Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,410
- 31,395
- Thread starter
- #101
KWANINI WATANZANIA HAWATAKI NA NI WAVIVU WA KUHOJI!
KWANINI KUHOJI IONEKANE NI KOSA AU UTOVU WA NIDHAMU?
ELIMU BURE
Wakati wa kampeni hapa duru tulihoji, kwanini Watanzania hawadai maelezo ya kina (details) kuhusu sera za vyama?
Tukasema mbele ya safari tusijeshangaa tukiuziwa mbuzi ktk gunia
Wapinzani wa UKAWA walikuwa na sera ya elimu bure. Wengi wakahoji kwa ukubwa wa wizara husika na udogo wa bajeti hilo linawezekanaje?
Tuliambiwa ni kupitia makusanyo ya kodi na ongezeko la wigo wa kodi ambayo hayakidhi viwango kwa sasa. At least walisema
CCM wakaiuchukua hoja ya wapinzani, tukasikia mgombea wao ambaye sasa ni Rais akiseama elimu itatolewa bure katika kiwango cha sekondari.
Wengine tukahoji kilishindikana nini miaka zaidi ya 20 na kipi kitafanyika tofauti sasa hivi? Tukaambiwa litawezekana chini ya falsafa ya Hapakazi
Awamu ya 5 ikaingia na kutoa uamuzi wa elimu bure, mabilioni yakipelekwa mikoani
Tunachoshuhudia ni wanafunzi kukalia mawe, wakisoma chini ya miti km chache kutoka Dar zilipo ofisi za serikali
Pesa zinazopelekwa hazikidhi mahitaji ya shule na changamoto zake
Tunaambiwa, tatizo linaonekana kusababishwa na wanafunzi waliokuwa hawendi shule.
Kwamba kuna ongezeko la wanafunzi baada ya elimu kutolewa bure
Kwa lugha zile zile za kawaida, tunaambiwa hiyo ni changamoto serikali inakabiliana nayo
Haya yanatokana na wananchi si serikali. Yaliposemwa majukwaani hakuna aliyehoji. Tulipohoji jamvini tulionekana 'wendawazimu' msimu wa vichwa kupata moto ulifika.
Tunachotakiwa leo si kuhoji tena matatizo ya elimu kama tunavyoambiwa
Tunatakiwa tuwaulize wahusika, hivi walitumia vigezo gani kusema elimu itatolewa bure?
Hoja ya ongezeko la wanafunzi waliokuwa hawaendi shule haina mashiko.
Nchi inajua idadi ya watoto na wananchi kwa ujumla.
Ilikuwaje tukaambiwa elimu itatolewa bure huku wahusika wakiwa hawana takwimu?
Je, walifanyi a kazi takwimu (homework) kabla ya kujiridhisha na kauli za elimu bure ?
Pili, kuna tofauti gani na mabilioni 21 yalitolewa kiholela bila kuhojia na hili la elimu bure?
Bilioni 21 zilitolewa bila mchanganuo wa kitaalamu, faida za muda mfupi na muda mrefu.
Hatukuhoji, kama ambavyo hatukuhoji elimu bure kwa uwezo gani?
Ndio maana tunasema, hii dhana ya kuimba tu kila kinachosemwa haitatusaidia.
Utamaduni wa kudhani kuhoji ni uhalifu, kupinga au utovu inatudumaza kifikra.
Tubadilike na kuhoji tukitaka majibu na si kumeza kila kitu bila kutafuna
Hizi mila za kuimba tu kila kitu bila kuhoji zinatuumiza kama taifa.
Hatuhoji, hivi tatizo letu ni lipi kati ya haya mawili, elimu bure au elimu bora
Lini tutasimama kwa muskatabali wa Taifa letu?
Tupo bize na name calling, hatuhoji tunasubiri ahadi nyingine tamu tamu tuimbe
Tusemezane
KWANINI KUHOJI IONEKANE NI KOSA AU UTOVU WA NIDHAMU?
ELIMU BURE
Wakati wa kampeni hapa duru tulihoji, kwanini Watanzania hawadai maelezo ya kina (details) kuhusu sera za vyama?
Tukasema mbele ya safari tusijeshangaa tukiuziwa mbuzi ktk gunia
Wapinzani wa UKAWA walikuwa na sera ya elimu bure. Wengi wakahoji kwa ukubwa wa wizara husika na udogo wa bajeti hilo linawezekanaje?
Tuliambiwa ni kupitia makusanyo ya kodi na ongezeko la wigo wa kodi ambayo hayakidhi viwango kwa sasa. At least walisema
CCM wakaiuchukua hoja ya wapinzani, tukasikia mgombea wao ambaye sasa ni Rais akiseama elimu itatolewa bure katika kiwango cha sekondari.
Wengine tukahoji kilishindikana nini miaka zaidi ya 20 na kipi kitafanyika tofauti sasa hivi? Tukaambiwa litawezekana chini ya falsafa ya Hapakazi
Awamu ya 5 ikaingia na kutoa uamuzi wa elimu bure, mabilioni yakipelekwa mikoani
Tunachoshuhudia ni wanafunzi kukalia mawe, wakisoma chini ya miti km chache kutoka Dar zilipo ofisi za serikali
Pesa zinazopelekwa hazikidhi mahitaji ya shule na changamoto zake
Tunaambiwa, tatizo linaonekana kusababishwa na wanafunzi waliokuwa hawendi shule.
Kwamba kuna ongezeko la wanafunzi baada ya elimu kutolewa bure
Kwa lugha zile zile za kawaida, tunaambiwa hiyo ni changamoto serikali inakabiliana nayo
Haya yanatokana na wananchi si serikali. Yaliposemwa majukwaani hakuna aliyehoji. Tulipohoji jamvini tulionekana 'wendawazimu' msimu wa vichwa kupata moto ulifika.
Tunachotakiwa leo si kuhoji tena matatizo ya elimu kama tunavyoambiwa
Tunatakiwa tuwaulize wahusika, hivi walitumia vigezo gani kusema elimu itatolewa bure?
Hoja ya ongezeko la wanafunzi waliokuwa hawaendi shule haina mashiko.
Nchi inajua idadi ya watoto na wananchi kwa ujumla.
Ilikuwaje tukaambiwa elimu itatolewa bure huku wahusika wakiwa hawana takwimu?
Je, walifanyi a kazi takwimu (homework) kabla ya kujiridhisha na kauli za elimu bure ?
Pili, kuna tofauti gani na mabilioni 21 yalitolewa kiholela bila kuhojia na hili la elimu bure?
Bilioni 21 zilitolewa bila mchanganuo wa kitaalamu, faida za muda mfupi na muda mrefu.
Hatukuhoji, kama ambavyo hatukuhoji elimu bure kwa uwezo gani?
Ndio maana tunasema, hii dhana ya kuimba tu kila kinachosemwa haitatusaidia.
Utamaduni wa kudhani kuhoji ni uhalifu, kupinga au utovu inatudumaza kifikra.
Tubadilike na kuhoji tukitaka majibu na si kumeza kila kitu bila kutafuna
Hizi mila za kuimba tu kila kitu bila kuhoji zinatuumiza kama taifa.
Hatuhoji, hivi tatizo letu ni lipi kati ya haya mawili, elimu bure au elimu bora
Lini tutasimama kwa muskatabali wa Taifa letu?
Tupo bize na name calling, hatuhoji tunasubiri ahadi nyingine tamu tamu tuimbe
Tusemezane