Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid, amesema maneno yanayotolewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa CUF ni CCM B. ni ujanja unaotumika kuwahadaa wananchi, ili wasitambue uswaiba wa Chadema na CCM.
Alisema Chadema ni chama chenye uswaiba mkubwa na CCM na kwamba, kimekuwa kikipewa fedha na makada wa chama tawala, ndio kimbilio la vigogo wanapohama chama tawala, Alibainisha hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa oporesheni kitaifa ya Zinduka, awamu ya pili itakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa Cuf kuwaeleza wananchi kuhusu mustakabali wa taifa hili.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Tangamano na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wa watu. mbunge huyo alisema kauli iliyoanza kutolewa hivi karibuni kuwa CUF ni CCM "B" ni njama ya vyama hivyo viwili yaani Chadema na CCM kuwahadaa kwa makusudi wananchi wasijue kuhusu uswahiba uliopo baina vyama hivyo. alisema Chadema ina uhusiano wa karibu na CCM kwani ni chama pekee cha upinzani kinachoungwa mkono na baadhi ya vigogo wa waliopo madarakani. katika Serikali ya CCM na hata waliostaafu, Chadema inaangaliwa kwa jicho la karibu na CCM sababu imeandaliwa kwa ajili ya wabunge au vigogo wa CCM kuhamia, nadhani wenyewe mnashuhudia hakuna kigogo anayehama CCM na kuthubutu kuja CUF kwa kuwa wanao tuna msimamo usiokuwa wa kuyumba. alisema Hamad Rashid.
Source Mwananchi Machi 24, 2011
Alisema Chadema ni chama chenye uswaiba mkubwa na CCM na kwamba, kimekuwa kikipewa fedha na makada wa chama tawala, ndio kimbilio la vigogo wanapohama chama tawala, Alibainisha hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa oporesheni kitaifa ya Zinduka, awamu ya pili itakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa Cuf kuwaeleza wananchi kuhusu mustakabali wa taifa hili.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Tangamano na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wa watu. mbunge huyo alisema kauli iliyoanza kutolewa hivi karibuni kuwa CUF ni CCM "B" ni njama ya vyama hivyo viwili yaani Chadema na CCM kuwahadaa kwa makusudi wananchi wasijue kuhusu uswahiba uliopo baina vyama hivyo. alisema Chadema ina uhusiano wa karibu na CCM kwani ni chama pekee cha upinzani kinachoungwa mkono na baadhi ya vigogo wa waliopo madarakani. katika Serikali ya CCM na hata waliostaafu, Chadema inaangaliwa kwa jicho la karibu na CCM sababu imeandaliwa kwa ajili ya wabunge au vigogo wa CCM kuhamia, nadhani wenyewe mnashuhudia hakuna kigogo anayehama CCM na kuthubutu kuja CUF kwa kuwa wanao tuna msimamo usiokuwa wa kuyumba. alisema Hamad Rashid.
Source Mwananchi Machi 24, 2011