Gazeti la Mtanzania: Utetezi wa kikabila wa Lowassa haukubaliki

Watanzania

JF-Expert Member
Jul 7, 2009
727
42
Ni jambo la kusikitisha kuwa gazeti la Mtanzania lipo si kwa ajili ya maslahi ya taifa bali kuangamiza nchi.

Katika habari iliyotoka leo 21.11.09 kwenye gazeti hili wanamtetea Lowasa kuwa kuna watu wanazungukia jimbo lake kutaka kugombea. Kibaya zaidi ni pale utetezi wao wa Lowasa unapoingiza mtazamo wa kuleta ubaguzi wa kikabila.

Gazeti hili linaandika eti Wamasai wameonewa vya kutoka sasa basi, kwani Lowasa ni Mbunge wa Wamasai? Jimbo la Lowasa kwa vyovyote vile kuna makabila mengine pia, na utetezi wa kupandikiza ubaguzi wa kikabila haukubaliki katika nchi yetu. Mbunge vilevile yupo kwa ajili ya taifa zima, siyo kwa ajili ya makabila yao, ndio maana huapa.

Hili ni gazeti linalostahili kupuuzwa na watanzania wote. Jukwaa la wahariri nalo pia litoe karipio lake kwa gazeti hili kwa kutoa utetezi wa kikabila.
 
Inawezekana haya ndiyo magazeti yanayoonekana yanaleta " the so called amani" katika nchi yetu.
Natamani kuwaita hawa watu wanaoendelea kuiharibu nchi yetu majina kama " nduli, joka kubwa" .........










NANYI MTAIFAHAMU HIYO KWELI NAYO KWELI ITAWAWEKA HURU
 
Hili gazeti liliandika juzi kwa wino mzito ukurasa wa mbele, uliokuwa na picha yangu, kwamba "Mtei amesambatishwa"! Nililisoma, nikasema kama gazeti linalomilikiwa na Rostam Aziz lingeniandika vizuri, ningekwenda kujitazama kwenye kioo kama nimebadilika au la. Habari yenyewe haikueleweka na haikuwa na kichwa wala mkia. Upuuzi mtupu.

Watanzania wafahamu tu kwamba mmiliki wa gazeti ni nani, na walipuuze kama linavyostahili. Hawa ni wafa maji, wapigania mafisadi.
 
Hili gazeti liliandika juzi kwa wino mzito ukurasa wa mbele, uliokuwa na picha yangu, kwamba "Mtei amesambatishwa"! Nililisoma, nikasema kama gazeti linalomilikiwa na Rostam Aziz lingeniandika vizuri, ningekwenda kujitazama kwenye kioo kama nimebadilika au la. Habari yenyewe haikueleweka na haikuwa na kichwa wala mkia. Upuuzi mtupu.

Watanzania wafahamu tu kwamba mmiliki wa gazeti ni nani, na walipuuze kama linavyostahili. Hawa ni wafa maji, wapigania mafisadi.

Pole Mzee Mtei: usisikitike sana kwani hili gazeti haliuzi nakala nyingi, limeporomoka kiasi kwamba jumla nakala zinazouzwa kwa wiki moja nzima ni chini ya theluthi moja ya nakala zinazouzwa na Mwanahalisi.

Kuporomoka huko kumetokana na kuwekwa Deatus Balile kuwa mhariri kama miezi miwili sasa. Balile anasifika kwa kazi moja kubwa -- kulamba viatu vya RA pamoja na EL -- hadi anachefua kufuatana na ripoti kutoka hapo New Habari.

Ripoti pia zinasema kuwa siku hizi hata yule hussein Bashe -- wa kitengo cha usambazaji naye huingilia katika kuweka headline katika stori ya mbele.
Yeye huyu alifukuzwa Mwananchi kwa kuendesha genge la wizi wa magazeti. Msomali huyu ameahidiwa na RA kuwa atamrithi Selelii mwaka kesho.
 
Pole Mzee Mtei: usisikitike sana kwani hili gazeti haliuzi nakala nyingi, limeporomoka kiasi kwamba jumla nakala zinazouzwa kwa wiki moja nzima ni chini ya theluthi moja ya nakala zinazouzwa na Mwanahalisi.

Kuporomoka huko kumetokana na kuwekwa Deatus Balile kuwa mhariri kama miezi miwili sasa. Balile anasifika kwa kazi moja kubwa -- kulamba viatu vya RA pamoja na EL -- hadi anachefua kufuatana na ripoti kutoka hapo New Habari.

Ripoti pia zinasema kuwa siku hizi hata yule hussein Bashe -- wa kitengo cha usambazaji naye huingilia katika kuweka headline katika stori ya mbele.
Yeye huyu alifukuzwa Mwananchi kwa kuendesha genge la wizi wa magazeti. Msomali huyu ameahidiwa na RA kuwa atamrithi Selelii mwaka kesho.


Ukiacha Mtanzania, kuna Rai la kila wiki ambalo nalo kazi yake kubwa ni kuwatetea RA na EL na mafisadi wengine kwa ujumla. Mhariri wake ni Boniface naye pia ni hodari kulamba viatu vya RA kwa namna ya kutia kichefuchefu. Kwa ujumla pale New habari kuna mtandao wa waandishi wa RA ambao unaundwa na Muhingo, Mwakiteleko, Balile, Manyerere, Makene, Sarah Mossi, Matinyi, na Mayage. Mtandao huu unashirikiana kwa kiwango fulani na Kibanda wa T. Daima.

Mtandao huo umesaidia sana kuporomoka kwa mauzo ya magazeti (ukiacha yale ya michezo) kiasi kwamba hata mishahara ni matatizo makubwa -- tofauti na ilivyokuwa wakati Rosemary Mwakitwange akiwa CEO.
 
Hili gazeti liliandika juzi kwa wino mzito ukurasa wa mbele, uliokuwa na picha yangu, kwamba "Mtei amesambatishwa"! Nililisoma, nikasema kama gazeti linalomilikiwa na Rostam Aziz lingeniandika vizuri, ningekwenda kujitazama kwenye kioo kama nimebadilika au la. Habari yenyewe haikueleweka na haikuwa na kichwa wala mkia. Upuuzi mtupu.

Watanzania wafahamu tu kwamba mmiliki wa gazeti ni nani, na walipuuze kama linavyostahili. Hawa ni wafa maji, wapigania mafisadi.

Hivi kwa nini na wewe tusikupuuze kwa kudhani kuwa Chama lazima kiongozwe na mkweo? Wewe mafisadi gani ambao umewapinga, juzi umezindua kitabu chako mkiwa na fisadi nyangumi. Nadhani nyie wote mna maslahi binafsi mnayopigania vingenevyo Mzee Mtei usingeweza kuchepusha demokrasia kwa maslahi ya mkweo. Rostam, Mengi, Mtei, JK, Lowassa na wengine wote mnatetea maslahi yenu tu.
 
Hivi kwa nini na wewe tusikupuuze kwa kudhani kuwa Chama lazima kiongozwe na mkweo? Wewe mafisadi gani ambao umewapinga, juzi umezindua kitabu chako mkiwa na fisadi nyangumi. Nadhani nyie wote mna maslahi binafsi mnayopigania vingenevyo Mzee Mtei usingeweza kuchepusha demokrasia kwa maslahi ya mkweo. Rostam, Mengi, Mtei, JK, Lowassa na wengine wote mnatetea maslahi yenu tu.

Ficha Upuuzi wako, usifiche Hekima yako
 
RA akiingiza tuu ukabila katika kumsafisha EL ndio kwanza atazidi kumharibia, data zote zipo, EL siyo Mmasai ni Mmeru aliyehamia Monduli. Tukiingiza hizi kampeni za ukabila, siasa zetu ambazo tayari ni mbovu, zitazidi kuharibika.
 
Hivi kwa nini na wewe tusikupuuze kwa kudhani kuwa Chama lazima kiongozwe na mkweo? Wewe mafisadi gani ambao umewapinga, juzi umezindua kitabu chako mkiwa na fisadi nyangumi. Nadhani nyie wote mna maslahi binafsi mnayopigania vingenevyo Mzee Mtei usingeweza kuchepusha demokrasia kwa maslahi ya mkweo. Rostam, Mengi, Mtei, JK, Lowassa na wengine wote mnatetea maslahi yenu tu.

Mkuu Una guts za kumwita Mzee Mtei Fisadi kwa Sababu hutumii jina lako halisi nadhani siku ukitumia jina lako halisi basi nadhani hutangoja watu wakuite Fisadi bali utajiita Mwenyewe ni Fisadi!

Lazima tuwaheshimu watu wanaotumia majina yao halisi hapa jamvini, wengi ambao hatutumii majina halisi inawezekana kuna vitu vingi vinatusuta, tunakuwa free kuwaita wengine mafisadi just because tunatumia majina Bandia! Kabla hujamuita member mwenzio ( aliyejisajili kwa jina halisi) Fisadi au aina yeyete ya Lugha ya Kutusi ni vyema ili kuweza uwanja sawa ( fair playing ground) ukajitambulisha kwa jina lako halisi ili na yeye akijibu alegations ajue anamjibu nani na siyo Ghost
 
Ni jambo la kusikitisha kuwa gazeti la Mtanzania lipo si kwa ajili ya maslahi ya taifa bali kuangamiza nchi.

Katika habari iliyotoka leo 21.11.09 kwenye gazeti hili wanamtetea Lowasa kuwa kuna watu wanazungukia jimbo lake kutaka kugombea. Kibaya zaidi ni pale utetezi wao wa Lowasa unapoingiza mtazamo wa kuleta ubaguzi wa kikabila.

Gazeti hili linaandika eti Wamasai wameonewa vya kutoka sasa basi, kwani Lowasa ni Mbunge wa Wamasai? Jimbo la Lowasa kwa vyovyote vile kuna makabila mengine pia, na utetezi wa kupandikiza ubaguzi wa kikabila haukubaliki katika nchi yetu. Mbunge vilevile yupo kwa ajili ya taifa zima, siyo kwa ajili ya makabila yao, ndio maana huapa.

Hili ni gazeti linalostahili kupuuzwa na watanzania wote. Jukwaa la wahariri nalo pia litoe karipio lake kwa gazeti hili kwa kutoa utetezi wa kikabila.

Tutayaona Mengi tu kuelekea 2010 si unakumbuka chuki ya Lowassa na Wachagga haswa wale wanaotawala jimbo la Arusha Mjini? ndo haya yote yalipoanzia! Sasa mbaya zaidi ni pale Mzee Mengi aliposimikwa cheo cha Ole (Chiefdom kama sikosea Ole Laibon for all Massais in EA) na akiwa si Mmasai huku Lowassa akiachwa toka hapo hana urafiki na Wachagga lakini anasahau Kilimanjaro kuna Wamassai na zamani hizo walimiliki the whole of Rift Valley from Nairobi to Kilimanjaro (hata Waingereza na Wajerumani waliheshimu hilo ndo maana kukawa na Massai corridor!) na all the tribes in the region coexisted together from time immemorial! Sasa wakianza politics kama hizi ni kuji-shoot own foot maana itabidi watueleze masuala ya Loliondo na haki za wakazi wa huko maana ardhi yao ilitaifishwa kipindi cha ujamaa na mambo mengine chungu nzima ukiacha Massai Ancestoral land huku tunapoelekea Mungu anajua hizi ni parochial politics ngojeni Moran wacharuke kudai ardhi yao toka Nairobi mpk Kilimanjaro! Sijui kutakalika!

Utofauti wa makabila ya wanaoishi Manyara, Kilimanjaro na Arusha ni pale tu Missionaries walipokuja na kuamua ku-settle milimani kwa vile Massai were hostile, ambapo Wachagga na makabila mengine kama Wameru waliwapokea (wachagga walikuwa wakikaa milimani kwa kuogopa kukaa on plain grounds ambazo zilikuwa grazing grounds for those Massai) na as a result wakaingia Ukristo as some sort of seeking protection (si unajua Wild Massai walikuwa wanakanyaga kila mtu aliyekutwa in their territory n ku-raid kila kijiji kipindi cha kiangazi kukusanya ng'ombe wao waliopewa na Ainga (Massai God))! Ila haya makabila yote yana uhusiano ukiangalia vizuri kuanzia Warombo, Wameru n.k. within the region wanashaabihana na Wamassai kuanzia mila zinafanana ukiangalia vizuri walikuwa wanatoboa, kutahiri wanawake na kuvaa kama Massai those times! the rest is history jamani tusianze haya!

Sasa ukiwa na mtu aliyetoka Iran na anayesaka Uraisi kwa udi na uvumba (Mmasai ambaye hata rika lake la jando linamkataa haujui boma lake la kutairiwa)! hawawezi jua kitu gani kinaendelea nchini hapa haswa on those traditional places watawachonganisha tu ili wafisadi zaidi! Ila Wamassai hawana shida na mtu haswa majirani zao!
 
Mkuu Una guts za kumwita Mzee Mtei Fisadi kwa Sababu hutumii jina lako halisi nadhani siku ukitumia jina lako halisi basi nadhani hutangoja watu wakuite Fisadi bali utajiita Mwenyewe ni Fisadi!

Lazima tuwaheshimu watu wanaotumia majina yao halisi hapa jamvini, wengi ambao hatutumii majina halisi inawezekana kuna vitu vingi vinatusuta, tunakuwa free kuwaita wengine mafisadi just because tunatumia majina Bandia! Kabla hujamuita member mwenzio ( aliyejisajili kwa jina halisi) Fisadi au aina yeyete ya Lugha ya Kutusi ni vyema ili kuweza uwanja sawa ( fair playing ground) ukajitambulisha kwa jina lako halisi ili na yeye akijibu alegations ajue anamjibu nani na siyo Ghost

Wewe acha kutisha watu, hapa JF tunaangalia pande zote, kama mtu ameleta hoja anapingwa kwa hoja zake. Sasa kama wewe unadhani hilo linahitaji kuwa na jina halisi mimi siwezi kukusaidia kwa hilo. Kwani una haki ya maoni yako
 
Yeye kasema tuwapuuze wenzie kwa sababu ya madhambi yao. Swali langu lilikuwa kwake kwa nini na yeye tusimpuuze kutokana na madhambi yake?

Mkuu
Mtei ( Anafahamika) amesema tuwapuuze Mafisadi ( wanafahamiki), wewe Gezaulole ( inawezekana ni Fisadi) unatoa shutuma kwa Mtei

Not Fair Mkuu
 
Mkuu
Mtei ( Anafahamika) amesema tuwapuuze Mafisadi ( wanafahamiki), wewe Gezaulole ( inawezekana ni Fisadi) unatoa shutuma kwa Mtei

Not Fair Mkuu

Wewe kwani una tatizo gani? Yeye kasema tuwapuuze na mimi nimemuuliza yeye kwa nini tusimpuuze na yeye? Wewe hapo imekuwa nongwa tatizo ni nini kwako hapo?
 
Mimi na wewe wote ni Waoga tu

Sawa inawezekana kweli. Lakini angalia maandishi yake mwenyewe anasema angeshangaa kama magazeti ya Rostam yangemwandika vizuri, na hivyo hivyo Rostam na Lowassa watashangaa kama magazeti ya Mengi yatawaandika vizuri. Ndiyo maana mimi nikasema hawa wote wana maslahi yao wanayopigania, kwa sababu wangekuwa wanapigania maslahi ya nchi wasingetumia magazeti yao kuchafuana.

Sasa kama kusema huko ni uwoga hapo nakubali
 
Sawa inawezekana kweli. Lakini angalia maandishi yake mwenyewe anasema angeshangaa kama magazeti ya Rostam yangemwandika vizuri, na hivyo hivyo Rostam na Lowassa watashangaa kama magazeti ya Mengi yatawaandika vizuri. Ndiyo maana mimi nikasema hawa wote wana maslahi yao wanayopigania, kwa sababu wangekuwa wanapigania maslahi ya nchi wasingetumia magazeti yao kuchafuana.

Sasa kama kusema huko ni uwoga hapo nakubali

Mkuu kama ungesoma bandiko langu hili with an open mind mabishano haya yasingeendelea

Ndege ya Uchumi

Mkuu Una guts za kumwita Mzee Mtei Fisadi kwa Sababu hutumii jina lako halisi nadhani siku ukitumia jina lako halisi basi nadhani hutangoja watu wakuite Fisadi bali utajiita Mwenyewe ni Fisadi!

Lazima tuwaheshimu watu wanaotumia majina yao halisi hapa jamvini, wengi ambao hatutumii majina halisi inawezekana kuna vitu vingi vinatusuta, tunakuwa free kuwaita wengine mafisadi just because tunatumia majina Bandia! Kabla hujamuita member mwenzio ( aliyejisajili kwa jina halisi) Fisadi au aina yeyete ya Lugha ya Kutusi ni vyema ili kuweza uwanja sawa ( fair playing ground) ukajitambulisha kwa jina lako halisi ili na yeye akijibu alegations ajue anamjibu nani na siyo Ghost

Lakini kwa sababu ulisoma huku uanjiandaa na Ligi ndo maana hukuelewa
 
Back
Top Bottom