Historia ya Wachagga: Koo, Kabila na Falme-Mangi

Mchungaji...Shukran...Naomba pia usisahau kuwa madhumuni halisi ya wewe kuanzisha thread hii ni baada ya kudai kuwa mimi kuliuliza suala hili kwenye ile thread nyingine haikufaa.
Na hivyo basi ningeomba Mnyika ajaribu kutowa maelezo ya kihistoria ili wengine wetu tuweze kuelewa kuwa usaliti huo wa Sina ni upi.
Siko hapa kuchaguwa upande upi ni mzuri ama upi ni mbaya...Inawezekana kweli ni msaliti na mimi sijui...Hivyo maelezo yangesaidia kwani ndio kuelimishana huko pamoja na kujengana kwa kuthamini na kueleweshana kuhusu historia ya Taifa letu kwa ujumla...Taifa nalo litanufaika pia na historia ya usaliti huo.....Usaliti ambao kwa kweli ni muhimu Mnyika auweke wazi kwani alisema ulisababisha damu ikamwagika dhidi ya Mdachi.
Ahsante.

Kwanza ningependa kuchukua fursa hii kumshukuru Mr Mushi kwa kuwa kisababishi cha kuanza mada hii ambayo imeleta na mengi katika kujifunza juu ya historia ya uchagani. Kutokuridhika kwako hukukaa kimya na kunung'unikia vitandani kama watanzania wengi walivyo, bali uliamua kutoa dukuduku lako ili kupata taarifa sahihi. Mimi naona hiyo ni hatua ya kijasiri na ya kishujaa. Mpaka sasa mheshimiwa Mnyika hajajitokeza kujibu tuhuma hizo hivyo inathibitisha kwamba ni kweli alisema na inaonekana hakuwa na uhakika na anachoongea. Mnyika ni miongoni mwa watu wengi katika jamii yetu ambao bila ya kuwa na taarifa sahihi iliyofanyiwa utafiti makini huibuka na kutoa matamko kwenye halaiki na hata kujiabisha kwa kudhani watanzania wote ni mbumbumbu. Sifahamu kabila lake au fani yake hasa ni nini lakini inaonekana dai alilolitoa dhidi ya mangi Sina wa Kibosho limetokana na kudandia historia asiyoijua mapana yake. Ni vizuri watu wakajifunza kuongea (hasa kwenye public) taarifa ambazo hata wakija kuulizwa baadaye watakuwa na uwezo wa kuzitetea kihoja na kuzithibitisha kitaalamu. Viongozi wa kwenye jamii ambao wanaongea tu chochote ni hatari kwa mustakabali wa taifa letu.

Nikirudi kwenye mada, hasa dai alilolitoa mheshimiwa Mnyika ni kwamba uhasama uliokuwepo kati ya mangi Sina na mangi Rindi (Mandara) wa old Moshi ni wa kihistoria. Hapo nyuma, yaani 1890, mangi Rindi kwa kuona kwamba alishindwa kukabiliana na nguvu zilizokuwa zikiongezeka kila kukicha za mangi Sina kule uchagani, aliamua kutumia fursa yake ya ukaribu na wakoloni kule kwenye boma lake kuwachochea dhidi ya mangi Sina na kuwaahidi kuwapa msaada wa askari na njia za kuendea Kibosho kumshambulia mangi Sina. Mangi Rindi alikuwa ameona fadhaa kubwa ya kushindwa kumsaidia mangi Ngamini kule Machame dhidi ya mdogo wake Shangali ambaye alikuwa akisaidiwa na askari wa mangi Sina kumwezesha kutawala Machame. Huku akimchochea kapteni Johannes ambaye naye alishakuwa amekereheshwa na kitendo cha mangi Sina kuchochea vita kule Machame kumng'oa Ngamini, mangi Rindi alifanikiwa kumshawishi kapteni Johannes mwaka ule wa 1890 kwenda kushambulia ngome ya mangi Sina huku akimsaidia kwa kumpa askari kadhaa. Katika vita hiyo mangi Sina alishindwa vibaya na kulazimishwa kujisalimisha ambapo aliingia mkataba na wakoloni wa kijerumani kuwa mtiifu na kuiunga mkono serikali hiyo. Mangi Rindi aliitumia hiyo nafasi kumtia adabu adui wake na hata kumchochea kapteni Johannes kwamba mangi Sina ayasalimishe kwa mangi Rindi pia maeneo ya Uru na Kirua-Vunjo aliyokuwa ameyaweka chini ya himaya yake, sharti ambalo kwa kusaini mkataba wa kujisalimisha ilibidi akubaliane nalo. Mangi Sina aliamriwa pia amwachie mangi wa Uru ambaye alikuwa amemkamata na kumweka kifungoni. Ingawa mangi Rindi aliona faraja kwa kumtia adabu adui wake wa siku nyingi, tatizo ni kwamba alikuwa ameshaanza kuwa mgonjwa na mwaka huo wa 1890 inasimuliwa kuwa muda mwingi alikuwa yuko kitandani akiugua (inasemekana alikuwa amepooza kutoka kiunoni kuelekea chini miguuni). Mangi Rindi Mandara alifariki baadaye mwaka huo wa 1890 na mtoto wake Meli Mandara akatawala.

Kwa hiyo utaona sababu vita ilipokuja baadaye kati ya mangi Meli na wakoloni wa kijerumani kwa nini mangi Sina aliwasaidia wakoloni dhidi ya mangi Meli. Ni mambo ya uhasama na visasi, lakini pia kumbuka mkataba ambao alilazimishwa kuusaini hapo nyuma kama sharti lake la kujisalimisha. Ni hayo tu kwa leo.
 
Kwanza ningependa kuchukua fursa hii kumshukuru Mr Mushi kwa kuwa kisababishi cha kuanza mada hii ambayo imeleta na mengi katika kujifunza juu ya historia ya uchagani. Kutokuridhika kwako hukukaa kimya na kunung'unikia vitandani kama watanzania wengi walivyo, bali uliamua kutoa dukuduku lako ili kupata taarifa sahihi. Mimi naona hiyo ni hatua ya kijasiri na ya kishujaa. Mpaka sasa mheshimiwa Mnyika hajajitokeza kujibu tuhuma hizo hivyo inathibitisha kwamba ni kweli alisema na inaonekana hakuwa na uhakika na anachoongea. Mnyika ni miongoni mwa watu wengi katika jamii yetu ambao bila ya kuwa na taarifa sahihi iliyofanyiwa utafiti makini huibuka na kutoa matamko kwenye halaiki na hata kujiabisha kwa kudhani watanzania wote ni mbumbumbu. Sifahamu kabila lake au fani yake hasa ni nini lakini inaonekana dai alilolitoa dhidi ya mangi Sina wa Kibosho limetokana na kudandia historia asiyoijua mapana yake. Ni vizuri watu wakajifunza kuongea (hasa kwenye public) taarifa ambazo hata wakija kuulizwa baadaye watakuwa na uwezo wa kuzitetea kihoja na kuzithibitisha kitaalamu. Viongozi wa kwenye jamii ambao wanaongea tu chochote ni hatari kwa mustakabali wa taifa letu.

Nikirudi kwenye mada, hasa dai alilolitoa mheshimiwa Mnyika ni kwamba uhasama uliokuwepo kati ya mangi Sina na mangi Rindi (Mandara) wa old Moshi ni wa kihistoria. Hapo nyuma, yaani 1890, mangi Rindi kwa kuona kwamba alishindwa kukabiliana na nguvu zilizokuwa zikiongezeka kila kukicha za mangi Sina kule uchagani, aliamua kutumia fursa yake ya ukaribu na wakoloni kule kwenye boma lake kuwachochea dhidi ya mangi Sina na kuwaahidi kuwapa msaada wa askari na njia za kuendea Kibosho kumshambulia mangi Sina. Mangi Rindi alikuwa ameona fadhaa kubwa ya kushindwa kumsaidia mangi Ngamini kule Machame dhidi ya mdogo wake Shangali ambaye alikuwa akisaidiwa na askari wa mangi Sina kumwezesha kutawala Machame. Huku akimchochea kapteni Johannes ambaye naye alishakuwa amekereheshwa na kitendo cha mangi Sina kuchochea vita kule Machame kumng'oa Ngamini, mangi Rindi alifanikiwa kumshawishi kapteni Johannes mwaka ule wa 1890 kwenda kushambulia ngome ya mangi Sina huku akimsaidia kwa kumpa askari kadhaa. Katika vita hiyo mangi Sina alishindwa vibaya na kulazimishwa kujisalimisha ambapo aliingia mkataba na wakoloni wa kijerumani kuwa mtiifu na kuiunga mkono serikali hiyo. Mangi Rindi aliitumia hiyo nafasi kumtia adabu adui wake na hata kumchochea kapteni Johannes kwamba mangi Sina ayasalimishe kwa mangi Rindi pia maeneo ya Uru na Kirua-Vunjo aliyokuwa ameyaweka chini ya himaya yake, sharti ambalo kwa kusaini mkataba wa kujisalimisha ilibidi akubaliane nalo. Mangi Sina aliamriwa pia amwachie mangi wa Uru ambaye alikuwa amemkamata na kumweka kifungoni. Ingawa mangi Rindi aliona faraja kwa kumtia adabu adui wake wa siku nyingi, tatizo ni kwamba alikuwa ameshaanza kuwa mgonjwa na mwaka huo wa 1890 inasimuliwa kuwa muda mwingi alikuwa yuko kitandani akiugua (inasemekana alikuwa amepooza kutoka kiunoni kuelekea chini miguuni). Mangi Rindi Mandara alifariki baadaye mwaka huo wa 1890 na mtoto wake Meli Mandara akatawala.

Kwa hiyo utaona sababu vita ilipokuja baadaye kati ya mangi Meli na wakoloni wa kijerumani kwa nini mangi Sina aliwasaidia wakoloni dhidi ya mangi Meli. Ni mambo ya uhasama na visasi, lakini pia kumbuka mkataba ambao alilazimishwa kuusaini hapo nyuma kama sharti lake la kujisalimisha. Ni hayo tu kwa leo.

Atakuja kujibu ngoja tusubiri.
 
Mangi Sina wa Kibosho (aliyeshika bunduki katikati ya maaskari wake). Picha ilipigwa mwaka 1894. Alifariki miaka 4 baadaye. Wageni waliomtembelea kwenye himaya yake walisimulia kama mtu aliyekuwa hodari na shujaa na alionekana mstaarabu na mpole (kama anavyoonekana kwenye picha) lakini alikuwa mtawala wa vita na asiye na huruma. Inasemekana mwaka 1890 aliposhindwa vita na wakoloni wa Kijerumani wakisaidiwa na Mangi Rindi wa Moshi, aliamuru wote wale ambao walisita kupigana vita au ambao hawakujulikana walipokuwepo wakati wenzao wanashinda usiku kucha kupambana kulinda ngome yake, wasakwe popote watakapopatikana na kuuawa.

Ikumbukwe pia jina la Kibosho ni jina lililotokana na utawala wa Mangi Sina. Kabla ya Mangi Sina eneo la Magharibi kidogo na ilipokuwepo ngome yake liliitwa Lambongo likiwa chini ya utawala wa ukoo wa Kirenga. Sina alipotwaa madaraka miaka ya 1870 akisaidiwa na askari katili kutoka Machame, alijenga ngome yake katika eneo lililokuwa likikaliwa kwa asili na ukoo wa Kiwoso ambao walimkaribisha na kumuunga mkono. Utawala wa Mangi Sina unaweza kukumbukwa kwa mambo makubwa matatu kihistoria:

  1. Historia ya nchi inaweza kubadilika ikiwa atapatikana mtawala mwenye maono makubwa na nia ya mabadiliko. Utawala wa Mangi Sina unatufundisha kwamba inawezekana kubadili kabisa mwelekeo wa nchi kama atapatikana kiongozi asiyeenda kwa mazoea na aliye makini. Inasemekana kabla ya utawala wa Mangi Sina wakibosho wengi walikuwa na kawaida ya kwenda kutumika kwa kufanya kazi mbalimbali Machame na kushiriki katika kutunza na kulinda mifugo mingi ya Mangi wa Machame. Mangi Sina aliijenga Kibosho iliyokuja kuwa utawala wenye mafanikio na amani kubwa kuliko zote uchagani enzi zake. Inasemekana wakati wa utawala wa Mangi Sina wakibosho walimiliki mifugo na mashamba na kuwa na amani bila kubugudhiwa na tawala zingine. Badala ya hofu ya kushambuliwa Walikuwa ndiyo washambuliaji.
  2. Ni utawala wa Mangi Sina ndiyo umetupa jina la nchi iliyokuja kujulikana maarufu kama Kibosho.
  3. Sina alichukua nchi ikiwa koloni la Machame na utawala uliozoea hofu ya kuchukua maamuzi magumu. Ilimchukua muda mrefu kubadilisha mtazamo huu wa jamii na hata kuthubutu miaka ya 1889 kupeleka maaskari wake kuishambulia Machame, kitu ambacho kilionekana kama ndoto za mchana kwa Wakibosho wengi. Mangi Sina aliipa Kibosho uhuru wa kujitawala na kujitegemea kabisa. Aliwapa Wakibosho ujasiri wa kwamba inawezekana.
Cena.jpg
 
Sawa...Aje kusema kama ni usemi wake binafsi...Hata hivyo wale waliomsapoti kama kina MKJJ na Wembe Mkali labda wanaweza kumsaidia...Ila ni muhimu sana na yeye akaja hapa na kutowa ufafanuzi kwasababu ya nafasi yake kwenye jamii...

John Mnyika
user_offline.gif

John Mnyika has no status.
JF Senior Expert Member
Join Date: Fri Jun 2006
Location: Tanzania
Posts: 627
Rep Power: 24
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_pos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif
reputation_highpos.gif

Thanks: 6
Thanked 276 Times in 97 Posts
Credits: 62,420


icon1.gif
Ya Kale Ni Dhahabu
Chambelecho cha maadhimisho ya Siku ya Mashujaa: Tunu yangu kwa wakina Kinjeketile

Na John John Mnyika

Kamaradi Kinjeketile na mashujaa wenzako popote mlipo! Hii ni tunu kwenu. Hidaya kwenu mliomwaga damu wakati mapambano kadhaa na Mreno na Mwarabu. Tuzo kwenu nyinyi mliopigana na Ujerumani wakati wa utawala na mliomwaga damu katika vita vya dunia. Heko ninyi ambao damu ilisafisha safari ya kumng’oa Nduli Amin. Heri wewe Sethi Benjamini na wote waliopotesha maisha katika hekaheka za kueneza Azimio la Arusha. Kumbukumbu kwenu mliotoa damu katika mikikimikiki ya mfumo wa vyama vingi kutoka Zanzibar mpaka bara. Damu yenu iliyomwagika haizoleki, ukiwa mlioucha hauzoeleki lakini fikra mlizosimamia hazizeeki. Mapambano bado yanaendelea!

Kwako Bushiri bin Salim wa Tanga, suriama wa kiarabu na kiafrika, pamoja na nia yako tenge ya kulinda maslahi katika biashara ya utumwa ulimwaga damu kwa kunyogwa Pangani baada ya kuongoza maasi makali dhidi ya kuingia kwa ukoloni wa Kijeruamani-damu yako ilimwagika pamoja na damu za wapiganaji wa Pwani, Morogoro mpaka uhehe. Ewe Mtemi Meli, uliowashinda wadachi mpaka mwenzio Sina alipokusaliti hatimaye wewe na mashujaa wenzako mkamwaga damu kaskazini mkilinda uhuru.Wewe Chifu Mkwawa, tunakukumbuka uliovyowaunganisha wahehe-toka Kalenga, Tosamaganga mpaka ulipoamua kuimwaga damu yako mwenyewe kuliko uhuru upotee mikononi mwako. Mtemi Isiki wa Tabora uliendesha mashambulizi ya kishujaa, hatimaye ukaamua kumwaga damu yako na ya familia yako kwa kujilipua na baruti ili tu usipate aibu ya uhuru kuchukuliwa mbele ya macho yako. Ewe Mtemi Makongoro wa Musoma, ulipambana kwa ushujaa mpaka ilibidi kikosi cha wanamaji kiletwe kupitia miji ya Mombasa na Kisumu kukumaliza.

Nakutunuku Kinjeketile kwa kuongoza vita vya kutisha vya Maji Maji kwa miaka kadhaa vilivyoanzia vilima vya Matumbi karibu na Kilwa. Nyinyi mlitaka kumwondoa mkoloni kwa nguvu na mlikuwa tayari kumwaga damu kuliko kuendelea kuishi bila ya uhuru. Mapambano yenu yalisambaa maeneo mengi ya ardhi yetu. Ninyi mlikuwa mashujaa kweli kweli mliojua umuhimu wa imani na falsafa katika mapambano-mkawapa watu ujasiri kwa dawa ya “Kugeuza risasi, Kuwa maji”. Pamoja na kushindwa vita na wazalendo zaidi ya laki moja kupoteza maisha katika wakati ambao ardhi ilikuwa na watu wachache yapo mapigano ambayo mlishinda. Pamoja na machifu 47 wa Kingoni kunyongwa damu yenu ilileta mabadiliko katika utawala. Kwa vyovyote vile damu nyingi kiasi hiki iliyomwagika kwa sababu ya kudai uhuru haiwezi kupuuzwa. Hivyo waraka huu ni tunu kwenu. Mapambano bado yanaendelea!

Nawaandikia waraka huu ninyi wahenga mashujaa muweze kurejea na kurekebisha historia. Najua mnaweza msirudi kimwili, lakini ni vyema kiroho mkandelea kuwa nasi. Fikra zenu za kimapambano hazipaswi kupotea. Kumbukumbu zenu za kishujaa hazistahili kufutika. Taifa lisilo na historia haliishi, linakufa. Kupotosha historia ya mashujaa ni kinyaa. Karibu kila eneo katika nchi yetu yupo shujaa ambaye anaweza kukumbukwa laiti kama historia zenu zingejulikana kizazi hata kizazi na kuwa chimbuko la kujiamini, kujithamini na uzalendo miongoni mwa Watanzania.

Julai 25 ilikuwa siku nyingine ambapo tulifanya maadhimisho ya kinafiki ya siku ya mashujaa. Mtanishangaa kwa kutumia dhana kali- “UNAFIKI”. Namaanisha!. Ni dhana ambayo mnaifahamu na hamkuipenda. Ndio maana hamkutaka kuishi katika unafiki wa kukubaliana ama kutumiwa na watawala. Mkaamua kupambana! Mkamwaga damu mkiukimbia unafiki. Sasa tunawakumbuka! Lakini nasema tena, tunawakumbuka kwa kufanya maadhimisho ya kinafiki ya siku ya mashujaa. Ndani ya dhana ya unafiki kuna tabia nyingi, mojawapo ni kunena tofauti na matendo na kutenda tofauti na kauli. Na ndiyo tabia tunayoifanya wakati wa maadhimisho ya siku ya mashujaa. Ndio maana nasema, tunafanya maadhimisho ya kinafiki.

Labda ni waambie wakina Kinjeketile, nini tulifanya huku kama ishara ya kuuadhimisha ushujaa wenu. Siku chache zilizopita 25 Julai, tulijumuika chini ya Amiri Jeshi Mkuu, kwa sasa ni Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yeye mwenyewe hakuwepo, alituma mwakilishi wake. Tulielezwa kwamba Rais yupo kwenye ziara ya kikazi Ujerumani!

Usiku mmoja kabla tuliwasha mwenge wa uhuru pale Mnazi mmoja. Halafu asubuhi yake gwaride lilijipanga kuwapokea wageni wa Kitaifa. Zikatolewa salam za Rais na wimbo wa Taifa ukapigwa kwa heshima yenu. Kikundi cha Buruji kikapiga “last post” na gwaride likaweka silaha begani. Askari sita waliojipanga vyema wakapindua silaha zao chini na baadae mizinga ikapigwa kwa ajili yenu huku watu wote wakiwa kimya. Gwaride likafanya “present arms” na kikundi cha buruji kikapiga “reveilles”. Gwaride likateremsha silaha na kufungua miguu.

Halafu silaha za asili ambazo nyingine nyinyi mashujaa mlizitumia zikawekwa kwenye mnara pamoja na maua. Baadhi ya silaha zilizowekwa ni pamoja na mkuki, ngao, sime, shoka, pinde na mishale. Hizi ni kumbukumbu sanifu za mapambano mliyoyafanya.

Hatimaye zikafuata sala na swala kutoka kwa viongozi wa dini wakiwakilishwa na sheikh, mchungaji, padri na maraji wa wahindu. Ingawaje sikumwona kiongozi wa dini ya jadi-ambao najua baadhi yenu nyinyi mashujaa na wahenga mliwaamini. Pengine dini za jadi zilitoweka na damu zenu. Gwaride likatoa tena heshima na wimbo wa taifa kupigwa ukafuatiwa na itifaki za viongozi wa kitaifa kuondoka. Wakabaki polisi kuzilinda silaha za kumbukumbu ya mashujaa mpaka jioni na hatimaye mwenge wa uhuru ukazimwa kama ishara ya mwisho wa maadhimisho ya kumbukumbu yenu ninyi mashujaa. Niwaulize wakina Kinjeketile, haya siyo maadhimisho ya kinafiki ya mashujaa? Pengine mtanijibu hapana!.

Ngoja niwaeleze masuala kadhaa halafu niwaulize tena. Siku hizi kuna kitu kinaitwa Bunge, hiki ni chombo cha juu chenye uwakilishi wa wananchi ambacho kunafanya maamuzi mbalimbali ambayo mengine huwa sheria. Chombo hiki ni kama yale mabaraza ya jadi yaliyokuwepo wakati wenu. Wiki iliyopita bunge lilijadili kuhusu maadhimisho ya vita vya Maji Maji ambavyo nyinyi wakina Kinjeketile mliviongoza. Miaka mia moja imepita toka damu yenu azizi ilipomwagika katika mapambano hayo ya kumwondoa mkoloni.Ungekuwepo najua ungekuwa Mbunge wa Kilwa, ungeshangaa sana-Eti maadhimisho ya vita mlivyovianza Kilwa na mapambano ya mwisho yakawa Songea, yanafanyika kinyume chake! Maadhimisho yameanzia Songea na waziri ameahidi pengine yataishia Kilwa. Chacha Wangwe, mbunge wa CHADEMA (wakati wenu hakukuwa na vyama vya siasa vyenye majina haya) jimbo la Tarime, yeye akahoji-kwanini bendera ya taifa isiwekwe rangi nyekundu kama ishara ya kuwakumbuka nyinyi mashujaa wetu? Naibu waziri wa habari na michezo, Mheshimiwa Emanuel Nchimbi-yeye akajibu, hakukuwa na sababu ya rangi nyekundu kuwekwa kwenye bendera ya Taifa kama ishara ya kuwakumbuka mashujaa. Eti, historia ya uhuru wa nchi yetu inaamuliwa kuanzia mkoloni wa mwisho aliyetutawala ambaye ni Muingereza. Sasa kwa kuwa tulipata uhuru wetu kwa amani bila kumwaga damu chini ya uongozi wa mwalimu Nyerere basi hakukuwa na sababu ya kuweka rangi nyekundu. Enyi mashujaa Kinjeketile na wenzako tunaowakumbuka leo mnakubaliana na jibu hili?

Ndio maana nikasema ni maadhimisho ya kinafiki. Tunanena tofauti na matendo. Nimesema awali, tunaanza maadhimisho ya leo kwa kuwasha mwenge wa uhuru halafu baadae tunaweka silaha za jadi. Kinjeketile na wenzako, iulizeni serikali- kama uhuru wetu tuliupata kwa amani, iulizeni serikali kwanini tunawasha mwenge wa uhuru na baadaye kuweka silaha za jadi? Tunanena tofauti na tunavyotenda? Iulizeni serikali, je harakati za mwisho za uhuru ni kipimo pekee cha historia ya nchi na hivyo kuwa kigezo pekee cha kuamua alama za nchi ikiwemo bendera?

Enyi mashujaa mlioambana kuulinda uhuru wetu dhidi ya wakoloni kuingia kuanzia wakati wa Mreno, Mwarabu na Mjerumani na kumwaga damu, mnakubaliana na majibu haya? Kushindwa kwenu na hatimaye ukoloni kuingia hakuondoi historia kuwa mlimwaga damu kwa ajili ya kulinda uhuru wa ardhi hii tukiyoirithi!

Enyi mashujaa mliopambana kuondoa ukoloni hususani ule wa Ujerumani mkamwaga damu, mnakubaliana na kumbukumbu hii? Kwamba mliyoyafanya si historia kuu kama historia ya uhuru toka kwa Mwingereza?

Enyi mashujaa, waulizeni wataalamu wa historia-baada ya Ujerumani kushindwa na makoloni yake yote kuwekwa chini ya halmashauri ya mataifa na baadaye baraza la udhamini, Tanganyika ikiwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza-si kwamba tulikuwa katika hatua za mwisho kabisa za kupewa uhuru ambao tayari tulishaupata kwa damu? Waulizeni pia, hakuna damu yoyote iliyomwagika wakati wa Mwingereza? Je, historia ya nchi yetu iliyojikita katika kipenzi chetu Nyerere imewajumuisha mashujaa wote wa ardhi hii?

Nasema kwa damu-kuanzia ushindi pamoja na kushindwa dhidi Mjerumani ambao ulileta mabadiliko katika mfumo wa utawala sanjari na mashujaa ambao walikuwa mstari wa mbele katika jeshi la Mwingereza na washirika wake katika vita dhidi ya Mjerumani, vile vita vya dunia ambavyo vilipiganwa pia katika ardhi yetu? Wakina nani walimwaga damu zaidi katika kile kinachoitwa ukombozi ulioletwa na majeshi ya mfalme Afrika (KAR) kama si nyinyi babu zetu?

Hojini serikali, hivi bendera hii ni ya Tanganyika au Tanzania? Jibu la Nchimbi limetolewa katika muktadha wa historia ya Tanganyika, Ingekuwa vipi jibu lingetolewa mintaarafu bendera ya Tanzania ambayo ilipatikana kutokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilihali visiwani kuna historia ya damu kumwagika ama kumwagwa wakati wa mapinduzi? Kama kweli tuna serikali ya mapinduzi Zanzibar na utawala wa Chama cha Mapinduzi(CCM), je ni mapinduzi yasiyo na ‘rangi nyekundu’?

Tunatenda tofauti na kauli! Tunafanya maadhimisho ya kinafiki. Wakina Kinjeketile tunawakumbuka kwa kuwa mlimwaga damu kupinga ukoloni na unyanyasaji. Mtuulize wajukuu zenu, je tunawaadhisha kwa kuendelea kupiga vita yale mliyoyakataa? Kwa hali ilivyo, wapo wanaotenda yale mliyoyakataa pamoja na kuwa wote kwa kauli tunawaenzi ninyi mashujaa. Tunapaswa sasa kuweka fikra zenu katika vitendo kwa ajili ya ukombozi wa taifa letu. Mwalimu Nyerere alikumbuka fikra zenu akatamka na kutenda kwamba uhuru, si uhuru wa maneno. Ni uhuru dhidi ya ujinga, uhuru dhidi ya maradhi, uhuru dhidi ya umaskini na baadaye akaongezea uhuru dhidi ya rushwa ama ufisadi. Enyi wahenga mashujaa, shukeni katika nyoyo za watoto na wajuu zenu, mtufanye kutokana na maadhimisho ya mwaka huu tuweke dhamira ya kupigana vita kwa zana kisasa kuleta mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli, kuleta haki na maisha bora. Hii ndiyo hidaya kwa damu yenu azizi. Sio siri, kwa sera bila silaha, mapambano bado yanaendelea!

Mwandishi wa makala hii ni mwanaharakati na mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia mnyika@yahoo.com na 0744 694 553

Kumbukumbu toka:http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_13.html
__________________
Kizazi Kipya, Maisha Mapya
New Generation, New Life

Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli
Real Change, Real Freedom

John Mnyika

The Following 3 Users Say Thank You to John Mnyika For This Useful Post: mpaka kieleweke (26th July 200, Mzee Mwanakijiji (25th July 200, wembemkali (28th July 200

JM enzi.
 
Ninakiri kwamba kuna hizi habari watu wanazizungumzia, lakini ni vigumu kuzithibitisha. Zinaonekana kama ni uvumi hivi kwa kiasi kikubwa. Ujasiri wa wanawake wa kimachame umekuwa mara kwa mara ukihusianishwa na mauaji yale yaliyotokea miaka ile ya 1886 ambapo wanaume kadha wa kadha wa kimachame waliuliwa kutokana na fitina ile iliyosukwa na mangi Sina kule Kibosho. Hii inadaiwa ilisababisha nyumba/familia nyingi za Machame, wanawake wabaki na kuwa ndiyo walezi wa familia. Hiyo ikafanya wanawake wawe na maamuzi makubwa katika mambo ya nyumba/familia. Kwa hiyo inasemekana kuwa ndiyo ilijenga utamaduni huo Machame wa wanawake kuwa ni jasiri na hata wenye kufanya maamuzi magumu katika jamii.
Exactly upo sahihi kabisa mkuu!
 
Mangi Sina wa Kibosho (aliyeshika bunduki katikati ya maaskari wake). Picha ilipigwa mwaka 1894. Alifariki miaka 4 baadaye. Wageni waliomtembelea kwenye himaya yake walisimulia kama mtu aliyekuwa hodari na shujaa na alionekana mstaarabu na mpole (kama anavyoonekana kwenye picha) lakini alikuwa mtawala wa vita na asiye na huruma. Inasemekana mwaka 1890 aliposhindwa vita na wakoloni wa Kijerumani wakisaidiwa na Mangi Rindi wa Moshi, aliamuru wote wale ambao walisita kupigana vita au ambao hawakujulikana walipokuwepo wakati wenzao wanashinda usiku kucha kupambana kulinda ngome yake, wasakwe popote watakapopatikana na kuuawa.

Ikumbukwe pia jina la Kibosho ni jina lililotokana na utawala wa Mangi Sina. Kabla ya Mangi Sina eneo la Magharibi kidogo na ilipokuwepo ngome yake liliitwa Lambongo likiwa chini ya utawala wa ukoo wa Kirenga. Sina alipotwaa madaraka miaka ya 1870 akisaidiwa na askari katili kutoka Machame, alijenga ngome yake katika eneo lililokuwa likikaliwa kwa asili na ukoo wa Kiwoso ambao walimkaribisha na kumuunga mkono. Utawala wa Mangi Sina unaweza kukumbukwa kwa mambo makubwa matatu kihistoria:

  1. Historia ya nchi inaweza kubadilika ikiwa atapatikana mtawala mwenye maono makubwa na nia ya mabadiliko. Utawala wa Mangi Sina unatufundisha kwamba inawezekana kubadili kabisa mwelekeo wa nchi kama atapatikana kiongozi asiyeenda kwa mazoea na aliye makini. Inasemekana kabla ya utawala wa Mangi Sina wakibosho wengi walikuwa na kawaida ya kwenda kutumika kwa kufanya kazi mbalimbali Machame na kushiriki katika kutunza na kulinda mifugo mingi ya Mangi wa Machame. Mangi Sina aliijenga Kibosho iliyokuja kuwa utawala wenye mafanikio na amani kubwa kuliko zote uchagani enzi zake. Inasemekana wakati wa utawala wa Mangi Sina wakibosho walimiliki mifugo na mashamba na kuwa na amani bila kubugudhiwa na tawala zingine. Badala ya hofu ya kushambuliwa Walikuwa ndiyo washambuliaji.
  2. Ni utawala wa Mangi Sina ndiyo umetupa jina la nchi iliyokuja kujulikana maarufu kama Kibosho.
  3. Sina alichukua nchi ikiwa koloni la Machame na utawala uliozoea hofu ya kuchukua maamuzi magumu. Ilimchukua muda mrefu kubadilisha mtazamo huu wa jamii na hata kuthubutu miaka ya 1889 kupeleka maaskari wake kuishambulia Machame, kitu ambacho kilionekana kama ndoto za mchana kwa Wakibosho wengi. Mangi Sina aliipa Kibosho uhuru wa kujitawala na kujitegemea kabisa. Aliwapa Wakibosho ujasiri wa kwamba inawezekana.
Mangi Sina ni huyo aliochuchumaa upande wa kulia na sio huyo alioshika bunduki kama unavyodai wewe, alichukua madaraka kutoka kwa mama yake Mamka/Manka aliyekuwa Mangi wa kike hapo Kibosho pia hakuna ukoo unaitwa kibosho/kiwoso kama unavyonadi wewe,

Mangi alitokea ukoo mkubwa wa Mushi wenye linage ndefu ya kifalme kutokea Mangi Kimboka hivyo ukoo wake unajulikana kama Mushi ya Kimboka (Mushi Kimboka)

Watu wengi wamekuwa wakipotosha historia ya kweli kwa makusudi au kutokujua na hii huleta hisia tofauti kwa sababu wengi wanakuja na oral stories za sehemu wanazotokea ei Machame, Moshi, Marangu etc ambazo hazina back up yoyote na mara nyingi zinakuwa biased na upande mmoja

Historia inayotambulika dunia nzima kabla ya kuja kwa wazungu Kibosho ilitawala zaidi ya 50% ya wachagga wote, ukienda Machame, Rombo, Ugweno, Mamba, Siha etc utakutana na majina ya Mangi Malamya/Malamia ambao wote asili yao ni Kibosho na walipelekwa kusimamia interest ya Mangi wa kibosho

Mangi mwenye influence kubwa katika historia ya umangi mdogo wa kichaga Machame
(Sababu Machame haikuwai kujitawala kabla ya wazungu) ni Shangali ambae amakulia Kibosho na alisimikwa kuwa Mangi Machame baada ya mtangulizi Mangi Ngamini wa Machame kushindwa vita na kukimbilia Moshi kwa Mangi wa huko old Moshi Mandara

Kwa kumalizia Mnyika na jopo lake ni matapeli wa historia ya kweli kwa interest zao binafsi labda umaharufu kisiasa

-Mangi Sina alifariki mwaka 1897 (Cause of deal old age)

-Mangi Meli alifariki mwaka 1900 (Cause of death hanging)

Note, kosa alilonyongwa nalo Meli mtoto wa Mangi Mandara/Rindi ndio kosa hilohilo walimnyonganalo Molelia mtoto wa Sina muda huohuo siku hiyohiyo 1900

Hapa unaweza kuona hakukuwa na usaliti wowote ule aliofanya "The Great Mangi Sina" zaidi ya poroja za kutaka kumchafua huyu mtawala bora kabisa kuwahi kutokea katika historia

Mangi alifariki miaka mitatu kabla ya Meli kunyongwa, mtoto wa mangi Sina na Mangi mpya kibosho Moleia alinyongwa pia muda huo huo Meli akinyongwa, mastermind wa hii yote vitabu vinasema alikuwa ni Marealle yote kwa yote hauwezi kumuita Marealle msalita kwa sababu hakukuwa na common interest baina yao ila kila mmoja alikuwa anatafuta interest kuongeza umaarufu wake
 
Ni kweli. Wamachame wengi waliona wamesalitiwa na mangi Sina wa Kibosho. Ingawa alishaonekana kuwa na shari lakini hawakutegemea hali ingefikia kuwa mbaya hivyo. Ndiyo maana walipoambiwa amefariki wengi walikwenda ili kumzika mtu wao waliomfahamu siku nyingi. Walikwenda majemedari wa vita na walikwenda hata watu wa ukoo wa mangi wa Machame. Ukumbuke pia kwamba pamoja na kwamba hapo nyuma Machame iliitawala Kibosho kwa mkono wa chuma lakini hawa walikuwa ni majirani walioishi kwa muda mrefu. Kulikuwa na kuoleana na wakibosho wengi walikuwa wakienda Machame kufanya biashara ndogo ndogo na kazi mbalimbali. Hata hivyo wamachame walionekana ni watu waliojisikia na kudharau wachaga wengine kitu ambacho hakikupokelewa vizuri sana na wegine kule uchagani. Kwa mfano, Baroni Von Der Decken, Mjerumani mvumbuzi aliandika (katika miaka ile ya 1860) jinsi wachaga wengine walivyojipanga kufanya hujuma dhidi ya Machame na husda ilivyokuwa kubwa dhidi ya wamachame kule uchagani. Kwa hiyo, kile alichokifanya mangi Sina dhidi ya Machame, kwa baadhi zilikuwa ni habari za mshituko lakini kwa wengine waliona kama huo ndiyo mwanzo wa mwisho wa vigogo wa kisiasa kule uchagani. Ni kitu kilichopokewa kwa hisia tofauti kule uchagani.

Kwa maelezo yaliyotolewa na Hans Meyer aliyoandika kuhusiana na safari zake kule uchagani (miaka ya 1886-1889), inaonekana ndiye mgeni pekee ambaye aliweza kugusia nyakati mauaji dhidi ya wamachame yalipofanyika. Alisimulia kwamba ni katika miaka ya 1886 (tofauti na alivyodhani Kathleen Stahl ambaye amekosea mambo kadha wa kadha ya kihistoria kule uchagani akirudisha nyuma miaka kwamba ni 1870's). Lakini hata hivyo kulikuwa na cha zaidi ya kilivyoonekana kwa wenyeji wa kawaida sehemu zile. Hii ndiyo inaonyesha jinsi siasa kule uchagani zilivyokuwa ni ngumu na zenye mambo mengi yasiyoeleweka kirahisi. Kathleen Stahl kwenye kitabu chake cha 'History of the Chagga People of Kilimanjaro' amegusia pia kitu kinachoonekana kilikuwa kikiendelea nyuma ya pazia hata kupelekea zahma ile iliyofanywa na mangi Sina dhidi ya wamachame. Ngamini Ndesserua (kaka yake Shangali) ndiyo alikuwa amejitangaza mtawala wa Machame wakati huo na watu kadha wa kadha wakawa wameambatana naye. Haifahamiki kwa uhakika nyakati lakini baada ya kifo cha mangi Ndesserua (inakadiriwa miaka ya 1879-1880) inaonekana ni watu fulani wa karibu na marehemu ndiyo waliyofahamu yaliyojiri (wanatajwa kuwa ni Nasua, Karawa, na Meenda ambao walikuwa ni ndugu waliokuwa karibu sana na mangi Ndesserua). Siri ilipikwa muda mrefu kuepuka watu kufahamu kwamba mtawala wao hayupo, lakini hata hivyo ni kwa sababu za kiusalama pia. Ilidaiwa vilevile (ni vigumu kuthibitisha hili lakini kama walivyodai hao wapambe akina Nasua) kuwa mangi Ndesserua siku za mwisho mwisho za uhai alitoa wosia kwamba mtoto wake mdogo Shangali ndiyo amrithi kwenye utawala na siyo Ngamini (ambaye ndiyo alikuwa mtoto mkubwa kwa wakati huo). Hii ndiyo iliyopelekea zengwe na mazingira tata yaliyokuja kuijiri Machame baadaye. Shangali alikuwa ni mdogo sana wakati huo (kama miaka 3 hivi) asiyeweza kabisa kupewa chochote kile cha maana kufanya katika ufalme. Hii timu ya akina Nasua baada ya kufahamu kwamba mangi Ndesserua amefariki walijikita kwenye propaganda na hadaa kwa umma kwamba mangi bado ni mgonjwa na akipona ana mambo muhimu ya kuwaeleza wananchi hivyo waendelee kutambika kumtakia heri na kupona haraka. Walipika mazingira hata ya kuleta waganga kutoka Mombasa ili ionekane kwamba kuna jitihada za kumpatia tiba wakati ilikuwa ni geresha na usanii. Hizi propaganda ziliendelea muda mrefu (inasemekana kama miaka 3 hivi) ingawa kuna dalili kwamba mangi Sina alifahamu mapema kilichotokea (inasemekana Nasua alikula yamini naye kumsaidia itakapofika wakati Shangali ana umri wa kuweza kukabidhiwa nchi). Walijitahidi kuvuta muda ili ifike kipindi cha kuweza kumtangaza Shangali kuwa ni mrithi wa mangi Ndesserua. Hata hivyo hali tata ilizidi kujiri kwenye nchi. Manung'uniko, majungu, uzushi, na hofu vilizidi kutawala kwenye jamii baada ya kupita muda mrefu bila mangi Ndesserua kuonekana kwenye 'public' kama walivyozoea miaka ya nyuma.

Hizo njama zilionekana kugomba mwamba. Kutokana na mazingira yalivyokuwa yakiendelea, moja kwa moja mtoto mkubwa wa mangi Ndesserua, Ngamini, alihisi kuna zengwe linaloendelea. Alijitosa na kutangaza kwamba sasa yeye ndiyo atakuwa akishughulikia mambo yote ya utawala wa nchi. Kutokana na jamii kuwa 'desparate', wengi walifarijika na kuambatana naye, ingawa wengine kwa kujua hatari ya mangi Ndesserua walihofia kujidhihirisha kuwa upande wake, ikiwa kweli bado mangi Ndesserua alikuwa hai. Hata hivyo, Ngamini kwa bahati mbaya hakujuwa kwamba mahasimu wake walishajipanga siku nyingi na alijiingiza kwenye mtego mbaya. Hii timu ilimpiga mkwara Ngamini kwamba alichokifanya ni uhaini na hawataweza kumtetea dhidi ya hasira za baba yake atakapopona. Ila kutokana na shinikizo la hali ilivyokuwa na jinsi ambavyo Ngamini alihisi kuwa safari zao hao jamaa (hasa Nasua) kuelekea Kibosho hazikuwa zinaelewekaeleweka vizuri, aliamua lolote na liwe lakini nchi haitaweza kuachiliwa iendelee hali ilivyo. Kuna uwezekano mkubwa hii ilikuwa ni miaka ya 1884, kabla ya mauaji yale ya kupangwa na mangi Sina hayajatekelezwa mwaka 1886. Cha kushangaza ni kwamba, wakati wakibosho wamekuja Machame kupiga ukunga kwamba mangi Sina amefariki, akina Nasua ndiyo walikuwa wa kwanza kuzipigia upambe na kuhamasisha kwamba hicho kilio kinawahusu sana wamachame na ni muhimu Ngamini kama kiongozi wa Machame aende kushughulikia mambo ya kisiasa Kibosho na kuhakikisha usalama kule. Kwa kuonekana kuafiki kile wakibosho walichokipendekeza, walihimiza pia watu wengine hasa maarufu waende Kibosho ili kushughulikia mazishi ya mangi Sina na kusaidia kumtawalisha mwingine.

Hata hivyo Ngamini alizipokea hizo taarifa kwa machale makubwa. Alihisi liko jambo. Inasemekana alipinga kabisa hilo wazo la wamachame kwenda Kibosho na alisema kwamba ili kudhihirisha kwamba ni fedheha kufanya hicho kitu atalala kwenye njia ya kuendea Kibosho akidai kwamba atakaye mruka kwenda Kibosho hatarudi. Akina Nasua waliendesha kampeni za upambe na fitina wakichochea watu kwamba Ngamini ni mtu mwoga asiyefaa kupewa hata usaidizi wa kushauri ukoo wake mwenyewe. Watu wengi waliingia kwenye mtego huu. Wengi hasa wale wa ukoo wa mangi wa Machame walimruka Ngamini wakaenda Kibosho. Wengine hasa majemedari hawakuthubutu kufanya hivyo bali waliingia porini na kutokea njia za kwendea Kibosho. Cha ajabu katika mshikemshike hiyo watu hawakugundua kwamba akina Nasua waliingia mitini na wala hawakwenda Kibosho. Inaonyesha dhahiri kulikuwa kweli na zengwe lililopikwa. Jitihada zao za kumshawishi Ngamini aende Kibosho zilishindwa vibaya. Hata hivyo yaliyojiri kule Kibosho yalisaidia sana kupunguza nguvu ya Machame na hasa Ngamini, maana majemedari wengi waliuawa na hata watu maarufu wa ukoo wa mangi wa Machame nao waliteketea. Kulikuwa na kilio kikubwa sana Machame. Ngamini alitangaza msiba mkubwa kwenye nchi na kutoa amri kwamba atakayejenga nyumba na mlango wake ukaelekea Kibosho kufa na afe, maana anaieletea nchi laana. Hii siri ya kilichojiri ilikuja kugundulika baadaye ingawa akina Nasua waliendelea kujiweka mbali na usaliti huo. Mashambulizi hayo ya 1886 yalimpa mwanya mangi Sina kufanya mashumbulizi baadaye Machame akilazimisha kwamba Ngamini akane kujitangaza kuwa mtawala wa Machame. Hiyo hata hivyo haikuwezekana kirahisi. Ilichukua mpaka 1890, baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe akina Nasua walivyovianzisha dhidi ya Ngamini wakipiga propaganda nyingi kwamba Ndesserua alitaka Shangali atawale kwa hiyo Ngamini amechukua nchi kwa nguvu. Mmishionari kutoka ufaransa, aliyeitwa Alexander Le Roy aliyefika Machame 1890, alitoa taarifa jinsi Machame ilivyokuwa imegeuka kuwa jaa la machafuko, nchi ikiwa inanuka uharibifu. Askari wa Nasua na wale wa mangi Sina waliungana dhidi ya waliomuunga mkono Ngamini na hata kufanya Machame iwe imekatika vipande vipande. Ni mwaka huo wa 1890 ndiyo Ngamini aliamua kuweka silaha chini, na kwa ushauri wa kapteni Johannes aliyekuwa bomani kule Moshi, aliamua yeye na familia yake kuhamia Moshi ili nchi itulie na kumwachia Shangali atawale Machame.

Ninakiri kwamba nimeandika kwa ufupi ufupi sana (briefly) na kuruka baadhi ya details. Mambo hayo ya wamachame na wakibosho, n.k. siku hizi yamekwisha. Ni mambo ya zamani za kale. Ninakubali lakini kwamba wako wazee ambao bado yanawasumbua. Maendeleo na maingiliano siku hizi yamefanya mitazamo ya watu ibadilike na watu siku hizi wanaoana bila kujali historia za zamani za kale. Hata hivyo, kufahamu historia ya kule unakokwenda kuoa/kuolewa ni msaada mkubwa.
Najua ni muda mrefu sana umepita tangu hii thread ianzishwe ila kwa kuwa sikuwahi kukutana nayo popote au kuiona ntajibu tu sababu hakuna namna nyingine,

Ss wenyewe hii stori kwetu ipo ila ni kwa version nyingine kwamba watoto wa kiume walikuwa wanatahiriwa pamoja kimakundi(Kibosho na Machame) na hivyo ilopofika zamu ya kwenda kutairiwa Machame basi huko wamachame wakawatairi watoto kwa hila kwa kukata dudu zao nusu/nzima kupekea watoto wote kutokea kibosho intake nzima kufariki, huku wenzao wakimachame wakifanikisha zoezi hill bila kupoteza watoto/vijana wao

Hii ilileta hasira sana Kibosho na wakaapa kulipiza kisasi kwa kuandaa karamu kwa wakijua Wamaachame wanapenda pombe na nyama basi wakaua na kwenda kupiga na huko Machame na kutawala kwa muda mrefu mpaka wakoloni walivyokuja

Lakini hizi zote ni stori tu ambazo hazina ukweli wowote ukweli ameandika Dundas tu katika kitabu chake

"Dundas ameandika kwamba tuliingia Machame na kuichapa fair and square, kwamba Machame ilikuwa ni tawala ndogo ya kimangi, kwamba Machame haikuwahi kuwa tishio kwa dollar nyingine za kichaga kabla ya wakoloni hasa waingereza na yote haya ni kweli sababu hakuna Mangi yoyote yule unaeweza kumtaja ambae alikuwa na umaarufu kuliko Sina na hii sio Machame tu bali uchagani kote

Mangi Sina aliingia Marangu na kuichapa fair and square, Sina aliingia Moshi na kuichapa ila alishindwa vunja boma la Mandara, hivyo hivyo Mandara alivyo ingia kibosho kwa usaidizi wa wajerumani na machief wote kasoro Machame ambayo ilikuwa chini ya Kibosho na kushindwa kuvunja ngome ya Mangi Sina kwa siku tatu wakiwa hawajafanikiwa kufuja ukuta wa boma hadi walipoamua kufikia makubaliano na mangi in only three conditions

1. Mangi Sina alitakuwa akubali kupeperusha bendera ya Ujerumani na sio ya sultan wa Zanzibar kama ilivyokuwa mwanzo

2. Mangi Sina alitakiwa kukubali na kuheshimu mamlaka ya tawala nyingine kama Mamba aliyokuwa akitawala hii iliamishiwa chini ya Mandara, pia alitakiwa kuacha Machame na Siha zijitawale na kuahidi kutovamia tena, pia kuheshimu title ya Mandara kama mangi mkuu

3. Alitakiwa kufungua ofisi ya akida "mswahili" atakae kuwa anareport taarifa zote za Kibosho kwa wajeruma HQ old Moshi

Mangi alikubaliana na conditions hizo zote na kuendelea na utawala wake kibosho na alikuja kurudishiwa Mamba kipindi cha Governor mpya Carl Peters baada Von Zelewsk kuondoka

Sababu wa kurudishiwa mamba ni kwamba baada ya Von Zelewisky (jina naweza kuwa nimekosea) rafiki wa Mandara kuondoka alikuja Governor Mpya Carl Peters alias mkono wa damu aliependelea zaidi Marangu na siasa za Marealle hivyo Mandara/Rindi kupoteza umaharufu wake

Historia ya Machame ilianza kushamiri baada ya vita ya kwanza ya dunia na mjerumani kumkabidhi Mwingereza uchagga, mwingereza alipendezwa zaidi na Machame sababu aliona wachaga wengine loyalty yao ipo kwa wajerumani ndio maana ali exile mamangi wengine wenye nguvu Mfano Ngilisho, Malamya kaka yake shangali pia na kuwapeleka Kismayo Somali huko ili kudhohofisha wenye nguvu na kutawala kirahisi

Von Zelewsk alishangazwa na boma la Mangi Sina "Mangi Sina Fortress" na kusema wazi Africa nzima hajaona finest defensive system kama hiyo ya boma la mangi ikumbukwe tu Von sio jina ni tittle anayotoa mfalme Kaiser mwenyewe kwa askari wenye weleti wa hali ya juu mno
 
Najua ni muda mrefu sana umepita tangu hii thread ianzishwe ila kwa kuwa sikuwahi kukutana nayo popote au kuiona ntajibu tu sababu hakuna namna nyingine,

Ss wenyewe hii stori kwetu ipo ila ni kwa version nyingine kwamba watoto wa kiume walikuwa wanatahiriwa pamoja kimakundi(Kibosho na Machame) na hivyo ilopofika zamu ya kwenda kutairiwa Machame basi huko wamachame wakawatairi watoto kwa hila kwa kukata dudu zao nusu/nzima kupekea watoto wote kutokea kibosho intake nzima kufariki, huku wenzao wakimachame wakifanikisha zoezi hill bila kupoteza watoto/vijana wao

Hii ilileta hasira sana Kibosho na wakaapa kulipiza kisasi kwa kuandaa karamu kwa wakijua Wamaachame wanapenda pombe na nyama basi wakaua na kwenda kupiga na huko Machame na kutawala kwa muda mrefu mpaka wakoloni walivyokuja

Lakini hizi zote ni stori tu ambazo hazina ukweli wowote ukweli ameandika Dundas tu katika kitabu chake

"Dundas ameandika kwamba tuliingia Machame na kuichapa fair and square, kwamba Machame ilikuwa ni tawala ndogo ya kimangi, kwamba Machame haikuwahi kuwa tishio kwa dollar nyingine za kichaga kabla ya wakoloni hasa waingereza na yote haya ni kweli sababu hakuna Mangi yoyote yule unaeweza kumtaja ambae alikuwa na umaarufu kuliko Sina na hii sio Machame tu bali uchagani kote

Mangi Sina aliingia Marangu na kuichapa fair and square, Sina aliingia Moshi na kuichapa ila alishindwa vunja boma la Mandara, hivyo hivyo Mandara alivyo ingia kibosho kwa usaidizi wa wajerumani na machief wote kasoro Machame ambayo ilikuwa chini ya Kibosho na kushindwa kuvunja ngome ya Mangi Sina kwa siku tatu wakiwa hawajafanikiwa kufuja ukuta wa boma hadi walipoamua kufikia makubaliano na mangi in only three conditions

1. Mangi Sina alitakuwa akubali kupeperusha bendera ya Ujerumani na sio ya sultan wa Zanzibar kama ilivyokuwa mwanzo

2. Mangi Sina alitakiwa kukubali na kuheshimu mamlaka ya tawala nyingine kama Mamba aliyokuwa akitawala hii iliamishiwa chini ya Mandara, pia alitakiwa kuacha Machame na Siha zijitawale na kuahidi kutovamia tena, pia kuheshimu title ya Mandara kama mangi mkuu

3. Alitakiwa kufungua ofisi ya akida "mswahili" atakae kuwa anareport taarifa zote za Kibosho kwa wajeruma HQ old Moshi

Mangi alikubaliana na conditions hizo zote na kuendelea na utawala wake kibosho na alikuja kurudishiwa Mamba kipindi cha Governor mpya Carl Peters baada Von Zelewsk kuondoka

Sababu wa kurudishiwa mamba ni kwamba baada ya Von Zelewisky (jina naweza kuwa nimekosea) rafiki wa Mandara kuondoka alikuja Governor Mpya Carl Peters alias mkono wa damu aliependelea zaidi Marangu na siasa za Marealle hivyo Mandara/Rindi kupoteza umaharufu wake

Historia ya Machame ilianza kushamiri baada ya vita ya kwanza ya dunia na mjerumani kumkabidhi Mwingereza uchagga, mwingereza alipendezwa zaidi na Machame sababu aliona wachaga wengine loyalty yao ipo kwa wajerumani ndio maana ali exile mamangi wengine wenye nguvu Mfano Ngilisho, Malamya kaka yake shangali pia na kuwapeleka Kismayo Somali huko ili kudhohofisha wenye nguvu na kutawala kirahisi

Von Zelewsk alishangazwa na boma la Mangi Sina "Mangi Sina Fortress" na kusema wazi Africa nzima hajaona finest defensive system kama hiyo ya boma la mangi ikumbukwe tu Von sio jina ni tittle anayotoa mfalme Kaiser mwenyewe kwa askari wenye weleti wa hali ya juu mno
Ndugu zanguni,
Nimevutiwa sana na huu uzi na sababu yake ni kuwa nimeandika kitabu ambacho utafiti wake ulinifikisha Machame na Old Moshi.

Halikadhalika utafiti huu ulinifungulia nyaraka zilizokuwako Machame zilizohifadhiwa kwa miaka 100.
Kama hili halitoshi nilihadithiwa historia iliyohifadhiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa takriban miaka 200.

Nataka nikuwekeeni hapa kipande kidogo katika yale niliyojifunza katika historia hii:

''Historia ya Wachagga imeandikwa kwenye upeo wa hali ya juu na Wazungu kiasi cha kumstaajabisha msomaji.

Inawezekanaje kwa Mzungu kutoka Ulaya mtu mgeni kuijua historia kwa undani wa kiasi kuweza kueleza mambo yaliyotokea miaka mingi sana iliyopita.

Mwandishi Mwingereza Charles Dundas ameandika historia ya Wachagga kwa kiwango cha kustaajabisha. Charles ameelezea mengi ambayo mtu hupata tabu hata kuyafikiri achilia mbale kuyajua hadi awe ameyasoma.

Wachagga wana hulka pale wanapompenda mgeni basi watampa lakabu inayoendana na heshima ya kabila lao.
Charles Dundas walimwita, Wasaoye-o-Wachagga, yaani Mzee wa Kichagga.

Historia ya Muro Mboyo aliyeishi Machame katika miaka ya katikati ya karne ya 19 imeishi katika simulizi za ukoo wake unaofahamika kama ukoo wa Nkya, ikipokelewa kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine kwa miaka inayofikia 200 kama ilivyoelezwa.

Historia hii haikupata kuandikwa popote kwa nia ya kuwa historia hiyo inaandikwa ili ije kusomwa.

Hata hivyo mtoto wake, Kirama Mboyo ameacha utajiri mkubwa wa nyaraka zilizoandikwa kwa hati ya mkono na nyingine zimepigwa chapa zinozoeleza historia ya babu zake waliomtangulia kiasi cha miaka 100 nyuma na kueleza pia historia yake mwenyewe pale ilipoingia karne ya 20.

Baadhi ya nyaraka hizi ziko katika mfano wa barua, taarifa na maelezo ya kawaida zina tarehe na zipo nyingine hazina tarehe wala jina la mwandishi.

Muhimu ni kuwa kumbukumbu hizi zinaeleza historia muhimu sana ya takriban miaka 200 nyuma ya Wachagga wa Machame na sehemu nyingine za jirani ambao walikuja kuwa Waislamu wa kwanza.

Hizi nyaraka kwa zile ambazo zina tarehe zinarudi nyuma miaka 100.

Kuanzia mwishoni mwa karne ya 19, kufuatia mgogoro wa Muro Mboyo na Mangi Ndeseruo Mamkinga (aliyetawala kuanzia 1855 – 1880), hadi kuingia karne ya 20, hali ya uchaggani haikuwa shwari.

Hali ya utulivu ilipatikana baada ya kuingia kwa Wamishionari kuanzia karne ya ishirini.

Wamishionari wa kwanza kuwasili walikuwa kutoka Ujerumani, Leipzig Mission na Uchagga nzima iliingia katika utulivu.

Utulivu ulizidi kushamiri hasa walipofika Waingereza baada ya Vita Kuu ya Kwanza (1914 – 1918).

Wakati wa utawala wa Wajerumani, Uchagga uliingia katika madhila makubwa na misiba mizito kwa watawala wao (waliokuwa wakijulikana kama Mangi) kukamatwa na kunyongwa kwa kuupinga ukoloni wa Wajerumani.

Tunaweza kuanzia hapa kurudi nyuma tukizipitia nyaraka hizi ili kupata historia ya Uchaggani kwa jumla ilikuwaje kabla ya kufika wakoloni Wajerumani ambao walitanguliwa na Wamishionari waliojiita pia ni wavumbuzi.''

Katika utafiti wangu mtawala wa kwanza kusoma historia yake ni Mangi Shangali Ndeseruo na nimesoma habari zake kutoka Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama ambae hapo juu kabla ya kuingia Uislam alijulikana kwa jina la Muro Mboyo.

1626208183615.png

Mangi Shangali Ndeseruo

20210713_233442.jpg
 
Ndugu zanguni,
Nimevutiwa sana na huu uzi na sababu yake ni kuwa nimeandika kitabu ambacho utafiti wake ulinifikisha Machame na Old Moshi.

Halikadhalika utafiti huu ulinifungulia nyaraka zilizokuwako Machame zilizohifadhiwa kwa miaka 100.
Kama hili halitoshi nilihadithiwa historia iliyohifadhiwa kutoka kizazi kimoja hadi kingine kwa takriban miaka 200.

Nataka nikuwekeeni hapa kipande kidogo katika yale niliyojifunza katika historia hii:

''Historia ya Wachagga imeandikwa kwenye upeo wa hali ya juu na Wazungu kiasi cha kumstaajabisha msomaji.

Inawezekanaje kwa Mzungu kutoka Ulaya mtu mgeni kuijua historia kwa undani wa kiasi kuweza kueleza mambo yaliyotokea miaka mingi sana iliyopita.

Mwandishi Mwingereza Charles Dundas ameandika historia ya Wachagga kwa kiwango cha kustaajabisha. Charles ameelezea mengi ambayo mtu hupata tabu hata kuyafikiri achilia mbale kuyajua hadi awe ameyasoma.

Wachagga wana hulka pale wanapompenda mgeni basi watampa lakabu inayoendana na heshima ya kabila lao.
Charles Dundas walimwita, Wasaoye-o-Wachagga, yaani Mzee wa Kichagga.

Historia ya Muro Mboyo aliyeishi Machame katika miaka ya katikati ya karne ya 19 imeishi katika simulizi za ukoo wake unaofahamika kama ukoo wa Nkya, ikipokelewa kutoka kizazi kimoja hadi kizazi kingine kwa miaka inayofikia 200 kama ilivyoelezwa.

Historia hii haikupata kuandikwa popote kwa nia ya kuwa historia hiyo inaandikwa ili ije kusomwa.

Hata hivyo mtoto wake, Kirama Mboyo ameacha utajiri mkubwa wa nyaraka zilizoandikwa kwa hati ya mkono na nyingine zimepigwa chapa zinozoeleza historia ya babu zake waliomtangulia kiasi cha miaka 100 nyuma na kueleza pia historia yake mwenyewe pale ilipoingia karne ya 20.

Baadhi ya nyaraka hizi ziko katika mfano wa barua, taarifa na maelezo ya kawaida zina tarehe na zipo nyingine hazina tarehe wala jina la mwandishi.

Muhimu ni kuwa kumbukumbu hizi zinaeleza historia muhimu sana ya takriban miaka 200 nyuma ya Wachagga wa Machame na sehemu nyingine za jirani ambao walikuja kuwa Waislamu wa kwanza.

Hizi nyaraka kwa zile ambazo zina tarehe zinarudi nyuma miaka 100.

Kuanzia mwishoni mwa karne ya 19, kufuatia mgogoro wa Muro Mboyo na Mangi Ndeseruo Mamkinga (aliyetawala kuanzia 1855 – 1880), hadi kuingia karne ya 20, hali ya uchaggani haikuwa shwari.

Hali ya utulivu ilipatikana baada ya kuingia kwa Wamishionari kuanzia karne ya ishirini.

Wamishionari wa kwanza kuwasili walikuwa kutoka Ujerumani, Leipzig Mission na Uchagga nzima iliingia katika utulivu.

Utulivu ulizidi kushamiri hasa walipofika Waingereza baada ya Vita Kuu ya Kwanza (1914 – 1918).

Wakati wa utawala wa Wajerumani, Uchagga uliingia katika madhila makubwa na misiba mizito kwa watawala wao (waliokuwa wakijulikana kama Mangi) kukamatwa na kunyongwa kwa kuupinga ukoloni wa Wajerumani.

Tunaweza kuanzia hapa kurudi nyuma tukizipitia nyaraka hizi ili kupata historia ya Uchaggani kwa jumla ilikuwaje kabla ya kufika wakoloni Wajerumani ambao walitanguliwa na Wamishionari waliojiita pia ni wavumbuzi.''

Katika utafiti wangu mtawala wa kwanza kusoma historia yake ni Mangi Shangali Ndeseruo na nimesoma habari zake kutoka Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama ambae hapo juu kabla ya kuingia Uislam alijulikana kwa jina la Muro Mboyo.

View attachment 1852235
Mangi Shangali Ndeseruo

View attachment 1852247
Hii ni historia kubwa sana Mzee Said inastahili uitengenezee kabisa uzi wake rasmi ili ipate michango tofauti tofauti

Vitabu vingi nilivyopitia vinaelezea kulikuwa na uhusiano mkubwa baina ya Sultan wa Zanzibar na Kilimanjaro ila havikuandika kama kulikuwa na uhusiano wakidini zaidi ya biashara, ingependeza uanzishe uzi rasmi kwa ajili ya Uislam Machame na Kilimanjaro yote
 
Kuna kitabu pia niliwahi kukutana nacho kilimtambulisha Mangi Sina kama Sultan wa Kibosho, nikikipata nakiunganisha hapa
 
Back
Top Bottom