Hivi sisi tukoje?

Walifanya sahihi kuonyesha ili iwe fundisho kwa watu wengine wanao ishi kiujanja ujanja mjini.
 
Walifanya sahihi kuonyesha ili iwe fundisho kwa watu wengine wanao ishi kiujanja ujanja mjini.
hapa sikubaliani na wewe kwa sababu wote wanaopigwa/kuchomwa moto mpaka kuuwawa si vibaka...kuna mwanafunzi wa chuo alishawahi kupigwa mpaka akauwawa eti kwa sababu alipita karibu na nguo zilizoanikwa na mtu mmoja akapiga kelele za mwizi...ingekuwa ni mimi nipo kwenye mamlaka husika ningeiangalia vizuri ile footage na wote walioakuwa wanamwagia mafuta/kumpiga/kumuwekea majani ili moto ukolee wote wangekutana na mvua kali ya sheria...!
 
Itv wako saihihi kabisa ,ila lazimama watoe tadhari kwamba picha hii sio nzuri kwani inatisha au haifai kwa watoto, wewe unaesema haikuwa saihi ngoja nikupe ethic nyingine anayo unatakiwa kufanya muandishi.kama kuna mtoto mdogo barabarani na kuna gari lina kuja kumgonga yule mtoto ki ethics za uwandishi unatakiwa upige picha lile tukio na sio kumuokoa huyo mtoto.kupiga picha kwako kutatoa fundisho kwa watu wengine .kama utaweza kupiga picha na kumuokoa ni jambo zuri ila lakwanzan ni kupiga picha :Thats News
 
Ni sahihi kwa kuwa hatuna askari nchi hii
waliopo ndo wanaowatuma.
kwa anaebisha ngoja yamkute utakuwa wa kwanza!!:poa

Mkuu, huu ni uvunjifu wa sheria zetu wenyewe, sasa wabunge wakijiongezea posho kimyakimya msilaumu kuwa hawakufuata taratibu na sheria za nchi.

Hakuna sheria ndogo au kubwa, sheria ni sheria tu.

Turudi kwenye mada, hawa ITV walitakiwa basi watoe tahadhari kuhusu picha watakazo onesha kuhusu tukio hilo la kijana kuchomwa moto mpaka kifo.
 
Tunashukuru kwa kutupa taarifa ya habari mbali mbali zinazotokea katika kona ya Tanzania katika nyanja zote pamoja na vipindi vyenu vinavyoelimisha jamii, tena BURE bila malipo yoyote, mbarikiwe sana.

Sasa nijikite kwenye kilichotokea jana katika taarifa yenu ya HABARI, habari ya kijana kuchomwa moto ni habari iliyochukua nafasi kubwa kwenye habari ya jana, japo napingana na watu kuchukua sheria mkononi, LAKINI kitendo chenu cha kuonyesha kijana yule akiwa anapigwa mpaka kuzirai huku akiwa emetapakaa damu na baada ya hapo kuchomwa moto mpaka kufa SIYO SAHAHI HATA KIDOGO.

Mmefanikiwa kukata vipande vya filamu pindi watu wanapokuwa wanapigana mabusu hongereni kwa hilo lakini vipi kuonyesha picha za watu waliokufa au hata kukatwa mapanga bila hata kutaarifu watazamaji, kuna kipindi huwa mnakwenda mbali kiasi cha kuonyesha hadi kinyesi bila hata ya kutoa taarifa kwa watazamaji wenu.

Please jirekebisheni, mimi siyo mwandishi wa habari lakini sidhani kama ethics za uandishi wa habari zinaruhusu mambo kama hayo, keep in mind kids are watching ITV too.

Hivi ITV ni bure? Asee tangu haya madish ya kichina yaanze kuleta chenga chenga mi nalipia ITV bana nina kama nusu mwaka sasa! Bure yao kwenye antena au dish gani mkuu
 
Picha ile haikuwa nzuri kuionyesha. Siku ile Mkulu anadondoka pale Jangwani hawakutuonyesha. Waliikatiza. Ya vibaka wanayakomalia!
 
@mende0, hapo juu nilikuwa nakujibu ile msg yako uliosema ukikuta kibaka anapigwa na wewe utashiriki kumsulubu...!
 
Du ile habari niliependa sanaa kwani imeua ndege wawili kwa jiwe 1.

1-imepeleka msg kwa vibaka,wezi,matapeli na makanjanja wote wanaojifanya wajanja wa mjini wazee wa mishen town.

2-vyombo vyetu vya usalama vimepata sms ya aibu ya kubweteka mpaka watu wanagushi na kukaa kimya pindi wapewapo taarifa na kufika too late.

Mkuu kuchukua sheria mikononi ni kosa, lazima tufuate sheria zetu.

Hii haina tofauti na wakurugenzi wa halmashauri wanaokula hela za miradi, ni makosa.
 
Yaani kwa ujumla hawa ITV & Radio1 thinktank cabinet yao ni ya vilaza kweli kweli, almost wana kila aina za facilities muhimu kwa waandishi wa habari, lakini habari zao bado zinakosa mvuto! ila watangazaji wao wakihamia vituo vingine wana perform wonders! sijui tatizo ni operating procedures au managerial

Wakienda wapi wanaperform: TBC ama Clouds? Kwa maoni yangu ITV ndio chombo ambacho kipo relatively free ukilinganisha na vingine vya hapa nchini na kwa msingi huo watangazaji wake wana nafasi ya kuperform vyema zaidi wakiwa hapo hapo ITV.
 
hapa sikubaliani na wewe kwa sababu wote wanaopigwa/kuchomwa moto mpaka kuuwawa si vibaka...kuna mwanafunzi wa chuo alishawahi kupigwa mpaka akauwawa eti kwa sababu alipita karibu na nguo zilizoanikwa na mtu mmoja akapiga kelele za mwizi...ingekuwa ni mimi nipo kwenye mamlaka husika ningeiangalia vizuri ile footage na wote walioakuwa wanamwagia mafuta/kumpiga/kumuwekea majani ili moto ukolee wote wangekutana na mvua kali ya sheria...!

Napata ufahamu hapa wewe hujawahi ibiwa kitu na hujakumbana na machungu ya kuibiwa wewe.
 
Kama unaona soo kuangalia si bora ufuatilie news za radio? Tv kuonesha ndo usahihi wenyewe. Sikubaliani na wewe hata kidogo.
 
MAY THE FORCE BE WITH YOU ALL !!!!!!!!!!!!!

Kama kuonyeshwa kibaka aliebondwa na kuchomwa ni injustice, mbona tumesha ona watu waki katwa vichwa, walio jivisha mabom na hata askari wa Israel wakiuwa baba na mtoto wake mdogo asiye na hatia?

Tunadai maendeleo. Yanapo kuja tuna yalaani. Tunadai uhuru wa habari, tunapopewa, tuna laani. Nini kitaturidhisha an kutufurahia?

TV ni yako. Iko nyumbani kwako. Ukiona kuna habari au documentary huipendi au haifai, simle. ZIMA. Waache wenzako waone.

Zungumzia kuhusu kitakacho kutoa kwenye uamskin lakini sio kuwapangia wengine nini waangalie.
 
Hivi ITV ni bure? Asee tangu haya madish ya kichina yaanze kuleta chenga chenga mi nalipia ITV bana nina kama nusu mwaka sasa! Bure yao kwenye antena au dish gani mkuu
Haya yanaweza kuwa na mantiki maana mimi natumia dish mediacom nina kama wiki tatu hivi ITV siipati kabisa licha ya fundi kuhangaika bila mafanikio.
 
Napata ufahamu hapa wewe hujawahi ibiwa kitu na hujakumbana na machungu ya kuibiwa wewe.
Hapana mkuu, nimeshaibiwa mara nyingi sana lakini kwa kweli sina ujasiri na wala haiingii akilini mwangu kumpiga ,kumwagia mafuta na kuua binadamu mwenzangu hata kama ni kibaka. Wewe ukisikia siku ndugu yako wa karibu amefanyiwa hivyo hata kama kweli ni kibaka ndiyo utajua nina maanisha nini. Wewe unayeshiriki kumuua kibaka huoni unafanya kosa kubwa kushinda alilofanya kibaka mwenyewe na unastahili adhabu kubwa kupita hata atakayepata kibaka kama angepatikana na hatia? Nakushauri ukikuta kibaka anachomwa ufanye kama wale wasamalia wema waliokuwa wanayatoa yale majani yalikuwa yanamuwakia moto.
 
wanatakiwa watoe warning juu ya images kama hizo-then waonyeshe mzigo mzima kama ulivyo bila ku-edit kitu
 
A person is torched to death in broad daylight and some people think that is okay. SMH!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom