Hamis Chaurembo: Dereva mjinga aliyeuwa abiria kwa mwendokasi Kigoma

Sema kuna mda maneno hua yanatimia mimi kuna mwanangu alisemaaga yeye hataki ushahidi siku ya mbanga watu walimtoa vipande vya nyama na beleshi
Siyo kuna mda, bali mara nyingi huwa hivyo. Labda kama hakusema vya kutosha hadi taarifa hiyo izame kwenye subconscious mind. Taarifa yoyote inayoofikia subconscious mind, iwe nzuri au mbaya, kiyakachofuatia ni utekelezaji.

Ikiwa alijiyabiria mabaya, subconscious mind itamuongoza kwenye mazingira ya kuyapata hayo mabaya kwa kiwango "alichotamani".
 
Nimewahi kupanda gari lake huyu jamaa. Nilijitahidi sana kumcontrol kuhusu mwendo. Abiria wenzangu waliishia kunidhihaki tu ati naogopa kufa wakati hukukwepeki. Lakini ilisaidia kwani alipunguza mwendo baada ya kuwa mkali sana.
Uoga nao pia ni akili!
 
Aliyekuwa Dereva na mmiliki wa gari ndogo, Hamis Chaurembo (27) maarufu kama SIMBA ambaye amefariki baada ya kupata ajali mbaya huko Kibondo Kigoma amezikwa jana.

Ila kuna cha kujifunza hapa kutokana na maneno ya baadhi ya marafiki zake.

"Baadhi ya A.K.A alizopambwa nazo ni pamoja na 'Mwendo wa rocket', ndege ya ardhini, Hamisi on fire' Titanic icon' Sukari ya Warembo'

"Alikuwa akitumia dk 20 hadi 25 kutoka Kibondo hadi Kakonko, watu walimpenda kwasababu ya ucheshi wake, alikuwa hana baya yeye anawasha gari hata kama amepata abiria mmoja.

"Ahadi aliyojiahidi imetimia, katika kauli zake aliwahi kusema

"Siku nikipata ajali ni lazima niondoke na abiria wote".
TITANIC ICON 😊
 
Mkuu asante kwa hii post japo ni ya kusikitisha sana. Na jamii nayo ina makosa. Walikuwa wanampamba na majina badala ya kuchukuwa hatua ikiwemo kususia gari lake.
Kama ambavyo wanazipamba Sauli, katarama na Newforce huku vyombo vya dola vipo jamaa wanapokea tu bukubuku alafu siku ikitokea ya kutokea wanaanza kujiliza. Mapumbavu kabisa haya matanzania. Mi hata nikiwa naumwa sipandi hizo gari.
 
Siyo kuna mda, bali mara nyingi huwa hivyo. Labda kama hakusema vya kutosha hadi taarifa hiyo izame kwenye subconscious mind. Taarifa yoyote inayoofikia subconscious mind, iwe nzuri au mbaya, kiyakachofuatia ni utekelezaji.

Ikiwa alijiyabiria mabaya, subconscious mind itamuongoza kwenye mazingira ya kuyapata hayo mabaya kwa kiwango "alichotamani".
Wacha blah blah na hizo subconscious na uongo mwingine. Maneno na Roho "Yohana 6:63" kwani pia Mungu aliumba kwa Neno hivyo unatakiwa uwe makini na nini unazungumza.😅😆😁😄😃
 
Mamlaka husika za mkoa wa kigoma ziangalie pia zile Toyota wish za kasulu kutokea mwembe togwa. Kuna siku tutaongea mengine kwenye jukwaa hilihili, polisi wetu wasipagawe sana na zile buku tatu tatu za madereva wa wish na probox.

Alafu unakuta probox inabeba abiria 15, yaani mbele kwa dereva mnakaa wanne hatari sana.
 
Miaka ya 2000 Mwanzoni, Urambo Tabora, kuna jamaa alikuwa akiendesha gari ya Halmashauri, mkonga. Alikuwa na mwendo usio wa kawaida. Alikuwa akisema siku mkisikia nimepata ajali, basi mtenge tu msiba.

Na kweli, ajali iliyomkuta, humtazami mara mbili. Alikua akiitwa Chonza kama sijamsahau jina.

Kuna wengine ni wagonjwa wa akili na wana leseni za udereva.
Wee chonza kumbe alishafariki? Yule alikuwa anaishi block Q? Baba khalid?
 
Hua inabeba mpaka 15 chief nimeshuhudia kwa macho yangu, kwenye buti kule ndio inakula nyomi ya kufa mtu.
Pale mbele was dereva wa4, kati wa4 Mpaka wa5 inategemea na unene wa abiria kule nyuma wanakaa 6-8 ... .noma sana nilipandaga Moja kutoka kyabaari kwenda Butiama aseee... Vifo vingine Mungu anasingiziwa.
 
Back
Top Bottom