Hoja Binafsi za Zitto na January:Je, Wabunge watalipa visasi

What???????????/ tafadhali nyambua sentensi yako,haitekelezeki kivipi?
Mkuu Josephine,
asante kwa picha!
profilepic25998_2.gif.jpg
 
Nilipata kumwona Zitto kwenye kipindi cha jambo Tanzania akielezea hoja yake hiyo. Aliielezea vizuri, akaonyesha ni vipi mapato ya fedha za kigeni yaongezeka sana kutokana na mauzo ya mazao ya mkonge. Nakumbuka to have said that " the world is now turning to organic products". Akatoa hata data ya deficity ya katani katika world market maana kwa sasa ni Brazil inayozalisha mkonge ila haina ardhi ya kutosha! Akaeleza magari yote ya kifahari duniani kwa sasa yanavyohitaji mazuria natural rather than artificial. Kwa hiyo soko lipo kama tutawekeza kidogo tu katika mkonge. Kama hoja hii imetupwa HATUNA BUNGE!!


Yaani wewe ndiyo unajua leo kwambahatuna Bunge? Bunge la wazee wastaafu ambao walikuwa watumishi wa umma unategemea wanaweza hata kuelewa Zitto anaongea ninin? But their days are numbered. Hata aliyegundua umeme kule Uingereza, siku anatoa hoja yake Bungeni alipuuzwa kabisa. Leo hii umeme ndio kila kitu katika maendeleo ya sayansi na technolojia!

Kaza buti Zitto, kaza buti January.....I can see a ray of hope at the end of the tunnel!
 
Upo sahihi. Tukianza na hoja ya Zitto. Mkonge kwa miaka mingi sana ulikuwa utatupatia Tanzania karibia 60% ya mapato ya fedha za kigeni wakati wa nyerere. Tanzania ilikuwa one of the top producers wa zao hili, kama sio number one in the world. Zao hili lilikuja kudondoka baada ya introduction ya synthetic fibre kwenye soko la dunia, ambayo ikawa a substitute to sisal based products kwa haraka sana mwisho wa miaka ya 70 hadi mwanzoni mwa 80; Lakini zao hili limeanza kuwa na soko zuri sana, hasa kutokana na mahitaji yake kwenye uzalishaji katika new industrialized countries kama China na kwingineko. Hivi sasa Brazil ndio number one producer, na hii ni nchi ya kumi kwa utajiri duniani in terms of GDP.

Sasa kama nchi kubwa kama Brazil wanaweka mkazo kwenye mkonge, kwanini isiwe sisi ambao tuna uwezo kabisa wa kuwa hata number moja kwa uzalishaji duniani? Pia Kilimo cha mkonge kikiendeshwa kwa ufanisi, kina uwezo wa kutuzalishia umeme ulio sawa na ule wa Richmond au IPTL i.e 100 MW; kinachohitajika kufanikisa hili la umeme wa 100 MW ni kutumia tu mabaki ya mkonge, ambayo hivi sasa yanatupwa tu porini. Hivyo, mkonge unaweza kuokoa nchi hii kiuchumi kwa kutupatia mapato ya kigeni, kutoa ajira kwa vijana huko vijijini na pia kutuzalishia umeme.

Hoja ya January pia ni muhimu sana kwani inalenga uanzishwaji wa Mamlaka ya kudhibiti Makazi na Ujenzi, kwani hivi sasa ujenzi huo unaenda kiholela holela, na hausaidii pato lolote la maana kwa taifa. Tanzania ni moja ya majiji yanayokuwa kwa kasi sana afrika in terms of real estate, na sekt ahii ina mchango mkubwa sana kwa GDP kutokana na ujenzi unaondelea kwenye kila kona ya majiji makuu ya Tanzania, lakini ukuaji wa sekta hii hauendi sambamba na ongezeo la mapato ya serikali kupitia kodi ya majengo/makazi, esp property tax. Kwa mfano, kama Dubai, na kwingineko, michango wa Real Estate kwenye GDP ni mkubwa sana kwa sababu ya udhibiti wa sekta hii. Nchi kwetu vilevile kuna tatizo la nchi kutokuwa na sheria juu ya makazi, hasa inayomlinda mpangaji dhidi ya mwenye nyuma; Hii ni mbaya hasa kwa kuzingatia kwamba katika mahitaji muhimu ya binadamu, makazi ni moja wapo kwani mahitaji ya msingi ya binadamu ni food, clothing and shelter/nyumba, chakula na malazi.

Hoja zote mbili za waheshimiwa hawa ilitakiwa ziungwe mikono na miguu, lakini kuanguka kwake ni dhahiri kwamba bunge letu halipo kwa ajili ya maslahi ya watanzania, bali maslahi binafsi ya wahusika.

Kama kawaida yako mchambuzi umezichambua hoja hizi mbili kwa ufupi na umahiri mkubwa, mkazo wangu ukiwa maeneo niliyoweka rangi nyekundu.
Suala la mkonge likiwa ni eneo mojawapo tu linaloweza kutuondoa kwenye janga hili la umaskini na kuwa tegemezi wa kuomba omba misaada kwa wazungu (nasema kwa uchungu mkubwa) achilia mbali madini, utalii, uvuvi na utajiri mwingine wote ambao nchi hii inao lakini inakosa usimamizi mzuri na kuliwa na mafisadi wachache.
Angalia nchi ilivyo na matatizo makubwa mfano umeme, angalia wizara ya nishati na madini inavyogubikwa na tuhuma kibao za ubadhirifu wa trillions of money.
Angalia nchi inavyokumbwa na janga la ukosefu wa ajira kwa vijana.... ufumbuzi tunao lakini still Serikali inajifanya kipofu.
Kwanini isijifunze kula na kipofu? kama imeamua kun'gata, basi ingeuma pia kidogo japo kutupunguzia machungu waTanzania!
Kwanini kila siku tushike nafasi za juu kwenye umasikini na kuwa ombaomba wakati tunazo opportunities za kuweka good records kama vile wazalishaji wakuu wa mkonge duniani?
 
Hivi kama zitto kaweka hoja mezani lazima alikua na point za kuitetea hoja.... je wamempa nafasi ya kuitetea hoja?

Na je hao waliopinga wana sababu gani kupinga.. tukiyajua hayo tunaweza kujadili vizuri

Angalau Kidogo January yeye alipata nafasi ya kuzungumza baada ya Waziri Tibaijuka kujibu hoja yake. January kikubwa aliomba Spika awaachie wabunge wengine watoa mchango na Spika Makinda akakubali na ndipo Ole Sendeka na Mbowe wakapewa fursa hiyo na kimsingi, kukubaliana na January. Lakini tofauti na January, kilichofanyika juu ya hoja ya Zitto ni udikteta uliotukuta wa Spika Makinda, kwani tofauti na january ambae alipewa dakika kadhaa kujibu mapigo ya Waziri Wa ardhi na pia kukubaliwa ombi lake la kuwapa wabunge nafasi ya kutoa michango yao, kwa upande wa Zitto, yeye hakupewa nafasi kujibu mapigo ya Waziri wa Kilimo na wala hakuna mbunge yeyote aliyepewa nafasi kufanya hivyo mbali ya Halima Mdee ambae aliomba mwongozo wa Spika na kupewa nafasi hiyo lakini huku akiingiliwa ovyo na Spika. Kina Lissu na wengine hawakufanikiwa katika jitiada za kuiokoa hoj ahii kwani miongozo yao ilizibiwa masikio na Makinda. Hoja ya Halima Mdee ambayo ili base kwenye kanuni, ingeweza kuokoa hoja ya Zitto iwapo Makinda angeacha kuikinga serikali katika hoja ile.
 
I have never seen useless wabunge kama hawa hoja ya msingi wanaleta mambo yao ya siasa but siwezi kuwalaumu sana kofia na fulana zinawasubiri 2015
 
Tunajua kila m2 anaukichaa wake ila tunatofautiana viwango kutokana na ulivyo uactivate mwenyewe. Ila ukiingia kwenye mfumo wa utawala wa chama cha mapinduzi unakuwa ushafanya TOTAL activation, wabunge wa CCM ni vilaza hakya nani
 
Leo, hoja ya Zitto kuhusu mkakati maalum wa kufufua zao la mkonge na ile ya January kuhusu umuhimu kulinda wapangaji zinawasilishwa bungeni. Je zitapita? Kwa mtazamo wangu, kuna uwezekano mkubwa kwamba, pamoja na umuhimu wa hoja hizi mbili, hoja hizi zitakwama, sababu kubwa ikiwa ni hasira ya wabunge juu ya msimamo wa Zitto na January kupinga ongezeko la posho.

Niliisikia hoja binafsi ya Mhe Zitto lakini skupata fursa ya kuisikia ya Mhe Makamba. Mhe Zitto alitoa data nyingi sana za kuthibitisha hoja yake laikini alipochemsha ni kutaka Bunge lipitishe azimio kuwa Serikali iufanye mwaka 2012 uwe mwaka wa kupanda mkonge. Azimio hili lilitosha kuondoa mantiki nzima ya hoja yake a mbunge aliyomba kurekebisha hoja hii japo niliweza kubaini hakuwa msomi kama Mhe Zitto aliweza kumgaragaza kikweli kweli kwa kuwa haiwezekani kwa mtu msomiambaye tayari amekwish kuonyesha ni uwekezaji kiasi gani unahitajika ili Tanzania iweze kurejesha hadhi yake katia akilimo cha mkonge aweze kupendekeza kupitishwa kwa azimio kuwa mwaka 2012 uwe mwaka wa kupanda mkonge ilihali hivi sasa tupo Februari 2012.

Kwa maoni yangu Mhe Zitto kwa kutumia kiburi cha usomi alitaka kulitrumia bunge kujipatia umaarufu katika kupendekeza kitu kisichowezekana.
 
Kama kawaida yako mchambuzi umezichambua hoja hizi mbili kwa ufupi na umahiri mkubwa, mkazo wangu ukiwa maeneo niliyoweka rangi nyekundu.
Suala la mkonge likiwa ni eneo mojawapo tu linaloweza kutuondoa kwenye janga hili la umaskini na kuwa tegemezi wa kuomba omba misaada kwa wazungu (nasema kwa uchungu mkubwa) achilia mbali madini, utalii, uvuvi na utajiri mwingine wote ambao nchi hii inao lakini inakosa usimamizi mzuri na kuliwa na mafisadi wachache.
Angalia nchi ilivyo na matatizo makubwa mfano umeme, angalia wizara ya nishati na madini inavyogubikwa na tuhuma kibao za ubadhirifu wa trillions of money.
Angalia nchi inavyokumbwa na janga la ukosefu wa ajira kwa vijana.... ufumbuzi tunao lakini still Serikali inajifanya kipofu.
Kwanini isijifunze kula na kipofu? kama imeamua kun'gata, basi ingeuma pia kidogo japo kutupunguzia machungu waTanzania!
Kwanini kila siku tushike nafasi za juu kwenye umasikini na kuwa ombaomba wakati tunazo opportunities za kuweka good records kama vile wazalishaji wakuu wa mkonge duniani?

Upo sahihi. Ni kama vile CCM ina agenda mahsusi ya kuhakikisha mtanzania hanyanyuki kutoka katika lindi la umaskini kwasababu kuna vitu vingine hata ukitumia common sense kabla ya kuamua, unakuwa umejituma kupita kiasi, kwani kwa hoja hizi mbili za Zitto na january, hata akili chini ya kiwango cha common sense inatosha kabisa kusaidia mtu kuja na uamuzi kuhusu nini ni sahihi na nini sio sahihi. Spika Makinda anachofanya analinda vitu viwili: Kwanza analinda kiti kwa kuepuka hali ya wabunge kukosa imani nae - bila ya kujua kwamba ilitakiwa alinde kiti chake cha ubunge ambacho ndicho kimempa kiti cha uspika, otherwise anayoyafanya hayatamrudisha tena bungeni; na kitu cha pili anacholinda ni Serikali, hata kwenya madudu ambayo yanaenda kwenye hansard ya umma (sio hansard ya bungeni kwani hata hii imeanza kuchakachuliwa); 2015 wapiga kura wa nchi hii watairudia hansard yao ya umma ili kufanya maamuzi iwapo wakipe CCM dhamana tena au lah ifikapo 2015. Huo ndio utakuwa wakati wa CCM sasa kulipa its dues.
 
Angalau Kidogo January yeye alipata nafasi ya kuzungumza baada ya Waziri Tibaijuka kujibu hoja yake. January kikubwa aliomba Spika awaachie wabunge wengine watoa mchango na Spika Makinda akakubali na ndipo Ole Sendeka na Mbowe wakapewa fursa hiyo na kimsingi, kukubaliana na January. Lakini tofauti na January, kilichofanyika juu ya hoja ya Zitto ni udikteta uliotukuta wa Spika Makinda, kwani tofauti na january ambae alipewa dakika kadhaa kujibu mapigo ya Waziri Wa ardhi na pia kukubaliwa ombi lake la kuwapa wabunge nafasi ya kutoa michango yao, kwa upande wa Zitto, yeye hakupewa nafasi kujibu mapigo ya Waziri wa Kilimo na wala hakuna mbunge yeyote aliyepewa nafasi kufanya hivyo mbali ya Halima Mdee ambae aliomba mwongozo wa Spika na kupewa nafasi hiyo lakini huku akiingiliwa ovyo na Spika. Kina Lissu na wengine hawakufanikiwa katika jitiada za kuiokoa hoj ahii kwani miongozo yao ilizibiwa masikio na Makinda. Hoja ya Halima Mdee ambayo ili base kwenye kanuni, ingeweza kuokoa hoja ya Zitto iwapo Makinda angeacha kuikinga serikali katika hoja ile.


Sio kweli hata kidogo kwani unataka kutupotosha, baada ya hoja ya Mhe zitto yupo kwa mujibu wa kanuni za bunge yupo mbunge aliyekuwa ameomba kurekebisha hoja binafis ya Mhe zitto hivyo alipatiwa nafasi, Namheshimu sana Mhe Zitto na mara nyingi huwa nakubaliana naye sana lakini katika hoja hii alichemsha sana katika kupendekeza maazimio, alifanikiwa sana kujenga hoja kuhus zao hili na nafasi ya Tanzania katika zao hili alipochemsha ni kutaka "Bunge lipitishe azimio kuwa Serikali itamke kuwa mwaka 2012 ni mwak wa kupanda mkonge. Kwa akil ya kawaida kwa wale waliosikiliza hoja ya Mhe Zitto, uwekezaji aliosema unahitajika kabla ya wakulima wadogo hawajakuwa intergrated katika kilimo cha mkonge hususan challenge ya kupata ardhi iliwezekana vipi aliombe bunge lipitishe azimio kuwa Serikali itamke kuwa mwak 2012 ni mwaka wa kupanda mkoge?

Tukubaline pendekezo hili ndilo lililofanya hoja yake kukosa mashiko kabisa kiasi cha mbunge asiye msomi kama yeye kuweza kumkosoa kisawaswa. Ni wasiwasi kama maudhui ya mapendekezo ndani ya hoja binafsi ya Mhe Zitto yalifanyiwa kazi na kamati ya wabunge wa CDM ili kuweza kuondoa dosari kama kupendekeza kitu kama hicho kilichosababisha hoja binafsi ya Mhe Zitto kupigwa technicla knock out?
 
Hivi kama zitto kaweka hoja mezani lazima alikua na point za kuitetea hoja.... je wamempa nafasi ya kuitetea hoja?

Na je hao waliopinga wana sababu gani kupinga.. tukiyajua hayo tunaweza kujadili vizuri

Mkuu walipinga kwa kuwa tu hoja imeletwa na Zitto tu na sio kuwa wlikuwa na hoja ya kuipinga !
 
Angalau Kidogo January yeye alipata nafasi ya kuzungumza baada ya Waziri Tibaijuka kujibu hoja yake. January kikubwa aliomba Spika awaachie wabunge wengine watoa mchango na Spika Makinda akakubali na ndipo Ole Sendeka na Mbowe wakapewa fursa hiyo na kimsingi, kukubaliana na January. Lakini tofauti na January, kilichofanyika juu ya hoja ya Zitto ni udikteta uliotukuta wa Spika Makinda, kwani tofauti na january ambae alipewa dakika kadhaa kujibu mapigo ya Waziri Wa ardhi na pia kukubaliwa ombi lake la kuwapa wabunge nafasi ya kutoa michango yao, kwa upande wa Zitto, yeye hakupewa nafasi kujibu mapigo ya Waziri wa Kilimo na wala hakuna mbunge yeyote aliyepewa nafasi kufanya hivyo mbali ya Halima Mdee ambae aliomba mwongozo wa Spika na kupewa nafasi hiyo lakini huku akiingiliwa ovyo na Spika. Kina Lissu na wengine hawakufanikiwa katika jitiada za kuiokoa hoj ahii kwani miongozo yao ilizibiwa masikio na Makinda. Hoja ya Halima Mdee ambayo ili base kwenye kanuni, ingeweza kuokoa hoja ya Zitto iwapo Makinda angeacha kuikinga serikali katika hoja ile.


Wadau kumbukeni mashamba yote ya mkonge yalishauzwa wa wawekezaji uchwara ambao wameshindwa kuyaendeleza. Na wengine ni viongozi ndani ya serikali. Hoja hii ingepita, ingeibua madhambi mengine yaliyojificha kwenye sekta ya kilimo cha mkonge.

Lakini hoja kutokupitiswa leo, si kifo cha wazo hilo za Zitto Kabwe. Kama kweli kuna potential ecomonic benefits kwa nchi, zinaweza kuvunwa hata bila ya kupitishwa na hoja ya wabunge waoasinzia Bungeni na kugonga gonga meza bila hata kujua walitendalo.
 
Leo, hoja ya Zitto kuhusu mkakati maalum wa kufufua zao la mkonge na ile ya January kuhusu umuhimu kulinda wapangaji zinawasilishwa bungeni. Je zitapita? Kwa mtazamo wangu, kuna uwezekano mkubwa kwamba, pamoja na umuhimu wa hoja hizi mbili, hoja hizi zitakwama, sababu kubwa ikiwa ni hasira ya wabunge juu ya msimamo wa Zitto na January kupinga ongezeko la posho.
Hilo nalo neno?!!! Hii ni kutokana na ubinafsi, umbumbu na ushabiki wa wabunge wa CCM
 
bila shaka ni suala la Posho hakuna mantiki ya wabunge kupinga hizi hoja,ila bila kujua kuwa wanawapa jamaa promo na huku wakijichimbia mashimo
 
Niliisikia hoja binafsi ya Mhe Zitto lakini skupata fursa ya kuisikia ya Mhe Makamba. Mhe Zitto alitoa data nyingi sana za kuthibitisha hoja yake laikini alipochemsha ni kutaka Bunge lipitishe azimio kuwa Serikali iufanye mwaka 2012 uwe mwaka wa kupanda mkonge. Azimio hili lilitosha kuondoa mantiki nzima ya hoja yake a mbunge aliyomba kurekebisha hoja hii japo niliweza kubaini hakuwa msomi kama Mhe Zitto aliweza kumgaragaza kikweli kweli kwa kuwa haiwezekani kwa mtu msomiambaye tayari amekwish kuonyesha ni uwekezaji kiasi gani unahitajika ili Tanzania iweze kurejesha hadhi yake katia akilimo cha mkonge aweze kupendekeza kupitishwa kwa azimio kuwa mwaka 2012 uwe mwaka wa kupanda mkonge ilihali hivi sasa tupo Februari 2012.

Kwa maoni yangu Mhe Zitto kwa kutumia kiburi cha usomi alitaka kulitrumia bunge kujipatia umaarufu katika kupendekeza kitu kisichowezekana.

Naelewa hoja yako lakini kikubwa hapa ni kwamba tunaelekea bajeti ya 2012-2013, mimi nadhani Zitto angeitumia bajeti ijayo itakayowasilishwa bungeni mwezi June, kama reference wakati wote wa kujenga hoja yake, na hii ingeipa hoja yake nguvu kubwa zaidi - kwa kusema kwamba kutokana na umuhimu wa zao hili....ni matarajio yangu kwamba kuanzia bajeti ya mwaka huu wa fedha, wizara ya kilimo itafanya haya haya na haya kuhusu zao la mkonge;

Iwapo zitto angefanya hayo kwa kulink na bajeti ijayo, waziri angeingia tu mtego wa kutoa ahadi kemkem kwamba watafanya hili na lile kwenye bajeti, then zitto kumsibiria na bajeti yake na kuanza nae upya.
 
Wadau kumbukeni mashamba yote ya mkonge yalishauzwa wa wawekezaji uchwara ambao wameshindwa kuyaendeleza. Na wengine ni viongozi ndani ya serikali. Hoja hii ingepita, ingeibua madhambi mengine yaliyojificha kwenye sekta ya kilimo cha mkonge.

Lakini hoja kutokupitiswa leo, si kifo cha wazo hilo za Zitto Kabwe. Kama kweli kuna potential ecomonic benefits kwa nchi, zinaweza kuvunwa hata bila ya kupitishwa na hoja ya wabunge waoasinzia Bungeni na kugonga gonga meza bila hata kujua walitendalo.

Wamiliki wakubwa wa mashamba hayo ni watanzania wenye asili ya ki-asia.
 
Naelewa hoja yako lakini kikubwa hapa ni kwamba tunaelekea bajeti ya 2012-2013, mimi nadhani Zitto angeitumia bajeti ijayo itakayowasilishwa bungeni mwezi June, kama reference wakati wote wa kujenga hoja yake, na hii ingeipa hoja yake nguvu kubwa zaidi - kwa kusema kwamba kutokana na umuhimu wa zao hili....ni matarajio yangu kwamba kuanzia bajeti ya mwaka huu wa fedha, wizara ya kilimo itafanya haya haya na haya kuhusu zao la mkonge;

Iwapo zitto angefanya hayo kwa kulink na bajeti ijayo, waziri angeingia tu mtego wa kutoa ahadi kemkem kwamba watafanya hili na lile kwenye bajeti, then zitto kumsibiria na bajeti yake na kuanza nae upya.

Ndio maana nahoji kama kweli aliwashirikisha wabunge wenzie katika kudraft mapendekezo. Ni lazima tukiri kuwa alifanya utafiti mzuri sana lakini tujue kuwa pale wapo katika mchezo wa siasa na sisi wote tupo katika mchezo wa siasa ndio maana tunajadili haya. kwa kuwa hoja hizi huwasilishwa mapema walikwishaikalia hoja ya Mhe Zitto na kumundalia mb unge atakayetumia Kanuni kuipiga knock technical out hoja yake.
kwa ufahamu wangu mambo yote aliyopendekeza Mhe Zitto ni ndoto za mchana kwa watendaji wa serikali ya CCM ambao hukaa kuvizia posho wakati wote.

Sababu ingine iliyofanya haja hiyo kutupwa ni kashafa zilizoko katika ubinafsishaji wa mashamba ya mkonge mojawapo likiwa shamba alilochukua CHAVDA aliyesababisha Mhe Lyatonga Mrema kuondolea katika baraza la mawaziri. Ndio maana Hoja hii ilitakiwa kukaliwa kweli kweli na kuandaliwa makakati wa pamoja kama chama.

Kwa kuwa CCM ni chama kikongwe na ina machinery ya serikali nyuma yake ilitumia 2011 kuusoma uwezo wa wabunge wa CDM mmoja mmoja na inabuni mikakati ya kuwamaliza pole pole. Mfano halisi ni wakati wa kuhitimisha hoja ya katiba mwanasheria Mkuu wa Serikali alikuwa antumia maneno kwa uangalifu mkubwa kuonyesha kuwa Mhe Tundu Lissu sio mstaarabu na muungwana k.m "Mimi nimefunddishwa kumsikiza mtu akiongea" "Mimi sikufundishwa kumnyooshea mtu mwingine mkono" n.k.

Hizi ni baadhi ya strategies ambazo CDM inabidi iwe aware nazo. Na wabunge wake wanapotaka kupeleka hoja binafsi kama hizi lazima ziandaliwe mkakati maalum. Nafikiri pia timingi ya hoja binafisi ya Mhe Zitto haikuwa nzuri sana baada tu ya kuwachafua wanaopaswa kumuunga mkono kuhus posho n.k
 
ccm haina wabunge, ina watu mbumbumbu, mazoba, wasifikiri, watu legelege, wasiofaa, hakika ccm ni kielelezo cha watu duni na mamluki kwa taifa lao.
 
Hivi Chavda na Kina SOMAIYA wapo wapi na kesi yao ya mashamba ya mkonge iliishaje ? Najaribu kuvuta kumbukumbu lakini naona "RAM" yangu haipati data
 
Back
Top Bottom