BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
| ||
|
| ||
|
Tunawashukuru viongozi wetu hawa kwa kuliona hilo. Hakuna sababu yoyote ya watu kuacha kufanya shughuli za maendeleo na badala ya kupaka wengine matope na kuponda kila ljambo jema ifanywalo na serikali.
Hali ya nchi yawatisha maaskofu
• Wakiri viongozi kuwatelekeza wananchi
na Datus Boniface
Tanzania Daima
MAASKOFU wakuu wawili wa makani ya Anglikana na Kilutheri Tanzania, wameonyesha huzuni na wasiwasi wao juu ya mwelekeo mzima wa taifa kutokana na mambo ya kusikitisha na kutikisa nchi kwa sasa.
Akizungumza jana katika ibada ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Kanisa la Usharika wa Kinondoni jijini Dar es Salaam, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Alex Malasusa, alisema taifa linaelekea kubaya kutokana na baadhi ya watu kuwa tayari hata kuua wenzao kwa ajili ya mali na madaraka.
Alisema kuwa hali imekuwa mbaya zaidi baada ya kujitokeza kundi la baadhi ya viongozi waliopewa dhamana ya uongozi kutowajali kabisa wananchi na kuwatumikia kama walivyoahidi na kuaminiwa wakati wakitafuta nafasi za uongozi.
Dk. Malasusa alionyesha kusikitishwa kwake na hatua aliyoiita ya kuchafuana majina na heshima kwa baadhi ya viongozi ili mmoja aonekana msafi katika jamii badala ya kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi.
Katika hilo, Malasusa alikemea vikali waumini wa Kikristo wanaoshiriki katika matendo maovu yakiwemo ya kutowatumikia watu ipasavyo na kuongeza kuwa hatanyamaza kuwakemea hadi watakapobadilika na hivyo kuiokoa nchi na janga la maangamizi.
Alisema ni wajibu wa Wakristo wenye dhamana ya madaraka kuiga mfano wa Akida aliyejitoa kumsaidia mfanyakazi wake aponywe na Yesu. Alisema kwa jinsi hali ya taifa ilivyo, ni wajibu wa viongozi wa Kikristo wenye madaraka kuiga mfano wake na kuwatumikia wananchi.
"Akida ni mfano wa mtu mwenye cheo ambaye alidiriki kujitoa kwa ajili ya kumsaidia mfanyakazi wake aponywe na Yesu, kwa jinsi taifa lilivyo leo ni jambo gumu kwao kuwajali wengine (wananchi)," alisema.
Kwa upande wake, Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dk Valentino Mokiwa, amesema ana huzuni kubwa kutokana na taifa kukabiliwa na mambo mazito likiwemo suala la ukosefu wa umeme, wakati huu taifa linapotimiza miaka 50 ya uhuru wake.
Akizungumza katika ibada ya harambee ya ujenzi wa mabweni ya Shule ya Sekondari ya Askofu Mkuu John Sepeku, Buza jijini Dar es Salaam jana, Mokiwa alisema hali ya taifa inaleta hofu kwa vile suala zima la umeme limeleta mtikisiko mkubwa kwa uchumi wa taifa.
Akizungumzia juu ya maendeleo ya elimu nchini, kanisa hilo limeitaka serikali kurudisha shule zote za dini ilizozitaifisha kabla ya Azimio la Arusha, ili zisaidie kuleta maendeleo ya elimu nchini.
Askofu Mkuu Mokiwa aliongeza kuwa serikali ilitumia nguvu kuchukua shule za dini zikiwemo zile za Kikristo na Kiislamu na sasa umefika wakati wa kuzirudisha kwa wamiliki wa mwanzo kwa vile kuna shule za serikali.
Askofu huyo alienda mbali zaidi na kusema kuwa kitendo kilichofanywa na Serikali wakati huo ingekuwa nchi za nje wangepelekana mahakamani, lakini kwa kuwa Tanzania ni nchi ya watu wapenda amani, wameamua kutumia busara kuzidai.
Askofu Mokiwa alisema Kanisa la Anglikana ndilo lililokuwa na shule nyingi ukilinganisha na madhehebu mengine na zilipokea wanafunzi bila kujali ni wa dhehebu gani.
Alizitaja shule hizo kuwa ni pamoja Sekondari za Minaki, Chidya, Loleza, Mazengo na Chuo cha Ualimu Korogwe na Ndwika. Aidha, kulikuwa na Hospitali za Mkomainda, Hospitali Teule ya Muheza na ile ya Mvumi Mission.
Alisema kutokana na kupokwa shule hizo dayosisi hiyo mpaka sasa hivi ina shule mbili tu ikiwemo Shule ya Msingi ya Mtakatifu Augustino ambayo inafundisha masomo yake kwa lugha ya Kingereza na shule hiyo ya Sekondari ya Askofu Mkuu John Sepeku ambayo ina kidato cha kwanza hadi cha nne.
Hata hivyo alisema kurudishwa kwa shule hizo kwenye taasisi za dini ikiwemo zile zilizokuwa zikimilikiwa na dini ya Kiislaam, zitasaidia kuleta changamoto kwa shule za Serikali kutoa elimu iliyo bora tofauti na sasa.
Naye Waziri Mkuu aliyejiuzulu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowasa, aliyekuwa mgeni rasmi katika harambee hiyo, alizitaka taasisi za dini kuwekeza katika vyuo vya ufundi.
Lowasa alisema watu wengi wanakimbilia kuwekeza katika shule za sekondari na kusahau kwamba kuna wale ambao wakimaliza kidato cha nne hawana pa kwenda ambapo vyuo kama hivyo vingekuwa ni kimbilio lao.
"Jamani vyuo vya ufundi ni muhimu sana kwa sasa, kwani takwimu zinaonyesha kuwa vijana wengi wameishia kidato cha nne na wanazurura mitaani, lakini hawa wangepelekwa katika vyuo vya ufundi, ni wazi kwamba tungezalisha ajira nyingi," alisema.
Lowasa alirudia usemi wake kuwa tatizo kubwa la ajira kwa vijana hapa nchini ni bomu ambalo linaweza kulipuka siku yoyote na kuifikisha nchi pabaya iwapo juhudi za makusudi zisipochukuliwa kukabiliana na janga hilo.
Katika harambee hiyo, Lowassa na rafiki zake walichangia jumla ya shilingi milioni 20. Aidha alishiriki kuendesha mnada ulioweza kukusanya jumla ya shilingi milioni 126.941 kati ya hizo milioni 60 zikiwa taslimu na zilizobaki zikiwa ni ahadi.
Ndugu yangu naomba nikusaidie kidogo kufikiri, hawa tunaowaita wanasiasa pia ni wa madhehebu ya kikristo, kiisilamu na hata wasio na dini pia, mathalani ww ni mkristo, kukicha wanakuandika kwa ufisadi (kweli/uongo), mchungaji akikemea utasema anafanya ama anataka kuwa mwanasiasa hapo, hivyo tuache wanasiasa wafanye watakavyo? wachungaji na/ama mashehe nao wanahaki kikatiba kwa sababu ni watanzania kuchagua/kuchaguliwa ktk nafasi za uongozi wa nchi hii, na kujadili pia. MNAPOAMINISHWA NA WENYE DHAMANA KWAMBA VIONGOZI WA DINI WASIONGELEE SIASA MJIONGEZE KUFIKIRI, OTHERWISE KICHWA CHA NINI SASA KAMA HUWEZI KUKITUMIA KUFIKIRI SI HERI UBAKI NA SHINGO PEKEEHawa mapadri na mashehe siasa wanaitakia nini? Wao wana yao na yanawashinda. Sikuhizi kila mtu amekua mwanasiasa. Akipewa mic basi lazima alete siasa. Tumeaza kuwa kama wananchi Ghana sasa.