HLRC kuiburuza serikali mahakamani kuhusu NSSF

Hapa umesema mkuu. Social security ni bomu linalosubiri kupasuka. Katika mazingira haya mifuko hii haimweki mwanachama mbele hata kidogo. Fikiria umechangia kwa miaka 10 baada tu ya kumaliza chuo ukiwa na miaka 24 baadae ukaamua kuacha kazi ili ufanye kazi zako zingine, je ni akili kweli kusubiri pesa yako miaka 26 baadae. Huu ni uporaji wa mchana. Ni muhimu watu tufanye utafiti wa kutosha juu ya ufanisi wa mifuko hii katika nchi zingine na kulinganisha na hali halisi ya maisha na mfumo wa jamii ya Kitanzania. Vinginevyo copy and paste itatuletea majanga mengi siku za usoni.
Naomba pia kujulishwa juu ya hili:
Hivi hizi pesa zinawekwa kwenye basis of interest earning au unazoweka ndizo hizo hizo unazorudishiwa baada ya hiyo miaka 60???
Hapa namaanisha kuwa ukinunua shares Presisionair, CRDB, Twiga Cement, TOL nk, wakipata faida kunakuwa na gawio lakini nasikia kila siku hii mifuko ina-inflate faida ila sijawahi kusikia wanachama wakipewa japo 10% ya faida hiyo!


 
hapa kuna uuaji fulani hivi unafanyika......na utani mkubwa kwa wafanyakazi aisee..
 
Kituo cha kutetea haki za binadamu nchini Tanzania kimesema kinaandaa taratibu za kuiburuza serikali mahakamani kwani kumkatalia mwanachama kuchukua hela zake kwa vile hajafikisha miaka 60 ni ukiukwaji wa haki za binadamu.Hii ni kwa sababu hakuna makubaliano yaliyofanyika kati ya mifuko husika na wanachama ili kuleta sheria hii ambayo ni mbaya na haramu hasa kwa wafanyakazi wa sekta binafsi......
DAWA NI KUCHAGUA CHAMA KINGINE CHA SIASA, chenye ahadi ya mtu kuchukua mafao muda wowote atakao yeye.
 
mnajua maana ya social security?
Unajua wewe gamba, maaana nyie mkishiba mnafikiri wote tumekula! Kazi nifanye mimi ujira wanapangie mamlaka ya mfuko wa jamii?

Kwa taarifa yako kabla ya hii sheria mimi nimechukua mafao yangu ppf mwaka jana, nimenunua gari, nimenua, kiwanja , na nimefanya finishing ya kanyumba kangu morogoro, nina miaka 43 tu.

Hii yakutaka watu wazeeke ndiyo waanze kukimbizana na mifuko wa sementi haikobaliki!
 
Jamani Mwenye number ya HLRC Tafadhali ninaomba anitumie, We need to support HLRC no mater what, Mimi nimepanga niache kazi next year then nichukue hela yangu ya NSSF nikalime, sasa mungu wangu mipango yangu yote imeishia kapuni.

Kwa kweli Kama Mbunge wako ame support this kweli hatakiwi kabisa kuwa mbunge wako.

Naomba mwenye ANSARD YA BUNGE ambayo imepitisha this tujue wabunge gani wamepitisha then tuanze kuwa andalia zengwe.
 
Katika nchi hii kuna mambo ya ajabu sana, na hili ni mojawapo. Wafanyakazi katika sheria hii mpya wana mambo muhimu ya kujiuliza:

Upitishwaji wa Sheria Hii Mpya
Sheria zote zinazopelekwa bungeni ikiwa pamoja na marekebisho yake, wadau hupewa na nafasi ya kuzijadili na kutoa maoni yao kabla ya kujadiliwa bungeni. Kwa nini mabadiliko ya sheria hayakujadiliwa, yakapitishwa kinyemela bila ya kupata maoni ya wenye mifuko yao? Wamiliki wa mifuko hii ni wafanyakazi, wala si serikali maana serikali haichangii chochote katika mifuko hii....

Mchango mzuri na mkakati mzuri wa muda mrefu na wa kati........Ufumbuzi wa muda mfupi ni lazima wafanyakazi tuikatae hii sheria ya kimaslahi kwa mfumo na kandamizi kwa wafanyakazi......Tuisapport LHRC na yeyote mwingine atakaye anzisha jitihada za kupinga hii sheria.

Kingine,Kila mmoja wetu anayeipinga hii sheria amwandikie mbunge wake,Kwa email,Message ya simu,Barua ya kawaida na hata kumpigia simu na kumweleza kuwa anamtaka mbunge wake huyo alifikishe jambo hili kama kilio cha dharura bungeni...Na kwamba mfanyakazi huyo atam hold mbunge wake huyo personally responsible kwa jinsi atakavyoonekana akishungulikia swala hili.

Wabunge waelezwe kwa uwazi kabisa kuwa jambo hili litakuwa moja ya vigezo vya kuwapima kama wanafaa kurudi bungeni au la come 2015.

Ni wakati muafaka sasa nguvu ya wafanyakazi ianze kuonekana ikijitetea bila kusubiri vyama maslahi kama TUCTA visivyo na meno wala utashi wa kuwatetea wafanyakazi.

Naomba kuwasilisha.
 
Hilo sasa ni la shirikisho la vyama vya wafanyakazi, sio michango tu ya wanachama. Ngoja tuone watalimaza vipi
 
Selikali, hivi kwa nini kila wakati mnakurupuka na mambo ya kuwaumiza wananchi badala ya kuwapa unafuu? Huu ni wizi na ukatili wa hali ya juu.:yawn:
 
Kwamba unatakiwa uchangie hata kama hujaajiriwa sh. 36,000 ambacho ni kima cha chini. Kwa hiyo kama hukuchangia no excuse. Kuna mtu alizungumzia kuhusu 'unemployment benefit'. Wenzetu kama huna ajira unalipwa na serikali, kwa hiyo huwezi kukosa hela ya kuchangia

Sijakupata vizuri Polisi, hapo kwenye shs 36,000. Hata hivyo hoja yangu ilikuwa kwenye criteria za kupata pension. Sijui kwenye haya mabadiliko ya sasa hivi wamefanya vipi, lakini ilivyokuwa ni kwamba ili mwanachama a-qualify kupata pension anatakiwa awe amechangia kwenye mfuko huo si chini ya miaka 10, na pia awe amefikia umri wa kustaafu. Kama umechangia kwa miaka 10 na zaidi lakini ukaondoka kwenye ajira kabla ya umri wa kustaafu (55 or 60 yrs) basi ulikuwa unaangukia kwenye withdrawal benefit.

Kumbukuka hii mifuki ina mafao (benefits) 7 hadi nane, na kila moja lina criteria zake.

Kuhusu unemployment benefit, its true kwa Tanzania hakuna kitu cha namna hiyo na hili fao la withdrawal kwa kiasi limekuwa ndio kimbilio la watu wanaoondoka kwenye ajira kabla ya umri wa kustaafu. Na limekuwa kwa kasi kubwa hasa baada ya kufanya reforms kwenye public sector - ambapo wafanyakazi wengi walipunguzwa, au/na mashirika kuuzwa.
 
vyama wa wafanyakazi viko wapi!! huu ni wakati wa kutetea haki za wafanyakazi.

nani alikuambia hii nchi inavyama vya wafanyakazi? Unaizungumzia tucta au nini? Kama ni tucta hamna kitu,serikali imepandikiza viongozi ambao ni tiss hvyo usitegemee lolote
 
Inasikitisha sana kuona siasa zinaingizwa kwenye mifuko yetu ya jamii. Hizi ni fedha zetu sisi kama wanachama ndio tulitakiwa kuziamulia ni vipi zitumike na vipi tupeane baada ya kufutwa kazi au kuacha kazi.

Kuna nini kimejificha hapa Mmekopa pesa zetu mmefanyia maendeleo kurudisha ngumu ndio mmeamua kuzipangia jinsi ya kuzichelewesha. Kwa kweli ni watanzania wachache sana wanaofikisha umri huu 55-60 watazisikia hizi pesa zao kaburini tu.

CCM kweli mmechoka kiasi hiki mmeshindwa kulipa watu mishahara kwa wafanyakazi mkakopa pesa zetu tena bila idhini yetu mmeshindwa kurudisha sasa mnajificha?

Hili kituo cha sheria tuko pamoja mpaka kieleweke hapana. watu wanafwatilia mafao yao leo tunaona wazee wenye umri huo mpaka wanakufa bila mafanikio tunakwendwa wapi kweli CCM wameshikwa pabaya
 
ukiwa 65yrs old, na umeshakula mafao yako unakuwa mzigo kwa private sector au jamii?

Mmh, hapa kidogo hujanishawishi mkuu, kuna wazee wana hali mbaya kweli mbona sioni hiyo jamii inavyowasaidia? Manake hawa wazee wa sasa tu shughuli, je siye wa mbeleni itakuwaje?

Na kama ni the so called social security, mbona ina watu na watu wa kuzitumia hizo pesa zenyewe? Mie niliyechangia nakataliwa kuzitumia kwa visingizio vya kuwa nitatunzwa nazo uzeeni, hiyo serikali inayozitumia sasa ni kwa makubaliano ya nani? Na je wanaokopeshwa nao ni kwa ruhusa ya nani? Mbona miye mchangiaji sipewi room ya kukopa? Sasa hivi naambiwa kuwa nitapewa mkopo wa nyumba, security ikiwa michango yangu, mimi shida yangu mtaji ili nijiwezeshe. Sasa kwa nini nishindwe kutumia hutu tumichango twangu kujikwamua jamani?

By the way, life span ya Mtanzania imesimamia wapi kwa sasa?
 
May you please tell what is not known......................

As an intro.........vijana wa sasa we need to get the wheel turning before retirement mkuu......mambo ya kuja kupewa mihela wakati huna nguvu ni ya nini sasa????? Just a philosophical change

Hii serikali ya CCM ni kishetani kweli. Wanadhani kila mtu anstahili kuburuza kama mtumishi wa Umma! 'Government employees live after retirement'.
 
Mkandara, tupo Tanzania, siyo Marekani. Mara ya kwanza ilipopitisha sheria ya kufuta NPF na kuanzisha NSSF walipitishwa sheria hiyo ya kutokujitoa kwa mwananchama ambaye hajafikisha retirement age, wafanyakazi walienda serikali na walishinda. Hivyo kukawa na schemes mbili zilizokuwa zikienda sambamba, ile inayoruhusu kujitoa na ile ya pension. Safari hii tena wanataka wawajaribu wafanyakazi, nina hakika serikali kutokana na nia yake ovu, lazima itashindwa.
Ya Tanzania hii hapa. Imeelezwa wazi kuwa mafao ya uzeeni yatatolewa kwa kustaafu kwa hiari (miaka 55-59) na kwa lazima miaka 60, tatizo liko wapi? Au hii sheria wameipandikiza hivi sasa haikuwepo kabla?

Kitu ambacho hakiingii akili kwangu ni kwa nchi (Tanzania) yenye matumaini ya umri wa kuishi usiofika miaka 53, unaweka kustaafu kuanzi miaka 55. Kwanza hawa HLRC wangelitetea hilo.
 
Mipango mingi ianyohitaji hela nyingi na inayotolewa ahadi za kisiasa huku wakijua serikali haina hela ya kutekeleza basi kimbilio lao ni mifuko ya hifadhi ya jamii. naamini wanaitengenezea mazingira ili kuhakikisha ni back up yao ya ahadi zao hata zisipokuwa na tija kwa kutumia hela ya wanachama bila ridhaa yao na kuwanyima wao wakihotaji. angalia ti miradi kama, machinga complex, kigamboni bridge, jengo la bunge, ppf tower et al. pia viongozi wa mifuko hii hawaangalii zaidi maslahi binafsi ya mchangiaji, hata hiyo mikopo ya nyumba wanayosema miaka na miaka haitolewa zaidi ya kujenga vitega uchumi kwa ajili ya matajiri
 
WHO statistics for Tanzania show life expectancy year 2010 is 51 years male, 54 years females. Implication is that on the average you be dead clean 9 years before you can access your social security savings. Where is the justice?. Now iam really really ashamed of upole na uvumilivu wetu.
 
Hivi hii sheria ilianza kama muswada kweli? na je, ilipitishwa na Bunge kweli..mbona sijapata kuisikia? Mfanyakazi yeyote hasa wa sekta binafsi hii sheria hii itakuwa ni msumari mrefu wa mwisho kwenye jeneza lake...Anayeishabikia huyo ni mwenda wazimu!

Enough is enough....hii haikubaliki hata nukta
 
Back
Top Bottom