Naona nisimulie kwa ufupi historia ya mangi Sina wa Kibosho kwa ajili ya msaada wa baadhi ya watu kwenye forum hii. Ukweli ni kwamba Sina halikuwa jina lake la asili alilopewa na wazazi wake. Kwa wale watakaotaka taarifa zaidi waniandikie kwenye email yangu hapo chini, ila hapa nitasema machache. Baba yake Sina aliitwa Kisaro ambaye alikuwa ni miongoni mwa watoto wa mwisho mwisho wa Iwere wa ukoo wa Urio wa Kibosho. Miaka ile ambayo Sina alikuwa ni kijana mdogo (inaaminika kama miaka 8 - 10 hivi) Machame ilikuwa ikitawala kule magharibi ya uchagani na iliikalia Kibosho kwa mkono wa chuma. Kuna wakati askari wa Machame walivamia Kibosho wakiituhumu kutengeneza silaha kinyemela. Waliua vijana wengi na watu wazima (hasa wanaume) na kuchoma moto nyumba na mashamba. Wapo walioweza kupona kwa kukimbia kujificha porini na mapangoni, na wale askari wa Machame walipokuwa wanarudi porini wakawakamata baadhi ya watu, wengine wakauawa lakini wachache walichukuliwa kama mateka wawapeleke kwa mangi wa Machame ili hatima yao ijulikane huko. Kati ya waliochukuliwa, alikuwepo kijana mdogo aliyekuwa akitetemeka sana kwa hofu (na inaelekea na baridi pia) ambaye yule jemedari wa askari wa Machame alimhurumia na kusema si vyema kumuua bali wakamwachie mangi wa Machame mwenyewe aamue.
Walipofika Machame ni ajabu kwamba mangi Ndesserua aliyekuwa akitawala Machame wakati huo ambaye alifahamika kama mtawala mkatili kupita kiasi alimpenda tu huyo mtoto na kuamuru kwamba akae katika boma la kwa mangi siku zote za maisha yake na apewe kazi za kusaidia pale kwa mangi. Hii ikamfaya yule mtoto ghafla akawa maarufu kule Machame. Inasemekana alikuwa ni mtiifu, hodari, mchapa kazi na alipendwa sana na jamii ya kwa mangi kule Machame na hata kwa watu wengine. Inasimuliwa kwamba alipenda sana kula mifupa pale kwa mangi hata wakamwita Sina (kimachame yaani kusina, kutafuna nyama na mifupa!), na hii kwa vile kwa mangi kila siku walikuwa na sherehe za hapa na pale, wakichinja ng'ombe na mbuzi kwa wingi, yaani nyama choma mbele kwa mbele na supu na mbege za kumwaga. Hili jina Sina ndilo lililokuja kuwa jina lake kabisa baadaye.
Kwa upendo mangi Ndesserua aliokuwa nao kwa Sina, alimwingiza katika jeshi lake la askari baada ya kwenda jando na hata inasemekana mara kwa mara alimwamini sana katika majukumu mbalimbali nyeti katika utawala kitu ambacho kilianza kuleta wasiwasi kwa baadhi ya wazee wa ukoo wa mangi kule Machame, wakimtahadharisha mangi Ndesserua kwamba Sina na uaminifu wote alionao lakini bado ni wa asili ya Kibosho. Hata hivyo mangi Ndesserua alimlea Sina kama jemedari na kwenda kwenye vita vingi mbalimbali hasa kule Masama, Yuri na Siha magharibi mwa uchagani. Kwa kweli Sina aliishi Machame kwa muda mrefu akiwa jemedari wa vita, mpaka wakati mangi Ndesserua alipoanza kuwa mgonjwa na kuhisi kwamba muda wake si mrefu sana, alimwambia ndugu yake Nassua (ambaye alim-recruit Sina kwenye jeshi) kwamba hali ya Kibosho si nzuri kisiasa, na ili kuepusha kuibuka kwa mtawala kama Lokilo kule Kibosho ambaye alileta matata kule uchagani, Nassua afanye hima kuhakikisha Sina anaenda kuwa mtawala kule Kibosho (ingawa hakutoka kwenye boma la Tatuo-Kirenga lililokuwa linautawala kule Kibosho). Na kwa vile mangi Wawa aliyekuwa anatawala Kibosho alikuwa ndiyo amefariki na hakuna mtawala Kibosho, waliitumia nafasi hiyo kwenda kumtawalisha Sina kwa nguvu Kibosho. Inasemekana watu wengi sana waliuawa kwa kupinga kitendo hicho na hasa ukoo wa Olotu Mallya ambao waliuawa karibu wote na waliobahatika kupona walikimbilia Old Moshi wanakoishi mpaka leo hii (kwa jina la Olotu). Kwa kutumia uhodari wake na uzoefu wake wa kivita, kwa muda mfupi Sina aliweza kuhamasisha vijana Kibosho na kuunda kikosi cha nguvu cha maaskari ambapo alifanya mashambulizi makali dhidi ya ukoo wa Tatuo-Kirenga uliokuwa maarufu kisiasa kule Kibosho ili auangamize kabisa amalize upinzani wa kisiasa dhidi ya utawala wake. Waliweza kupona wachache kwa kujificha porini, wengine waliweka yamini ya kuwa waaminifu kwake na wachache walitorokea Vunjo-Mwika wanakotumia jina la Urio hadi leo.
Haukupita muda mrefu makali ya Sina ya kulelewa kama jemedari wa vita yalianza kuwa shubiri kule uchagani. Aliiangukia Mweka ambayo ilikuwa ikitawaliwa na ukoo wa Tesha na kuilazimisha kujisalimisha. Tayari Uru ilishakaa chonjo baada ya kugundua siasa za Kibosho zimebadilika ghafula. Matukio mbalimbali ya kihistoria kwa wakati huo uchagani inaonyesha kwamba Sina alitawalishwa kuwa mangi wa Kibosho katika miaka ya 1876-1878, kwa sababu masimulizi yanaonyesha kwamba si muda mrefu sana baada ya Sina kutawala Kibosho mangi Ndesserua wa Machame alifariki (ca. 1880). Bila kutaka kwenda ndani sana katika historia, kwa kile ambacho pia kilionekana ni njama za kuitiisha Machame chini ya amri yake baada ya kufa kwa Ndesserua, mangi Sina alipeleka wapambe Machame wakipiga ukunga (tangazo la kilio) kuwa mangi Sina naye amefariki hivyo wamachame (waliomtawalisha) wakamzike na kuangalia ni nani wa kumtawalisha. Hii ilikuwa ni njama kali iliyopangwa Kibosho, kwani wamachame wengi walikwenda 'kwenye kilio' na kwa vile hawakwenda kivita basi waliangukia katika mikono ya Sina ambaye aliwaua karibu wote isipokuwa wachache waliobaki wakafanikiwa kutoroka na kurudi. Askari wa Kibosho walikwenda Machame wakachoma mashamba na nyumba na kutia hasara kubwa. Hata hivyo, wamachame walikataa kujitiisha chini yake hali ambayo ilileta vita vya mara kwa mara na Machame kuzidi kuhujumiwa na mangi Sina. Kitendo hiki alichokifanya Sina dhidi ya Machame kilizusha hofu kubwa sana uchagani dhidi yake hasa kutokana na utawala wa Machame ulivyokuwa ukiheshimika. Hali hii ni kama ilimpa morali zaidi mangi Sina ambaye aliiangukia Uru kwa kishindo na kwa muda mfupi Uru ikajisalimisha. Akaishambulia Mbokomu nayo ikajisalimisha na wakachukua mateka wengi (na hapo ndipo pia Ndegeruo aliyekuja kuitwa Marealle alipochukuliwa mateka naye kupelekwa Kibosho). Mangi Sina akatumia nafasi ya kuwa na Ndegeruo katika himaya yake kwenda kushaishambulia Vunjo na kumtawalisha Ndegeruo Marealle kule Marangu. Kufikia miaka ya mwishoni mwa 1880 mangi Sina alishatiisha maeneo mengi sana kule uchagani na kutawala anga la kivita, hofu yake ikisikika na kuhisika kila kona kule uchagani.
Hata hivyo mpinzani wake mkuu alikuwa mangi Rindi Mandara wa Old Moshi. Mangi Sina na mangi Rindi walibaki kuwa watawala wawili kule uchagani katika miaka ya 1880 waliofanya vita kila kukicha wakigombania maeneo ya mipaka ya utawala ili kuteka watu kuwauza kwa waarabu kama watumwa. Ingawa waliogopana na kuonekana kama waliheshimiana, lakini kitendo cha mangi Sina kumchokonoa mara kwa mara mangi Mandara kwa kushambulia maeneo jirani na himaya yake, kilimnyima usingizi Mandara na hata kuamua kufanya vita ya kufa na kupona dhidi ya mangi Sina katika mwaka 1888 akishirikiana na watawala wengine kule uchagani waliochoka adha za mangi Sina. Pamoja na kumchangia mangi Sina, bado Mandara na washirika wake walishindwa vibaya. Kitendo cha mangi Sina kuishambulia tena Machame 1890 huku akimsaidia Shangali dhidi ya kaka yake Ngamini, kilimtia katika hatihati kubwa na ukoloni wa kijerumani uliokuwa umeshashika hatamu kule Old Moshi. Huku wakichochewa na mangi Mandara walimvamia mangi Sina katika boma lake katika vita kali iliyopiganwa kwa siku mbili. Mangi Sina alijisalimisha katika vita hiyo, aliamua kushusha bendera ya sultani wa Zanzibar iliyokuwa ikipepea katika boma lake na kuridhia kuwa mshirika wa serikali ya kikoloni ya kijerumani. Hii vita ndiyo iliyopelekea tamati ya vita vya mangi Sina kule uchagani.
Mangi Sina ni mtawala wa Kibosho aliyejulikana sana kwa uhodari wake wa kupanga na kupigana vita. Anakumbukwa kama aliyeijenga Kibosho ikawa ni utawala uliojitegemea (kutoka katika makucha ya Machame) na kuwa wenye nguvu nyingi kabisa kule uchagani. Inasemekena wakati wa utawala wake wananchi wa Kibosho walilala mlango wazi (yaani kutokana na amani katika himaya yake), walipanda na kuvuna kwa wingi, walikula na kusaza. Ingawa madhara ya malezi yake kwa mangi Ndesserua yalionekana katika maisha yake yote ya utawala (kama waingereza wanavyosema - You will be like your mentor) kutokana na ukatili wake wa kutisha na kupenda vita kama sera ya utawala, mangi Sina alisisitiza kilimo bora kwa watu wake ambapo inasimuliwa kuwa alisisitiza kilimo cha mbolea, na kutoa usalama wa hali ya juu kwa watu wake ambao inasemekana walikuwa wakichunga mifugo yao hadi mbali bila ya woga wowote ule. Pamoja na utawala wa mkono wa chuma wa mangi Sina kule Kibosho na matatizo makubwa ya kiusalama aliyosababishia tawala zingine kule uchagani, mangi Sina bado ataendelea kukumbukwa sana Kibosho kwa maana katika utawala wake wakibosho waliishi kwa usalama mkubwa na mafanikio ya kimaisha. Hawakujua njaa wala kupungukiwa, na jina lao likawa kubwa katika historia. Mangi Sina alifariki mwaka 1897 kutokana na matatizo ya tumbo. Mtoto wake aliyeitwa Ilmollelian alitawalishwa ingawa kwa bahati mbaya siasa za uchagani zilichafuka na akanyongwa mwaka 1900 pamoja na watawala wengine wa wachaga kwa tuhuma za uhaini dhidi ya serikali ya kikoloni ya kijerumani.
Ahsanteni, email yangu ni kay.cm@hotmail.co.uk.
Walipofika Machame ni ajabu kwamba mangi Ndesserua aliyekuwa akitawala Machame wakati huo ambaye alifahamika kama mtawala mkatili kupita kiasi alimpenda tu huyo mtoto na kuamuru kwamba akae katika boma la kwa mangi siku zote za maisha yake na apewe kazi za kusaidia pale kwa mangi. Hii ikamfaya yule mtoto ghafla akawa maarufu kule Machame. Inasemekana alikuwa ni mtiifu, hodari, mchapa kazi na alipendwa sana na jamii ya kwa mangi kule Machame na hata kwa watu wengine. Inasimuliwa kwamba alipenda sana kula mifupa pale kwa mangi hata wakamwita Sina (kimachame yaani kusina, kutafuna nyama na mifupa!), na hii kwa vile kwa mangi kila siku walikuwa na sherehe za hapa na pale, wakichinja ng'ombe na mbuzi kwa wingi, yaani nyama choma mbele kwa mbele na supu na mbege za kumwaga. Hili jina Sina ndilo lililokuja kuwa jina lake kabisa baadaye.
Kwa upendo mangi Ndesserua aliokuwa nao kwa Sina, alimwingiza katika jeshi lake la askari baada ya kwenda jando na hata inasemekana mara kwa mara alimwamini sana katika majukumu mbalimbali nyeti katika utawala kitu ambacho kilianza kuleta wasiwasi kwa baadhi ya wazee wa ukoo wa mangi kule Machame, wakimtahadharisha mangi Ndesserua kwamba Sina na uaminifu wote alionao lakini bado ni wa asili ya Kibosho. Hata hivyo mangi Ndesserua alimlea Sina kama jemedari na kwenda kwenye vita vingi mbalimbali hasa kule Masama, Yuri na Siha magharibi mwa uchagani. Kwa kweli Sina aliishi Machame kwa muda mrefu akiwa jemedari wa vita, mpaka wakati mangi Ndesserua alipoanza kuwa mgonjwa na kuhisi kwamba muda wake si mrefu sana, alimwambia ndugu yake Nassua (ambaye alim-recruit Sina kwenye jeshi) kwamba hali ya Kibosho si nzuri kisiasa, na ili kuepusha kuibuka kwa mtawala kama Lokilo kule Kibosho ambaye alileta matata kule uchagani, Nassua afanye hima kuhakikisha Sina anaenda kuwa mtawala kule Kibosho (ingawa hakutoka kwenye boma la Tatuo-Kirenga lililokuwa linautawala kule Kibosho). Na kwa vile mangi Wawa aliyekuwa anatawala Kibosho alikuwa ndiyo amefariki na hakuna mtawala Kibosho, waliitumia nafasi hiyo kwenda kumtawalisha Sina kwa nguvu Kibosho. Inasemekana watu wengi sana waliuawa kwa kupinga kitendo hicho na hasa ukoo wa Olotu Mallya ambao waliuawa karibu wote na waliobahatika kupona walikimbilia Old Moshi wanakoishi mpaka leo hii (kwa jina la Olotu). Kwa kutumia uhodari wake na uzoefu wake wa kivita, kwa muda mfupi Sina aliweza kuhamasisha vijana Kibosho na kuunda kikosi cha nguvu cha maaskari ambapo alifanya mashambulizi makali dhidi ya ukoo wa Tatuo-Kirenga uliokuwa maarufu kisiasa kule Kibosho ili auangamize kabisa amalize upinzani wa kisiasa dhidi ya utawala wake. Waliweza kupona wachache kwa kujificha porini, wengine waliweka yamini ya kuwa waaminifu kwake na wachache walitorokea Vunjo-Mwika wanakotumia jina la Urio hadi leo.
Haukupita muda mrefu makali ya Sina ya kulelewa kama jemedari wa vita yalianza kuwa shubiri kule uchagani. Aliiangukia Mweka ambayo ilikuwa ikitawaliwa na ukoo wa Tesha na kuilazimisha kujisalimisha. Tayari Uru ilishakaa chonjo baada ya kugundua siasa za Kibosho zimebadilika ghafula. Matukio mbalimbali ya kihistoria kwa wakati huo uchagani inaonyesha kwamba Sina alitawalishwa kuwa mangi wa Kibosho katika miaka ya 1876-1878, kwa sababu masimulizi yanaonyesha kwamba si muda mrefu sana baada ya Sina kutawala Kibosho mangi Ndesserua wa Machame alifariki (ca. 1880). Bila kutaka kwenda ndani sana katika historia, kwa kile ambacho pia kilionekana ni njama za kuitiisha Machame chini ya amri yake baada ya kufa kwa Ndesserua, mangi Sina alipeleka wapambe Machame wakipiga ukunga (tangazo la kilio) kuwa mangi Sina naye amefariki hivyo wamachame (waliomtawalisha) wakamzike na kuangalia ni nani wa kumtawalisha. Hii ilikuwa ni njama kali iliyopangwa Kibosho, kwani wamachame wengi walikwenda 'kwenye kilio' na kwa vile hawakwenda kivita basi waliangukia katika mikono ya Sina ambaye aliwaua karibu wote isipokuwa wachache waliobaki wakafanikiwa kutoroka na kurudi. Askari wa Kibosho walikwenda Machame wakachoma mashamba na nyumba na kutia hasara kubwa. Hata hivyo, wamachame walikataa kujitiisha chini yake hali ambayo ilileta vita vya mara kwa mara na Machame kuzidi kuhujumiwa na mangi Sina. Kitendo hiki alichokifanya Sina dhidi ya Machame kilizusha hofu kubwa sana uchagani dhidi yake hasa kutokana na utawala wa Machame ulivyokuwa ukiheshimika. Hali hii ni kama ilimpa morali zaidi mangi Sina ambaye aliiangukia Uru kwa kishindo na kwa muda mfupi Uru ikajisalimisha. Akaishambulia Mbokomu nayo ikajisalimisha na wakachukua mateka wengi (na hapo ndipo pia Ndegeruo aliyekuja kuitwa Marealle alipochukuliwa mateka naye kupelekwa Kibosho). Mangi Sina akatumia nafasi ya kuwa na Ndegeruo katika himaya yake kwenda kushaishambulia Vunjo na kumtawalisha Ndegeruo Marealle kule Marangu. Kufikia miaka ya mwishoni mwa 1880 mangi Sina alishatiisha maeneo mengi sana kule uchagani na kutawala anga la kivita, hofu yake ikisikika na kuhisika kila kona kule uchagani.
Hata hivyo mpinzani wake mkuu alikuwa mangi Rindi Mandara wa Old Moshi. Mangi Sina na mangi Rindi walibaki kuwa watawala wawili kule uchagani katika miaka ya 1880 waliofanya vita kila kukicha wakigombania maeneo ya mipaka ya utawala ili kuteka watu kuwauza kwa waarabu kama watumwa. Ingawa waliogopana na kuonekana kama waliheshimiana, lakini kitendo cha mangi Sina kumchokonoa mara kwa mara mangi Mandara kwa kushambulia maeneo jirani na himaya yake, kilimnyima usingizi Mandara na hata kuamua kufanya vita ya kufa na kupona dhidi ya mangi Sina katika mwaka 1888 akishirikiana na watawala wengine kule uchagani waliochoka adha za mangi Sina. Pamoja na kumchangia mangi Sina, bado Mandara na washirika wake walishindwa vibaya. Kitendo cha mangi Sina kuishambulia tena Machame 1890 huku akimsaidia Shangali dhidi ya kaka yake Ngamini, kilimtia katika hatihati kubwa na ukoloni wa kijerumani uliokuwa umeshashika hatamu kule Old Moshi. Huku wakichochewa na mangi Mandara walimvamia mangi Sina katika boma lake katika vita kali iliyopiganwa kwa siku mbili. Mangi Sina alijisalimisha katika vita hiyo, aliamua kushusha bendera ya sultani wa Zanzibar iliyokuwa ikipepea katika boma lake na kuridhia kuwa mshirika wa serikali ya kikoloni ya kijerumani. Hii vita ndiyo iliyopelekea tamati ya vita vya mangi Sina kule uchagani.
Mangi Sina ni mtawala wa Kibosho aliyejulikana sana kwa uhodari wake wa kupanga na kupigana vita. Anakumbukwa kama aliyeijenga Kibosho ikawa ni utawala uliojitegemea (kutoka katika makucha ya Machame) na kuwa wenye nguvu nyingi kabisa kule uchagani. Inasemekena wakati wa utawala wake wananchi wa Kibosho walilala mlango wazi (yaani kutokana na amani katika himaya yake), walipanda na kuvuna kwa wingi, walikula na kusaza. Ingawa madhara ya malezi yake kwa mangi Ndesserua yalionekana katika maisha yake yote ya utawala (kama waingereza wanavyosema - You will be like your mentor) kutokana na ukatili wake wa kutisha na kupenda vita kama sera ya utawala, mangi Sina alisisitiza kilimo bora kwa watu wake ambapo inasimuliwa kuwa alisisitiza kilimo cha mbolea, na kutoa usalama wa hali ya juu kwa watu wake ambao inasemekana walikuwa wakichunga mifugo yao hadi mbali bila ya woga wowote ule. Pamoja na utawala wa mkono wa chuma wa mangi Sina kule Kibosho na matatizo makubwa ya kiusalama aliyosababishia tawala zingine kule uchagani, mangi Sina bado ataendelea kukumbukwa sana Kibosho kwa maana katika utawala wake wakibosho waliishi kwa usalama mkubwa na mafanikio ya kimaisha. Hawakujua njaa wala kupungukiwa, na jina lao likawa kubwa katika historia. Mangi Sina alifariki mwaka 1897 kutokana na matatizo ya tumbo. Mtoto wake aliyeitwa Ilmollelian alitawalishwa ingawa kwa bahati mbaya siasa za uchagani zilichafuka na akanyongwa mwaka 1900 pamoja na watawala wengine wa wachaga kwa tuhuma za uhaini dhidi ya serikali ya kikoloni ya kijerumani.
Ahsanteni, email yangu ni kay.cm@hotmail.co.uk.