Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Kasema atakata rufaa kwa wananchi wa arusha sio mahakani tena star tv walikuwa live!
 
Wana JF,

Nimesikia sasa hivi kupitia TBC 1 radio kuwa Mahakama Kuu Kanda ya Arusha iliyokuwa ikisikiliza kesi ya kupinga ushindi wa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) imeshatoa hukumu asubuhi hii na kwamba Mhe. Gobbless Lema amenyang'anywa Ubunge mezani na Jaji Gabriel Rwakibarila.

Hivyo kuanzia leo Mhe. Godbless Lema si Mbunge tena na Jimbo la Arusha Mjini liko wazi.My take: Hukumu hii itaacha maswali mengi sana ndani ya mioyo na vichwa vya Watanzania. Kwamba hukumu ya Kesi hii ilikuwa imepangwa kimkakati na Chama Cha Magamba kwa kuitumia Mahakama kumnyang'anya Lema na CHADEMA jimbo hili kwa makusudi ili Uchaguzi urudiwe.

Inasikitisha kuwa sababu zilizotolewa na upande wa walalamikaji ambao ni WANACHAMA 3 WA CCM hazikuwa na uzito wa kutengua matokeo ya Ubunge wa Jimbo la Arusha mjini. Ikumbukwe kuwa mgombea wa Ubunge wa CCM Bi Matilda Buriani aliyebwagwa chini na Godbless Lema hakufungua kesi hiyo wala hakuwahi kutokea kwenye Mahakama hiyo kutoa ushahidi kwamba Lema alitoa kauli za udhalalishaji, matusi na kashfa kwa Bi Buriani. Kwanini mgombea wa CCM asemewe na watu wengine ilhali mwenyewe kakaa kimya??

CCM wamecheza rafu katika hili. Hata hivyo hata kama Uchaguzi utaitishwa leo hii WEMBE NI ULEULE ULIOMNYOA SIOI SUMARI KULE ARUMERU EAST. CCM wasifurahie kuwa wamepata mteremko wa kurudisha jimbo hilo mikononi mwao. Wasahau. Kama wanabisha waitishe Uchaguzi waone kilichomzuia kuku kukojoa. CCM kimedhihilisha kuwa ni Chama Cha Mafisadi na Chama Cha Mahakama-CCM. Hakika Tanzania bado tuna safari ndefu ya kufikia Demokrasia ya kweli!!

Nawasilisha.

tupo pamoja! Na Tz ya CDM isisahau kuwa! SUCCESS DWELL ON THE EDGE!
 
Wakuu samahani kuna mtu anaweza tuwekea matokeo ya Mh Kamanda Lema na yule mama Mam.vi kipindi kile cha Uchaguzi 2010?
 
ukweli ni kwamba Lema's popularity na credibility iko juu kwa sasa, naamini anasubiri uchaguzi utangazwe kwa hamu kubwa
 
hawa magamba ni bure wanajisumbu Arusha hawatapata kitu, hiyo hukumu inaonekana kutengenezwa hukumu ilishajulikana kabla ya kutangazwa.
 
Option one: Hapana, asubiri uchaguzi mwingine Arusha mjini ndani ya miezi mitatu ya sheria za uchaguzi ni kifupi zaidi ya muda wa kusikiliza kesi na siku zote demokrasia gharama na uchaguzi mpya utatumika kuijenga CHADEMA

Option two: Ndiyo, afuate sheria kwa misingi ya utawala bora na kupunguza gharama ya uchaguzi, japokuwa wanasema Justice delayed is denied! Bado tuiamini mahakama

Option three: Sijui, maana kwa vyovyote vile CCM inalitaka jimbo la Arusha (mjini) itatumia nguvu imeshika dola na uchaguzi watahonga na kuiba kura na hata mahakama ile ya kangaroo watahonga na kuchelewesha matokeo kuikomoa Arusha na kupata ushindi hapo baadae!

Maelezo zaidi ya hizo options!
 
This is an insult. Hapa mnamaanisha sisi hatutakiwi CDM, maana yake na narudia tena maana yake CDM ni chama cha kikristo na wakristo tu!!

kwani waislamu hatuna mungu kaka? mbona povu hivyo,taratibu bwana. hiki ni chama chetu sote njoo gari kubwa
 
ccm na lowasa na hii serikali mnachotafuta arusha mtakipata

CDM itashida ila itakuwa fundisho kwa wagombea kutumia lugha ya matusi na uongo ambao umekuwa fasheni.Hapo issue sio lowasa ila ni kulinda amani ya nchi kwa mtu kuamua kumtukana mwenzie
 
Please mwenye hukumu yote ya kesi ya Lema aweke hapa ili tuweze kuijadili kwa uwazi na ukweli na tujue uhalali wa hukumu yenyewe maana mda huu ni emotion zaidi ndo zinatuongoza kutoa maoni hatuna facts ya kutosha.
 
serkali ya magamba haina issue ndio maana inaanzzisha vitu. usikute hata uchaguzi wa arumeru ulitengenezwa. hizo ni sarakasi gani ssm wanacheza. naona hapa ahwaeleweki. unajua angeshinda mccm hii kesi ingebaki mahakamani.
 
Heshima kwako Mkuu Makene.

We hope Arusha ni ngome ya CDM no matter what lakini lazima tukio hili la kuvuliwa ubunge kwa Lema tulipe uzito stahiki. Kuna vita iko mbele ya kurejesha jimbo hili, tusiipuuze kama tulivyojipanga na kushinda Arumeru lazima tuweke juhudi zaidi kushinda Arusha Mjini.

Katika hili lazima ieleweke kwamba, CCM wamekuwa kwa muda wote wakilitamani jimbo la Arusha mjini na kutawala halmashauri hiyo ndiyo maana walikuwa radhi kupindisha sheria ili meya wao ashinde na walitumia kila aina ya umafia imekuwa.

Haitashangaza kama watafanya umafia na ujambazi dhidi ya Demokrasia kulichukua jimbo hili. We really need to be serious na kuweka mkakati wa makusudi dhidi ya mbinu chafu za CCM. Wako tayari kufanya lolote kupata wanachokihitaji. Mfano; ni tukio la kuwakatakata mapanga wabunge wa CDM kule Mwanza.
Upo sahihi kabisa mkuu. Hili ndilo ninaloliona na mimi. Arumeru mashariki si mhimu kwa CCM kama ilivyo Arusha mjini. Kwa CCM kuikosa Arusha mjini ni hasara kubwa sana. So watatumia hila na mbinu zozote ziwezekanazo kuhakikisha wanalipata lile jimbo. Lakini kama viongozi wa CHADEMA watakuwa imara, kufanya hivyo kwaweza kuwa ni jambo jema kwa kuwa kutasababisha Libya nyingine nchini. Na hivyo kuuondoa uongozi wa CCM madarakani kwa nguvu ya Umma na kuikana democrasia uchwara ambayo huwa daima inapokwa.
 
yani hata CHADEMA wasipofanya kampeni, jimbo bado litabakia mikononi mwao tu.
ushauri wangu kwa CHADEMA ni kuinvest katika security ya kura, wala hakuna haja ya
kujikita aana kwene kampeni.
 
CDM itashida ila itakuwa fundisho kwa wagombea kutumia lugha ya matusi na uongo ambao umekuwa fasheni.Hapo issue sio lowasa ila ni kulinda amani ya nchi kwa mtu kuamua kumtukana mwenzie
Nitaridhika kwamba mahakama inatenda haki iwapo tu, na matokeo ya ubunge wa segerea yatatenguliwa. Otherwise, mahakama za bongo zinafanya kazi ya kisiasa kuliko kazi za kitaaluma.
 
Naona hawa jamaa wana mpango wa kuimaliza CHADEMA. Nadhani hapa wametengua ubunge wake mara moja. Lakini tusistuke kuona na ile kesi nyingine inayowakabili ya maandamano Arusha inasikilizwa haraka haraka na kutolewa hukumu ambayo itatustua wengi. Ikiwa na maana kuwa viongozi wetu wa CDM pamoja na Lema kuswekwa ndani. Nadhani ndio mahesabu yao ya kukiua chama chetu. Lakini tujipe moyo maana sisi tuna Mungu atatusimamia.
 
Nabii amosi upo wapi juu ya hii nchi ?,,upo wapi juu ya ccm......................................mungu toa hukumu ya hakiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii...ccm uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
kuvuliwa kwa lema mahakama haikutumia busara ya kutosha kwani hata shahidi zilizotolewa hazitoshi kumvua jamaa ubunge,na pia hata uchaguzi ukifanyika leo kiti kitarudi kwa lema ,sasa jaribu kuangalia garama zote hizo za kurudia
uchaguzi ni mwananchi wa kawaida anayeumia.
 
C wametengeneza hukum za kipirato ili wapate jimbo
kusudi waangalie wapi walikosea kuiba kura! Sasa Safari hii tunabana kila kona!
Mbona tutawasachije wanao hesabu kura
tatajipanga road kama taa!!!!!!
 
Wanajamii hivi kuna mtu mwenye rekodi ya matokeo ya uchaguzi jimbo la Arusha mwaka 2010? kama ipo niaomba ili tufanye tathmini ya uchaguzi mdogo ujao ikiwezekana tufanye projection pia... Wakati wao wanawaza wamsimamishe nani sisi tunafanya tathmini tutashinda kwa kiwango gani. Hatua 2,000 mbel yao.....
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom