Hongera Tundu Lissu: Hoja ya kurudisha Tanganyika!

siku nikiona tumetengana na zanzibar wana midebwedo hawa, nitafurahi sana, kwasababu malalamishi yao huwa yananikera kuliko nzi wa choo cha kilabuni.
 
Lissu apongezwe. Lissu ameweza kutamka hadharani kuwa tunaihitaji Tanganyika na serikali ya Tanganyika.

Zitto alikusanya saini/sahihi za wabunge za kutaka Pinda aachie nagazi.
Rai: Lissu pia kusanya saini/sahihi za wabunge wanaotaka Serikali ya Tanganyika irudi.

Lissu ametumia marekebisho ya 10 ya mabadiliko ya katiba ya Zanzibar kama kianzio cha kudai Tanganyika.

Katika kuiunda upya EAC tumeazimia pia kuwa na Shirikisho. Tulishaanza fast track ya kuleta hili Shirikisho.
Lissu anaweza kutumia uratibu na uundwaji wa Shirikisho la Afrika Mashariki kama hoja nyengine ya kudai serikali ya Tanganyika. Hoja hii inaungwa mkono na mwanzilishi wa muungano. Mwalimu Nyerere anasema:
"Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili - ya Zanzibar na ya Tanganyika ..." Uk 12 .link ya kitabu hii Tanganyikayetu

Lissu, Mnyika/ Zitto ukikichukua bungeni kitabu hiki, Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania na kukisoma kwa wabunge hiyo sehemu ya ukurasa wa 11-12 utapata pia sahihi za wabunge wa CCM. Utaweza kuanzisha kundi la G220 na serikali ya Tanganyika inarudi bila ya upinzani.

Baada ya kukusanya sahihi hizo na matokeo ya kura hapa JF link kura itabakia kuwasilisha hoja binafsi ya kuundwa kwa serikali ya Tanganyika tu.

Uongozi Wetu Na Hatma Ya Tanzania (by Nyerere)
 
Nafikiri wewe hujaelewa kwa nini watu wanadai muungano wa mkataba,ukiangalia kijografia tanganyika ndio inayo muhitaji zanzibar ukiangalia moja ni bahari kuu ya zanzibar. Hiyo ni moja tu ya mambo ambayo ita wacost . Sisi upande wetu tunataka uhuru hasa hata muungano hatuutaki kwa vile black coloni limetuganda ndio tunapapatua at least tupumulie hapo wa mkataba. But if there's possible to be independent defenetly we gonna be happy 4reva

GHIBUU,

..tuelimishe basi kuhusu suala la bahari kuu ya Zanzibar na faida tutakazopata wa-Tanganyika kwa kuwa na "muungano wa mkataba." kumbuka kwamba tumejumuika hapa kwa lengo la kufahamishana.

..mimi kwa upande wangu, nikizingatia hali ya kila upande kutokuridhika na muungano huu, na zaidi kuutuhumu upande wa pili, nadhani moving forward ni vizuri tukawashirikisha na wenzetu[eac au sadc] ktk mkataba wowote ule unaohusu Tanganyika na Zanzibar.

..tuchukulie hilo suala la bahari kuu. Kwa uelewa wangu Zanzibar inapaka na Kenya kwa upande wa baharini. Sasa kama kuna mkataba wowote ule kuhusiana na masuala ya bahari kuu basi ni bora ukahusisha Kenya,Tanganyika,Zanzibar, na hata nchi nyingine, ili kuepuka hali ya kutokuaminiana ambayo imekuwepo muda wote wa muungano wetu.

..pia kuna extreme theories kwamba the 10 miles coastal strip ya Tanganyika and east africa ni eneo la Zanzibar. bado hata ktk mazingira hayo naamini nchi[Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi,..] zote ambazo zitakuwa landlocked zitalazimika kuwa na mkataba wa Zanzibar. sioni ulazima wa kuwa na "muungano wa mkataba" mahsusi kwa ajili ya Tanganyika na Zanzibar.

..LET ZANZIBAR GO!!!!
 
Last edited by a moderator:
Rais wa Jamhuri ya muungano ana mamlaka gani kule zanzibar? maana hawezi kuteua wakuu wa mikoa? wakuu wa wilaya? akienda kule hawezi kukagua gwaride! wazanzibar wana wimbo wa taifa, bendera! akitembelea rais wa kigeni kule zanzibar anapigiwa mizinga 21 kuonyesha zanzibar ni dola!
 
Ingawaje mie si mwana cdm, nilikumbushwa mengi kwa staili ya kisheria. Pia nilijifunza mengi kutoka hotuba yake hasa kuhusu sheria ya muungano na katiba ya muungani ambavyo kwa tafsiri yake ni vitu viwili tofauti. Nilipata historia nzuri jinsi ARTICLE 11 zilivyoongezwa na kufikia 22. Sasa naelewa kwa nini kuna malalamiko pande zote. Nikikumbuka hotuba mbili za BABA YETU alizotoa 24 March 1995 na 1 May 1995 alitabiri yote yanayotokea na yatakayotokea. Kwa kweli BABA YETU WA TAIFA alikuwa kiona mbali. Mola atuepushe na na aliyotabiri na ile laana ya dhambi kututafuna endapo union itavunjwa aliowaita "walafi wa madaraka".
 
Wacheni uvivu ,hongera kwa lipi jipya ,yaani nyie kazi yenu kutoa hongera ,yalipokuja ya mafisadi mkatoa hongera leo mnatoa hongera,,,,,,,,,,,,,, ! Hapatakiwi tena hongera kinachotakiwa ni kuunga mkono kwa maandaamano ,ni lini WaTanganyika mtaandamana kuidai Tanganyika na kuunga mkono hoja ya Mh.Lisu.

WaZanzibar kama waZanzibari wameandamana kudai mamlaka zaidi ya Nchi yao .
WaTanganyika mnabaki kulalamika pembeni ,tayari wana raisi,bendera ,jeshi yaani hamna mmekaa kama watu wenye choyo ! Wakati mnayo haki ya kuuliza Tanganyika ipo wapi ?
 
we need our country back!

.. nasema tena na tena Tanganyika yenu haipatikani mapaka muanzishe somesing like UAMSHO ili watanganyika milio lala muamke na kujitambua nyinyi ni nani, mapaka sasa mnajiono ni watanzania mkasahau asili yenu. Aidha kana mnataka tanganyika yenu leteni Zanzibar MoU mkubali kuwa mtabeba madeni yote ya Tanzania maana nyie ndio mliokopa sio Zanzibar, bila ya hiyo Zanzibar itatumia kura yake ya turufu kuuwa kufufuka kwa Tanganyika kama tulivyotumia kuuwa wazo la uraia wa nchi mbili, someni viruzi katiba yetu mpya sisi ni nchi kamili na na tuna kura ya veto katika muungano.
 
Watanganyika tuwe na misimamo mingine ambayo ni ya kizalendo kama hoja hii ya Tundu Lissu Bungeni.
Nmeipenda hoja ya Tanganyika.
Kama Wazanzibari wameweza kujitoa katika muungano na wakawa na sera moja juu ya muungano(iwe CCM au CUF).

Gazeti la Nipashe leo 5 Julai 2012, (uk. wa 4)lina kichwa cha habari:

"Lissu ataka Serikali ya Tanganyika irudi

Na Muhibu Said, Dodoma
Kambi ya upinzani Bungeni imesema muungano wa Tanganyika na Zanzibar unakabiliwa na hatari kubwa ya kuvunjika kutokana na kitendo cha Zanzibar kujitangazia uhuru, na kwa hiyo ni wakati mwafaka sasa wa kuanzishwa tena kwa Seikali ya Tanganyika."

Mh Lissu ametoa argument yenye mantiki ya kutosha Bungeni kutetea hoja hii.
Kama walivyokubaliana kule Zanzibar(CCM na CUF) , kambi ya CCM Bungeni tunawaomba waone mantiki ya hoja ya Mh Lisuu katika hili suala la Muungano na hatma yake.
Tanganyika inabidi irudishwe kutokana na yaliyotokea Zanzibar , na kuelekea kukubalika na viongozi wote.
Wabunge wa CCM tafadhali walione hili bila woga.
Nawasilisha

masopakyindi: Hao kina Tundu Lissu waache kutumia hoja ya utanganyika kwa ajili ya maslahi yao kisiasa! Hivi nani anaweza kutuelezea hapa umuhimu wa hoja hii kwa mwananchi wa kawaida? acheni kuchezea kodi zetu na kutuingiza kwenye matumizi yasiyo na mashiko kwa watanzania kwa sababu uchu wenu wa madaraka bana!
 
masopakyindi: Hao kina Tundu Lissu waache kutumia hoja ya utanganyika kwa ajili ya maslahi yao kisiasa! Hivi nani anaweza kutuelezea hapa umuhimu wa hoja hii kwa mwananchi wa kawaida? acheni kuchezea kodi zetu na kutuingiza kwenye matumizi yasiyo na mashiko kwa watanzania kwa sababu uchu wenu wa madaraka bana!
Mkuu naona hujaielewa hoja yangu.
Ni kwamba , hata kama tuanupenda muungano, swala hili limesha pitwa na wakati kwa sababu upande wa pili tunaoungana nao wameshaukana kwa maana ya kubadili kabisa vifungu vya serikali ya Zanzibar, ambavyo vinauweka muungano pemneni.

Nilivyo muelewa Tundu Lissu ni kwamba kama hkuna aliyediriki kuhoji mabadiliko hayo ya katiba ya Zanzibar, siye Tanganyika tunasubiri nini?
Ni heri Tanganyika yetu ikarudi tena.
Hiyo ndiyo argument nzima.

Kwa mfano rahisi unaoweza kuelwa ni kama umeoa bibi mzuri, hakutaki na karudi kwao kapokelewa kwa maandishi, sasa kujifaraguza kwa baba mkwe unasubiri nini? si kipigo na matusi ya wakwe tu?

Kama ni matusi , kuchomewa nyumba , makanisa hata kuwekewa vidole machoni, hilo waTanganyika tumeshafanyiwa, twasubiri nini!
 
Mkuu naona hujaielewa hoja yangu.
Ni kwamba , hata kama tuanupenda muungano, swala hili limesha pitwa na wakati kwa sababu upande wa pili tunaoungana nao wameshaukana kwa maana ya kubadili kabisa vifungu vya serikali ya Zanzibar, ambavyo vinauweka muungano pemneni.

Nilivyo muelewa Tundu Lissu ni kwamba kama hkuna aliyediriki kuhoji mabadiliko hayo ya katiba ya Zanzibar, siye Tanganyika tunasubiri nini?
Ni heri Tanganyika yetu ikarudi tena.
Hiyo ndiyo argument nzima.

Kwa mfano rahisi unaoweza kuelwa ni kama umeoa bibi mzuri, hakutaki na karudi kwao kapokelewa kwa maandishi, sasa kujifaraguza kwa baba mkwe unasubiri nini? si kipigo na matusi ya wakwe tu?

Kama ni matusi , kuchomewa nyumba , makanisa hata kuwekewa vidole machoni, hilo waTanganyika tumeshafanyiwa, twasubiri nini!


Nafikiri kama mtaacha unafiki na kuwa wawazi na wakweli kama Tundu Lissu basi mumekwisha. Waliounda Muungano hawapo sasa mnaogopa ninhi?
mnatakiwa muwe na uthubutu na udhati kama walivyo Znz katika kutetea maslahi ya nchi yenu sio kulalama
 
Nitakujibu kwa sasa sina net natumia simu,nitakupa hoja usiwe na wasi. niweradhi
GHIBUU,

..tuelimishe basi kuhusu suala la bahari kuu ya Zanzibar na faida tutakazopata wa-Tanganyika kwa kuwa na "muungano wa mkataba." kumbuka kwamba tumejumuika hapa kwa lengo la kufahamishana.

..mimi kwa upande wangu, nikizingatia hali ya kila upande kutokuridhika na muungano huu, na zaidi kuutuhumu upande wa pili, nadhani moving forward ni vizuri tukawashirikisha na wenzetu[eac au sadc] ktk mkataba wowote ule unaohusu Tanganyika na Zanzibar.

..tuchukulie hilo suala la bahari kuu. Kwa uelewa wangu Zanzibar inapaka na Kenya kwa upande wa baharini. Sasa kama kuna mkataba wowote ule kuhusiana na masuala ya bahari kuu basi ni bora ukahusisha Kenya,Tanganyika,Zanzibar, na hata nchi nyingine, ili kuepuka hali ya kutokuaminiana ambayo imekuwepo muda wote wa muungano wetu.

..pia kuna extreme theories kwamba the 10 miles coastal strip ya Tanganyika and east africa ni eneo la Zanzibar. bado hata ktk mazingira hayo naamini nchi[Kenya,Uganda,Rwanda,Burundi,..] zote ambazo zitakuwa landlocked zitalazimika kuwa na mkataba wa Zanzibar. sioni ulazima wa kuwa na "muungano wa mkataba" mahsusi kwa ajili ya Tanganyika na Zanzibar.

..LET ZANZIBAR GO!!!!
 
Kuna mpuuzi mmoja kachangia kuhusu eneo la ardhi, naomba ajibu hili: 1964 wakati tanganyika na zanzibar zinaungana jiografia ya ardhi ilikuaje?
 
Nafikiri kama mtaacha unafiki na kuwa wawazi na wakweli kama Tundu Lissu basi mumekwisha. Waliounda Muungano hawapo sasa mnaogopa ninhi?
mnatakiwa muwe na uthubutu na udhati kama walivyo Znz katika kutetea maslahi ya nchi yenu sio kulalama
Wewe ni mtu wa Oman, hata muungano ukivunjika utahusika vipi?
 
Na huo ndo msimamo wa CDM kama kutakuwa na ulazima wa kuwa muungano. Sisi tunaamini katika mapendekezo ya muungano wa serikali tatu...Zanzibar, Tanganyika na ya Muungano. Na me nadhani huu ndo wakati na muafaka wa kulijadili hili jambo ili wananchi nao wawe wamehusika kuliko ilivyokuwa hapo nyumba ambapo muungano ulikuwa ni utashi wa viongozi wetu.
 
Back
Top Bottom