Hamad Rashid kujitoa CUF leo?

Hako kajamaa kana uchu wa madaraka nakenyewe.. Wanasiasa wetu bwana matumbo yao kwanza watz badaye
 
Ajitoe CUF kwani bado mwanachama wao? si walishamvua uanachama siku nyingi huyu au kuna Hamad mwingine?
 
Saa 4 haijafika? Mbona hakuna habari au jamaa ameingia mitini?
 
Hamad Rashid: CUF ijitoe serikali ya mseto

na Asha Bani


MBUNGE wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), amelaani matumizi ya nguvu za Jeshi la Polisi wakati wa chaguzi mbalimbali huku akikishauri chama chake kujiondoa katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa baina yao na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana na kutowasaidia wananchi.
Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu, Hamad alisema kuwa ameshangazwa na nguvu kubwa ya Jeshi la Polisi iliyotumika katika uchaguzi mdogo wa Bububu uliomalizika hivi karibuni na hivyo kusababisha kujeruhi wananchi bila sababu.
Alisema CUF iliingia katika serikali ya mseto kwa lengo la kuweka uhuru na haki lakini wameshindwa kufikia azima hiyo na kwamba ikiwa muafaka huo ni kwa maslahi ya watu wachache basi wajitoe.
“Mimi nashangaa sana hayo mazungumzo sijui yalikuwa ya nini na ‘ndoa’ ilikuwa ya nini kama ilikuwa ni kwa masilahi ya watu wachache huku wananchi hawanufaiki nayo, wanapigwa risasi, basi CUF wajiondoe kama si kwa masilahi ya wananchi wote,” alisema Hamad.
Hata hivyo, Hamad alisema Serikali ya Zanzibar inaundwa na vyama viwili, hivyo ni dhahiri kwamba CCM na CUF ndio wametumia nguvu katika kuvikandamiza na kuhujumu vyama vidogo vya siasa ambavyo havikuwa na serikali.
Katika uchaguzi huo wa Jumapili ambao CCM iliibuka kidedea ikifuatiwa na CUF na Chama kipya cha ADC, vurugu kubwa zilizuka huku matokeo hayo yakipingwa vikali.
Hapo kwenye red tu kapigilia msumari,sasa wanaposimama wakina mtatiro na vibaraka wenzake pale jangwani kukanusha inakuwaje hapa?Asante amadi kwa kuanza kudai talaka...
 
Mashauri yanayopelekwa mahakamani kama hili la Hamad kupinga kuvuliwa ubunge yangekuwa yanaamuliwa haraka sana. Sioni uhalali wa Hamad kuendelea na ubunge ilhali si mwanachama wa chama chochote eti tu kwa sababu shauri lake halijaamuliwa na mahakama. It is costly to the taxpayer.
 
Ina maana mpaka sasa haijajulikana press conference ilikuwa ni ya nini..? No updates zozote..?
 
Hapo kwenye red tu kapigilia msumari,sasa wanaposimama wakina mtatiro na vibaraka wenzake pale jangwani kukanusha inakuwaje hapa?Asante amadi kwa kuanza kudai talaka...
CDM ilikataa ushirika na CUF bungeni kwa kuwa CUF ilikuwa na ushirika na CCM serikalini Zanzibar. Unakumbuka mashambulizi ya huyu Rashid kwa Mbowe na kambi nzima ya upinzani bungeni? Do not trust this crook. Hata yeye yupo kwa maslahi ya tumbo lake tu.
 
CDM ilikataa ushirika na CUF bungeni kwa kuwa CUF ilikuwa na ushirika na CCM serikalini Zanzibar. Unakumbuka mashambulizi ya huyu Rashid kwa Mbowe na kambi nzima ya upinzani bungeni? Do not trust this crook. Hata yeye yupo kwa maslahi ya tumbo lake tu.
Kweli mkuu huyu jamaa ni mnafiki wa kutupwa,alipovuliwa kiongozi wa upinzani bungeni aliongea sana na kutaka kuleta kanuni zake za kiajabu ajabu huku akijua atasaidiwa na mumewe gamba....
 
Kuna waislamu wajanja


Kila siku zinavozidi kwenda mbele ndio tunazidi kurudi nyuma badala ya kupiga hatua katika kuchangia hoja.Hoja iliyopo hapa ni ya Hamad Rashid na hakuna kilichoongelewa dini ya aina yoyote ile,sasa imekuaje kuanzisha hoja ya uisilamu badala hoja iliyokusudiwa.Halafu baadae useme waisilamu wakorofi kwasababu wamejibu kwa jazba?Come on people kama unahisi huna hoja ni bora unyamaze kuliko kuchafua hali ya hewa.Watanzania wanachafuliwa na watu wachache wasio na hoja zenye muelekeo mzuri.
 
Back
Top Bottom