Exclusive: Ikulu hawataki MNF ijenge "twin towers" karibu yao

Je majengo yote yaliyoko Dar ya vitega uchumi yahamishiwe Dodoma au ni hili la MNF tu? Au mnapendekeza kuwa watu wasiwekeze tena Dar kwani tayari kumeshajazana au ni MNF ndio wataongeza kisichowezekana kuwepo? Hivi, ingekuwa taasisi ya kigeni ungeweza kusema security issue.. taasisi ya Mwalimu inatishia usalama wa Ikulu? really! Kwani walioenda kumtumia mkapa kuvunja sheria na waliopandikiza watu wao kwenye Ikulu ya JK leo hii walivunja wapi ili waingie? Usalama wa Ikulu hautishiwi na majengo!

Lakini si kila cha kumwenzi Nyerere ni halali, na ni kweli si salama kujenga hayo majengo marefu kuzunguka ikulu. Pia umesema Wachina ni wabia, hao ni hatari kabisa kua karibu na Ikulu. Halafu kwa kua ni biashara Ikulu itashindwa kuzuia wapangaji wasiowataka kupanga ndani ya hilo jengo karibu na Ikulu.

Uhusiano wa wahusika na CCJ si nongwa ili mradi CCJ imepewa uwanja halali wa kupambana kisiasa na uhuru wote kwenda kwenye vyombo vya sheria - kama ni kweli pia si nongwa maana ni ubinadamu tu kua hutampedelea mpinzani wako hasa unapojua unampa power mdomoni. CCJ wapo kutuonyesha uwezo wao wa kupambana na CCM wala si kuonewa huruma na CCM.
 
inawezekana pia likawa limeingia kwenye security zone ya ikulu na hayo mengine hayajaingia! hatujui mpaka wa security zone ni wapi

watu wa mipango miji labda wanaweza kutusaidia kwa hili
 
Kwani lazima taasisi hiyo ijenge karibu na Ikulu???? halafu iweje mimi ninadhani kwanza tungefanya utafiti maeneo yale katika mipango miji imepanga vipi matumizi ya ardhi eneo lile kwani nina kumbuka kuna kipindi Wawekezaji walitaka kujenga hoteli ya nyota tano karibu ya eneo hilo walikataliwa.
Ombi langu ndugu zangu JF inasomwa na wengi sana na taaswira ya taasisi hii ni aina ya michango itolewayo na kuchangia. Hivi karibuni kumezuka tabia ya kuleta vitu visivyo wiva vizuri hapa jamvini. Sasa wageni tuwaalikao wanatuona vipi?????
Ninajua hili litawakwaza baadhi yetu lakini ni lazima lisemwe au tunataka MOD afanye mchujo??????
 
Wakuu zangu,
Kusema kweli mnachekesha sana..Yaani tumeingia Ubepari pasipo kufahamu umuhimu wa majengo ktk revenue za mji yetu!?... akili zenu bado za Kijamaa kabisa kuliko hata Nyerere mwenyewe kiasi kwamba ajengo marefu kwetu ni maghorofa tu! sababu ati usalama wa IKULU, tunamwogopa nani haswa? Maanake marais wetu hawakosi vijiweni na sehemu ambazo hazina usalama kabisa, tunalinda kitu gani haswa!

Hivi kuna mtu kati yenu anaweza kunambia ni kiasi gani cha fedha mji kama New York unaingiza kutokana na kodi za upangaji!...Au jiulizeni miji yote ya North Amerika inaendeleza hizo states kwa sababu gani? Kisha mnazungumzia ati MNF wakajenge Temeke sijui Tandika hali kuna Taasisi za serikali na chama zinapewa viwanja mjini pasipo hata kulipia gharama kamili...Ni kiasi gani MNF watapangisha jengo kama hilo huko Temeke au Tandika...hata nyie mkipata kiwanja huko hamtajenga lakini wepesi kusema WAKAJENGE!..

Hapa swala sio MNF ila ni sababu zinazotolewa na Ikulu kuhusiana na uwekezaji... kisha basi ni rahisi kwenu kukubali wananchi wafukuzwe toka makazi yao kwa ajili ya Uwekezaji tena sehemu nyingine watu kuuawa lakini mmekuwa wazito kufikiria jambo hili lenye manufaa makubwa na pato la Halmashauri zetu. Ukitazama ramani ya Dar utalia machozi kuona tunajibana bana kutokana na ukomunist wetu (roho mbaya)....

Wakuu zangu tumeingia Ubepari ni lazima tufanye kazi Kibepari, Halamashauri za miji zinatakiwa kujiendesha, halmashauri zinatakiwa kukuza miji yao na moja ya mipango mikubwa ni pamoja na kuvutia wawekezaji ktk real estate ambako pato kubwa la halmashauri hizi hutokea. Hadi leo kodi za parking area zinachukuliwa na mtu binafsi, kodi za nyumba zote za serikali ni mali ya serikali sio Halmashauri, Hakuna kodi za Wapangaji (rent) na kama ipo inakwenda serikali kuu,kisha mnadai serikali hai control njia za uchumi..

Kifupi Tanzania bado kabisa tunatumia fikra za KIKOMUNISTkatika kuendesha biashara na hii ni moja ya matatizo makubwa yanayosababisha Corruption za viongozi wetu. Na ndio maana hawataki kuhamia Dodoma kwa sababu za kipuuzi kama hizi.kama serikali walielewa Dodoma hakufai kwa nini wakajenga Bunge Dodoma hali makao makuu yao wakayaacha Dar. Kwa nini wasijenge Bunge Dar tukajua moja, kuliko kila siku za bunge hawaishi misafara ya kurudi Dar..
 
Wakuu zangu,
Kusema kweli mnachekesha sana..Yaani tumeingia Ubepari pasipo kufahamu umuhimu wa majengo ktk revenue za mji yetu!?... akili zenu bado za Kijamaa kabisa kuliko hata Nyerere mwenyewe kiasi kwamba ajengo marefu kwetu ni maghorofa tu! sababu ati usalama wa IKULU, tunamwogopa nani haswa? Maanake marais wetu hawakosi vijiweni na sehemu ambazo hazina usalama kabisa, tunalinda kitu gani haswa!

Hivi kuna mtu kati yenu anaweza kunambia ni kiasi gani cha fedha mji kama New York unaingiza kutokana na kodi za upangaji!...Au jiulizeni miji yote ya North Amerika inaendeleza hizo states kwa sababu gani? Kisha mnazungumzia ati MNF wakajenge Temeke sijui Tandika hali kuna Taasisi za serikali na chama zinapewa viwanja mjini pasipo hata kulipia gharama kamili...Ni kiasi gani MNF watapangisha jengo kama hilo huko Temeke au Tandika...hata nyie mkipata kiwanja huko hamtajenga lakini wepesi kusema WAKAJENGE!..

Hapa swala sio MNF ila ni sababu zinazotolewa na Ikulu kuhusiana na uwekezaji... kisha basi ni rahisi kwenu kukubali wananchi wafukuzwe toka makazi yao kwa ajili ya Uwekezaji tena sehemu nyingine watu kuuawa lakini mmekuwa wazito kufikiria jambo hili lenye manufaa makubwa na pato la Halmashauri zetu. Ukitazama ramani ya Dar utalia machozi kuona tunajibana bana kutokana na ukomunist wetu (roho mbaya)....

Wakuu zangu tumeingia Ubepari ni lazima tufanye kazi Kibepari, Halamashauri za miji zinatakiwa kujiendesha, halmashauri zinatakiwa kukuza miji yao na moja ya mipango mikubwa ni pamoja na kuvutia wawekezaji ktk real estate ambako pato kubwa la halmashauri hizi hutokea. Hadi leo kodi za parking area zinachukuliwa na mtu binafsi, kodi za nyumba zote za serikali ni mali ya serikali sio Halmashauri, Hakuna kodi za Wapangaji (rent) na kama ipo inakwenda serikali kuu,kisha mnadai serikali hai control njia za uchumi..

Kifupi Tanzania bado kabisa tunatumia fikra za KIKOMUNISTkatika kuendesha biashara na hii ni moja ya matatizo makubwa yanayosababisha Corruption za viongozi wetu. Na ndio maana hawataki kuhamia Dodoma kwa sababu za kipuuzi kama hizi.kama serikali walielewa Dodoma hakufai kwa nini wakajenga Bunge Dodoma hali makao makuu yao wakayaacha Dar. Kwa nini wasijenge Bunge Dar tukajua moja, kuliko kila siku za bunge hawaishi misafara ya kurudi Dar..

Mkuu, watu hawapangi katikati ya nji kwa sababu tu ni fahari kukaa huko. Kinachowavuta huko ni ukaribu na urahisi wa huduma. Kutokana na huduma mbovu ( muda unaopotezwa kuingia na kutoka City Centre yetu, namna ya kutembea aktikatikati ya mji, matatizo ya parking, umeme usioaminika n.k.) zilizopo katikati ya mji mabepari wa maana hawako tayari kulipa hayo mapesa ambayo wenye majengo wanadhani ni haki yao. Ukizingatia idadi ya maghorofa yanayojengwa sasa hivi bila kuboresha infrastructure, mpaka hapo hilo jengo la MNF litakapomalizika watakaotaka kupanga humo watabaki wamachinga peke yao. Kama wanataka kuendekeza ubepari basi hapo wangejenga kitu modest zaidi, k.m. hoteli ambayo wangempa mtu ai-manage kwa niaba yao. Huu mradi wao ni bomu na kama watajenga watajuta. Hakuna bepari wa maana ata-invest kwenye kitu kama hiki.

Amandla......
 
Lakini si kila cha kumwenzi Nyerere ni halali, na ni kweli si salama kujenga hayo majengo marefu kuzunguka ikulu. Pia umesema Wachina ni wabia, hao ni hatari kabisa kua karibu na Ikulu. Halafu kwa kua ni biashara Ikulu itashindwa kuzuia wapangaji wasiowataka kupanga ndani ya hilo jengo karibu na Ikulu.

Huo uwezo wa serikali ya kidemokrasia kuwaamulia private entity nani awe mpangaji au asiwe wao Ikulu wameupata wapi? Hivi Ikulu kwako ni kama jumba la mfalme?
 
Kwani lazima taasisi hiyo ijenge karibu na Ikulu???? halafu iweje mimi ninadhani kwanza tungefanya utafiti maeneo yale katika mipango miji imepanga vipi matumizi ya ardhi eneo lile kwani nina kumbuka kuna kipindi Wawekezaji walitaka kujenga hoteli ya nyota tano karibu ya eneo hilo walikataliwa.
wewe serikali yawekezekana wakija nyumbani kwako na kukuambia uhamishe kitanda kwa sababu kinatishia usalama wa taifa utahamisha bila maswali. Ni hatari.

Ombi langu ndugu zangu JF inasomwa na wengi sana na taaswira ya taasisi hii ni aina ya michango itolewayo na kuchangia. Hivi karibuni kumezuka tabia ya kuleta vitu visivyo wiva vizuri hapa jamvini. Sasa wageni tuwaalikao wanatuona vipi?????

Ukiishi kwa kufikiria ati nani atafikiri ninii au watu watanionaje au sijui wageni watafikiria nini unajiweka katika huruma yao. Maisha na mawazo ya mwanadamu ni mchanganyiko ya chungu na tamu, furaha na karaha, ya busara na ya upuuzi, ya kimwili na ya kiroho.. wenzetu wachina wanaona ni mambo ya ying and yang!
 
Hivi ukiwa ghorofa za juu Ardhi House hauoni Ikulu? Au wizara ya elimu? Ni nani anahakikisha kuwa wote wanaotembelea majengo haya wana nia njema? Kisingizio cha usalama does not hold water. Hasa wakati huu wa Google Earth!

Amandla.......
 
Good thread lakini kama kawa hukufika mbali ukaweka sisije!!!

Mwanakijiji ukweli ni kwamba kuna hilo tatizo la security zote na ni bahati mbaya baadhi ya majengo yalipenya hiyo porous vetting syste yetu na kuweza kuendelea, mfano ni hilo pembeni ya nyumba za "watumishi" karibu na hospitali

there are two ways to deal with this matter positively, bila kulialia kama ambavyo tumeona viongozi wa CCJ wakifanya [nasema hivi kwasababu CCJ inakua maarufu zaidi kwa kulalama kuliko kupata mbinu mbadala za kuachieve wanachotaka

  • kwanza wajenge hizo ghorofa sita kama wanavyoweza kupewa hiyo hati
  • pili wauze hilo eneo wajenge nyingine elsewhere kwenye kuruhsiwa, maeneo yama ya mkapa tower, exim tower au hata ali hassan mwinyi road
kwani nani alisema lazima wawe karibu na ikulu?? mji wenyewe uko congested, barabara hakuna [hata mtu akiachia hewa chafu - inachukua masaa hewa ku-clear], sasa kwanini basi nao wasingeenda hata kigamboni, karibu na chuo cha mwalimu nyerere kutafuta eneo na kuweka hicho kitega uchumi??

Mmmm, akili za mbayuwayu changanya na za kwako. Bila shaka utapata jawabu.
 
Mkuu, watu hawapangi katikati ya nji kwa sababu tu ni fahari kukaa huko. Kinachowavuta huko ni ukaribu na urahisi wa huduma. Kutokana na huduma mbovu ( muda unaopotezwa kuingia na kutoka City Centre yetu, namna ya kutembea aktikatikati ya mji, matatizo ya parking, umeme usioaminika n.k.) zilizopo katikati ya mji mabepari wa maana hawako tayari kulipa hayo mapesa ambayo wenye majengo wanadhani ni haki yao. Ukizingatia idadi ya maghorofa yanayojengwa sasa hivi bila kuboresha infrastructure, mpaka hapo hilo jengo la MNF litakapomalizika watakaotaka kupanga humo watabaki wamachinga peke yao. Kama wanataka kuendekeza ubepari basi hapo wangejenga kitu modest zaidi, k.m. hoteli ambayo wangempa mtu ai-manage kwa niaba yao. Huu mradi wao ni bomu na kama watajenga watajuta. Hakuna bepari wa maana ata-invest kwenye kitu kama hiki.

Amandla......
Mkuu wangu upo Dar au unaandika kwa kufikiria tu... Kifupi nothing in Dar make sense kabisa inapofikia maswala ya feza na gharama. Leo hii upangaji mjini ofisi moja sii chini ya dollar 1000 nyumba ya msajili u NHC, kijiofisi cha mtaa wa Chagga utalipa Usd 600. Majengo mapya yote wanalipa sii chini ya Usd 2000 hadi 4000. Na swala la kuishi nyumba za NHC au msajili mjini wanatoza Usd 50,000 hadi 100,000 kwa ufunguo tu yaani nyumba ya serikali wanaingiza jina lako kama mpangaji wa NHC au Msajili..Kila kitu ni Usd hazipokelewi hela za madafu mkubwa...hakuna kitu kinaingia mfuko wa serikali wala Halmashauri ila kwa kina chumia tumbo - Hii ndio Tanzania yetu.

Yes, kuna mambo mengi sana mabovu, tumeujenga mjii juu ya Infrastructure mbovu na tunaendelea kujenga na sii kwamba tumesimamisha ujenzi ili kuanza kuboresha miundo mbinu, sasa nachoshindwa mimi kuelewa why jengo hili la MNF ndio liwe issue?..Je, leo tumesahau kabisa kwamba MNF ni taasisi iliyoanzishwa na mwalimu! Kweli, ndio kusema tumekosa kabisa kuweka heshima yetu kwa kiongozi aliyetufikisha hapa tulipo kwa sababu tu ya Uadui baina ya wanachama au wafuasi wake..
Hivi kweli Demokrasia inaweza fanya kazi kwetu ikiwa Upinzani maana yake kwetu ni Uadui?..
Kwa mtazamo wangu, sioni kabisa sababu kufikia hali kama hii kiasi kwamba MNF inatazamwa kama ni chombo cha kina Butiku..Kisha basi kuna tatizo gani Butiku anapowakosoa viongozi wetu inapohusu code of conduct?
 
Back
Top Bottom