EWURA waridhia kupandisha bei mafuta, bei mpya hizi hapa!

Status
Not open for further replies.
BP WATAISHITAKI EWURA NA KUTAKA WALIPWE HASARA WALIYOPATA KWA KUUZA MAFUTA KWA BEI YA HASARA: NA KUFUNGIWA KWA KUWA MGOMO WAO ULIKUWA HALARI:






Fuatilia: na Wale wanaobisha kilakitu bisheni na hili,
 
Huu ni utapeli wa serikali dhidi ya watanzania.
kama kawaida, wametusikiliziaaa, wakaona tumetulia, bajeti yao imepita, then, wamepandisha bei.
 
tumia ubongo kufikiri na sio macho tuu kusoma basi, huelewi kitu kaaa kimya, inawezekana huna hata gari so hujui uchungu wa sisi wenye kutumia fedha zetu, elezea bei imepandaje toka 2004 hadi 2114 nipe formula kama unayo, mimi nipo jikoni nasema ewura wanatudanganya, bisha kwa hoja, unasoma huo utumbo na unakubali??

Je unajua kama ewura waliwaomba wauza mafuta wauze kwa hasara na wiki hii watawafidia kwa kupandisha bei?

Walikuwa wana uza 2040, that means wakashushwa kwa tshs 36, na sasa wamerudishiwa ile 36 x 2 = 72 + ths ( ya usumbufu) bado unachekelea tuu ujinga unaofanywa na watu wachache

Whatever you say, Hujajibu swali langu la msingi. Wamerekebisha nini kwenye hiyo costing model??!!!unachotaka kutuaminisha hapa ni kwamba costing model iliyotumika kupata 2004 ni tofauti na ya sasa iliyotumika kupata 2114.
 
Maneno na maandiko yoyote yale, hata kama yatafanywa kwa ufasaha na umakini mkubwa kupita maelezo hayana maana yoyote ile kama matendo yatokanayo na hayo hayaisaidii jamii.
Wapumbavu siku zote hung'anga'na kwenye maneno na maandiko tu lakini werevu wanahangaikia zaidi matendo yanayowasaidia kuondokana na shida zao.
EWURA inaisaidia vipi serikali kuinua hali za kiuchumi za wananchi masikini?
EWURA siyo muhuri wa makampuni ya mafuta kuhalalisha bei wanazozitaka?
EWURA siyo mzigo usio na faida yoyote kwa mtanzania wa kawaida kupitia tozo zake?
 
Maisha magumu magunmu magumu magumu ikifika 2015 petrol itakuwa 4000 kilo ya sukari 6000 maharage 4000
...Kweli tupu nilikuwa kigoma kilo ya sukari 2,800/= tena ya kutoka Zambia. Sijui Mtibwa na Kagera Sugar nao kwishney??
 
Jumamosi Bajeti inapita, Jumapili bei ya mafuta inapanda....Na bado ya umeme nayo inapanda muda si mrefu...

CCM yajenga nchiiiiii!!!
 
Umenivunja mbavu aisee! Ila ni kweli hivi kweli serikali inaweza kujifunga?

<font size="4"><span style="font-family: comic sans ms">BP imefungiwa kwa miezi mitztu inz maana serikali imejifungia yenyewe? Kama ni hivyo basi EWURA ni mtori sana.</span></font>
<br />
<br />
 
Nafikiri sasa EWURA lazima ijuna ifanye kazi kisayansi zaidi sio kisiasa. Lazima wajue kuwa kwenye biashara hakuna siasa. Ni budu washirikiane na wadau wote katika kupanga bei na kusimamia hilo sio kuleta bla bla za kisi asa
 
tatizo la kufikiria kutumia masaburi ndo hili. Kwani tuna visima hapa TZ? bei ya mafuta yanapangwa na soko la dunia na sisi ni sehemu yake. Hata akiongoza slaa hamna anachoweza kufanya labda kama atagundua visima kule kwao karatu. Think kwa kutumia upstairs.
Pamoja na kwamba bei ya mafuta inapangwa na soko la dunia, tatizo kubwa la nchi yetu ni utitiri wa kodi, usimamizi mbovu wa uchumi wetu unaopelekea shilingi yetu kukosa nguvu ya soko na ufisadi, na kwa taarifa yako hivi vyote vinataka mtu makini, chama makini na serikali makini kuvisimamia (ambavyo havipatikani ccm) vinginevyo kwa "umasaburi" wenu mtabaki mkisema yeyote akiongoza ndivyo itakavyokuwa.

Kama wewe unafikiri vyema uliwahi kujniuliza Kenya wanaagiza wapi mafuta yao kiasi kwamba bei nchini kwao ni rahisi kulinganisha na kwetu licha ya ulanguzi wa ubadilishanaji peza mipakani? Hata wao waagiza kwenye soko lile lile tunalokwenda sisi kwa hiyo hapa anayefikiri ki "masaburi" au kwa kutumia "tumbo" au "downstairs" utakuwa wewe na wenzako wote wenye mawazo kama ya kwako.
 
Hivi ni gharama kiasi gani pamoja na manunuzi hawa mabepari huwa wanatumia kuingiza lita moja ya mafuta hapa nchini?Maana naona kuna usanii huwa unafanywa,wanatuchezea.
 
Neng'uli nachojaribu kufanya hapa ni kuonyesha kuwa , wafanyabiashara wa mafuta walikuwa na haki ya kugoma wiki iliopita hii sio sahihi ndugu yangu ,EWURA hawakukosea chochote , serikali iliondea sehemu ya kodi zake , na EWURA walitimiza wajibu wao kwa kuhahakisha bei inashukai . Bei iliyopanda saivi ni kutokana exchange rates ya US dollar vs Tsh , na si vingenevyo .
 
hivi mmemuelewa mtoa mada? au unabisha bisha, Ewura wali2mia formula iliyokuwa ikitumika hapo zamani kabla ya mgomo, na hiyo ni baada ya kugundua kuwa formula mpya imekosewa kitaalamu,.

[h=3]TAARIFA KWA UMMA KUHUSU BEI ELEKEZI/KIKOMO ZA MAFUTA AINA YA PETROLI KUANZIA TAREHE 15 AGOSTI 2011[/h]

Kama ilivyo ada, na kulingana na Kanuni ya Kukokotoa bei za
bidhaa za mafuta ya petroli bei zimekuwa zikikokotolewa na kutangazwa na
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kila baada ya wiki mbili.
EWURA inatangaza bei elekezi/kikomo za mafuta ya petroli nchini zitakazoanza kutumika
kuanzia Jumatatu, Tarehe 15 Agosti 2011. Bei hizi zimekokotolewa kwa kuzingatia kanuni mpya
iliyoanza kutumika mwanzoni mwa mwezi huu. Pamoja na kutambua bei elekezi/kikomo za bidhaa
mbalimbali za petroli nchi nzima, ni muhimu kuzingatia yafuatayo:



(a) Bei za jumla na rejareja kwa aina zote za mafuta zimepanda ikilinganishwa na bei zilizokokotolewa kwa ajili ya kuanza kutumika tarehe 1 Agosti 2011 ambazo zilitangazwa tarehe 3 Agosti 2011. Katika toleo hili bei zimepanda kama ifuatavyo: Petroli TZS 100.34 sawa na asilimia 5.51, Dizeli TZS 120.47, sawa na asilimia 6.30 na Mafuta ya taa TZS 100.87, sawa na asilimia 5.30. Mabadiliko haya ya bei za mafuta nchini yametokana na kupanda sana kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na kuendelea kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania ikilinganishwa na dola ya Marekani (sarafu ambayo hutumika katika manunuzi ya bidhaa za mafuta kwenye soko la dunia).

Kwa mfano, kwa viwango vya bei zilizotumika katika chapisho hili, bei katika soko la dunia zimepanda kwa wastani wa asilimia 5.42 na thamani ya shillingi ya Tanzania imeshuka kwa shilingi 47.12 (asilimia 2.96) kwa dola moja ya Marekani. Bei za jumla kwa kulinganisha matoleo haya mawili zimepanda kama ifuatavyo: Petroli TZS 110.34 sawa na asilimia 5.70; Dizeli TZS 120.47 sawa na asilimia 6.54; na Mafuta ya Taa TZS 100.87 sawa na asilimia 5.49.


(b) Bei za rejareja na za jumla zingepanda zaidi endapo formula ya zamani ingeendelea kutumika. Kwa kulinganisha vigezo vilivyo katika fomula ya zamani na fomula mpya, bei za mafuta zingekuwa kama ifuatavyo:

Aina ya Mafuta
Bei za Rejareja (TZS/L)
Bei za Jumla (TZS/L)
Kwa Formula ya zamani
Kwa Formula Mpya
Kwa Formula ya zamani
Kwa Formula Mpya
Petroli
2,298.33
2,114.12
2,230.07
2,046.62
Dizeli
2,213.36
2,031.31
2,140.80
1,963.81
Mafuta ya Taa
2,188.89
2,005.40
2,116.33
1,937.90


Kama inavyoonyesha kwenye jedwali hapo juu, formula mpya inaendelea kutoa unafuu kwa watumiaji ukilinganishwa na kama fomula ya zamani ingetumika. Ni dhahiri kuwa vigezo viwili vikubwa vinavyochochea kupanda kwa kasi kwa bei ya mafuta nchini ni kupanda kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania ukilinganisha na dola ya Marekani, sarafu ambayo inatumika kuagizia mafuta hayo.



(c) Kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2008, bei za bidhaa za mafuta ya petroli zitaendelea kupangwa na soko. EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa za mafuta.



(d) Kampuni za mafuta zipo huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani ilimradi bei hizo ziko chini ya bei kikomo (price cap) kama ilivyokokotolewa na fomula iliyopitishwa na EWURA na ambayo ilichapwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 5 la tarehe 9 Januari 2009 na marekebisho yaliyofanywa mwezi Julai 2011.



(e) Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana na yakionyesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika. Pale ambapo inawezekana kuchagua, wateja wanashauriwa kununua bidhaa za mafuta kutoka kwenye vituo vinavyouza mafuta kwa bei ndogo zaidi ili kushamirisha ushindani. Ni kosa kuuza mafuta bila kuweka mabango ya bei inayoonekana vizuri kwa wateja na adhabu itatolewa kwa kituo husika.



(f) Wanunuzi wanashauriwa kuhakikisha kuwa wanapata stakabadhi ya malipo inayoonesha jina la kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei kwa lita. Stakabadhi hiyo ya malipo itatumika kama kidhibiti cha mnunuzi wa mafuta endapo kutajitokeza malalamiko ya ama kuuziwa mafuta kwa bei ya juu kuliko bei kikomo; ama endapo utakuwa umeuziwa mafuta yenye kiwango cha ubora kisichofaa.

A: BEI ZA REJAREJA

Bei Elekezi
Mji
Petroli
Mafuta ya Taa
Dizeli
(TZS/LT)
(TZS/LT)
(TZS/LT)
Dar es Salaam
2,114
2,005
2031
Arusha
2,198
2,089
2115
Arumeru
2,198
2,089
2115
Karatu
2,216
2,108
2133
Monduli
2,203
2,095
2121
Ngorongoro (Loliondo)
2,275
2,166
2192
Kibaha
2,119
2,010
2036
Bagamoyo
2,125
2,016
2042
Kisarawe
2,121
2,013
2038
Mkuranga
2,124
2,015
2041
Rufiji
2,142
2,033
2059
Dodoma
2,173
2,064
2090
Kondoa
2,205
2,096
2122
Kongwa
2,170
2,061
2087
Mpwapwa
2,174
2,065
2091
Iringa
2,178
2,069
2095
Kilolo
2,183
2,074
2100
Ludewa
2,244
2,135
2161
Makete
2,237
2,128
2154
Mufindi
2,188
2,079
2105
Njombe
2,206
2,098
2124
Bukoba
2,329
2,220
2246
Biharamulo
2,303
2,194
2220
Karagwe
2,345
2,236
2262
Muleba
2,320
2,211

kipi bora , bei mpya au ya zamani ?
hawa wafanyabiashara wanataka kuigezia kibao EWURA for their own interest , hakuna jingine hapa
 
tatizo la kufikiria kutumia masaburi ndo hili. Kwani tuna visima hapa TZ? bei ya mafuta yanapangwa na soko la dunia na sisi ni sehemu yake. Hata akiongoza slaa hamna anachoweza kufanya labda kama atagundua visima kule kwao karatu. Think kwa kutumia upstairs.

Siyo Kweli ni uongo wa kimagamba, wala sina sababu ya kukwambia kwa nini maana unalo jibu.
 
Wewe una matatizo binafsi, Elimu ya kuungaunga una maana gani? We ndo mshamba unayejisikia una elimu ambayo haikukufungua akili.Au ndo ulikaa darasani peke yake. Watu wamesoma kutokana na historia za wazazi wao. Wengine wamepata vibarua ndo wanatumia hizo pesa kujisomesha. We mshukuru mungu wazazi wako walikuwa na uwezo wa kukulipia ukasoma bila kusimama.
Mi nasikitika kwamba kukosa uwezo wa kufikiri na kubwatuka maneno yasiyo chujwa, ni ishara tosha ulifauru kwa kudesa. Hekima kichwani hamna.

Mkuki wa moto jamani tupunguze makali!

Jamaa katupa mkuki msituni!
 
hiyo chart mbona inaonyesha bei imeanza kupanda tena
 

Attachments

  • Capture.PNG
    Capture.PNG
    9.6 KB · Views: 22
HUU NI UTHIBITISHO KUWA EWURA WALIDANGANYA NA KUTOA USHAURI POTOFU KWA SERIKALI, WANAPASHWA KUCHUNGUZWA NA KUFUNGULIWA MASHITAKA KWA KUSABABISHA HASARA KWA WANANCHI, SERIKALI AMKENI, ACHENI KUWATUMIA WATU WENYE ELIMU ZA KU-UNGA-UNGA, HAYA NI MATUNDA YAKE

Nilipotoa Mada zangu kuwa EWURA ndio Tatizo wengi mlipinga, mmeona ugumu wa maisha sasa!!!! Tupaze sauti zetu kwa nini wasinge tuachie zile bei zetu za mwanzo tulikuwa tunapata mafuta kwa 2040-2080 na wale wazee wa BP 2100-2150 sasa nini wamefanya?????

Costing Accountant.
katongo2002@gmail.com







TAARIFA KWA UMMA KUHUSU BEI ELEKEZI/KIKOMO ZA MAFUTA AINA YA PETROLI KUANZIA TAREHE 15 AGOSTI 2011


Aina ya Mafuta
Bei za Rejareja (TZS/L)
Bei za Jumla (TZS/L)
Kwa Formula ya zamani
Kwa Formula Mpya
Kwa Formula ya zamani
Kwa Formula Mpya
Petroli
2,298.33
2,114.12
2,230.07
2,046.62
Dizeli
2,213.36
2,031.31
2,140.80
1,963.81
Mafuta ya Taa
2,188.89
2,005.40
2,116.33
1,937.90
Kama inavyoonyesha kwenye jedwali hapo juu, formula mpya inaendelea kutoa unafuu kwa watumiaji ukilinganishwa na kama fomula ya zamani ingetumika. Ni dhahiri kuwa vigezo viwili vikubwa vinavyochochea kupanda kwa kasi kwa bei ya mafuta nchini ni kupanda kwa bei ya mafuta kwenye soko la dunia na kushuka kwa thamani ya shilingi ya Tanzania ukilinganisha na dola ya Marekani, sarafu ambayo inatumika kuagizia mafuta hayo.
A: BEI ZA REJAREJA

Bei Elekezi
Mji
Petroli
Mafuta ya Taa
Dizeli

(TZS/LT)
(TZS/LT)
(TZS/LT)
Dar es Salaam
2,114
2,005
2,031
Arusha
2,198
2,089
2,115
Arumeru
2,198
2,089
2,115
Karatu
2,216
2,108
2,133
Monduli
2,203
2,095
2,121
Ngorongoro (Loliondo)
2,275
2,166
2,192
Kibaha
2,119
2,010
2,036
Bagamoyo
2,125
2,016
2,042
Kisarawe
2,121
2,013
2,038
Mkuranga
2,124
2,015
2,041
Rufiji
2,142
2,033
2,059
Dodoma
2,173
2,064
2,090
Kondoa
2,205
2,096
2,122
Kongwa
2,170
2,061
2,087
Mpwapwa
2,174
2,065
2,091
Iringa
2,178
2,069
2,095
Kilolo
2,183
2,074
2,100
Ludewa
2,244
2,135
2,161
Makete
2,237
2,128
2,154
Mufindi
2,188
2,079
2,105
Njombe
2,206
2,098
2,124
Bukoba
2,329
2,220
2,246
Biharamulo
2,303
2,194
2,220
Karagwe
2,345
2,236
2,262
Muleba
2,320
2,211

Hii nchi inakwenda kusiko jamani...na chakushangaza watanzania tumelala tunaona sawa...lol!
 
Kitendo cha Serikali kufyata mkia kwa wafanya Biashara ni usaliti kwa Wananchi tunawataka warudishe Bei ya mafuta taa ya awali...hawa viongozi legelege na Serikali legelege Nchi imewashinda kuongoza kila mtu anajiamulia lakufanya kwahiyo wananchi tutarajie mikwaju zaidi.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom