Escrow yazidi kuvimba: CHADEMA wampatia kibarua kizito Rais Kikwete kuelekea Hotuba yake kesho

Inaelekea wafadhili wanamawasiliano ya moja kwamoja na ukawa. Inamaana ukawa wataulizwa kwanza kama wameridhika na kama hawajaridhika mbinyo uendelee. Lakini raisi wetu namwamini atawanyoa wote anaweza kuwaambia siwanyoi ila kwenye baraza la wazee ananyoa kipara

Hana ubavu huo subiri tuone.
 
Tuseme yote lakini Rais anapofikia hatua za kutoamini PCCB na CAG ambapo viongozi wake aliwateua yeye mwenyewe basi nchi ina ombwe kubwa la uongozi. Vyombo hivi vinapaswa kuvunjwa mara moja kama taarifa zake hazitafanyiwa kazi na badala yake kuundiwa chombo kingine sijui cha kutoka mbinguni kufanya uchunguzi wa kina.

Na wazee wa Dar es salaam (kama si wa CCM), baada ya hotuba ya Rais eidha mtatoka mashujaa au mtadhalilika sana. Ni busara zenu tu ndiyo zitalinusuru taifa
 
Ni kipindi chake cha mwisho cha urais so hata asipowachukulia hatua mafisadi wa escrow kina Muhongo na genge lake hana cha kupoteza
 
Yeah this ujumbe from bodi ya wadhamini we call it surgical precise, it is like taking mr president from medical theatre to the political theatre, nani atasaini hati ya upasuaji katika huu upasauji wa kisiasa ? kuna uwezekano yeye akapona lakini chama kikafa kabisa.
 
Chadema mbona benki ya Kanisa Mkombozi Benki mnaogopa kuitaja kama moja ya benki iliyohusika kuficha fedha za walalahoi, mnaitaja tu Stanibic bank wakati hizi benki zote ni adui wa Watanzania, mnaogopa kuitaja benki yenu ya Kanisa.
 
kwa sababu walipoingia ikulu hawakujua kama Mungu amewaingiza. hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea ktk uzushi(ufisadi)wao, na mioyo yao nyenye ujinga (kibuli) ikatiwa giza. wakajinena kuwa wenyehekima (wenyenyumba) wakapumbazika; wakaubadili utukufu wa Mungu( ikulu) wakafanya biashara ya kuuza meno ya tembo. war 1:21-23
 
Hana ubavu huo subiri tuone.
Mara nyingi mambo kama haya yana uchokonozi kama ulivoona bungeni unakuta watu wana data nyingi na wanazikeep ukileta ubishi wanakusanifu tu ukidhani umeshinda wanatupia kabarua au kadocument kamoja unalegea.

Kipindi hiki tulichopumzika baada ya lile bunge watuhumiwa pamoja na watuhumu waliendelea kufetch more data hawa wengine za kujilinda na wenzao za kushambulia ni kama usajili mpya wa data.

Hiyo barua hapo ni ndefu sana inaweza kuwa likitabu au compendium na watuhumiwa wanaweza kuja na manual zaidi ya kumi kwa utetezi .Ila kikubwa ni kuwafyeka hao nnchi itulie hata kama hawana kosa ni uwajibikaji wa kisiasa ni kumsaidia raisi hivi uwaziri unakuwa kwenye akili au damuni?
 
Hawa wazee wa Dar nao seheme ya shida nchi hiii. Hawawezi kuhoji hata kidogo juu hili? Nawashauri kesho wajiondoe uvivu wauvae uzalendo...kikinuka ndo wa kwanza kuathirika. Hatuko tayari kuona upuuzi huu ukiendelea.
mkuu hao wazee wa ccm bei yao ni pilau tu na miguo ya kijani,kwanza hata akili ya kuhoji hawana!
 
Chama cha matamko na malalamiko. Subirini kesho Rais ataeleza kila kitu kwa ufasaha. Najua Arkado u,epokea kiasi kikubwa kwa Mengi na hasira yote hii ina siri ndani yake
 
Back
Top Bottom