Gwajima wa kanisa la Ufufuo na ving'ora barabarani

mfianchi

Platinum Member
Jul 1, 2009
11,867
8,270
Niko Old Bagamoyo road nasikia ving'ora vinapigwa kutoka kwenye gari inabidi kuweka gari pembeni nikihisi ni Mheshimiwa au mgonjwa anapita nashangaa kuona Hummer nyekundu na msururu wa magari ukipita kwa kasi na hayo magari yamebandikwa Picha ya mheshimiwa askofu anakaribishwa nyumbani.

Sijui huyu bwana karuhusiwa na nani kwa kutupigia ving'ora na kupita kwa kasi kama kiongozi wa nchi. Sasa hata matapeli wanajidai hii nchi sijui tunaenda wapi?

4.jpg
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Niko Old Bagamoyo road nasikia ving'ora vinapigwa kutoka kwenye gari inabidi kuweka gari pembeni nikihisi ni Mheshimiwa au mgonjwa anapita nashangaa kuona Hummer nyekundu na msururu wa magari ukipita kwa kasi na hayo magari yamebandikwa Picha ya mheshimiwa askofu anakaribishwa nyumbani.

Sijui huyu bwana karuhusiwa na nani kwa kutupigia ving'ora na kupita kwa kasi kama kiongozi wa nchi. Sasa hata matapeli wanajidai hii nchi sijui tunaenda wapi?

Sioni cha ajabu kwani Mamiss wanasindikizwa na msafara kuzunguka DSM, juzi bia ya ndovu ilikuwa na itifaki yake toka airport, basi ujue hakuna formula yoyote anaweza kufanya chochote hapa bongo usishangae ndugu yangu.
 
umekichukia king'ora? au umemchukia alibebwa na ham'ma?
sijaona tatizo, ukiona hivyo si lazima uruhusiwe na mtu
kiongozi wa kiroho ni mkubwa kuliko, kiongozi wa kundi la wezi
hata ana kofia ya kuwa raisi, any way hii ni nchi yetu na wananchi ndiyo sisi,
hata mimi hakuna kitu kinachoniudhi kama makelele ya adhana
 
Ndani ya Tz yote yanawezekana, juzi si umesikia dogo alikula lifti ya polisi toka mikumi hadi dar akiwa na fulushi la bangi kiulaini kabisa. Na wale jamaa wanaofunga mtaa kwa sababu ya ngoma(sijui na nini vile) usiku kucha vipi nao. Bongo tambalale.
 
umekichukia king'ora? au umemchukia alibebwa na ham'ma?
sijaona tatizo, ukiona hivyo si lazima uruhusiwe na mtu
kiongozi wa kiroho ni mkubwa kuliko, kiongozi wa kundi la wezi
hata ana kofia ya kuwa raisi, any way hii ni nchi yetu na wananchi ndiyo sisi,
hata mimi hakuna kitu kinachoniudhi kama makelele ya adhana

Usije ukadondoka kwa kijiba cha roho mwe!
 
nenda west africa ukaone..ni kitu cha kawaida...ungejua hao ndo wanaowaombea hata nyie msingewasumbua...umeona wivu au una matatizo gani..
 
Kuna kuja utawala mwingine , kuna watu wamekosa platform..na ndio hao ambao wanaweza hata kuwalaza chini, kuwashindisha njaa, kuwatia umasikini na kuwadumaza fikra wale wasiojua kweli huku wakitakiwa kuimba na kusujudu...
 
Kuna kuja utawala mwingine , kuna watu wamekosa platform..na ndio hao ambao wanaweza hata kuwalaza chini, kuwashindisha njaa, kuwatia umasikini na kuwadumaza fikra wale wasiojua kweli huku wakitakiwa kuimba na kusujudu...

Gwajima alikuwa anatoka Japan na korea kuhubiri amekuwako huko kwa miezi kadhaa, washirika wake ambao ni walipa kodi walikuwa wanampokea..wala hahitaji publicity kama unavyofikiri..kanisa lake lina watu si chini ya elfu ishirini na tano, kama publicity alishapata hadi amechoka...nakushauri nenda hapa...

Ufufuo na Uzima

gctc

iyo gari mnayompiga nayo mawe, amepewa huko huko japan kama zawadi kwasababu anahubiri sana huko japan, korea na china,,,,waumini wake wamemnunulia na ni haki yake kuliendesha...wala msihangaike hivyo...mwacheni ahubiri injili, na mwacheni waumini wake wamfurahie kwa kurudi kwake...
 
Mzee Ubungo (LOL) sikudhani kama nawe upo miongoni mwao hao ...kama ndivyo basi umefilisika..ipo siku uatalalal nje na familia yako. BWANA ASIFIWE!

wala haiko hivyo...mimi sikuwepo hapo, lakini nimefagilia sana walivyofanya, kusema kweli nimepigiwa simu na kuambiwa yaliyotokea kwasababu mimi siko hapo bongo,,na nimefurahi sana. kama niko bongo, saa hizi ni saa nane na nusu usiku kwa saa za Dsm, nani yuko macho kwenye computer sasahivi Dar?...

unaposema nitalala nje na familia yangu, kwasababu gani? unajua kuna swali moja nilikuuliza ile majuzi kuwa "how old are you", kwasababu inaonyesha bado umri wako ni mdogo na ninaogopa kufupisha fikra zangu kujibizana na mtoto mdogo.....I wish you knew me, lakini bahati mbaya you will never know me kwasababu hapa tunatumia majina bandia...ila, nafikiri wa kulala nje ni wewe. hata kama siko miongoni mwao, I appreciate what they do, and siwezi kubisha kuwa, kile wanachofanya na mimi kimenifanya hadi nikawepo hapa kwenye nafasi niliyonayo, ambayo ni ya hali ya juu sana...nashukuru Mungu. ila nawaonea huruma watu walio mbali na upeo kama ngoshwe, kwasababu siku zote huwa wanapinga mambo ya Mungu, kwasababu tu wao ni wakatoliki.....wewe ndo utafilisika na si mimi...tupinge ndani ya miaka hii mitano nani kati yangu mimi na wewe atafisilika...you will remember these words...!!!!!!!!!!!!!
 
Niko Old Bagamoyo road nasikia ving'ora vinapigwa kutoka kwenye gari inabidi kuweka gari pembeni nikihisi ni Mheshimiwa au mgonjwa anapita nashangaa kuona Hummer nyekundu na msururu wa magari ukipita kwa kasi na hayo magari yamebandikwa. Picha ya mheshimiwa askofu anakaribishwa nyumbani. Sijui huyu bwana karuhusiwa na nani kwa kutupigia ving'ora na kupita kwa kasi kama kiongozi wa nchi .sasa hata matapeli wanajidai hii ncxhi sijui tunaenda wapi

Kaaz kwelikweli. Sasa huyu mkulu kama anapenda sifwa na utukufu kwanini asinunue helikopta yake ili at least asiwakwaze wengine wasiohusika?
 
Wewe unamdharau Askofu, eee! Unadhani ni mtu mdogo? Uliza wazee wako nao watakuambia. Acha apigiwe ving'ora bwana. Kwani nani mwenye hakimiliki ya hivyo vitu?
 
wala haiko hivyo...mimi sikuwepo hapo, lakini nimefagilia sana walivyofanya, kusema kweli nimepigiwa simu na kuambiwa yaliyotokea kwasababu mimi siko hapo bongo,,na nimefurahi sana. kama niko bongo, saa hizi ni saa nane na nusu usiku kwa saa za Dsm, nani yuko macho kwenye computer sasahivi Dar?...

unaposema nitalala nje na familia yangu, kwasababu gani? unajua kuna swali moja nilikuuliza ile majuzi kuwa "how old are you", kwasababu inaonyesha bado umri wako ni mdogo na ninaogopa kufupisha fikra zangu kujibizana na mtoto mdogo.....I wish you knew me, lakini bahati mbaya you will never know me kwasababu hapa tunatumia majina bandia...ila, nafikiri wa kulala nje ni wewe. hata kama siko miongoni mwao, I appreciate what they do, and siwezi kubisha kuwa, kile wanachofanya na mimi kimenifanya hadi nikawepo hapa kwenye nafasi niliyonayo, ambayo ni ya hali ya juu sana...nashukuru Mungu. ila nawaonea huruma watu walio mbali na upeo kama ngoshwe, kwasababu siku zote huwa wanapinga mambo ya Mungu, kwasababu tu wao ni wakatoliki.....wewe ndo utafilisika na si mimi...tupinge ndani ya miaka hii mitano nani kati yangu mimi na wewe atafisilika...you will remember these words...!!!!!!!!!!!!!

nimekwambia siko Dar, pia sitembei kwa mguu mimi, ukipenda naweza kukusaidia hata wewe uondokane na kutembea kwa miguu. tuache bifu tuchangie mada, yatosha...

Sina Bifu mzee..nakuambia ukweli halisi. Hata kama upo Mbingu ya saba ni vyema ukaelewa pia umri mkubwa, mahali ulipo, uwezo wako wa kifedha au mali, hadhi yako, elimu uiyonayo nk ni misingi tu ya kukusaidia wewe na jamii inayokutegemea ili hali kwa upande mwingine uweze kuishi vizuri na wenzako.

Kufanikiwa kwako kielimu au kimali na kujua kwako mambo, isiwe chachu ya majigambo, dharau, kujikweza, kujitutumua na kujiona sasa wewe ni bora kuliko wengine katika kila kitu kwenye huu ulimwenguni. Vinginevyo, utaonekana limbukeni mabele ya waungwana!!. Fikra za mtu anayejua huwa aziendi na kujigamba, kujitetea kusiko kikomo, kuona yeye ni kila kitu nk. Uungwana ni pamoja na kukubali kukosolewa Kumbuka umri si tija katika kuyaona, kuyaelewa na kuyatafsri mambo bali ni kipimo tu cha kujua umekumaihs ya hapa duniani. Kwani hata busara ya mtu haipimwi kwa ukubwa wa umri wake.

Na iwapo una umri mkubwa na umesoma, una mali nk na hutaki uelewa na kuona wenzio hawastaili kutoa hoja kwa uhuru, hiyo itakuwa ni kipimo cha mtu asiejua atokako wala aendako!.

Tukitaka kujua ndani ya hili jukwaa nani yupo wapi, ana umri, ana elimu gani, anafanya nini, na anamiliki nini, nadhani hili jukwaa, unaweza kujiona wewe si kitu kabisa katika ulimwengu huu.

Kila mtu ana haki ya kutoa maoni na mtazamo wake hapa na sio kushambuliana mzee. Kama umeelewa somo, chukua hatua za kiuungwana.

Tuendelee kuchangia mada kwa amani na upendo mzee.
 
Bora huyo alijiamulia kujiongoza wale wa TBL walikuwa na Traffic kabisa sijui yale mafuta ilijaza serikali kwenye pikipiki?
 
iyo gari mnayompiga nayo mawe, amepewa huko huko japan kama zawadi kwasababu anahubiri sana huko japan, korea na china,,,,waumini wake wamemnunulia na ni haki yake kuliendesha...wala msihangaike hivyo...mwacheni ahubiri injili, na mwacheni waumini wake wamfurahie kwa kurudi kwake...

Dah mm hii sikuijua kabisa kha!
Kakobe nae huwa anapiga piga route za huko sijui atapewa helcopter au kondoo wamekimbia?
 
siku hizi watu wameamua kujichukulia madaraka ,,sijui hawaelewi maana ya ving'ora?
 
Back
Top Bottom