Fahamu desturi za makabila kabla hujaoa/olewa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,890
6,899
Makabila hayatofautiani lugha pekee, ila mila na desturi pamoja na mahusiano kwenye ndoa zao pia huwa ni jamii inayojitofautisha na jamii ya kabila au makabila mengine.

Kuchepuka kwa wanandoa kwa baadhi ya makabila ni jambo la kawaida na wala halileti misukosuko mikubwa kwenye mahusiano katika jamii yao, limezoeleka na laonekana ni la kawaida tu. Usiyezoea desturi hiyo usioe/kuolewa huko, la sivyo utajimaliza kwa blood pressure kwa jambo ambalo katika desturi zao ni la kawaida sana.

Kuna rafiki yangu moja aliwahi kuniambia kuwa, kama ukimpenda mke wangu mchukue tu, niliduwaa na sikuamini kama mwanaume mwenzangu tena msomi aweza kuniambia hivyo na kuiachia green light kwa mke wake. Ikabidi nipunguze ukaribu kwao maana nimeanza kuzoeleka mno na ni kinyume kabisa na desturi zetu na kidini.

Kuna desturi twaambiwa katika jamii fulani ya wafugaji, jamaa ukifika nyumbani kwako na kuona jamaa kaweka mkuki mlangoni, we subiri amalize shughuli humo ndani, akitoka mpishe aende zake nawe maisha yaendelee na mke wako. Hilo likitokea kwa baadhi ya makabila itafumuka vita kali kati ya wasaksoni na wabaribariani✍🤣🤠

Matatizo ya ndoa nyingi kuvunjia mikanganyo mingi ni kutokana na kutofanyia utafiti wa tofauti za desturi zenye kupata mikanganyiko katika mahusiana, upekee wa desturi za mwenzi na mila zao. Tunakutana tu mijini na kuanza maisha bila kufanya utafiti na kufahamiana kutosha, na yatakayojilia, Lord God have mercy on us.
 
Hata mkioana watu wa kabila moja, kama hamtakuwa tayari kuchukuliana na kuvumiliana ndoa lazima iwashinde tu. Watu wanaoana leo, ila wanakuja kufahamiana vizuri na kukomaa baada ya miaka 10-15. Kuna kazi kubwa ambayo wote mnatakiwa kuifanya kwa uwazi bila kutegeana, ili kufanikiwa. Not a bed of roses at all.
 
Situation hii yaweza kutokea kama utafiti wa kutosha ungefanyika kubla ya kuanza mahusiano ya karibu zaidi
 

Attachments

  • FB_IMG_1679987820907.jpg
    FB_IMG_1679987820907.jpg
    20.6 KB · Views: 6
Nimeshindwa kabisa kuelewa kwanini mtu unamlinda mtu (18+) asifanye ngono na mtu mwingine.
 
Hata mkioana watu wa kabila moja, kama hamtakuwa tayari kuchukuliana na kuvumiliana ndoa lazima iwashinde tu. Watu wanaoana leo, ila wanakuja kufahamiana vizuri na kukomaa baada ya miaka 10-15. Kuna kazi kubwa ambayo wote mnatakiwa kuifanya kwa uwazi bila kutegeana, ili kufanikiwa. Not a bed of roses at all.
Mazoea hujenga tabia ambazo zikiendekezwa huwa desturi, tukifanya utafiti na kuelewa yawahusuyo wenzi wetu kwa mila, tabia na desturi zao, hatutakwazwa wala kushangaa kwa yanayojilia, Kwamba tutakuwa tumeyaelewa na kuyapokea kwa moyo na kuyaishi yatakayojitokeza kutokana na desturi zao kwa yanayojitokeza kutokana na mila, tabia na desturi zao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom