Hongera sana na asante kwenu The Islamic Foundation!!

KAUMZA

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
699
237
Naipongeza sana Taasisi hii ya The Islamic Foundation kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya hapa nchini kwetu Tanzania.

Pia naupongeza sana uongozi wa Manispaa ya Morogoro chini ya Meya wake Mhe Nondo na Mkurugenzi Bw Jorvis kwa kutambua mchango wake hadi kuitunuku Taasisi hii Cheti cha shukrani "Certificate of appreciation" katika kuleta maendeleo ya watu bila kuzingatia dini ama itikadi ya mtu.

Katika kipindi kifupi, The Islamic Foundation imefanikiwa kuchimba visima virefu na vifupi vyenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 300 katika kata mbalimbali za manispaa ya Morogoro. Kata ya Mji mkuu imebahatika kupata visima viwili (2) na pia inajengewa ofisi ya kata ya kisasa kabisa.

Katika kata ya Kilakala kwa mujibu wa diwani wa kata hiyo Bw Ribon Mkali, The Islamic Foundation imewekeza katika ujenzi wa vyumba vinne (4) madarasa vinavyojengwa kwa matofali ya block yaliyolazwa. katika ujenzi huo wananchi wa kata hiyo walichangia kiasi cha Tsh 200,000/ na Islamic Foundation imechangia zaidi ya Tsh milioni 40.

Katika kata ya Mji mpya, kwa mujibu wa Diwani wa kata hiyo Bw Wenceslaus, Taasisi ya The Islamic Foundation imechangia kiasi cha Tsh milioni moja kwa ajili ya kufanya ukarabati wa mfumo wa maji katika zahanati katani humo.

Samweli Msuya wa kata ya Mbuyuni anaielezea The Islamic Foundation kama Mkombozi wa kweli kwa jamii ya wana Morogoro na Tanzania kwa ujumla. Ameelezea kuwa viongozi wake ni wasikivu, wenye huruma na wenye imani.

Kwa kila kisima kirefu kilichochimbwa wamefunga jenereta kwa ajili ya kuvuta maji (kwa maeneo yasiyo na umeme)na wameweka Tank lenye ujazo wa lita 5,000.

Pia kwa kujali elimu na kuizingatia, The Islamic Foundation wanamiliki shule saba (7) na wameweza kujenga misikiti 700 nchi nzima. Pia wanatoa ufadhili kwa watoto wanaoshindwa kulipia gharama za masomo katika shule za msingi na sekondari na wanategemea kuanzisha bodi ya mikopo ya elimu ya juu.

Zaidi katika kuisaidia serikali kupambana na umasikini wameweza kutoa mitaji kwa wajane na vijana na pia wameanzisha kitengo maalumu kwa ajili ya councelling kwa vijana waathirika wa madawa ya kulevya.


Kuhusu haki ya kupata habari, wamewezesha kusimama imara kwa Radio Imaan na Tv Imaan.

Tunashukuru: "Mmeahidi, mkatimiza. Na ALLAH ni Shahidi"

Mwenye macho haambiwi Tazama
 
haya ndio mnatakiwa kuyafanya siku zote si kukimbilia kuua wenzenu na kupiga kelele za mfumo kristo kila siku

dunia ya leo bila elimu dunia na huduma nzuri kwa jamii hamtaenda popote

endeleeni kuwaomba kama wanasaidia wasaidia huduma za afya, elimu, maji ndio tanzania itaendelea ..... na pia kutumia kura zenu kwa umakini kuchagua watu makini watakaoendesha serikali itakayopiga maendeleo mbele kwa kusaidiana na haya mashirika ya kidini
 
Naipongeza sana Taasisi hii ya The Islamic Foundation kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya hapa nchini kwetu Tanzania.

Pia naupongeza sana uongozi wa Manispaa ya Morogoro chini ya Meya wake Mhe Nondo na Mkurugenzi Bw Jorvis kwa kutambua mchango wake hadi kuitunuku Taasisi hii Cheti cha shukrani "Certificate of appreciation" katika kuleta maendeleo ya watu bila kuzingatia dini ama itikadi ya mtu.

Katika kipindi kifupi, The Islamic Foundation imefanikiwa kuchimba visima virefu na vifupi vyenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 300 katika kata mbalimbali za manispaa ya Morogoro. Kata ya Mji mkuu imebahatika kupata visima viwili (2) na pia inajengewa ofisi ya kata ya kisasa kabisa.

Katika kata ya Kilakala kwa mujibu wa diwani wa kata hiyo Bw Ribon Mkali, The Islamic Foundation imewekeza katika ujenzi wa vyumba vinne (4) madarasa vinavyojengwa kwa matofali ya block yaliyolazwa. katika ujenzi huo wananchi wa kata hiyo walichangia kiasi cha Tsh 200,000/ na Islamic Foundation imechangia zaidi ya Tsh milioni 40.

Katika kata ya Mji mpya, kwa mujibu wa Diwani wa kata hiyo Bw Wenceslaus, Taasisi ya The Islamic Foundation imechangia kiasi cha Tsh milioni moja kwa ajili ya kufanya ukarabati wa mfumo wa maji katika zahanati katani humo.

Samweli Msuya wa kata ya Mbuyuni anaielezea The Islamic Foundation kama Mkombozi wa kweli kwa jamii ya wana Morogoro na Tanzania kwa ujumla. Ameelezea kuwa viongozi wake ni wasikivu, wenye huruma na wenye imani.

Kwa kila kisima kirefu kilichochimbwa wamefunga jenereta kwa ajili ya kuvuta maji (kwa maeneo yasiyo na umeme)na wameweka Tank lenye ujazo wa lita 5,000.

Pia kwa kujali elimu na kuizingatia, The Islamic Foundation wanamiliki shule saba (7) na wameweza kujenga misikiti 700 nchi nzima. Pia wanatoa ufadhili kwa watoto wanaoshindwa kulipia gharama za masomo katika shule za msingi na sekondari na wanategemea kuanzisha bodi ya mikopo ya elimu ya juu.

Zaidi katika kuisaidia serikali kupambana na umasikini wameweza kutoa mitaji kwa wajane na vijana na pia wameanzisha kitengo maalumu kwa ajili ya councelling kwa vijana waathirika wa madawa ya kulevya.


Kuhusu haki ya kupata habari, wamewezesha kusimama imara kwa Radio Imaan na Tv Imaan.

Tunashukuru: "Mmeahidi, mkatimiza. Na ALLAH ni Shahidi"

Mwenye ihaambiwi Tazama


Kwenye RED haPO,Kweli Maji yamezidi Unga...Ndo Ratio gani hii?????
 
Safi sana Islamic Foundation..masikini aliyechoka akipatiwa maji na chakula lazima ashukuru..

Na msidhani mi muislam..

mimi sina dini..ila naamini kuna muumba.
 
Safi sana Islamic Foundation..masikini aliyechoka akipatiwa maji na chakula lazima ashukuru..

Na msidhani mi muislam..

mimi sina dini..ila naamini kuna muumba.
Safi sana kwa kujiingiza kwenye mambo ya ukweli kuhusu tunachotakiwa kufanya kama taasisi za dini..hapo hutasikia mkristo wala mpagani au mwislamu mwenzio akukejeli ila kwa mwendo wa radio imaani bado ni tatizo kwa waislamu makini
 
Hizo shule7 zinatosha kuwachukua watoto wote kwenye hyo misikiti700 tumieni akili jengeni mashule kwanza au kwasa7bu mmefeli sana hamhitaji kusoma
 
haya ndio mnatakiwa kuyafanya siku zote si kukimbilia kuua wenzenu na kupiga kelele za mfumo kristo kila siku

dunia ya leo bila elimu dunia na huduma nzuri kwa jamii hamtaenda popote

endeleeni kuwaomba kama wanasaidia wasaidia huduma za afya, elimu, maji ndio tanzania itaendelea ..... na pia kutumia kura zenu kwa umakini kuchagua watu makini watakaoendesha serikali itakayopiga maendeleo mbele kwa kusaidiana na haya mashirika ya kidini

eti 'na pia 2mieni' inamaan waislam ndo wamewachagua viongoz wabov ambao mpaka ss wamesababisha taifa le2 kukosa maendeleo? Acha unazi ww!
 
Hii ni maendeleo. Mikakati endelevu inahitaji. Pamoja na juhudi hizi tushirikiane na kuchagua viongoz wenye uzalendo ili na rasilimali za taifa zisaidie katika haya,then after ten years we will see we are somewhere.
Allah awe nanyi.
 
eti 'na pia 2mieni' inamaan waislam ndo wamewachagua viongoz wabov ambao mpaka ss wamesababisha taifa le2 kukosa maendeleo? Acha unazi ww!

Acha uvivu wa kufikiri wewe unafikiri bila waislam wa maeneo kama lindi, mtwara, pwani na tanga ccm ingekua na majimbo mengi hivi?....na walikuwepo wagombea wazuri tu wa CUF, chadema,etc ila ccm wakawa wanaomba kura misikitini
 
Ila ningewaomba kwenye redio na TV yenu elimisheni umma juu ya uzri wa uislamu na siyo propoganda za kutukana dini nyingine hapo mtakuwa mmefika.TUnachohitaji kujua ni nini kizuri kwenye dini ya uislamu hatuhitaji dhihaka au matusi kwa dini nyingine.Mkiweza hapo wengi tutaisikiliza ili kufuata mahibiri mema.
 
Bara tatizo la udini mi naweza sema halipo na kule Zanzibar kuna tatizo kubwa zaidi ya udini. Ni vigumu kutumia udini kwenye maeneo yenye mchanganyiko wa watu kwa hapa Bara na ufanikiwe.
 
Well done Islamic Foundation! Nilisikia pia wanampango wa kujenga chuo kikuu kanda ya ziwa sijui mchakato umefikia wapi. Inshallah ALLAH awafanyie wepesi, tumechoka waislamu kutukanwa kuwa hatupendi elimu kumbe ni kutokana na ujinga wa wapuuzi wachache wanaojiita BAKWATA wanafisadi tu mali za waislamu wakituacha hatuna mbele wala nyuma.
 
Naipongeza sana Taasisi hii ya The Islamic Foundation kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya hapa nchini kwetu Tanzania.

Pia naupongeza sana uongozi wa Manispaa ya Morogoro chini ya Meya wake Mhe Nondo na Mkurugenzi Bw Jorvis kwa kutambua mchango wake hadi kuitunuku Taasisi hii Cheti cha shukrani "Certificate of appreciation" katika kuleta maendeleo ya watu bila kuzingatia dini ama itikadi ya mtu.

Katika kipindi kifupi, The Islamic Foundation imefanikiwa kuchimba visima virefu na vifupi vyenye thamani ya zaidi ya Tsh milioni 300 katika kata mbalimbali za manispaa ya Morogoro. Kata ya Mji mkuu imebahatika kupata visima viwili (2) na pia inajengewa ofisi ya kata ya kisasa kabisa.

Katika kata ya Kilakala kwa mujibu wa diwani wa kata hiyo Bw Ribon Mkali, The Islamic Foundation imewekeza katika ujenzi wa vyumba vinne (4) madarasa vinavyojengwa kwa matofali ya block yaliyolazwa. katika ujenzi huo wananchi wa kata hiyo walichangia kiasi cha Tsh 200,000/ na Islamic Foundation imechangia zaidi ya Tsh milioni 40.

Katika kata ya Mji mpya, kwa mujibu wa Diwani wa kata hiyo Bw Wenceslaus, Taasisi ya The Islamic Foundation imechangia kiasi cha Tsh milioni moja kwa ajili ya kufanya ukarabati wa mfumo wa maji katika zahanati katani humo.

Samweli Msuya wa kata ya Mbuyuni anaielezea The Islamic Foundation kama Mkombozi wa kweli kwa jamii ya wana Morogoro na Tanzania kwa ujumla. Ameelezea kuwa viongozi wake ni wasikivu, wenye huruma na wenye imani.

Kwa kila kisima kirefu kilichochimbwa wamefunga jenereta kwa ajili ya kuvuta maji (kwa maeneo yasiyo na umeme)na wameweka Tank lenye ujazo wa lita 5,000.

Pia kwa kujali elimu na kuizingatia, The Islamic Foundation wanamiliki shule saba (7) na wameweza kujenga misikiti 700 nchi nzima. Pia wanatoa ufadhili kwa watoto wanaoshindwa kulipia gharama za masomo katika shule za msingi na sekondari na wanategemea kuanzisha bodi ya mikopo ya elimu ya juu.

Zaidi katika kuisaidia serikali kupambana na umasikini wameweza kutoa mitaji kwa wajane na vijana na pia wameanzisha kitengo maalumu kwa ajili ya councelling kwa vijana waathirika wa madawa ya kulevya.


Kuhusu haki ya kupata habari, wamewezesha kusimama imara kwa Radio Imaan na Tv Imaan.

Tunashukuru: "Mmeahidi, mkatimiza. Na ALLAH ni Shahidi"

Mwenye macho haambiwi Tazama

penye red!
 
Back
Top Bottom