kasyabone tall
JF-Expert Member
- Sep 13, 2009
- 254
- 59
Wanafunzi wanaswa wakifanyiana mitihani
WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.
Mwanafunzi huyo, Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.
Tanzania Daima ilimshuhudia mtuhumiwa huyo akihojiwa na Michael Andekisye, ambaye ni Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo.
Msajili huyo alisema kuwa kitambulisho alichokuwa akikitumia kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.
Kaduma alifafanua mbele ya ofisi hiyo kuwa aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.
"Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani," alisema Kaduma.
Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).
tutarajie nini kutoka kwa wasomi hawa wanaosomeshwa kwa kodi yetu
WATU watatu, akiwamo mwanafunzi wa kidato cha sita katika Shule ya Sekondari ya Azania, jijini Dar es Salaam wamekamatwa wakiwafanyia mitihani wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), wanaosoma ngazi ya stashahada ya juu pamoja na shahada.
Mwanafunzi huyo, Frank Kaduma, aliyekuwa anamfanyia mtihani mwanafunzi aliyemtaja kwa jina moja la Tina, alikuwa ameahidiwa na mtu aliyemuunganisha na mtahiniwa huyo kuwa baada ya kutoka kwenye mtihani huo angelipwa sh 150,000.
Tanzania Daima ilimshuhudia mtuhumiwa huyo akihojiwa na Michael Andekisye, ambaye ni Msajili wa Wanafunzi chuoni hapo.
Msajili huyo alisema kuwa kitambulisho alichokuwa akikitumia kumfanyia Tina mtihani kilikuwa na jina la Christian Mbago, mwanafunzi wa mwaka wa tatu.
Kaduma alifafanua mbele ya ofisi hiyo kuwa aliitwa na rafiki yake ambaye hata hivyo hakutaka kumtaja jina, na baadaye alimuunganisha na mtahiniwa na kukubaliana kiasi hicho cha fedha baada ya kazi hiyo kumalizika.
"Mimi ninasoma Azania, nachukua PCM (Fizikia, Kemia na Hisabati), rafiki yangu anasoma masomo ya biashara na mtihani wa leo una hisabati, hivyo juzi nilikuja naye ili anionyeshe darasa na leo ndiyo nimekuja kumfanyia mtihani," alisema Kaduma.
Wakati mwanafunzi huyo akihojiwa, mwanafunzi mwingine, John Kapinga, alikamatwa na kupelekwa katika ofisi ya msajili baada ya kukutwa akimfanyia mtihani mwanafunzi wa mwaka wa tatu chuoni hapo, Joel Mlengule, anayesoma Stashahada ya Juu ya Hifadhi ya Jamii (Advanced Diploma in Social Protection).
tutarajie nini kutoka kwa wasomi hawa wanaosomeshwa kwa kodi yetu