Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,028
- 144,382
Ukiacha matatizo ya kiafya(magonjwa, n.k), watanzania wana matatizo mengi huku wakiwa wamepoteza matumaini ya matatizo yao kutatuliwa na mfumo huu mbovu wa kiutawala tulionao. hivyo, yoyote wa kuwapa matumaini, watamfuata mradi tu awe na mamlaka na zaidi awe na kipaji cha kuigiza mbele ya hadhara kubwa ya watu huku akionyesha kuwapa matumaini.
Hii ndio hulka ya Binadamu kama ilivyokuwa wakati wa Yesu kwa watu kumfuata Yesu awatatulie matatizo yao ambayo walikuwa wameshayakatia tamaa.
Nimetolea mfano wa Yesu kukumbusha na jinsi gani Mwanadamu aliekata tamaa anaweza kumfuata Mwanadamu mwenzake na hata kuwa mfuasi mradi tu awe na imani juu ya huyo mtu au akijua mtu huyo ana madaraka na hivyo anaweza kuyatumia kumsaidia hasa mtu huyo anapotumia style ya kukusanya watu na kuahidi kutatua matatizo yao.
Ukiwa na madaraka, unahitaji kipaji cha kuigiza mbele ya makundi makubwa ya watu, huku kwenye maswala ya kiimani, unachohitaji na kufanya watu wakuamini kuwa wewe ni Nabii basi kazi unakuwa umeimaliza/
Hata kwa waganga wa kienyeji hali ni hio hio hasa kwa watu ambao changamoto walizonazo katika maisha, hazina suluhiso mfano maradhi yasiyotibika, n.k.
Babu wa Loliondo watu walimfuata kwa misingi hiyo hiyo na hata Mwamposa leo watu wanamfuata kwa misingi hiyo hiyo ya kupatiwa majawabu ya matatizo waliyonayo katika maisha ikiwemo pia kutimiza ndoto zao au matamanio yao.
Wanaomfuata Makonda ni wahanga waliokataa tamaa wa huu mfumo mbovu wa kiutawala na usiowajibika. Hivyo, kupitia Makonda, wanaamini Makonda anaweza kuwasaidia, ila nachoweza kuwaambia watu hawa ni kuwa, majibu yao watayapata baada ya muda wa maigizo kuisha.
Makonda atamaliza ziara yake, lakini sio kero za watanzania kwasababu anahangaika na matotizo na sio chanzo cha matatizo ya watanzania.
Pia, msisahau kuna uchaguzi wa serikali za mitaa hivi karibuni na uchaguzi mkuu mwakani.
Hii ndio hulka ya Binadamu kama ilivyokuwa wakati wa Yesu kwa watu kumfuata Yesu awatatulie matatizo yao ambayo walikuwa wameshayakatia tamaa.
Nimetolea mfano wa Yesu kukumbusha na jinsi gani Mwanadamu aliekata tamaa anaweza kumfuata Mwanadamu mwenzake na hata kuwa mfuasi mradi tu awe na imani juu ya huyo mtu au akijua mtu huyo ana madaraka na hivyo anaweza kuyatumia kumsaidia hasa mtu huyo anapotumia style ya kukusanya watu na kuahidi kutatua matatizo yao.
Ukiwa na madaraka, unahitaji kipaji cha kuigiza mbele ya makundi makubwa ya watu, huku kwenye maswala ya kiimani, unachohitaji na kufanya watu wakuamini kuwa wewe ni Nabii basi kazi unakuwa umeimaliza/
Hata kwa waganga wa kienyeji hali ni hio hio hasa kwa watu ambao changamoto walizonazo katika maisha, hazina suluhiso mfano maradhi yasiyotibika, n.k.
Babu wa Loliondo watu walimfuata kwa misingi hiyo hiyo na hata Mwamposa leo watu wanamfuata kwa misingi hiyo hiyo ya kupatiwa majawabu ya matatizo waliyonayo katika maisha ikiwemo pia kutimiza ndoto zao au matamanio yao.
Wanaomfuata Makonda ni wahanga waliokataa tamaa wa huu mfumo mbovu wa kiutawala na usiowajibika. Hivyo, kupitia Makonda, wanaamini Makonda anaweza kuwasaidia, ila nachoweza kuwaambia watu hawa ni kuwa, majibu yao watayapata baada ya muda wa maigizo kuisha.
Makonda atamaliza ziara yake, lakini sio kero za watanzania kwasababu anahangaika na matotizo na sio chanzo cha matatizo ya watanzania.
Pia, msisahau kuna uchaguzi wa serikali za mitaa hivi karibuni na uchaguzi mkuu mwakani.