Hasira hazijatosha, haiwezekani JK adharau na sisi tukae kimya..!

Mkuu Mbogo31 kwa taarifa tu ni kwamba hata Polisi wetu sasa wamechoka na kiukweli hawaishi kwa kutegemea mishahara ila wanaishi kwa kuchukua rushwa kila siku. Nani asiyejua sasa kwamba Polisi hawawezi tena kumudu maisha bial rushwa? Hawafanyi hivyo kwasababu wanapenda, wanazidiwa. Siwatetei lakini ninachojaribu kuonyesha ni kwamba tukifanya jambo hapa na ikakolea sawasawa Polisi wetu kuhamia upande wa wananchi ni rahisi sana. Kwanza wengi husema ninyi fanyeni, sisi tunavua uniform tunawaunga mkono. Wako na sisi tufanye kazi inayotakiwa, la msingi ni mpango kamili.

Nakubaliana na wewe kabisa, mimi pia nimesha wahi kuongea na wanajeshi hawa JWTZ wao wanasema wanatii madaraka yaliyowekwa na wananchi na watatii maamuzi ya wananchi ya kuwaondoa madarakani hao walio waweka na sio wao kupindua, sasa kinachosubiriwa ni sisi wanachi kuikataa serikali na wao wakiona kweli tunadhamira ya kweli watatulinda, sasa swali tuanaza vipi? maana kwa kweli mtu unaefikiri sawasawa huwezi kuvumilia huu uoza unaoendelea ndani ya serikali labda uwe kichaa. nihatari sana na ni janga kubwa sana kwa kizazi chetu, yaani fikiria huduma za kijamii zote hovyo halafu mawaziri wanatafuna pesa ya umma, ma rc, ma dc wakurugenzi, makatibu, wahasibu wa ngazi zote serikalini? ni pesa ngapi inafujwa ambayo ingeboresha maisha ya mtanzania?
 
Inabidi tumwajibishe kikwete kwa njia yeyote ile. Na kukaa kwake kimya ni dhahiri kwamba anayajua yote yanayotokea na ameyabariki kwa nguvu zake zote. Yeye na mawaziri wako pale kutukomesha sisi wananchi kwa ujinga wetu na wanafanya vile kwa makusudi kabisa wakifahamu kwamba hakuna mtanzania ambaye atathubutu kuwaaambia chochote, naamini leo hii tungesimama na kuukataa udhalimu wao wasingetuzuia kwani nguvu ya wengi ni nguvu ya Mungu, tunahitaji mtu mmoja tu atuunganishe tuwaonyeshe kwamba hatupendii wanavyotufanya wajinga kiasi hiki.

Uko sawa sana Mkuu, tukisimama tuna uwezo mkubwa wa kuwaonyesha kwamba hatutaki wayafanyayo. Tulifanye hili tarehe 28/04/2012 na hii ni ijumaa kabla hawajaanza porojo zao za Katiba mabyo nayo tutaigomea maana haina maana kwa hali hii tuliyonayo.
 
Nakubaliana na wewe kabisa, mimi pia nimesha wahi kuongea na wanajeshi hawa JWTZ wao wanasema wanatii madaraka yaliyowekwa na wananchi na watatii maamuzi ya wananchi ya kuwaondoa madarakani hao walio waweka na sio wao kupindua, sasa kinachosubiriwa ni sisi wanachi kuikataa serikali na wao wakiona kweli tunadhamira ya kweli watatulinda, sasa swali tuanaza vipi? maana kwa kweli mtu unaefikiri sawasawa huwezi kuvumilia huu uoza unaoendelea ndani ya serikali labda uwe kichaa. nihatari sana na ni janga kubwa sana kwa kizazi chetu, yaani fikiria huduma za kijamii zote hovyo halafu mawaziri wanatafuna pesa ya umma, ma rc, ma dc wakurugenzi, makatibu, wahasibu wa ngazi zote serikalini? ni pesa ngapi inafujwa ambayo ingeboresha maisha ya mtanzania?

Hii serikali kuilazimisha kufanya tunayotaka ni rahisi sana maana wenyewe kwanza wameshaaza kuchanganyana sana, tukifanya kuonana idadi ya kutosha hapo Uwanja wa Mnazi mmoja watahangaika sana na watafanya changes tunazotaka maana zipo wazi wala hazihitaji maongezi.
 
Wakuu mbona tunakuwa washabiki na hoja lege lege kujadili masuala mazito.

Ndg zangu wana jf hivi kweli bunge halina kifungu kingine cha katiba cha kutengua hizo siku 14 na badala yake iwe masaa au siku moja? make mm sioni kama serikali hii ya kitumwa kama itabadilika hivi karibuni.Kila mara tumeona mambo haya yakijirudiarudia, kumbukeni madaktari msimamo wao kuhusu Dr. mponda mpaka leo hakuna kinachoendelea.Kama kweli tuko serious na hii issue we need calzimatic guys who can mobilize pp to riot unless nothing would change till 2015.
cc wana A-town tumefedheheshwa sana na hotuba ya pm jana.Nimekubali kwamba pm wetu ni kama mwanakondoo tu hata kama atapelekwa kwenye madhabahu yeye yuko tayari kufa kwa ajili ya wenzake.hongera pinda unyenyekevu wako iko siku utapata shida isiyo ya kwako.
 
Uko sawa sana Mkuu, tukisimama tuna uwezo mkubwa wa kuwaonyesha kwamba hatutaki wayafanyayo. Tulifanye hili tarehe 28/04/2012 na hii ni ijumaa kabla hawajaanza porojo zao za Katiba mabyo nayo tutaigomea maana haina maana kwa hali hii tuliyonayo.

sasa 2fanye nini? Au wakuu mko kwenye mkakati kma ndiyo bs m2julishe 2jue 2nalianzishaje.pa1 sana wakuu.
 
Ndg zangu wana jf hivi kweli bunge halina kifungu kingine cha katiba cha kutengua hizo siku 14 na badala yake iwe masaa au siku moja? make mm sioni kama serikali hii ya kitumwa kama itabadilika hivi karibuni.Kila mara tumeona mambo haya yakijirudiarudia, kumbukeni madaktari msimamo wao kuhusu Dr. mponda mpaka leo hakuna kinachoendelea.Kama kweli tuko serious na hii issue we need calzimatic guys who can mobilize pp to riot unless nothing would change till 2015.
cc wana A-town tumefedheheshwa sana na hotuba ya pm jana.Nimekubali kwamba pm wetu ni kama mwanakondoo tu hata kama atapelekwa kwenye madhabahu yeye yuko tayari kufa kwa ajili ya wenzake.hongera pinda unyenyekevu wako iko siku utapata shida isiyo ya kwako.

Mkuu Snyamairo hapa tukisubiri 2015 nina hakika tutakufa wengi maana nakuhakikishia hawa majambazi watafanya lolote wawezalo ili wasitoke madarakani, tukae tukijua wazi kwamba uchaguzi wa 2015 utakuwa ni mgumu kuliko fikra zetu zinavyotuonyesha sasa. Binafsi sioni kama tutafika 2015 kama hali yenyewe ni hii, sishauri kupindua serikali lakini nashauri kuiadabisha serikali waone kwamba kuna ulazima wa kuwajibika na hili linawezekana tena sana.
 
sasa 2fanye nini? Au wakuu mko kwenye mkakati kma ndiyo bs m2julishe 2jue 2nalianzishaje.pa1 sana wakuu.

Sambamba mimi nimeshauri tugomee kila kitu na tubaki majumbani kuanzia 28/04/2012 Ijumaa. Katiba ikija pia tugome maana ni wizi mtupu unatungwa hapo hata tukitoa maoni watayaweka kapuni kisha kuweka upumbavu wao ili sisi tusiwe na nguvu popote. Tusitegemee kabisa serikali hii kutengeneza katiba ya kuruhusu wananachi wawabane katika hali ya ubadhirifu mkubwa namna hii, ni ndoto kabisa kwahiyo hata hiyo Katiba mimi kwangu haifanyi kazi wala haitobadilisha chochote zaidi ya useless documents mpya maofisi kwa hao wezi wenyewe.
 
Jamani ndivyo alivyoumbwa kwa sura ya kutabasamu sasa afanyeje. Hakuna sababu yoyote ya kutanguliza dhana ya umwagaji damu.

Sishauri kumwaga damu, nashauri kuishinikiza serikali kufanya tunayoyataka sisi wananchi maana kwa sasa imeshaonekana wazi kwamba wao ni wezi na hatujasemama sisi ni wao wenyewe wamesemana na kukabana wenyewe. Sasa wasituletee maigizo tunataka uwajibikaji tena kwa wakati sio mambo ya kuambiwa eti JK anamsubiri Asha Migiro ndio afanye mabadiliko, kwani Migiro ndio nani hapa Tanzania? Mtu ashindwe kazi UN ndio tuletewe sisi, Migiro akapumzike na JK afanye mabadiliko ya kweli kwa kuwaweka watu wanaoweza kufanya kazi tuone ufanisi unaotakiwa. Hakuna dharau mbaya kama hii JK aliyoionyesha kwa jambo hili maana ni jambo gumu kwa serikali yake na yeye kasema ni upepo tu unapita kwahiyo msijiuzulu utapita. Nahisi mganga wake anamdanganya na ningetamani nimjue huyo mganga ili tuanze naye kimya kimya, hakuna lisilowezekana.
 
Haiwezekani kabisa mtu ku-post masuala ya Kanumba na Freemason kwenye jukwaa la siasa bali kwa malengo maalum, kwanza kuna tetesi nyingi kwamba haya mawili yanahusiana. Mimi sitaki kuyaongelea haya lakini najaribu kuonyesha ni jinsi gani wanahangaika kupotosha uma wa watanzania ili waache mambo ya msingi wajadili mambo ya kipuuzi yasiyo na tija kabisa na maisha yao.

Hakika JK anaweza kuwa yeye anahusika na haya mambo, haiwezekani tupewe matangazo ya kipuuzi namna hii wakati nchi iko kwenye janga kubwa kama hili. Imefikia mahali wanaiba pesa hadi wanatuambia kama na ninyi mnataka hela nendeni Freemason, nani kawaambia tunataka hela za mashetani? JK ni mwenye dharau kubwa kwa wananchi wake na hili alilosema kwamba ni upepo ataugundua siku si nyingi kwamba ni dhoruba itapokuwa inavuma kwa nguvu kubwa kiasi cha kumfanya asilale wala asisafiri maana ndege itaangushwa na mawimbi makubwa.
 
bwana matusi mheshimiwa matusi lusinde kule arumeru alisema ukiwasikia wana wa tanzania wanapiga kelele ujue c c m imewatia mimba na jumatatu watajifungua PM KWELI jumatatu katupeka kizimbani na nesi wao makinda kasema mafisadi(g8) mawaziri wasijali maana hata wabunge hawakumbuki kile wachokuwa wanasema kwavile hata kanuni za bunge lao hawazijui jeuri hiyo inachangiwa na mtalii wetu maarufu JMK eti HUO NI UPEPO UNAPITA ama kweli hao ndio CCM lakini tumechoka HATA akina gadafi,mubaraka,na yule sijui wa algeri pia walikuwa na viburi lakini leo siwaskii tena sijui wanatawala nchi gani leo
 
bwana matusi mheshimiwa matusi lusinde kule arumeru alisema ukiwasikia wana wa tanzania wanapiga kelele ujue c c m imewatia mimba na jumatatu watajifungua PM KWELI jumatatu katupeka kizimbani na nesi wao makinda kasema mafisadi(g8) mawaziri wasijali maana hata wabunge hawakumbuki kile wachokuwa wanasema kwavile hata kanuni za bunge lao hawazijui jeuri hiyo inachangiwa na mtalii wetu maarufu JMK eti HUO NI UPEPO UNAPITA ama kweli hao ndio CCM lakini tumechoka HATA akina gadafi,mubaraka,na yule sijui wa algeri pia walikuwa na viburi lakini leo siwaskii tena sijui wanatawala nchi gani leo

Tuonane Mnazi mmoja siku ya Ijumaa tarehe 28/04/2012, kama ukiiona ngumu goma kwa kukaa tu nyumbani na usiende popote siku hiyo. Hatufanyi fujo ila tunaamua tu kugomea kila kitu kuishinikiza serikali ifanye mabadiliko yenye tija kwa Taifa letu.
 
Jahazi la Clouds FM lipo hewani na mambo yake sasa hivi, tuwasikilize tuone nao wana nini leo maana Zitto yuko nao leo
 
Hawa Wakuu hawajawa na mazungumzo marefu hapa isipokuwa wameongea kwa ufupi sana, nilichoona Nape amekuwa mpole sana akisema kwamba wabunge wana haki ya kujadili utendaji wa serikali na serikali inatakiwa kusikiliza ila na yeye anafikiri kwamba serikali ina mjadala kwenye kufanya kinachotakiwa.
 
Nahisi hasira za Wadanganyika hazijatosha kabisa, nilihisi zimefikia kiasi cha kufanya jambo lakini kwa hili nimegundua bado kabisa. Nasema hivi kwasababu sikutegemea kabisa kwa ufuska wote huu uliofanywa na Serikali hii kwa rasilimali za Taifa hili na uliosemwa wazi na wabunge JK akalikalia kimya na wananchi wakanyamaza na kubaki tu wakinong'ona huku chini chini tena kwa woga ule wa mwaka 1947.

Kwa uelewa wangu mwepesi kwenye mambo ya siasa nilitegemea mambo kadhaa, kwanza nilitegemea kabisa kwamba kwa hili lazima JK atafanya jambo la kuonyesha kujibu tuhuma nzito zilizotupiwa serikali yake aidha kwa kuwashauri mawaziri wake wajiuzulu kupunguza munkari wa jamii ya Watanzania kwa ujumla wake, au nilitegemea basi bunge lingeonyesha dalili ya kufanyia kazi hoja iliyotarajiwa kupelekwa mezani kwa Spika tangu wiki iliyopita. Lakini ajabu kubwa ni kwamba bunge limeyeyusha na JK katoa msemo ambao kiukweli sijaamini kwamba kautoa yeye au kasingiziwa, eti kasema huo ni "upepo na utapita tuu.." hii ni dharau kubwa kuliko ninazozijua kwakuwa hii imetoka na kusikika, inamaanisha mnajisumbua na hamuwezi kufanya chochote.

Kikubwa kuliko vyote kilichonifanya nione kwamba hasira zetu bado kabisa ni kitendo cha Wadanganyika kukaa kimya pamoja na matusi hayo kutoka kwa JK, ni ajabu kubwa mno hiyo. Niliamini kabisa kwamba kwa misemo hii kutoka kwa JK wakati huu basi ilikuwa imefika wakati Wadanganyika watoke na kudai wanachokitaka maana kiko wazi tayari. Kwani kulikuwa na ugumu gani leo watu wote wakasema hawaendi popote hadi mawaziri watoke, ama hadi bunge liongeze siku na kuamua kumtwangia PM kura ya kutokumwamini? Kama hasira zimetosha basi nahisi kilichobaki ni mobilization, kimsingi tutakuwa resources tunazo kwa maana ya watu na hasira zao. Kinachotakiwa ni kuelekeza hizo resources kwenye kazi fulani kwa manufaa ya Taifa hili.

Something has to be immediately, we have to hit the iron while it's still Hot otherwise JK atathibitisha alilolisema "huu ni upepo na utapita.." We have to instead prove what Sugu said, .."hii ni dhoruba na haitapita hivi hivi, lazima iondoke na sehemu legelege kama sehemu yote".

I'm not suggesting a strike as far as no mobilization for that at the moment, nashauri ingewezekana kesho wote tutulie walau kwa kesho tu tusifanye chochote tuone JK atasema nini kuhusu sisi Wadanganyika kukaa tu kimya maana itambidi kuongea. Kama kuna mwenye plan mbadala tujadiliane, tupate mawazo kutoka pande zote maana hata CCM hili linawakera waziwazi.

We ***** kweli rais wetu makini hawezi fanya maamuzi juu ya porojo urojo za zito kabwela na wenzie kwa ushahidi wa JF!!
 
We ***** kweli rais wetu makini hawezi fanya maamuzi juu ya porojo urojo za zito kabwela na wenzie kwa ushahidi wa JF!!

Ondoka usingizini, ushahidi haupo JF bali unatoka kwa CAG na sio porojo ni ushahidi wa kitaalamu, kaza akili yako kidogo utapata mwanga kwamba tunaongelea nini hapa. Vinginevyo naamini unajua unachofanya na kama ndivyo tayari nishatoa tahadhari kwa watu kama wewe kuukana ujinga wao maana haya yatazigharimu familia zenu, nina hakika itakapokubidi wewe kukimbia mkeo na watoto watapata shida sana maana hawataweza hizo mbio utakazokimbia wewe.
 
Ninyi mods mnaonyesha dalili mbaya kwa kuhamisha hii topic maana suala la Kanumba na Freemason limekaa hapa muda mrefu na hamkulihamisha, dalili mbaya huanza hivi hivi. Kama jukwaa lenu ni ccm semeni mapema tutafute alternative pia, kama sio ccm semeni wazi kama mimi nimevunja sheria popote nielewe la kufanya. Mnatumika kupotosha umma au kwa njia nyingine ninyi ni sehemu ya watanzania waoga, tunahitaji msemo wenu.
 
Back
Top Bottom