kaburunye
JF-Expert Member
- May 12, 2010
- 672
- 74
Jamani kwani Gwajima ana jeshi la polisi? ebu msilete za kuleta hapa. Mnamlaumu Gwajima kana kwamba aliamrisha aje apokelewe airport na kupewa escort ya police. Shida mnakurupuka tu bila kujua ilikuwaje. Na mkitaka details kwa nini Gwajima alipewa escort si mkamwone IGP Mwema au kamanda Kova.
Hakuna mtu anayeweza kujiamulia tu kuwa police wampe escort. Kama jambo hili halijawafurahisha basi msimlaumu Gwajima. Yeye alikuwa Japan akihubiri injili, karudi kafika airport kakuta washirika wake (watoto wake wa kiroho) wamekuja kumpokea. Sasa ni kipi kinachowakera? Hebu leteni mada za maana hapa na si mambo ya majungu yasiyo na maana. Tabia za udaku usio na maana hautusaidii chochote.
Na kwa taarifa yenu bado muda kidogo sana Gwajima atakuwa anatembea na escort ya police kama mwana wa mfalme. Mbona Yesu siku moja aliingia Yerusalemu akiwa juu ya mwanapunda na tena mwanapunda akatandikiwa kanga (kwa mara ya kwanza). Gwajima ni mtumishi wa Mungu na anastahili heshima yake. Maandiko yanasema mtu akimtumikia Mungu, Mungu atamweshimu. Na sasa kam Mungu anamweshimu wewe ni nani umdharau.
Hongera sana IGP Mwema kwa kumpa huyu mtumishi wa Mungu escort ili awahi kufika kanisani ambako maelefu ya washirika walikuwa wanamsubiri. Keep it up and God bless you.
Hakuna mtu anayeweza kujiamulia tu kuwa police wampe escort. Kama jambo hili halijawafurahisha basi msimlaumu Gwajima. Yeye alikuwa Japan akihubiri injili, karudi kafika airport kakuta washirika wake (watoto wake wa kiroho) wamekuja kumpokea. Sasa ni kipi kinachowakera? Hebu leteni mada za maana hapa na si mambo ya majungu yasiyo na maana. Tabia za udaku usio na maana hautusaidii chochote.
Na kwa taarifa yenu bado muda kidogo sana Gwajima atakuwa anatembea na escort ya police kama mwana wa mfalme. Mbona Yesu siku moja aliingia Yerusalemu akiwa juu ya mwanapunda na tena mwanapunda akatandikiwa kanga (kwa mara ya kwanza). Gwajima ni mtumishi wa Mungu na anastahili heshima yake. Maandiko yanasema mtu akimtumikia Mungu, Mungu atamweshimu. Na sasa kam Mungu anamweshimu wewe ni nani umdharau.
Hongera sana IGP Mwema kwa kumpa huyu mtumishi wa Mungu escort ili awahi kufika kanisani ambako maelefu ya washirika walikuwa wanamsubiri. Keep it up and God bless you.