Exclusive: Ikulu hawataki MNF ijenge "twin towers" karibu yao

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Habari nilizonazo ni kwamba MNF (Mwalimu Nyerere Foundation) walitaka kujenga jengo la ghorofa 14 na 20 twin towers kama kitegauchumi kitakachoiwezesha taasisi kujiendesha yenyewe bila kutegemea michango ambayo kwa sasa haipatikani toka kwa mtu yoyote yule. Jengo hilo ilikuwa lianze kujengwa tangu mwaka jana lakini cha kusikitisha ni kwamba Wachina CRJE ambao ndio wajenzi walipotaka wapate building permit wajenge Halmashauri ya Jiji Ilala wakawaambia kwamba hawawezi kutoa building permit kwa sababu eneo hilo halipaswi kujengwa majengo yanayozidi gorofa 6 au tano sikumbuki vizuri.

Wakasema kwamba maagizo hayo yametoka kwenye kikao kilichofanyika Ikulu. Lakini ukiangalia katika eneo ambalo linadaiwa kwamba ni Security zone ya Ikulu yapo majengo mengine ambayo ni marefu na moja linaendelea kujengwa as we speak lina gorofa zaidi ya 20 pale karibu na Ocean Road.

Taasisi wamejaribu kupata waiver kwa kuwa ni mradi uliobuniwa na Baba wa Taifa mwenyewe wakati akiwa Mwenyekiti Mwanzalishi wa Taasisi. Ikulu imeziba masikio. wanadai Taasisi wapewe eneo jingine. Kama ni kupewa eneo jingine lazima liwe kwenye central area ili kuweza kupata wateja wauhakika kama ilivyodhamiriwa ili kuweza kurejesha fedha za Wachina na wabia wengine kama ADB, World Bank etc waliojitolea kuchangia ujenzi huo.

Ni wazi kwamba Ikulu wanakataa makusudi maana hakuna sababu yoyote ya kushindwa kuruhusu jengo linalobeba jina la Baba wa Taifa kujengwa katika eneo hilo kwa kuwa yapo majengo mengine marefu zaidi.

Vyanzo vya ndani vinasema watu wa Ikulu wanaogopa sana kuipa ujiko taasisi hiyo hasa kutokana na mwamko unaoendelea taratibu wa mawazo na fikra za Mwalimu kuhusu Taifa na hasa baadhi ya watu mashuhuri ambao sasa hawaoni tatizo kujipanga na fikra hizo. Lakini nyuma ya yote ni hofu kuwa yawezekana wakuu wa sasa wa MNF wanahusiana na CCJ na kama taasisi ikiweza kujijenga namna hiyo inaweza kuwa huru kweli na tishio hasa ikiwa karibu hivyo na Ikulu.

Hivyo, sitoshangaa endapo taasisi wakajikuta wanahamishiwa pembezoni mwa jiji...
 
this is serious!
tatizo HASA HASA NI NINI?

-i mean hao CCJ wamekuwa mwiba kiasi hicho?
-au tuseme hao CCM hawana confidence kiasi hicho?
-au wameona ile mbinu ya ''magumashi kwenye masanduku ya kura'' haita work this tym around?
 
Lakini MKJJ,

Fikra za Mwl Nyerere si zilikuwa kuendeleza Dodoma? Au mwishowe alibadili mawazo?

Kujenga ghorofa kama hilo katikati ya Dar ni kuchangia tatizo liliopo.

Mimi napendekeza wapeleke 'maendeleo' Dodoma, wakawekeze huko!!
 
Lakini MKJJ,

Fikra za Mwl Nyerere si zilikuwa kuendeleza Dodoma? Au mwishowe alibadili mawazo?

Kujenga ghorofa kama hilo katikati ya Dar ni kuchangia tatizo liliopo.

Mimi napendekeza wapeleke 'maendeleo' Dodoma, wakawekeze huko!!
jaribu kurejea hoja ya ''AZMA'' ya huo mjengo....
SIO KUENDELEZA DODOMA BANA...
huo mjengo is one thing,and DODOMA is another cup of tea
 
Good thread lakini kama kawa hukufika mbali ukaweka sisije!!!

Mwanakijiji ukweli ni kwamba kuna hilo tatizo la security zote na ni bahati mbaya baadhi ya majengo yalipenya hiyo porous vetting syste yetu na kuweza kuendelea, mfano ni hilo pembeni ya nyumba za "watumishi" karibu na hospitali

there are two ways to deal with this matter positively, bila kulialia kama ambavyo tumeona viongozi wa CCJ wakifanya [nasema hivi kwasababu CCJ inakua maarufu zaidi kwa kulalama kuliko kupata mbinu mbadala za kuachieve wanachotaka

  • kwanza wajenge hizo ghorofa sita kama wanavyoweza kupewa hiyo hati
  • pili wauze hilo eneo wajenge nyingine elsewhere kwenye kuruhsiwa, maeneo yama ya mkapa tower, exim tower au hata ali hassan mwinyi road

kwani nani alisema lazima wawe karibu na ikulu?? mji wenyewe uko congested, barabara hakuna [hata mtu akiachia hewa chafu - inachukua masaa hewa ku-clear], sasa kwanini basi nao wasingeenda hata kigamboni, karibu na chuo cha mwalimu nyerere kutafuta eneo na kuweka hicho kitega uchumi??
 
jaribu kurejea hoja ya ''AZMA'' ya huo mjengo....
SIO KUENDELEZA DODOMA BANA...
huo mjengo is one thing,and DODOMA is another cup of tea

Injinia ana point muhimu sana, hasa kama unakumbuka "zidumu fikra sahihi za mwenyeheri"!!!
 
Je majengo yote yaliyoko Dar ya vitega uchumi yahamishiwe Dodoma au ni hili la MNF tu? Au mnapendekeza kuwa watu wasiwekeze tena Dar kwani tayari kumeshajazana au ni MNF ndio wataongeza kisichowezekana kuwepo? Hivi, ingekuwa taasisi ya kigeni ungeweza kusema security issue.. taasisi ya Mwalimu inatishia usalama wa Ikulu? really! Kwani walioenda kumtumia mkapa kuvunja sheria na waliopandikiza watu wao kwenye Ikulu ya JK leo hii walivunja wapi ili waingie? Usalama wa Ikulu hautishiwi na majengo!
 
hawa sisijei hawa WAMEKUWA THREAT kwenye chama cha de-novo
hahahahahaha!
 
jaribu kurejea hoja ya ''AZMA'' ya huo mjengo....
SIO KUENDELEZA DODOMA BANA...
huo mjengo is one thing,and DODOMA is another cup of tea


'Azma' haijatengenezwa kwa sementi useme haibadiliki.

Kama haiwezekani ( na kweli haiwezekani, si tu kwa ajili ya usalama wa Ikulu, pia kwa sababu nilizokwisha taja kabla) wabadilishe hiyo azma!
 
Je majengo yote yaliyoko Dar ya vitega uchumi yahamishiwe Dodoma au ni hili la MNF tu? Au mnapendekeza kuwa watu wasiwekeze tena Dar kwani tayari kumeshajazana au ni MNF ndio wataongeza kisichowezekana kuwepo? Hivi, ingekuwa taasisi ya kigeni ungeweza kusema security issue.. taasisi ya Mwalimu inatishia usalama wa Ikulu? really! Kwani walioenda kumtumia mkapa kuvunja sheria na waliopandikiza watu wao kwenye Ikulu ya JK leo hii walivunja wapi ili waingie? Usalama wa Ikulu hautishiwi na majengo!

you are very right MMM, tatizo sasa wao wameona hivyo na dawa si kupiga mbinja bali kuangalia mbadala... msipoangalia mtaishia kuwa kama mtikila ila mtamzidi kidogo kwenye kulialia!!!

WHERE IS GT WHEN YOU NEED HIM?

nothing personal against CCJ but too much complaining is linked to certain psychotic disorders... KUMBUKA NYERERE ALIWAHI KUELEZEA JINSI WALIVYO-DEFY SOME EXPECTATIONS ZA WABAYA WAO KWA KUFANYA WASICHOTEGEMEA... TODAY IF MNF WAKIAMUA KUJENGA KWINGINE BASI HAWATANYIMWA HIYO PERMIT

TRY IT
 
Kwani fikra za kuendelea kutumia hii IKULU ya sasa bado zinalindwa kihivyo?. Mbona kama TWIN TOWERS ni eneo la karibu zaidi ukiacha hilo la Ocean Road?. Kwa nini Wasihamishe IKULU kupisha Uwwekezaji wa maendeleo ya Nchi?. Usalama uko wapi ikuwa hapa ofisi za shuhuli binafsi kama za WAMA zilishawahi kuruhusiwa kufanyia mambo humo humo IKULU?.
 
De Novo.. CCJ haihusiani na ujenzi wa MNF wala MNF haihusiani na CCJ. NI watu wengine ndio wenye hofu hizo. Ninachozungumzia hapa ni MNF ambayo ni taasisi ambayo Nyerere mwenyewe aliianzisha na toka wakati huo alikuwa ameshapata na hilo eneo.. sasa kwa nini leo wahamishwe? Kisa CCJ?

Hakuna mtu anayelia lia kuhusu CCJ ila kama kudai haki na usawa ni kulia lia basi tutalia sana kwani hakuna aibu kulia ukidai haki yako. Unataka tukae tu kimya na kukubali kwa sababu "serikali imesema". Yaani serikali ije kutusukumiza halafu tukubali kusukumwa kwa sababu tukilalamika tutakuwa tunalia lia. Haya ndiyo mawazo yamewafanya watanzania kuwa wanasukumwa sukumwa na serikali yao.

kwenye CCJ mstari umeshachorwa hatuuvuki..
 
'Azma' haijatengenezwa kwa sementi useme haibadiliki.

Kama haiwezekani ( na kweli haiwezekani, si tu kwa ajili ya usalama wa Ikulu, pia kwa sababu nilizokwisha taja kabla) wabadilishe hiyo azma!


Majengo yaliyopo na mengine yanayojengwa yasitishwe au ni hii MNF ndiyo inatakiwa kubadilisha azma yake?
 
As long as Kikwete ni rais Ikulu na as long as Salim Ahmed Salim na Joseph Butiku wako MNF kibali hakitatolewa.
 
Juzi juzi kuna kichaa aliingia Ikulu. Hivi alipitapitaje pale getini?
 
Habari nilizonazo ni kwamba MNF (Mwalimu Nyerere Foundation) walitaka kujenga jengo la ghorofa 14 na 20 twin towers kama kitegauchumi kitakachoiwezesha taasisi kujiendesha yenyewe bila kutegemea michango ambayo kwa sasa haipatikani toka kwa mtu yoyote yule. Jengo hilo ilikuwa lianze kujengwa tangu mwaka jana lakini cha kusikitisha ni kwamba Wachina CRJE ambao ndio wajenzi walipotaka wapate building permit wajenge Halmashauri ya Jiji Ilala wakawaambia kwamba hawawezi kutoa building permit kwa sababu eneo hilo halipaswi kujengwa majengo yanayozidi gorofa 6 au tano sikumbuki vizuri.

Wakasema kwamba maagizo hayo yametoka kwenye kikao kilichofanyika Ikulu. Lakini ukiangalia katika eneo ambalo linadaiwa kwamba ni Security zone ya Ikulu yapo majengo mengine ambayo ni marefu na moja linaendelea kujengwa as we speak lina gorofa zaidi ya 20 pale karibu na Ocean Road.

Taasisi wamejaribu kupata waiver kwa kuwa ni mradi uliobuniwa na Baba wa Taifa mwenyewe wakati akiwa Mwenyekiti Mwanzalishi wa Taasisi. Ikulu imeziba masikio. wanadai Taasisi wapewe eneo jingine. Kama ni kupewa eneo jingine lazima liwe kwenye central area ili kuweza kupata wateja wauhakika kama ilivyodhamiriwa ili kuweza kurejesha fedha za Wachina na wabia wengine kama ADB, World Bank etc waliojitolea kuchangia ujenzi huo.

Ni wazi kwamba Ikulu wanakataa makusudi maana hakuna sababu yoyote ya kushindwa kuruhusu jengo linalobeba jina la Baba wa Taifa kujengwa katika eneo hilo kwa kuwa yapo majengo mengine marefu zaidi.

Vyanzo vya ndani vinasema watu wa Ikulu wanaogopa sana kuipa ujiko taasisi hiyo hasa kutokana na mwamko unaoendelea taratibu wa mawazo na fikra za Mwalimu kuhusu Taifa na hasa baadhi ya watu mashuhuri ambao sasa hawaoni tatizo kujipanga na fikra hizo. Lakini nyuma ya yote ni hofu kuwa yawezekana wakuu wa sasa wa MNF wanahusiana na CCJ na kama taasisi ikiweza kujijenga namna hiyo inaweza kuwa huru kweli na tishio hasa ikiwa karibu hivyo na Ikulu.

Hivyo, sitoshangaa endapo taasisi wakajikuta wanahamishiwa pembezoni mwa jiji...

Kwa Point ya usalama hapa IKULU wanasababu ambazo kwa mtu yeyote rational atakubali kuwa ni risk sana kwa Ikulu kuzunguukwa na majengo ya kibiashara yanayoizi urefu IKULU yenyewe, yaani mtu anaweza kuwa juu ya ghorofa ya 10 akaona what is taking placing on the ground of The State House.

But Ili IKULU ioneshe kuwa hoja yao ina nguvu walitakiwa ama kubomoa au kusimamisha ujenzi wa majengo yote yanayozidi ghorofa 6 katika perimeter ambayo wao wanaiona ni security zone. Vinginevyo watakuwa wanaruhusu Politics kuchukua mkondo wake na kwa kuwa hili halijafanyika basi inanilazimu kuamini hoja ya Mkjj ina ukweli
 
Majengo yaliyopo na mengine yanayojengwa yasitishwe au ni hii MNF ndiyo inatakiwa kubadilisha azma yake?

Yaani hujanielewa MKKJ, mimi sipo dhidi ya MNF!! Ninachosema ni kuwa, kama wanazibiwa (au wanaona kuwa wanazibiwa) basi wakawekeze kwingine, Tanzania si moja?

Kama kuna majengo mengine yanayojengwa na hayafuati utaratibu huo wa 'ghorofa 6 mwisho', basi ndiyo, na yenyewe yasitishwe!!
 
Back
Top Bottom