hili ni upi, maana inaoneka hawakutaki tena.

I mean, ni vizuri kujua shuruba za wafungwa, lakini stori za prayer times au meal schedule za vyakula vya jela na daily regimen za lupango ni zile zile. Bondo na Ndondo. Kulima na Wanyampara. Funza na Uji. Kuhesabiwa na Kulala. Jumapili Nyama. Sigara ni dili. Kwishne. Wamarekani wanasema, same ol' shit!

Kwa hiyo Mwandishi cut that extraneous stuff, tuambie kesi ya Hosea mwenyewe iliishaje, na muulize ex-Mhariri atueleze vizuri alikamatwa kamatwaje?

Ex-Mhariri atuandikie kwanza kitabu kuhusu soo lake la kusingiziwa. Tukishawishika na uaminifu wake ndio tutasoma kitabu chake cha pili kuhusu hali ya maisha ya jela. Na alivyo dili na lile tatizo sugu kubwa zaidi jela. Forget sigara, japo matatizo yote inasemekana yanaanzia kwenye tamaa ya sigara.


Mkuu
Mahakama za bongo na polisi wenyewe ni bora mahakama ya wazee wa mabaraza ama balozi wa nyumba kumi Na polisi ni bora ya SUNGUSUNGU ama polisi wa mtemi mirambo WARUGARUGA.

Kwanini organi zetu hizo hazifanyi kazi kufuata sheria ,kanuni na taratibu zao ama mwongonzo wao ktk kazi zao.

Na sheria zao hazina taratibu ila wanachofanya ni hiyo kesi inamhusu nani yani nani mshitakiwa na nani mshitaki.

Mfano watu walishuhudia LIVE DITOPILE akichomoa silaha na kuua nini mahakama ilifanya zaidi ya kumpitisha kwenye lango la ma jaji?

Ama leo hii mtu akikusingizia WIZI wa kuku polisi watakutia kolokoloni huku wakiendelea na uchungunzi.Mbona wameshindwa kutiwa kolokoloni hao MAFISADI na uchunguzi uendelee zaidi??

Ama mbona hawakumpa mda KASUSULA mda wa kutosha arudishe hizo fedha wanazodai kakwapua?

Nadhani unaelewa nataka kuongea nini.Yani ya kwamba Hizo sheria unazosema HAZIFUATI ndio maana wanatupwa jela wanao vumbua UFISADI na MAFISADI.

Leo hii wewe unaweza ishi huko uliko miaka 20 lakini ukatia mguu pale uwanja wa ndege ukitokea ulikokua na FISADI akakuchongea kesi ya kwamba kabla ya kuondoka ULIBAKA na kei hiyo ikakutia jela kwa MBONGO tena kifungo cha maisha.
unaweza jitetetea wakati huo ulikua na miaka 5 .Lakini wataleta msichana kwa wakati huo alikua na miaka 2 na huyo msichana anakili kweli ulimbaka.Utashangaa sana lakini upo gerezani.
 
inashangaza mtu aliyeshitakiwa na kukutwa na hatia ya kupokea rushwa anageuzwa shujaa. Utawala wa sheria unasema ni guilty na kama ni kweli alionewa au la haijalishi, nikuwa mahakamani ushahidi uliwekwa akaonekana mwenye hatia. Kama alionekana ameoonewa ni kwa sababu aidha yeye mwenyewe alijiseti up kwa kutofuata maadili ya kazi na hivyo kuwekwa mtegoni kirahisi. Kama alionewa inasikitisha lakini ni vizuri akubali kuwajibika kwa makosa yake yeye mwenyewe.

a. Unapoenda kumhoji mtu hasa kwenye mazingira ya namna hiyo, hakikisha unajilinda vizuri kucover your back. Kwa mfano, mahojiano usifanyie chumba cha hoteli, lazima iwe public place, pili usikubali mtu akupe zawadi yoyote ya kificho pasipo yeye mwenyewe kutia sahihi au kuonesha kuwa anachokupa si rushwa (mnakumbuka ya Mtikila na Rostam?, Rostam hakuweza kudai Mtikila alichukua rushwa!).

b. Pili alikuwa na nafasi ya kukata rufaa kama aliona ameonewa lakini kama baada ya ushauri wa wanasheria wake ni kuwa hakuwa na chance ya kushinda, the record will remain kuwa yeye alikuwa ni mla mrushwa na akubali kuwa aliifanya makosa, na amejifunza na yuko tayari kuanza kujenga upya maisha yako. Tunapowakatalia wananchi kuwaimbia sifa mafisadi na kuwashangilia waliojiuzulu kwa kashfa tusigeuke na kuanza kuwaimbia sifa za kuonewa mwandishi aliyekutwa na hatia ya kula rushwa na ambaye ametumikia kifungo chake.

Tanzania hii kama mtu na familia yake anaweza kufungwa kwa kubaka basi na hapo hapo tusishangae kwamba na yeye anaweza kua kaonewa, tuwe tunaangalia pande mbili.

Soma hapa
"Tulipofika nje nikawaomba nimtaarifu dereva wangu ili arudi ofisini, lakini hawakukubali na waliondoka na mimi hadi polisi Oysterbay ambako nililala huko," anasema."Pia nilisikia kuwa hata dereva wangu alikamatwa baadaye na yeye alilala Central Police kwa kosa la uzururaji nadhani."Anasema kwa mlolongo huo wa matukio alijua kabisa kuwa hawa watu hawakuwa na nia njema naye na mpango huo ulikuwa kumkomoa, kwani dereva hakuwa na kosa lolote.

Sasa kama walichopata wamekipata kwanini na dereva na yeye wamkamate?

Kesi ina utata kwa pande mbili ila tusikikimbilie tu ushujaa wa mzee wakijiji kwani ni mawazo yake.

Nakumbuka pia kesi ya ya yule mwanamuziki watanzania wengi walisema ilikua na utata kutokana na kwamba alifungwa na watoto wake.

Siamini kama baba mbakaji anaweza kuwaambia watoto wake wote washirikiane naye ubakaji.Mtoto mmoja naweza kufikiria mara mbili lakini ukoo mzima asitokee hata mmoja aliyepinga wazo lake la kubaka? come on.

Halafu wewe Wakijiji pamoja na uandishi wako nakuhoji watu na kuishi marekani, ushindwe hata kutuletea jina la hospitali aliyokufa Balali au kama umeshindwa picha ya marehemu hata kaburi lake? au na wewe huko marekani uligaiwa unyamaze? Ulisema utatafuta hospitali ili uwahoji madokta.
Tueleze kama na wewe ulipewa kidogo unyamaze
 
Mh, ni kweli kuna maswali yanahitaji majibu ya kujitosheleza:

Mhariri Mkuu unakwenda kukutana na 'mshukiwa' wako hotelini? pekee yenu?

Inanikumbusha vile hawa baadhi ya waandishi wanavyokwenda kwenye ofisi na majumba ya wahindi kufanya uharamia wa kudai rushwa kwa kutumia vihabari vya kutishia. Kuna baadhi ya waandishi kazi yao ni kutafuta rushwa kwa kutishia kuandika jambo gazetini.

Ushauri: Andika kitabu tu kinachoelezea maisha ya jela na umshukuru mungu kuwa umetoka salama

mnakuwa kama hamumjui hosea bwana ni mafia, kukutana hoteli si hoja alikuwa anatafuta habari au ukweli wa habari hata angemwambia wakutane makaburini angeenda pia, sielewi kama habari ilikuwa imeshatoka angechukua rushwa ili nini sasa naamini hii hosea alitaka kuizima habari.MI NADHANI TUITAFUTE HIYO KASHFA YA HOSEA YA KUHUSIKA NA RUSHWA THEN TUIONGANISHE NA HILI TUKIO
 
Wakuu watu wangapi iwa tunashuhudia wanabambikiwa kesi??Mbona mnataka kuleta mijada isiyo ya lazima tunaona watu wanabambikiwa bangi mfukoni na polisi kesi kibao za kubambikiwa.........cha mhimu hapa tufanyaje kumkoma Hosea aliye mwalibia maisha Zephania ...huku yeye akipeta.Hivi na kwa nini hili swala la huyu mwandishi halipewi uzito wa aina yake naona vyombo vya habari vimekaa kimyaaaaaa....
 
kama hii habari ya kubambikiziwa kesi ni kweli inauma sana!!! na kwa nini ukubali kwenda kuonana na Hosea? kama alikuwa na shida angekuja ofisini kwako. na kama ilithibitika alitoa rushwa basi hiyo habari ilikuwa ya ukweeli
 
Back
Top Bottom