Hongera Ridhiwani Kikwete!!!

bado kidogo watamteua kuwa jaji, hililinchi bwana yaani jaji mkuu unakaa kupiga picha na hako kajamaa badala ya kuwahi kutoa hukumu za haki au nawewe ndo kujipendekeza tu kwa mkulu.

Chuki itakupeleka wapi wewe>?!>:
Kweli miafrika mingine ovyo kabisa,kwani kunya anye kuku akinya bata kaharisha!Utakufa nacho kiriba cha roho,kwani aliyekupa wewe mfupa ndiye aliyempa mwenzio nyama na nyama bila ya mfupa haitaitwa nyama hivyo wote sawa tuu acha chuki binafis wewe!
 
mama salma huyu ridhwani ni mwanawe wa kumzaa?

samahani kama suala hili litawakwaza
 
Chuki itakupeleka wapi wewe>?!>:
Kweli miafrika mingine ovyo kabisa,kwani kunya anye kuku akinya bata kaharisha!Utakufa nacho kiriba cha roho,kwani aliyekupa wewe mfupa ndiye aliyempa mwenzio nyama na nyama bila ya mfupa haitaitwa nyama hivyo wote sawa tuu acha chuki binafis wewe!

hongera mkuu, lakini was he alone? mbona inaonekana ni kama ni yeye peke yake ndiye alikuwa commissioned kuwa advocate?
Halafu punguza hasira
 
Hana la kufanya msimdanganye mtoto miaka mitano tu watakua watakaorekebisha hii, hii pass degree ya chini kuliko zote na ku disco habari kamili muulizeni prof shivji na mjue ilikuaje dr juma akaukwaa ujaji. Sasa nisichoelewa mama kikwete anafanya nini kwenye benchi la hao watunga sheria? hawa majaji ni waajabu sana hivi hawaoni wenzao wa pakistani wanavyofanya kazi? yaani wanahitaji hii familia yenye elimu ya kawaida tu kupata picha za michuzi? halafu bahati mbaya hao wanaoitwa marafiki wa Ridhiwana wengine ni matapeli wakubwa hapa mjini inamaana hata state machinery haina nafasi ya kuwashauri nini kinategemewa kwenye umma na familia ya kwanza? I agree na wote wanoashangaa hiki kituko halafu michuzi na elimu yake ndogo akumbushwe matumizi ya blog, blog sio family album hayo ayaweke kwenye face book, ama kweli ushamba ni kitu kibaya ujuzi pekee hautoshi ankal unafanya vizuri lakini kuna mambo ya msingi hayapandi, hebu jamani wana JF wenye ujuzi na haya mambo na matumizi yake msisubiri kualikwa tunaomba muwe karibu na libeneke ili liendelee kutoa mchango kwenye jamii kwa namna hii watu watamuachai ankal na familia yake ya kikwete
 
Nina wasiwasi na credibility yake; kwani nasikia huko Mlimani alikwisha pigwa disco ila mambo yakafanyika na kuonekana amefauru!!!

hujakosea
alienda kusoma masters hull university baada ya mwaka mmoja hata postgraduate cert hakupata
na huko kazini IMMMA anakofanya hayupo kazini mara kibao, amekuwa akisafiri kila siku sijui hata hiyo training alikuwa anafanya saa ngapi
mawakili wetu kazi ipo kweli kweli
 
Hongera Ridhiwani kazi nzuri....nafurahi kuwa umeweza kuwa busy na siasa lakini pia hujasahau karia yako..big up
Ila media na taasisi zingine za umma za TZ zinatia aibu sana yaani....anyway Karl Max alisema haya kweli njaaaaa inaharibu kila sekta....hatuwezi kushangaa SHOBO lililoonyeshwa na media na majaji hapo! tafsiri ni moja tu.........NJAAA

Mix with yours
 
huyo mwanamke wa kwanza kapiga picha na majaji kwa sababu na yeye kijana wake ni muhitimu au??


Ni Mhe. Madam JaJi Salima Kiwete by dat day !!! waweza kuona tofauti nyingine hapa huyo jamaa wa Kulia alivyopoteza umakini kwenye masuala mengine na kumkodolea macho kijana wa JK labda ndio protokali za Kiserikali zilivyo hivyo...Jaji Mkuu anateuliwa na Mhe. Rais, asipoonyesha ushirikiano kwa Mhe Rais ni sawa na kutoheshimu fadhira za uteuzi wake kwani kwenye mchujo majina ni mengi, kwa nini usiwe mwingi wa fadhira ikiwa wewe pekee umeonekana na kuteuliwa.

IMG_6301.JPG

Hongera mwanangu anasema Mama Salma Kikwete
huku Jaji Mkuu Mh. Augustino Ramadhani akishuhudia
 
Hizi picha ziko kwenye blogy ya Michuzi,ambayo amekuwa propanganist wa CCM na viongozi wa serikali.
Amechukua nafasi ya gazeti la UHURU na MZALENDO.
 
Kwa watu tunaomjua huyu dogo,kuwa Wakili ,ni kuidhalilisha profession ya Sheria
Tanzania.Hii profession inakwenda chini kila siku,mawakili wengi ni wapo kuihujumu serikali ya Tanzania na mamluki wa nje.Angalieni mikataba feki !

Hapo IMMA advocates kuna majina ya akina Karume,Chenge and kikwete!

Haya mambo iko siku yatafika mwisho ,na wananchi tutarise up!
 
Kwa hiyo ina maana huyu jamaa atakuwa anapanda kizimbani na kutetea wateja wake na kufanya cross examination na mambo mengine kama hayo?
 
Mkuu ni ukweli usiopingika kwamba taaluma ya sheria Tanzania siku hizi ni ya kutayarisha mafisadi. Fikiria mikataba aliyoandika na kusaini Ringo Tenga, Mkono, n.k. Ni wizi mtupu.

ipo siku lakini yote haya yatakwisha na wezi wote watakiona cha moto.
 
Mimi nadhani mawakili wengi bongo ni shysters na wengi wao wapo wapo tu. Kwanza mawakili wakali bongo ni kina nani? Sijui kwa nini tu nina mashaka na justice system ya bongo.....
 
Ndugu yangu kwa sababu ni rithwani ndio yamekuwa hayo huamini kwamba watu hubadilika na kuja kuwa viongozi na watendaji kwenye jamii zao hata kama walikuwa kina nani ? hujasikia zile habari za majambazi waliogeuka wachungaji , wakonda wa daladala waliokuja kuwa maraisi kama chiluba wa zambia na yule raisi wa sasa wa brazil hiyo ni mifano michache watu hubadilika hata kama kuna nini kwahiyo huyu mtu asihukumiwe kwa makosa au mambo yake ya zamani tuangalie wakati wa sasa tunachangamoto na mambo mengi ya kutatua zaidi ya hili haswa kubadilisha mentality ya watanzania kama wewe
 
Ndugu yangu kwa sababu ni rithwani ndio yamekuwa hayo huamini kwamba watu hubadilika na kuja kuwa viongozi na watendaji kwenye jamii zao hata kama walikuwa kina nani ? hujasikia zile habari za majambazi waliogeuka wachungaji , wakonda wa daladala waliokuja kuwa maraisi kama chiluba wa zambia na yule raisi wa sasa wa brazil hiyo ni mifano michache watu hubadilika hata kama kuna nini kwahiyo huyu mtu asihukumiwe kwa makosa au mambo yake ya zamani tuangalie wakati wa sasa tunachangamoto na mambo mengi ya kutatua zaidi ya hili haswa kubadilisha mentality ya watanzania kama wewe


Hizi ndizo changamoto za kutatua ndugu yangu, au hujui tatizo linahitaji kutibiwa mapema zaidi??...pia,tofautisha mabadiliko ya tabia ya mtu na weledi katika profesheni husika..SHERIA, kama ilivyo UDAKTARI na UHANDISI ni baadhi ya kazi ambazo si mtu yoyote anaweza kufanya, inahitaji mhusika kufuzu na kuwa timilifu katika fani husika..
 
Ndugu yangu kwa sababu ni rithwani ndio yamekuwa hayo huamini kwamba watu hubadilika na kuja kuwa viongozi na watendaji kwenye jamii zao hata kama walikuwa kina nani ? hujasikia zile habari za majambazi waliogeuka wachungaji , wakonda wa daladala waliokuja kuwa maraisi kama chiluba wa zambia na yule raisi wa sasa wa brazil hiyo ni mifano michache watu hubadilika hata kama kuna nini kwahiyo huyu mtu asihukumiwe kwa makosa au mambo yake ya zamani tuangalie wakati wa sasa tunachangamoto na mambo mengi ya kutatua zaidi ya hili haswa kubadilisha mentality ya watanzania kama wewe

Shy acha ujinga .Huwezi kumfananisha Ridhiwani na Chiluba au Lula Da Silva wa Brazil it is a joke.
Hawa hawakuwa na baba zao RAIS!

Chiluba alimng'oa Rais Kaunda kwa kura huru,alitoka kwenye Trade Union movement.Uzuri wa Wazambia sio mbumbumbu kama mimi na wewe.
Uzuri wanaweza kumvote out mtu yoyote yule,na kumpeleka mahakamani kiongozi yoyote mla rushwa.Pamoja na kumchagua Chiluba,alikuwa disgraced vilevile ndio maana hayuko madarakani.
Lula Da Silva yeye alitoka Workers party.Sijiu kigezo gani umetoa hapa .
 
Note kwamba mwaka 2005 ilikuwa zamu ya mama kumpigia kampeni baba nchi nzima.
Sasa 2010 ni zamu ya baba kwa mbinu zile zile za mama kuzunguka Tanzania kumuuza baba.
Nchi zi ni mali yao? Muulize hiyo pesa anayotumia inatoka wapi? usishangae atapokelewa na maRC na maDC na maRPC na atatembea kwa ving'ora. Wajinga ndio waliwao.
 
Labda pengine hoja ya kulaumu fani ya sheria kwa ujumla wake kutokana na mapungufu au maovu ya watu wachache inaleta hisia za ambazo zina maswali mwengi!!. Binafsi naona hao mawakili (wanasheria) wao wanatumika kama sambamba na wataalaumu wengine (professionals) na hivyo kila kesi ni vizuri ikahukumiwa kwa vigezo vya maelezo yake.



Ukiondoa hao walitajwa katika makashfa ya EPA na Richmond ( Mkono Advicates, IMMA Advocates, Chenge, Mwanyika, Donald Chidowu, Edward Hosea, Capt. Sanze, Malegesi, Ringo Tenga, nk) wapo wataalamu wengi tu katika hii nchi ambao wameifikisha hapa tulipo wakiwa wanatuhumiwa kwa kufanya maovu kwa ajili ya manufaa binafsi aidha kwa kutumia nyazifa zao kwa uzembe wa makusudi kabisa au kushindwa kutimiza wajibu . Baadhi yao ni hawa hapa ambao sidhani kuwa ni mawakili:
  1. B.W. Mkapa
  2. Bazil Pesa Mlamba
  3. Gray Mgonja
  4. Anna Mkapa
  5. Zakhia Meghiji
  6. Daniel Yona
  7. E.N. Lowassa
  8. Rajab Maranda et al
  9. JEETU Patel "Jitu Tapeli"
  10. Devendra Vinodbhai Patel
  11. Amit Nandy,
  12. Ketan Chohan,
  13. Johnson Lukaza,
  14. Bahati Mahenge,
  15. Davies Kamungu,
  16. Godfrey Mosha
  17. Manase Mwakale
  18. Eddah Mwakale,
  19. Bosco Kimela
  20. Amatus Liumba
  21. Shailesh Pragji Vithlani
  22. Tanil Jumar Chandulal Somaiya
  23. Dk. Rashidi
  24. Dr. Marehemu Balali
  25. M. Msabaha
  26. Nazir Karamagi
  27. Arhtur Mwakapugi
  28. Patrick Rutabanzibwa
  29. Singi Madata
  30. Theophilo Bwakea
  31. Stephen Mabada
  32. Godson Makia
  33. Dick Tewa
  34. Gideon Nassari
  35. Julius Sarota
  36. Mwita Wangwe
  37. Athanas Mbawala
  38. James Mwalilimo
  39. Rostam Azizi.
Hawa ni baadhi tu ambao wametuhumiwa katika hali moja au nyingine kukwamisha maendeleo ya nchi hii ukiachia wale ambao pia waliusika katika mchakato wa kujiuzia nyumba za Umma.
 
Kwani vigezo vya kumteua mtu kuwa wakili wa kitegemea ni nini?

Kitu kingine watanzania wenzangu tuache ku poliiliticise kila kitu mwishowe tukakuwa hatumaa maana tunawalaumu watu kuingiza siasa kwenye mambo ya singi wakati sisi hata kutambua thread hii iwekwe kwenye forum gani tunashindwa .
 
Back
Top Bottom