Hawara aliyempiga kibuti aukwaa u-Jaji... Kidume ajipanga upya!

jamani ndoa ngumu sana mtu asikwambie ongea tu kama hujaoa au kuolewa. kuna watu nawafahamu wamewekewa sumu na wake zao wakanusurika kufa lakini wanasameheana na mpaka leo wanaishi tena mapenzi motomoto sembuse kupigana kibuti?

"It is better to live with a devil whom you know than a angel you dont know"
 
Kuna njemba m'moja wa karibu kanitonya leo hii asubuhi ya kuwa anajipanga upya kurejesha majeshi..........kwa mzazi mwenzie ambaye ana karibu miaka 5 tangia ampige kibuti..................utetez i wake ni kuwa hawakuachana kwa ubaya na yakuwa mwenzie sasa huo ugali wa ujaji ni mkubwa sana haipendezi akiula pekee yake......................

Jiingine adai ni sababu za kiubinadamu nazo zimemkalia kooni kwa kipindi hivi ya kuwa mwenzie amekuwa akimlilia kwenye simu kila siku ya kuwa aache kumnyanyasa kwa kumpiga kibuti kwa hiyo kumrudia atakuwa kaitika wito na......kumtendea ubinadamu aache kuwa na masimango ambayo kidume anahisi yanamletea tafurani hata yeye.........

lingine anadai haifai jaji aonekane ni kapera wakati mzazi mwenzie yupo ila ni harakati za pimbi tu ndizo zilimtia majaribuni.................... ....

hii ni sahihi kweli???????????.............. .kurudia matapishi yako mwenyewe eti mkate umewiva na tumbo lina wakawaka kwa njaa....................sina uhakika kwenye hilo............Nisaidieni namna ya kumshauri kidume mwenye macheche nguli.......

Mkuu Ruta, hakuna muda maalum wa wanandoa kuamua kurudiana. Kama wote wameridhia kuipa ndoa yao nafasi nyingine basi mie sioni tatizo. Ni heri tu.

 
Last edited by a moderator:
Kwa kuwa tunatofautiana, kwa kuwa tuna mioyo tofauti. Kwa kuwa huyo mdada kaona hapo ndio mwisho wa mambo yote. Aende kwa amani. Ila mimi@Rutashubanyuma hata urudi na Ghorofa, miaka mitano? Yani hata mmoja nitajiuliza mara 70. Mmmh mwanaume au mwingine, hapana...Nooooooo.

Hapana kabisa labda kama sikukupenda Mwanzo. Yani nikupende nikupe moyo wangu, na damu yako nibebe, na mtoto wako nimlee miaka mitano. Afu uone nimefanikiwa ujilete lete......ha ha ha lazima utakuwa house boy wangu kama nitaamua kukurudisha walahi. Khaa yani miaka mitano?

Aku.....ulizaliwa peke yako au? Kwanza miaka mitano yote hiyo wengine hawajaniona? He he he anatafuta kazi ya house boy huyo. Halafu na huyo dada anajitafutia matatizo tu. WE KIBABA ka hicho unakileta ndani cha nini? SI kitakutesa balaa? Manake atatafuta kusikika hata mahali ambapo hatakiwi kusikika. Ohoooo unanidharau eeh zitakuwa nyingi umo ndani mpaka basi. Mwanaume wa kiafrika au mwingine? Tena usiombe awe mchagga au Mhaya.

[MENTION]LD[/MENTION] yawezekaa unayoyasema ni sahihi lakini mwana mpotevu akirudi kundini mpokee.....usilipize kisasi .....mwachie Muumba atajua la kumfanya........labda uwe nawe umeshikwa na mwingine lakini kama bado mpe nafasi ya mwisho nadhani atakuwa kuna kitu kajifunza hapo...............na watu wa namna hii mara nyingine huwa wanakuja kuwa bomba haswa..............
 
  • Thanks
Reactions: LD
LD yawezekaa unayoyasema ni sahihi lakini mwana mpotevu akirudi kundini mpokee.....usilipize kisasi .....mwachie Muumba atajua la kumfanya........labda uwe nawe umeshikwa na mwingine lakini kama bado mpe nafasi ya mwisho nadhani atakuwa kuna kitu kajifunza hapo...............na watu wa namna hii mara nyingine huwa wanakuja kuwa bomba haswa..............

Sipingi kusamehe, NI Amri na ni lazima.....Lakini kuungana mwili mmoja kwenye ndoa kufa na kuzikana ni maamuzi magumu sana hata Mungu analijua hilo. Nikipata neema ya kusamehe na amani ya moyo nitamrudisha. Hapa ni NEEMA ya MUNGU sio akili yangu.
 
ni sahihi kabisa kurudia matapishi hasa kama matapishi yenyewe ukila yana virutubisho ndani yake....
acha jamaa arudi bwana wakagawane mema ya nchi..ila ni ruksa kupiga kibuti mema yakiisha
 
Ni yule mama mrembo yule? Ana miguu bomba na rangi ya mtume ya ukweli dah, pale hata madame Rita hagusi aisee.
 
what goes on must come around,aa mi sishauri mimi binafsi ukiniudhi nikakuacha nimenyimwa moyo wa tamaa hata ujenge gorofa na magari na utajiri wakutisha ,hapo pembeni yangu kwenye kanyumba chakupanga sikutaki tena sina historia yakurudisha mapenzi nyuma enough its enough,ninaishi kwa philosophy hii ,siishi kwenye hii dunia milele napita tu,
Rutashubanyuma hujambo wewe ??
 
mh..hawara? sasa si waoane? ila kama anamrudia kwa sababu ya mpunga sikubaliani nae, ila kama kwa sababu ya kumpenda sawa..
 
Haya ndo yale nilisema hapa kuwa,jamii ina makengeza kwenye baadhi ya mambo.Ili upate cheo fulani ni lazima uwe na ndoa.Ujinga mkubwa huu.Ndoa ni nini?Eti unapokua na mke unakua na heshima na unajiheshimu,ujinga mwingine huu.Upofu huu sijui utaisha lini?

tena huu ujinga unazidi kukua mpaka imefikia hatua kuwa mtu asiopoa au kuolewa kama anakuwa anakosa heshima flani ivi kwenye jamii zetu
 
Huyo mwanaume hana upendo wa kweli full stop..Ina maana yule mwanamama asingeukwaa ujaji asingemfikiria kumrudia...
Mwenzie sasa atakula na majaji wenzie!..Matawi ya juu, yakheeee
 
Huyo anendakwenye tanuru la kuyeyushia chuma cha pua. Lazima tatoka baruti huyo muda si mrefu. Miaka mitano halafu jimama anapata ujaji................! muda si mrefu atakujia na madai kibao juu ya kuibiwa 'mke' wake huyo.
 
second chance , wapo wanao amin , kwahiyo ikiwa anaona namna gani vip na arudishe majeshi chini ,, aaangalie ,, sio kuwa issue kubwa hiyo, ila aangalie asije kuwa na ugonjwa waka cheki kwanza, LOL.
 
Mkuu, huyu njemba yawezeka akawa na maradhi ya UKahaba (pimbi). Na kama alivodokeza kua tabia hiyo ndiyo ilioleta mushkeli katika uhusiano, kabla ya kumpiga ndula mzazi mwenzie, ilhali ye ndie aliefumwa. Mkuu, Ukahaba unatibika kwa therapy ikiwemo Yoga. Kitu kingine mwambie atilie maanani mtoto. Ama kuhusu kurudisha majeshi kwa sababu ya ugali, yote kheri, mwalim. Ila aendelee kuvaa suruali, asiweke akili yote kwenye ugali akasahau wajibu wake.
 
Kuna njemba m'moja wa karibu kanitonya leo hii asubuhi ya kuwa anajipanga upya kurejesha majeshi..........kwa mzazi mwenzie ambaye ana karibu miaka 5 tangia ampige kibuti..................utetezi wake ni kuwa hawakuachana kwa ubaya na yakuwa mwenzie sasa huo ugali wa ujaji ni mkubwa sana haipendezi akiula pekee yake......................

Jiingine adai ni sababu za kiubinadamu nazo zimemkalia kooni kwa kipindi hivi ya kuwa mwenzie amekuwa akimlilia kwenye simu kila siku ya kuwa aache kumnyanyasa kwa kumpiga kibuti kwa hiyo kumrudia atakuwa kaitika wito na......kumtendea ubinadamu aache kuwa na masimango ambayo kidume anahisi yanamletea tafurani hata yeye.........

lingine anadai haifai jaji aonekane ni kapera wakati mzazi mwenzie yupo ila ni harakati za pimbi tu ndizo zilimtia majaribuni........................

hii ni sahihi kweli???????????...............kurudia matapishi yako mwenyewe eti mkate umewiva na tumbo lina wakawaka kwa njaa....................sina uhakika kwenye hilo............Nisaidieni namna ya kumshauri kidume mwenye macheche nguli.......

anatamani naye akafaidi rushwa kubwa za mamaaaa
 
kwenye suala la mapenzi ya watu wawili ni vigumu sana kusemea mioyo yao, wanaweza kuwa na sababu ambayo kwangu naiona kama ni weak ya kuwa ni wazazi kwa hiyo watudiana for the sake of mtoto wao, lakini mara nyingi wanaweza kurudiana kwa sababu zao binafsi na si kwa ajili ya mtoto/watotot kwani kabla ya kutengana walishakuwa na huyo mtoto na hawakujali maslahi yake iweje leo ghafla ionekane ni sehemu ya muunganiko wao? hy jamaa aseme ukweli tu ni huo wadhifa ndio unamfanya amrudie huyo mwanamke na mara watakaporudiana mchezo utarudi pale pale upimbi hatauacha, kama ni manyanyaso yataendelea tena na dharau juu kuwa huyo mama hazungushi kwake n.k. kwa upande wangu BCB 'baby come back' huwa haina nafasi.... maisha ni kusonga mbele nyuma mwiko utageuka jiwe la chumvi...
 
Back
Top Bottom