Hawa wake za viongozi waliotoa msaada Hanang ni taasisi? Imesajiliwa lini na chanzo chake cha mapato ni kipi?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,753
218,340
Kwa kweli tunawashukuru sana wale wote waliojitolea kwa hali na mali kusaidia wahanga wa Hanang , na tunachukua nafasi hii kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu ili awajazie pale palipopungua, Amina.

Hata hivyo ni vizuri tukafahamu huko ilikotokea misaada hii , wala haijawahi kuwa dhambi kufahamu chanzo cha msaada wowote ule , lengo la kujua hili ni kuepuka magenge ya utakatishaji wa fedha ama kupokea misaada ya wauza unga.

Hawa wanaojiita Wenza wa Viongozi ni akina nani , ni wake zao au ni nyumba ndogo zao? hii Taasisi ya wenza wa viongozi imesajiliwa lini na wapi , namba ya usajili wao ni ipi na malengo yao ni yapi? wanapata wapi hela za kutoa misaada hii na ni nani anayewapa hela hizo na kwanini?

Screenshot_2023-12-19-18-35-06-1.png


Tukiacha mambo haya bila kuhoji iko siku watakuja Watoto wa viongozi , binamu wa viongozi au Hata umoja wa wazazi wa viongozi

Ni vema utaratibu unaoeleweka ukatumika kwa yeyote anayetaka kuchangia chochote kwenye maafa , badala ya kuleta makundi yasiyo na tija yoyote .

Naomba kuwasilisha .
 
Tuambie zile harambee zenu zote huwa pesa mnapeleka wapi maana hazifiki kwa walengwa heri mpaka umewaona na umepata shauku ya kuhoji ni kuwa lengo limetimizwa kwa walengwa!
 
Sioni kama kuna tatizo mkuu, tuwe wamoja katika kusaidia wengine kama hali inaruhusu, tusianze kutupiana mawe na kukatishana tamaa wakati watu wamepata matatizo na wanahitaji kusaidiwa, kwa kufanya hivyo hatutakuwa tumewatendea haki wahanga
 
Tuambie zile harambee zenu zote huwa pesa mnapeleka wapi maana hazifiki kwa walengwa heri mpaka umewaona na umepata shauku ya kuhoji ni kuwa lengo limetimizwa kwa walengwa!
Japo hoja yako iko nje ya mada , lakini hebu weka ushahidi wa uzushi wako
 
Sioni kama kuna tatizo mkuu, tuwe wamoja katika kusaidia wengine kama hali inaruhusu, tusianze kutupiana mawe na kukatishana tamaa wakati watu wamepata matatizo na wanahitaji kusaidiwa, kwa kufanya hivyo hatutakuwa tumewatendea haki wahanga
Ulipaswa kuelewa hoja yangu
 
Sioni kama kuna tatizo mkuu, tuwe wamoja katika kusaidia wengine kama hali inaruhusu, tusianze kutupiana mawe na kukatishana tamaa wakati watu wamepata matatizo na wanahitaji kusaidiwa, kwa kufanya hivyo hatutakuwa tumewatendea haki wahanga
Ni tatizo hata kama wewe huoni...

Eti wake wa viongozi. Hivi ni viongozi gani hao maana kila mtu ni kiongozi. Hata wewe ni kiongozi kama sio kwenye taasisi fulani basi hata kwenye familia yako..
 
Back
Top Bottom