Hivi mtu akifa na hela zake ziko benki na Mpesa, tukiwa na cheti cha kifo tunaweza fuatilia?

Kuna taratibu za mirathi, kama marehemu kaacha wosia juu ya mgawanyiko wa mali basi itakuwa rahisi kuzipata, lakin zaid ya hapo utazungushwa sana, lakin pesa utazipata kama zilivyo

mkuu kuna uwezekano wa msimamizi wa mirathi kwa mfano kaka wa marehemu kwenda benk kutoa fedha za mirathi za watoto wa marehemu bila uwepo wao
 
mkuu kuna uwezekano wa msimamizi wa mirathi kwa mfano kaka wa marehemu kwenda benk kutoa fedha za mirathi za watoto wa marehemu bila uwepo wao
Kwa nini msimamizi wa mirathi awe kaka wa marehemu wakati mjane yupo na ana akili timamu?
 
Kwanza poleni kwa msiba mkuu.

Fateni taratibu zifuatazo: Kwanza wanafamilia wakae kikao na kuandaa muhtasari wa kikao ambao pamoja na mambo mengine; utampendekeza msimamizi wa mirathi ya marehemu (endapo marehemu hakuacha wosia).

Baada ya hatua hiyo hapo juu, msimamizi wa mirathi ya marehemu aliyependekezwa atapaswa akathibitishwe na Mahakama (endapo hakuna pingamizi), ambapo atapewa 'hati ya usimamizi wa mirathi ya marehemu'. Kama marehemu alikuwa muislamu, mtaenda Mahakama ya mwanzo, kama marehemu alikuwa mkristo basi mtaenda Mahakama ya Wilaya/Mahakama ya hakimu mkazi, lakini kwa Mahakama ya Wilaya/Mahakama ya hakimu mkazi basi kuna maombi maalumu ambayo yanapaswa kuandaliwa na wakili na ndiyo yanapelekwa mahakamani, isipokuwa mkienda Mahakama ya mwanzo ambapo mtajaza tu fomu maalumu.

Viambatanisho muhimu ambavyo msimamizi wa mirathi aliyependekezwa kwenye kikao anatakiwa kuwa navyo ni cheti cha kifo cha marehemu na orodha ya mali za marehemu.

Bilashaka umenielewa mkuu. Karibu ununue Kitabu changu chenye jina; DONDOO MUHIMU ZA NAMNA YA KUKABILIANA NA KESI ZA ARDHI, JINAI, MADAI, MIRATHI NA NDOA HASA KWA WASOMAJI WASIO WANASHERIA NA WANASHERIA WACHANGA:SOMO FUPI LA SHERIA KWA VITENDO. Bei ni TZS 10,000 tu. Nipo Dodoma ila mikoani natuma pia. Au naweza kukutumia softcopy ukipenda. Aksante.

mkuu kwanza ningependa kukipata kitabu chako kinacho husu sheria katika mfumo wa soft copy

pili ningependa kuuliza swali, kuna uwezekano wa kufungua faili la mirathi kwa mtu aliye fariki miaka kumi iliyopita licha ya kuwa msimamizi wa mirathi nae alisha kufa miaka kadhaa iliyopita ?
 
Hio dealth certificate huwa hawaipokei bank wala mpesa, wanapokea death certificate tu. Sijui hata kwanini!

Warudishie RITA hio dealth certificate, halafu waambie wakupe death certificate. Halafu nenda mahakama ya mwanzo fungua shauri la kuomba kufungua mirathi ya huyo marehemu, mahakama watawapa barua ya usimamizi wa mirathi ndio mwende bank au huko mpesa mkazitoe hela, kama kuna nyumba au kiwanja kaacha mtauza. NA KAMA MAREHEMU AMEACHA MADENI, MTALIPA!

Usipo fanya hivo, jiandae na kesi ya uhujumu uchumi kwa kujipatia pesa kutumia njia ya udanganyifu (Hata kama hela ni Sh 2,000/=, uhujumu uchumi haina dhamana).
Nguvu yote hii sababu jamaa kakosea kuandika herufi moja tu???
Ifike mahali maswala mazito tuyape uzito wake , linalojadiliwa hapa ni kubwa kuliko makosa ya mwandiko
 
Sasa Mwanamke kama huyo Wewe ni wa nini? Yaani why do you have such a woman ?

Kama mmeamua kuishi pamoja maana yake ni lazima kuwe na Transparency na Truth.

Kitu kama ATM au Mpesa is very Common.

Like me; simu yangu Muda mwingi ipo kwa mikono ya my wife, au Mimi nikiwa na shida ya hela ya haraka nachukua Kadi yake naenda Bank ATM kutoa hela, like wise yeye pia . those are very common details kwa wanandoa.

Sijaona Essence ya huu Uzi
Huna hela wewe inawezekana mke wako ndio ana hela
Unawajua wanawake wewe?
 
Kwa nini msimamizi wa mirathi awe kaka wa marehemu wakati mjane yupo na ana akili timamu?

nadhani hii ni kutokana na shinikizi kutoka kwa ndugu wa upande wa marehemu na kutokuwepo kwa usawa au ukandamizajibwa kijinsia kwa upande wa wanawake
 
Mzee baba huko hazina ndipo kwenye shida.mara nyingi Bank hutoa check mapema na kuzipeleka hazina.Sasa kasheshe ni cheki kutoka hazina kurudi mahakamani.Haloo ni mwendo wa nenda rudi kesho.mara hazijasainiwa.mara hazionekani.zikionekana utaambiwa njoo wiki ijayo tena kwa maneno matamu wale watu hazina Mungu anawaona.kila siku ni story.mimi nilikua nikiambiwa njoo wiki ijayo narudi kesho asubuhi.nilifanya hivyo miezi sita chek zikatoka ila jasho la meno lilinitoka

Hawana huruma ,mtu umefiwa na mpendwa wako bado unamachungu bado wakuzungushe kwenye hela ambayo siyo ya kwao inaboa sana
 
Mme unamficha mkeo kiasi hicho ? Si aibu kwa mkewe aliyebaki duniani na kuonyesha kuwa hakupendwa na mmewe duu
 
FRESHMAN wewe kama mwanaume umetafuta mali na mke wako kipenzi lakini ukitangulia kuondoka hizo mali zinauzwa warithi wanagawana. Sasa kama una nyumba moja wakishagawana yeye utu uzima ushawadia, kukimbizana hawezi tena, unafikiri yeye ataenda wapi.

Nawaza nimpoteze babachanja wangu halafu nyumba yangu nilivyoisotea Mimi na yeye iuzwe ili warithi wapate chao halafu Mimi nikaanze kutafuta makazi.

Maumivu juu ya maumivu
Hapo ni kufiwa na kufiwa na ujane ujane×1000 maumivu kuzidi, watu wanadhambi kubwa sana.
 
Mimi nilishaufanya mchakato huo nikiwa msimamiz wa mirathi. Death Certificate ni ka document kamoja tu, unapoenda huko M pesa au Bank kufatilia pesa unapaswa uwe na Document ya Kikao cha Familia kilichokuteua kuwa msimamiz wa mirathi, Uwe na nakala Za hukumu ya Mahakaman nk.

Hapo kama kaacha Mke inabidi ndio afatilie. Wewe kama aliyefariki ni kaka yako tambua kuwa huna sifa ya kuwa mrithi kabisa kisheria.Warithi halali hapo ni Mke na Watoto na Wazazi wa Marehem.
Watu wanapenda kuridhi mali za ndugu zao hata kama naye ana mke na watoto, hanaga huruma kabisa.
 
Fuateni taratibu zote za kuteua msimamizi wa mirathi. Ikiwemo pia kwenda mahakamani.

Mahakama ikishatoa nyaraka za kumteua msimamizi wa mirathi, huyo ndiye atakayefuatilia kwa bank na kampuni ya simu ili kupata pesa.

Kumbuka kuwa jukumu la msimamizi wa mirathi ni kutambua na kukusanya mali na madeni yote ya marehemu. Jukumu la pili ni kugawa mali kwa warithi halali kisheria.

Hivyo, Msimamizi wa mirathi atakayeteuliwa ndiye atakayefuatilia na kupewa hizo pesa. Naye atazigawa kwa warithi halali kwa mujibu wa sheria.

Kwa suala lako, ingependeza huyo mke ndio apewe usimamizi wa mirathi.
Kudos
 
mkuu kuna uwezekano wa msimamizi wa mirathi kwa mfano kaka wa marehemu kwenda benk kutoa fedha za mirathi za watoto wa marehemu bila uwepo wao

Ndio upo.. maana pesa anaekewa msimamiz wa mirathi.. cheque ikitoka
 
Ndio hivyo Mkuu; huwezi kuwa hakimu wa kesi ambayo una maslahi nayo. Msimamizi wa mirathi anatakiwa kuwa neutral.
dudus I disagree with you. Ndio maana nimekwambia nenda kajiridhishe. Sikutaka kubishana khs hili. Ila naona umenilazimisha niongee kwa urefu.

Nimeona in practice na nina uhakika ninachokisema. Mbona hata ukigoogle kesi za mirathi zipo nyingi tu utaona mke kapewa usimamizi? Hata hili umeshindwa kusearch? Na kama ni mwanafunzi wa sheria mbona precedent ziko nyingi tu ukisoma utaona?

Mke anaweza kuwa msimamizi wa mirathi ya mumewe. Kuwa na interest ktk urithi hakumfanyi yeye kuwa judge in her own case. Kumbuka mahakama ndio inateua sio yeye. Yeye anaomba tu usimamizi. Pili, baada ya kugawa kwa mujibu wa sheria anatakiwa kuifahamisha mahakama khs mgao huo na kufunga mirathi. Kwa hiyo bado yuko subject to mahakama.

Na ndio maana kama muda ukipita bila mirathi kukamilika au kufungwa, mtu au mrithi anaweza kwenda kuomba kutengua uteuzi wake msimamizi wa mirathi kwa ground ya kushindwa kusimamia mirathi vizuri ndani ya muda.
 
Ila mimi hii hoja nimeiangalia kwa masikitiko sana na namna ya Maisha ya sasa yanavyokwenda.

Ni dhahiri kwamba mahusiano ya ndoa mengi hayana mpango chochote. Yaani watu wanaishi siku ziende.

How could that be mke hajui password ya Mpesa ya Mume wake ? How could that be mke au mume hajui ATM password ya mwenzi wake ?

Kuliko kuishi maisha ya kipumbavu kama hayo ni bora nisiwe na mwanamke.

Ninachojua mimi Mke wako au Mume wako ndio mtu wa kwanza Kwenye maisha yako kujua hizo details. It is such a shame mtu kufungua thread na kutuambia mke hajui password za ATM na MPESA. Huu ni WIZI unataka kufanyika. Na ndugu wa Marehemu watizame hili suala kwa karibu ; huenda kuna kitu bado hakipo sawa.

Ungesema utaratibu wa kufuatilia Mali za Marehemu kama vile Majumba, Viwanja, pesa zake ndani ya Bank n.k ingekuwa ni SAWA kuomba Ushauri na utaratibu.

But Akaunti ya MPESA au ATM , mke hajui, that is shame!

Yaani Mimi kama huyo aliyekufa ni kaka yangu; literally mwanamke atachukua share ndogo sana maana sioni kama ni Mtu mwenye akili ikiwa hujui hizo details za mtu unaelala nae kitanda kimoja na probably mna watoto . USELESS!

Anyway, .... tambua Mahakamani haitokuwa peke yako, bali ni familia halisi ya marehemu. Ndugu zake pamoja na watoto, wazazi kama wapo hai ambao watapewa nafasi pia.

maisha hayawezi kuwa so simple Kwenye hiyo chain.
Mkuu umeongea points tupu aisee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom