Hamad Rashid: CHADEMA ni chaka la wanaokimbia CCM

Mshume Kiyate

JF-Expert Member
Feb 27, 2011
6,766
894
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid, amesema maneno yanayotolewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa CUF ni CCM B. ni ujanja unaotumika kuwahadaa wananchi, ili wasitambue uswaiba wa Chadema na CCM.
Alisema Chadema ni chama chenye uswaiba mkubwa na CCM na kwamba, kimekuwa kikipewa fedha na makada wa chama tawala, ndio kimbilio la vigogo wanapohama chama tawala, Alibainisha hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa oporesheni kitaifa ya Zinduka, awamu ya pili itakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa Cuf kuwaeleza wananchi kuhusu mustakabali wa taifa hili.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Tangamano na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wa watu. mbunge huyo alisema kauli iliyoanza kutolewa hivi karibuni kuwa CUF ni CCM "B" ni njama ya vyama hivyo viwili yaani Chadema na CCM kuwahadaa kwa makusudi wananchi wasijue kuhusu uswahiba uliopo baina vyama hivyo. alisema Chadema ina uhusiano wa karibu na CCM kwani ni chama pekee cha upinzani kinachoungwa mkono na baadhi ya vigogo wa waliopo madarakani. katika Serikali ya CCM na hata waliostaafu, Chadema inaangaliwa kwa jicho la karibu na CCM sababu imeandaliwa kwa ajili ya wabunge au vigogo wa CCM kuhamia, nadhani wenyewe mnashuhudia hakuna kigogo anayehama CCM na kuthubutu kuja CUF kwa kuwa wanao tuna msimamo usiokuwa wa kuyumba. alisema Hamad Rashid.
Source Mwananchi Machi 24, 2011
 
Sema sema sema mheshimiwa ni la mwiisho Chadema ni chama cha Kikanda, kikabila na Kidini zaidi.
 
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid, amesema maneno yanayotolewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa CUF ni CCM B. ni ujanja unaotumika kuwahadaa wananchi, ili wasitambue uswaiba wa Chadema na CCM.
Alisema Chadema ni chama chenye uswaiba mkubwa na CCM na kwamba, kimekuwa kikipewa fedha na makada wa chama tawala, ndio kimbilio la vigogo wanapohama chama tawala, Alibainisha hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa oporesheni kitaifa ya Zinduka, awamu ya pili itakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa Cuf kuwaeleza wananchi kuhusu mustakabali wa taifa hili.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Tangamano na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wa watu. mbunge huyo alisema kauli iliyoanza kutolewa hivi karibuni kuwa CUF ni CCM "B" ni njama ya vyama hivyo viwili yaani Chadema na CCM kuwahadaa kwa makusudi wananchi wasijue kuhusu uswahiba uliopo baina vyama hivyo. alisema Chadema ina uhusiano wa karibu na CCM kwani ni chama pekee cha upinzani kinachoungwa mkono na baadhi ya vigogo wa waliopo madarakani. katika Serikali ya CCM na hata waliostaafu, Chadema inaangaliwa kwa jicho la karibu na CCM sababu imeandaliwa kwa ajili ya wabunge au vigogo wa CCM kuhamia, nadhani wenyewe mnashuhudia hakuna kigogo anayehama CCM na kuthubutu kuja CUF kwa kuwa wanao tuna msimamo usiokuwa wa kuyumba. alisema Hamad Rashid.
Source Mwananchi Machi 24, 2011

kufirisika ki fikra na kisiasa!! CDM ni chama makini kinachovutia wananchi wengi hata kutoka ndani ya vyama vingine mbalimbali ccm/cuf vikiwemo kwa sababu ya kusimamia ukweli na kupinga ufisadi kwa dhati. Kina historia njema machoni mwa watanzania,na ni chama mbadala kuwavusha watanzania katika changamoto za leo baada ya ccm kushindwa.
 
hivi huyu mchangiaji namba mbili amekaa kama jina lake la pili kama litaongezewa helufi 'u' na kusomeka hafifu, shame to him.
 
JAMANI mwacheni mh.Rashid alonge kwani siku hizi bila kuisema CDM hujawa maarufu.CDM ni mti wa maembe siku hizi kila mwnasiasa anataka kuangua apate tunda kwa afya yake.Rusha jiwe Mh.Rashid wakusikie, mwenyekiti wako Prof.Pumba ndiyo zake siku hizi kabla hajalala lazima atamke CDM.PEOPLESSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS
 
Nimeipenda sana hii kweli CUF wamekomaa Kisiasa. CDM ni chama cha maigizo na chama cha watu wanaotaka kupanda kwa haraka, chaka la watu wanaotetea matumbo yao wakiona wamekosa vyama vingine au umaarufu wao umeondoka kwenye vyama vyao wanakimbilia chadema, mifano mingi. Lwakatare wa CUF, SHIBUDA CCM, na wengine wengi.

Sio wapinzani wakweli ila wanamaslahi, NDO maana siasa za wana CDm wakongwe ziko tofauti angalia Mheshimiwa Mwenyekiti wa kamati ya Nishati (ZITTO) great!!!!!!!!!!
 
Sema sema sema mheshimiwa ni la mwiisho Chadema ni chama cha Kikanda, kikabila na Kidini zaidi.

SIONI AJABU kwa kauli yako: Mulianza na ukabila/ukanda-watanzania wakawajibu "NO", na CDM ikawa nchi nzima (siyo km cuf ambayo kimsingi ni pemba (kidogo unguja). Mkaja na hoja ya udini, watanzania wakawajibu tena "NO" baada ya CDM kuwa na wanachama wa dini na madhehebu mbalimbali na wasio na dini kila mkoa (lakini cuf ndo cha udini maana almost 99.9% ni islams). Mkasema ni chama cha vurugu/uchochezi na umwagaji damu, watanzania kwa mara nyingine wakawaambia "NO:, wakafanya maandamano ya kisiasa kwa misingi ya sheria za nchi ktk mikoa 4 ya kanda ya ziwa maelfu kwa maelfu bila hata kupigana makofi. Kwa sasa mumeanza na kuwa CDM kinasaidiwa na mataifa ya nje kifedha kuchochea vurugu, nchi za nje nazo zimewajibu "NO" na kwamba waziri Simba alete uthibitisho-ambao naye jana kakanusha kuwa hakusema hayo ilihali aliyasema mchana kweupe. Great thinker huwa hafuati upepo husema ukweli; hivyo nakushauri ndugu yangu uwe mkweli badala ya kufuata propodanga za cuf (ccm B), uhusiano ambao hawawezi kujitoa machoni mwa watanzania kwa sasa!!! CDM kwa sasa kiko imara na kukipiga madogo ya ushabiki ni kujidhalilisha mwenyewe machoni mwa watanzania-think!!!
 
Hamad kwisha kazi!ww ulitaka waende wapi?CUF na Ccm mmeungana,kilichoko cuf ndicho kilichoko ccm,pia wanaangalia chama kipi kinapendwa na wtanzania,kip kinalengo la dhati la kumkomboa mTz,kipi kiko angalao 90% ya tz.uende cuf kiko 0.005% ya tz ili iweje?mwisho nimtie moyo kuwa kigogo wa ccm anayetoka pemba pekee ndiye anaweza kujiunga cuf.lakini wengine wote People' Power!
 
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid, amesema maneno yanayotolewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa CUF ni CCM B. ni ujanja unaotumika kuwahadaa wananchi, ili wasitambue uswaiba wa Chadema na CCM.
Alisema Chadema ni chama chenye uswaiba mkubwa na CCM na kwamba, kimekuwa kikipewa fedha na makada wa chama tawala, ndio kimbilio la vigogo wanapohama chama tawala, Alibainisha hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa oporesheni kitaifa ya Zinduka, awamu ya pili itakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa Cuf kuwaeleza wananchi kuhusu mustakabali wa taifa hili.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Tangamano na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wa watu. mbunge huyo alisema kauli iliyoanza kutolewa hivi karibuni kuwa CUF ni CCM "B" ni njama ya vyama hivyo viwili yaani Chadema na CCM kuwahadaa kwa makusudi wananchi wasijue kuhusu uswahiba uliopo baina vyama hivyo. alisema Chadema ina uhusiano wa karibu na CCM kwani ni chama pekee cha upinzani kinachoungwa mkono na baadhi ya vigogo wa waliopo madarakani. katika Serikali ya CCM na hata waliostaafu, Chadema inaangaliwa kwa jicho la karibu na CCM sababu imeandaliwa kwa ajili ya wabunge au vigogo wa CCM kuhamia, nadhani wenyewe mnashuhudia hakuna kigogo anayehama CCM na kuthubutu kuja CUF kwa kuwa wanao tuna msimamo usiokuwa wa kuyumba. alisema Hamad Rashid.
Source Mwananchi Machi 24, 2011

hadisi adisi......................!!

mfa maji.............................??
 
Hao Viongozi wote wa CUF walitoka Wapi? hata yeye alikuwa Mshauri wa Rais Mwinyi wakati huo haupati madaraka hayo kama wewe sio CCM
 
hivi huyu mchangiaji namba mbili amekaa kama jina lake la pili kama litaongezewa helufi 'u' na kusomeka hafifu, shame to him.

Huwezi kulificha Pembe la ng'ombe. Udini na Ukanda unawamaliza. japo mnaliangalia kwa jicho la kengeza
 
JAMANI mwacheni mh.Rashid alonge kwani siku hizi bila kuisema CDM hujawa maarufu.CDM ni mti wa maembe siku hizi kila mwnasiasa anataka kuangua apate tunda kwa afya yake.Rusha jiwe Mh.Rashid wakusikie, mwenyekiti wako Prof.Pumba ndiyo zake siku hizi kabla hajalala lazima atamke CDM.PEOPLESSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSSS


Thanx.
 
Umaarufu haupatikani bila kuitaja cdm. Hata JK anajua hilo
 
Hamad Rashid amegeuka kuwa mropokaji baada ya kukosa nafasi ya kuwa mkuu wa kambi ya upinzani. Ataropoka mengi; msikilizeni tu maana roho yake inauuma kweli kweli siyo mchezo. Pole yakhe; hii Tanganyika siyo kisiwa.
 
Nimeipenda sana hii kweli CUF wamekomaa Kisiasa. CDM ni chama cha maigizo na chama cha watu wanaotaka kupanda kwa haraka, chaka la watu wanaotetea matumbo yao wakiona wamekosa vyama vingine au umaarufu wao umeondoka kwenye vyama vyao wanakimbilia chadema, mifano mingi. Lwakatare wa CUF, SHIBUDA CCM, na wengine wengi......

Umesahau kubwa lao mtaalam wa kukurupuka .. DR Silaha.
 
hilo nalo neno, ongezea mkuu kuwa hata kura zote bungeni za CUF zinaenda CCm dhidi ya CDM sasa sijui mshirika wa CCM ni yupi.
Hao Viongozi wote wa CUF walitoka Wapi? hata yeye alikuwa Mshauri wa Rais Mwinyi wakati huo haupati madaraka hayo kama wewe sio CCM
 
Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid, amesema maneno yanayotolewa na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa CUF ni CCM B. ni ujanja unaotumika kuwahadaa wananchi, ili wasitambue uswaiba wa Chadema na CCM.
Alisema Chadema ni chama chenye uswaiba mkubwa na CCM na kwamba, kimekuwa kikipewa fedha na makada wa chama tawala, ndio kimbilio la vigogo wanapohama chama tawala, Alibainisha hayo juzi alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa oporesheni kitaifa ya Zinduka, awamu ya pili itakayoendeshwa nchi nzima kwa viongozi wa Cuf kuwaeleza wananchi kuhusu mustakabali wa taifa hili.
Katika mkutano huo ulifanyika katika Uwanja wa Tangamano na kuhudhuriwa na Umati mkubwa wa watu. mbunge huyo alisema kauli iliyoanza kutolewa hivi karibuni kuwa CUF ni CCM "B" ni njama ya vyama hivyo viwili yaani Chadema na CCM kuwahadaa kwa makusudi wananchi wasijue kuhusu uswahiba uliopo baina vyama hivyo. alisema Chadema ina uhusiano wa karibu na CCM kwani ni chama pekee cha upinzani kinachoungwa mkono na baadhi ya vigogo wa waliopo madarakani. katika Serikali ya CCM na hata waliostaafu, Chadema inaangaliwa kwa jicho la karibu na CCM sababu imeandaliwa kwa ajili ya wabunge au vigogo wa CCM kuhamia, nadhani wenyewe mnashuhudia hakuna kigogo anayehama CCM na kuthubutu kuja CUF kwa kuwa wanao tuna msimamo usiokuwa wa kuyumba. alisema Hamad Rashid.
Source Mwananchi Machi 24, 2011


Hivi hakuna sheria ya kuwa-recall wabunge?? Maana takataka kama hizi hazifai kuwakilisha wananchi. I like sheria za RSA zilizomtoa Mbeki madarakani!!
 
Kwa sasa, ndg zangu wana CUF ni vema mkafikiri jinsi ya kuwahamasisha watanzania ili wakipende chama chenu, bila hivyo yangu macho, siku si nyingi CUF kitapotea machoni mwa watanzania. Mlidhani kujiunga na CCM mtakuwa salama, hakika hapo mlicheza bahati na sibu, tunaelewa kuwa Chatu hata akishiba ustarabu wake ni wa muda mfupi tu. Subiri mumuone chatu huyo kama atawasalimisha.Kale kamchezo ka baba na mama naona hamkajui, time it will tell you.
 
Back
Top Bottom