Martoism
Member
- May 31, 2012
- 36
- 21
Huwezi amini kinachoendelea hivi sasa katika viunga vya manispaa ya Iringa mjini, Askari wasio na idadi wenye silaha nzito pamoja na magari yaliyofungwa vitaambaa vyekundu kuashiria hali ya hatari yanarandaranda kutisha wananchi, aidha wasifanye maandamano, fujo au wasihudhurie kabisa mkutano wa CHADEMA Unaotarajiwa kufanyika uwanja maarufu wa mwembetogwa.
Hivi sasa niko eneo moja linaitwa Kihesa, mbunge wa viti maalumu Mh, Chiku Abwao amezingirwa na FFU kwenye gari yake, huku Mh, Msigwa akikaririwa leo na kituo cha Redio cha Ebony FM kuwa chama chake hakitafanya maandamano bali watafanya mkutano wa hadhara kuanzia saa 8 mchana hadi 12 jioni.
Ntaendelea kuwajuza kila linalojiri wakuu.....