Nimeota ndoto ya ajabu sana, eti viongozi wa sasa/wastaafu kibao na wafanyabiashara wamejazana pale MAELEZO kila mmoja anataka kuongea na waandishi wa habari! Waliopewa nafasi ya awali kuzungumza na waandishi ni wale watuhumiwa wa ufisadi (unawajua!). Msemaji wa mafisadi kwa niaba ya wenzake wengi anakiri kwamba wao ndio wameifikisha hii nchi hapa ilipo kwa ufisadi wao, anadokeza kwamba kuanzia kwenye EPA mpaka kwenye Richmond wao ndio wahusika wakuu, baada ya kukiri, mmoja wao anasimama kwa uchungu na KUWAOMBA watanzania msamaha!
Baada ya mafisadi kumaliza na kuomba msamaha huku waandishi wakibaki vinywa wazi ikafuata zamu ya kiongozi wa jeshi la polisi, anasimama mbele ya vyombo vya habari na kukiri kwamba jeshi lake kwa wakati tofauti limewanyanyasa raia bila makosa, jeshi lake mara kwa mara limewatia ulemavu raia wasiokuwa na hatia, jeshi lake limemwaga damu za raia wema, mfano mwembechai, msitu wa pande, Zanzibar (2001) nk. Baada ya kusema hayo huku akijifuta machozi anawaomba RADHI waathirika wote na wananchi kwa ujumla!
Hii ndoto vituko, baada ya kiongozi wa polisi kumaliza, akaja yule kiongozi wa bendi yetu. Tulimpa uongozi miaka ile atuongozee bendi yetu ili iweze kushindana na bendi nyingine katika soko la muziki wa dansi.Alipopewa mic akaangua kilio kikubwa, eti anaomba msamaha, eti anasema wakati wa uongozi wake badala ya kuiendeleza bendi yetu alifikia mahali akawa anachukua magitaa, drums, mpaka keyboards anajimilikisha. Mbali ya mshahara mzuri aliokuwa anaupata na uhakika wa marupurupu kibao baada ya kustaafu, bado aliendelea kujilimbikizia vifaa vya bendi. Nae kama waliotangulia akawaomba radhi washabiki wake pamoja na uongozi wa bendi kwa ujumla!
Huwezi amini ndoto imekatikia pabaya, mara nikashtuka, jasho mwili mzima ilikuwa ni saa mbili asubuhi tayari! Baadhi ya watu ambao hawakupata fursa ya kuongea mpaka ndoto yangu inakatika ni pamoja na aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar na Mkurugenzi wa TAKUKURU. Mwenyekiti ZEC sijui angesemaje hasa kuhusu Matokeo ya uchaguzi wa 1995 na 2000? Ukiacha mwenyekiti natumaini Mkurugenzi nae angesema jambo lolote kuhusu Richmond. Hii ndoto ya ajabu sana!
Baada ya mafisadi kumaliza na kuomba msamaha huku waandishi wakibaki vinywa wazi ikafuata zamu ya kiongozi wa jeshi la polisi, anasimama mbele ya vyombo vya habari na kukiri kwamba jeshi lake kwa wakati tofauti limewanyanyasa raia bila makosa, jeshi lake mara kwa mara limewatia ulemavu raia wasiokuwa na hatia, jeshi lake limemwaga damu za raia wema, mfano mwembechai, msitu wa pande, Zanzibar (2001) nk. Baada ya kusema hayo huku akijifuta machozi anawaomba RADHI waathirika wote na wananchi kwa ujumla!
Hii ndoto vituko, baada ya kiongozi wa polisi kumaliza, akaja yule kiongozi wa bendi yetu. Tulimpa uongozi miaka ile atuongozee bendi yetu ili iweze kushindana na bendi nyingine katika soko la muziki wa dansi.Alipopewa mic akaangua kilio kikubwa, eti anaomba msamaha, eti anasema wakati wa uongozi wake badala ya kuiendeleza bendi yetu alifikia mahali akawa anachukua magitaa, drums, mpaka keyboards anajimilikisha. Mbali ya mshahara mzuri aliokuwa anaupata na uhakika wa marupurupu kibao baada ya kustaafu, bado aliendelea kujilimbikizia vifaa vya bendi. Nae kama waliotangulia akawaomba radhi washabiki wake pamoja na uongozi wa bendi kwa ujumla!
Huwezi amini ndoto imekatikia pabaya, mara nikashtuka, jasho mwili mzima ilikuwa ni saa mbili asubuhi tayari! Baadhi ya watu ambao hawakupata fursa ya kuongea mpaka ndoto yangu inakatika ni pamoja na aliyekuwa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Zanzibar na Mkurugenzi wa TAKUKURU. Mwenyekiti ZEC sijui angesemaje hasa kuhusu Matokeo ya uchaguzi wa 1995 na 2000? Ukiacha mwenyekiti natumaini Mkurugenzi nae angesema jambo lolote kuhusu Richmond. Hii ndoto ya ajabu sana!