Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 983
- 207
Kumekuwa na taarifa kutoka vyombo mbalimbali vya habari kuwa kuna Wanaccm wanaotaka kupata nafasi za uongozi hususani ubunge katika uchaguzi ujao kusambaza kadi feki za chama hicho miongoni mwa wapiga kura.
Imeripotiwa kwenye gazeti la Majira la tarehe 22.09.09 na la leo tarehe 29.09.09 kwenye maoni ya mhariri kuwa huko katika jimbo la Moshi (V) kumesambazwa kadi nyingi feki na mmoja wa anayedaiwa kuutaka ubunge wa eneo hilo. Maeneo mengine kama Shinyanga pia yameripotiwa kuwa na maelfu ya kadi zinazodaiwa kuwa feki za CCM.
Hii ina maanisha nini? Ni kwamba hawa wanaozisambaza wameamua kununua mashine za kuchapa ama kudurufu, au mfumo mzima wa uchapaji na usambazaji hausimamiwi ipasavyo na wakuu wahusika, au kuna baraka kutoka juu?
Kama kila mtu anaweza kuchapa na kusambaza kadi za chama anaweza kufanya hivyo, kwa nini asiweze pia kuchapa na kusambaza vitambulisho vya wapiga kura na hata shahada za kupigia kura?
Imeripotiwa kwenye gazeti la Majira la tarehe 22.09.09 na la leo tarehe 29.09.09 kwenye maoni ya mhariri kuwa huko katika jimbo la Moshi (V) kumesambazwa kadi nyingi feki na mmoja wa anayedaiwa kuutaka ubunge wa eneo hilo. Maeneo mengine kama Shinyanga pia yameripotiwa kuwa na maelfu ya kadi zinazodaiwa kuwa feki za CCM.
Hii ina maanisha nini? Ni kwamba hawa wanaozisambaza wameamua kununua mashine za kuchapa ama kudurufu, au mfumo mzima wa uchapaji na usambazaji hausimamiwi ipasavyo na wakuu wahusika, au kuna baraka kutoka juu?
Kama kila mtu anaweza kuchapa na kusambaza kadi za chama anaweza kufanya hivyo, kwa nini asiweze pia kuchapa na kusambaza vitambulisho vya wapiga kura na hata shahada za kupigia kura?