Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

Wachungaji wana tabia chafu za kuwatumikisha waamini wao, akiwa maarufu kidogo tu ni shida, hata mkewe nyumbani hafanyi tena kazi.,kutwa waumini wanampikia, wanamlimia mashamba.[eeeh... baba mchungaji/mama mchungaji] wametekwa akili zao zote. Huu sio uungwana wachungaji acheni makuu !!?
 
Muache alindwe,yule mchungaji anamtegemea Mungu sana ukisikiliza mahubiri yake utajua hivyo.Ana vita yake anayopigana na Ibilisi,watabiri na wanasiasa anaowapinga kila siku........usisahau pia ana Hummer yake .....lol na mara nyingi watu ni wengi wanaotaka kumuona wale walinzi ni wakuweka taratibu tu za kuonana nae na kuhakikisha yu salama na anatupiga injili kama kawaida as well as kutoa mapepo yanayotutesa.Basi we usiweke geti kwa kuwa Mungu atakulinda kwako???wala kule benki ulikoweka hela zako,ziombee tu lakini kusiwe na ulinzi?????

...Talk about FAITH...!

 
Kwani ni mchungaji yupi halindwi?.Kuna mambo ya rohoni,hufanywa kiroho,kuna mambo ya mwilini hufanywa kimwili.Paroko huwa na timu ya vijana kama wawili au wanne,mchungaji wa kilutheri huwa na wazee wa kanisa,hawa ndio walinzi.Kwa upande wa mchungaji Gwajima ni kutokana na huduma yake,anapambana na wazito waliochukua wenzao misukule,wengi wao ni vingozi wa siasa na wafanyabiashara.Hivyo kupewa ulinzi kama raisi ni sawa.Kwanini raisi alindwe?Hali kadhalika kiongozi yeyote anapaswa kuwa na ulinzi.Wala sio kusema amtumainie mwanadamu....hiyo sio sahihi.Ni haki yake kupewa ulinzi.

...Again, Talk about FAITH...!

 
Jani Jioni nilikutana na hiki kipindi katika luninga ya SIBUKA, ' Saa ya ufufuo na uzima' cha Pastor Josephat Gwajima [http://www.ufufuonauzimaministries.org/]. Suala lililonishangaza ni ulinzi aliyokuwa akipewa na walinzi wake waliovalia kama walinzi wa maraisi (walkie talkie radio et cetera). Je hawa 'wachungaji' wa kileo hawana imani na mazingira yao ya kazi? Naomba kueleweshwa katika hili.
Mbona unatupa link ya kiingredha,kwani hana ya kiswahili?
 
Wala usishangae, haya yote Yesu aliyasema, ni dalili za mwisho wa nyakati. People have turned Jesus to big profitable businesses.

Wanaowafuata hao ni wapuuzi wa imani na kama yupo humu na aniambie nimthibitishie .............. wezi watupu hasa mama Rwakatale
 
Joyce Paul nimependa dansi yako, je ww huhitaji bodyguard wa kukulinda na wenye uchu.....
 
Kadri unavyokuwa tajiri kwa njia za ubabaishaji ndivyo unavyohitaji ulinzi madhubuti!
 
Suala la kulindwa na walinzi kama rais linaweza kuwasitua wengi lakini mimi naona hata rostam analindwa sana na vyombo vya usalama na ndio maana anatumwa kwenda kututafutia wafadhili.

Bado ukitizama utaona hata jabazi sugu akikamatwa analindwa sana na polisi hivyo hata muhalifu analindwa. Suala la kushangaa ni kwa nini walinzi hao wawe na mafunzo ya kibinafsi kwa maana ya mafunzo kama ikulu??
Kama wangetumia kampuni binafsi au wanajeshi wastaafu ni sawa sasa anapo tengeneza jeshi lake kanisani ni hatari kutokea kundi baya la umafia ndani ya taasisi za dini.

Kuunda kikosi cha watu wenye miwani mieusi na radio call ili kumufanya gwajima awe kama rais sasa hiyo ni tofauti na ni suala la kukemea kwani si la kiroho.

Ulinzi kanisani unatakiwa hasa kipindi hiki ambacho mch antony lusekelo aliibiwa tshs 20m

upo ukweli kwamba kuna uhasama wa wachungaji kutokana na biashara na siasa.
Gwajima ni adui mkubwa wa gedrude rwakatare kwani amehamia tanganyika peckers na kuvuta waumini wote wa mikocheni b .

Mtikila alipewa kazi na ccm kumushambulia gwajima baada ya kumuhusisha kikwete na msukule wa amina chifupa.
Sasa mogogoro hii inahitaji ulinzi
 
Ukisoma gzt la kiu la leo utakuta mchungaji maarufu dsm anahusika na uchawi misukule.
Sasa gwajima anatoa misukule. Anaye lengwa hapo ni mama rwakatare
 
Yesu alikuwa anafuatwa na watu wengi kuliko huyo Gwajima, mbona hakuwa na mabodigadi?

Umeambiwa ujaribu kuacha mlango wako wazi kisha umuombe mungu wezi wasiibe uone! gwajima sio yesu richa ya kumuomba mungu ulinzi pia ni lazima awe na self defence kutokana na vita ya kimwili na kiroho zinazo muandama
 
Umeambiwa ujaribu kuacha mlango wako wazi kisha umuombe mungu wezi wasiibe uone! gwajima sio yesu richa ya kumuomba mungu ulinzi pia ni lazima awe na self defence kutokana na vita ya kimwili na kiroho zinazo muandama

haaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeluuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuyaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Jambo usillolijua sio vizuri kulitolea hukumu........!!!!!! mtumishi wa Mungu huyu kulindwa usishangae pamoja kuwa na maadui wengi sana kiroho waliojaribu hata kuumua kiroho na kuamua kumshambulia kimwili pia.....ameshawahi kutumiwa majambazi .....home kwakwe na Mungu akawapofusha macho yao wakakutana naye yeye mwenyewe na wakamuuliza wewe mtoto baba yako yupo wapi? Ameshawahi kutaka kupigwa Kisu kanisani ...ndani ya kanisa......sasa no research no wright to speak!!!
 
Usiku umeendelea sana na Asubuhi hii Karibu sana Mwana wa Adamu Atarejea. Kila mmoja atapewa fungu lake bila kujali ni watu wangapi uliwapotosha kwa mafundisho yasiyo na msingi katika Mungu Muumbaji. Hakika, Usiku umeendelea sana, mwenye kuweza kufuatilia yote haya yanayotokea, basi anapaswa aisome vizuri sana na kuielewa Biblia yake (kwa msaada wa Roho Mtakatifu) ili asije jukuta naye amesombwa na Manabii wengi wa Uongo ambao wameigeuza Imani ya Bwana wetu Yesu Kristo kama mtaji wao huku nyuma yao yupo yule anayewatumia ili wawadanganye wanadamu kwa Mafundisho yanayopoteza watu. Yote haya yanayotokea, hakuna jipya kwani yote YAMEANDIKWA KWENYE BIBLIA. Pia Tafuta hicho Kitabu kwenye SIGNATURE YANGU na Mungu atakufunulia yote.
 
Jambo usillolijua sio vizuri kulitolea hukumu........!!!!!! mtumishi wa Mungu huyu kulindwa usishangae pamoja kuwa na maadui wengi sana kiroho waliojaribu hata kuumua kiroho na kuamua kumshambulia kimwili pia.....ameshawahi kutumiwa majambazi .....home kwakwe na Mungu akawapofusha macho yao wakakutana naye yeye mwenyewe na wakamuuliza wewe mtoto baba yako yupo wapi? Ameshawahi kutaka kupigwa Kisu kanisani ...ndani ya kanisa......sasa no research no wright to speak!!!
Ndugu yangu listen to yourself, unayoshuhudia yanadhibitisha hoja ya waliowengi kuwa mchungaji haitaji ulinzi make Mungu anamlinda mwenyewe. Swali kama usemayo nikweli je ulinzi wa nini. kamausemayo ni kweli kuwa anawapofusha macho waliomjia kumdhuru ulinzi wa nini? So ama anaitaji ulinzi wa kidunia kwakuwa hana nguvu za kimungu za kumlinda auhaitaji ulinzi wa kidunia kwakuwa ana nguvu za kimungu za kumlinda.
 
Back
Top Bottom