Hamis Chaurembo: Dereva mjinga aliyeuwa abiria kwa mwendokasi Kigoma

Kuna siku natokea Dodoma niko kwenye speed ya 120km/Hr ikatokea V8 ikani-ovetake. Si nikasema nile nayo ligi, kufika speed ya 160km/Hr nikasema hivi nikipata ajali kwa mwendo huu kweli nitapona?

I later slow down to 80km/Hr nikaiacha V8 ikipotea machoni kwangu

Kusema kweli Ajali nyingi huchangiwa na Mwendokasi

Mwendokasi unaua....

Poleni kwa misiba
Tatizo sio mwendo kasi bali mwendo kasi kwenye nchi gani na barabara gani.Nchi zetu miundombinu bado ni changamoto,unakuta barabara ni highway ila ina viraka na mashimo kama chandarua uku watumiaji wengine wa barabara nao wamejiachia bila kujali chochote.
 
Tatizo sio mwendo kasi bali mwendo kasi kwenye nchi gani na barabara gani.Nchi zetu miundombinu bado ni changamoto,unakuta barabara ni highway ila ina viraka na mashimo kama chandarua uku watumiaji wengine wa barabara nao wamejiachia bila kujali chochote.
Umesema sahihi Mkuu, barabara zote zingekuwa walau kama hicho kipande cha Kimara mwisho hadi Kibaha ingekuwa nzuri zaidi, maana unakuwa unaendesha bila kuwa na wasiwasi wa ubovu wa barabara.

Kama Nchi tuna safari ndefu sana kwenye upande wa miundombinu.

Kwa kweli JPM atazidi kukumbukwa kwenye hili eneo.
 
Kiukweli ndo maana Safari za misafara sizitaki, ukiongozana na mtu anapepea nawe utatamani kupepea
Sahihi Mkuu, yaani unakaa unasema hivi kwanini nisifike walau speed 160km/hr ukifika speed hiyo unasema kwanini nisimalize kabisa dashboard 😜

Kuja kutahamaki watu wanaimba parapanda italia 😭
 
Tatizo sio mwendo kasi bali mwendo kasi kwenye nchi gani na barabara gani.Nchi zetu miundombinu bado ni changamoto,unakuta barabara ni highway ila ina viraka na mashimo kama chandarua uku watumiaji wengine wa barabara nao wamejiachia bila kujali chochote.
Bongo kama huna chuma kizito barabarani achana na spidi, spidi ni yawatu wazito wenye vyuma vizito
 
Aliyekuwa Dereva na mmiliki wa gari ndogo, Hamis Chaurembo (27) maarufu kama SIMBA ambaye amefariki baada ya kupata ajali mbaya huko Kibondo Kigoma amezikwa jana.

Ila kuna cha kujifunza hapa kutokana na maneno ya baadhi ya marafiki zake.

"Baadhi ya A.K.A alizopambwa nazo ni pamoja na 'Mwendo wa rocket', ndege ya ardhini, Hamisi on fire' Titanic icon' Sukari ya Warembo'

"Alikuwa akitumia dk 20 hadi 25 kutoka Kibondo hadi Kakonko, watu walimpenda kwasababu ya ucheshi wake, alikuwa hana baya yeye anawasha gari hata kama amepata abiria mmoja.

"Ahadi aliyojiahidi imetimia, katika kauli zake aliwahi kusema

"Siku nikipata ajali ni lazima niondoke na abiria wote".
Madereva wa Probox akili zao zinafurahisha sana. Tazama huyu anavyoendesha

View: https://youtu.be/Kp-IqS9N1AI?si=RJ2O3TMRBgw3xaFR
 
Kibondo - Kakonko kuna kilometers 43. Kwa probox ikitembea kwa kilometers 100 kwa saa constantly, itatumia dakika 25 plus au minus.
Kabla ya kuweka lami barabara hiyo bado iliruhusu vijana wa probox kuchezea kwenye mia na zaidi. Hivi imewekwa lami tutegemee vilio zaidi hasa Hiace na Probox za Kibondo - Kasulu.
 
Sio kweli…kutoka Kigoma mjini Kibondo unafika around saa 5 na Kakonko around 6 na nusu mchana ukiwa unaelekea Mwanza kwa basi
Ukitokea kigoma au kasulu unaingia kakonko kwanza ndio kibondo ukiwa unaelekea mwanza
 
Sio kweli…kutoka Kigoma mjini Kibondo unafika around saa 5 na Kakonko around 6 na nusu mchana ukiwa unaelekea Mwanza kwa basi
Ukitokea kigoma au kasulu unaingia kakonko kwanza ndio kibondo ukiwa unaelekea mwanz
 
Aiseee Khamis alikuwa shemeji angu duuuuh kiukweli tulikuwa tukimwambia sana juu ya mwendo ona sasa dada angu kabaki mjane ila yote kwa yote marehemu hasemwi vibaya.
 
Back
Top Bottom