Taifa Digital Forum
Member
- Jun 4, 2022
- 68
- 184
Jeshi la Polisi wilaya ya Kibiti limemkamata Rashid Mkinga (36) kwa tuhuma za kutengeneza Vyeti feki vya kuzaliwa. Tukio hilo lililotokea Januari 15, 2024 majira ya saa 1 usiku katika Kitongoji cha Kibiti B, Kata na Wilaya ya Kibiti Mkoani Pwani.
Katika mahojiano ya awali yaliyofanywa na Jeshi la Polisi, Mkinga amekiri kuhusika na vitendo hivyo kwa kushirikiana na Dkt. Abdul Salim Msemo (53) mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Idara ya Afya ambaye pia amekamatwa na Vyombo vya Dola.
Watuhumiwa hao wamekutwa na Kompyuta tatu (03) zilizokuwa na nakala za Vyeti vya Kuzaliwa na Taaluma za watu mbalimbali, Bima za Afya 15 zenye taarifa zinazotofautiana, Vyeti vya Ndoa na Vyeti vya Kuzaliwa.
Mkinga anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Ikwiriri kilichopo Rufiji na muda wowote yeye na mwenzake watafikishwa Mahakamani baada ya taratibu za kisheria kukamilika.
Katika mahojiano ya awali yaliyofanywa na Jeshi la Polisi, Mkinga amekiri kuhusika na vitendo hivyo kwa kushirikiana na Dkt. Abdul Salim Msemo (53) mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Idara ya Afya ambaye pia amekamatwa na Vyombo vya Dola.
Watuhumiwa hao wamekutwa na Kompyuta tatu (03) zilizokuwa na nakala za Vyeti vya Kuzaliwa na Taaluma za watu mbalimbali, Bima za Afya 15 zenye taarifa zinazotofautiana, Vyeti vya Ndoa na Vyeti vya Kuzaliwa.
Mkinga anashikiliwa katika Kituo cha Polisi Ikwiriri kilichopo Rufiji na muda wowote yeye na mwenzake watafikishwa Mahakamani baada ya taratibu za kisheria kukamilika.