Habari wana jf mimi nina rafiki yangu wa karibu sana alikua ana mpenzi wake walikua wanapendana sana.Ila hasa hasa alieonesha upendo wa dhati ni binti ambae alijitorea mambo mengi kwa ajiri ya huyu jamaa yangu kwani kwao na binti angalau mambo si mabaya na waliweza kukaa kwenye uhusiano takribani miaka minne na haikuwahi kusika au kufahamika kua huyu binti alikua na uhusiano na mtu mwingine pale mtaani kwetu hata siku moja.Huyu dada baada ya kumaliza kidato cha nne alikwenda Tanga ili kurudia mtihani wa kidato cha nne pindi tu ameondoka walikuja walimu wapya wa shule ya msingi ghafra jamaa yangu akawa ameanza mahusiano na mwalimu mmoja baada ya wiki mbili wakawa wameanza kuishi pamoja mpaka sasa ni mwaka wa tatu wako pamoja na wamesha zaa mtoto mmoja na jamaa yangu kisha toa mahari ili afunge ndoa na huyu mwalimu. Mara nyingi turiendelea kuandikana sms na huyu dada za kusalimiana na kutakiana maisha mema. Siku moja nikapokea ujumbe kutoka kwake kua ananipenda sana ila alikua anashindwa kuniambia na anataka tuoane. Nili mkataria nikamwambia ni swala ambalo hariwezekani kwani yeye alikua mpenzi wa rafiki yangu nita mueleza je? Jamaa yangu ili anielewe. Aliniambia mambo kama manne kuwa jamaa atakuwa mnafiki na kumzibia riziki kwani alimuacha hata bila kumtendea kosa lolote. Pili ingekua yeye ndio alimuacha alikua na haki ya kuraum. Tatu labda wangeacha kwa ajiri ya migogoro baina yao pia angelaumu. Bado anaendelea kunisisitiza nia yake ya kuishi na mimi nikafikia wakati kumuambia kua anatafuta njia ya kuripiza kisasi kwa ajiri ya kumuumiza jamaa yangu lakini amekataa vya kufa anadai yeye anacho angalia ni maisha yake ya baadae na sio visasi kwani mimi ninamfaa. Kiukweli kwangu mimi huyu binti nimetokea kumpenda ili niweze kuishi nae lakini tatizo ni huyu rafiki yangu atanichukuliaje? Jamani naombeni ushauri wenu