Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,409
- 31,393
- Thread starter
- #141
TUNARUDI NYUMA 'KIDEMOKRASIA'
KILA ENEO NA MATATIZO, NINI KINAENDELEA?
Mwanzoni mwa miaka ya 1990 wakati wa mageuzi, ilikuwa ni marufuku kufanya mikutano ya kisiasa nje ya CCM. Baada ya mfumo wa vyama vingi, hali haikubadilika.
Ilikuwa Polisi kufukuzana na vyama mitaani kamata kamata na kila aina ya vurugu
Hali iiendelea hadi Mwl alipohoji, wanaofanya mikutano wanavunja sharia gani?
Tangu wakati huo mikutano ikaruhusiwa na kuwa jambo la kawaida.
Ilikuwa ni sehemu ya maisha ya Watanzania . Hakukutokeaa tatizo la aina yoyote.
Kazi ya Polisi ilikuwa kutoa ulinzi pale inapohitajika na kufuatilia panapokuwa na uvunjifu wa Amani kwa namna moja au nyingine, na ilitokea nadra sana.
Tangu awamu ya tano iingie madarakani hali imezorota sana, kwamba, mikutano ya siasa imekuwa kama 'uhalifu'. Kumekuwa na marufuku zisizo na sababu za aina yoyote.
Ni awamu ya tano, waziri mkuu yupo ktk rekodi akiwataka Polisi wazuie mikutano
Mikutano ya kisiasa ni haki ya kikatiba ya mwananchi, waandalizi na wasikilizaji.
Si jukumu la serikali kuratibu mikutano hakuna 'msimu' wa siasa kama inavyoelezwa
Ipo mamlaka ya vyama vya siasa inayoangalia utaratibu mzima wa utendaji wa vyama.
Si jukumu la Polisi kubashiri matatizo yanayoweza kutokana na mikutano hiyo.
Polisi hawa wabashiri ndio wanaoshindwa kuzuia uhalifu unaolisumbua taifa sasa
Hili limepelekea wananchi kuliangalia jeshi la Polisi kwa jicho la kutumikia matakwa ya wanasiasa nje ya kanuni za utumishi.
Kwa mantiki, ipo sehemu ya jamii isiyo na Imani na jeshi la polisi
Huko Bungeni kuna mapambano kati ya naibu Spika na wabunge wa Upinzani.
Kwa ufupi kuna kila sababu za kuamini naibu Spika ameshindwa kuunganisha Bunge.
Bunge linayumba, limepoteza heshima na nguvu kama mhimili unaojitegemea
Serikalini hali nayo inasikitisha, Rais akitueleza vilaza, waziri akisema ni wahadhiri
Hakuna kuheshimu taratibu za ngazi za serikali.
Hatuoni mantiki za Rais kuelekeza ujenzi wa barabara ndani ya Jiji, ili hali kuna serikali ya mkoa, Jiji n.k. Na tangazo la ujenzi huo likitolewa sehemu ya kiroho
Baada ya uchaguzi, tuliandika katika safu hii Taifa limegawanyika, na kazi ya awali ya Rais Magufuli ni kuliunganisha. Hakuna taifa linalofanikiwa likiwa katika vipande.
Kwasasa Taifa limegawanyika Zaidi kuliko hapo awali
Yapo mambo yanayosumbua wananchi wajiulize, nini hasa kinafichwa na serikali hii kwa kutumia nguvu za dola?
Kuna kitu gani serikali ya awamo ya tano inaogopa kisiwekwe wazi?
Wananchi wanajiuliza, nguvu za kuzuia mikutano ya kisiasa zimelenga kuficha nini?
Kwavile serikali imekuwa inatenda 'mambo' kwa uwazi utumbuaji na uwajibikaji, nini inahofia hadi kuzuia mikutano ya wapinzani, ya kawaida kabisa?
Kwa hali ya ilivyo, kila kitu kipo kipo, hakuna anayejua nini kinafanyika Zaidi ya shamra shamra za majipu, ukurupukaji na maamuzi yanayoumiza wananchi kama la sukari
Tunabomoa misingi ya demokrasia tuliyojenga kwa gharama kubwa na kutupa heshima
Tunarudi enzi za Polisi kukimbizana na wapinzani bila sababu za maana.
Tunaishi kwa hofu ya kuzuia wananchi wasijadili hatma zao eti watachonganishwa.
Serikali inayojiamini haigopi tuhuma au uzushi, hii ya 5 inaogopa hata kivuli chake
Tusemezane
KILA ENEO NA MATATIZO, NINI KINAENDELEA?
Mwanzoni mwa miaka ya 1990 wakati wa mageuzi, ilikuwa ni marufuku kufanya mikutano ya kisiasa nje ya CCM. Baada ya mfumo wa vyama vingi, hali haikubadilika.
Ilikuwa Polisi kufukuzana na vyama mitaani kamata kamata na kila aina ya vurugu
Hali iiendelea hadi Mwl alipohoji, wanaofanya mikutano wanavunja sharia gani?
Tangu wakati huo mikutano ikaruhusiwa na kuwa jambo la kawaida.
Ilikuwa ni sehemu ya maisha ya Watanzania . Hakukutokeaa tatizo la aina yoyote.
Kazi ya Polisi ilikuwa kutoa ulinzi pale inapohitajika na kufuatilia panapokuwa na uvunjifu wa Amani kwa namna moja au nyingine, na ilitokea nadra sana.
Tangu awamu ya tano iingie madarakani hali imezorota sana, kwamba, mikutano ya siasa imekuwa kama 'uhalifu'. Kumekuwa na marufuku zisizo na sababu za aina yoyote.
Ni awamu ya tano, waziri mkuu yupo ktk rekodi akiwataka Polisi wazuie mikutano
Mikutano ya kisiasa ni haki ya kikatiba ya mwananchi, waandalizi na wasikilizaji.
Si jukumu la serikali kuratibu mikutano hakuna 'msimu' wa siasa kama inavyoelezwa
Ipo mamlaka ya vyama vya siasa inayoangalia utaratibu mzima wa utendaji wa vyama.
Si jukumu la Polisi kubashiri matatizo yanayoweza kutokana na mikutano hiyo.
Polisi hawa wabashiri ndio wanaoshindwa kuzuia uhalifu unaolisumbua taifa sasa
Hili limepelekea wananchi kuliangalia jeshi la Polisi kwa jicho la kutumikia matakwa ya wanasiasa nje ya kanuni za utumishi.
Kwa mantiki, ipo sehemu ya jamii isiyo na Imani na jeshi la polisi
Huko Bungeni kuna mapambano kati ya naibu Spika na wabunge wa Upinzani.
Kwa ufupi kuna kila sababu za kuamini naibu Spika ameshindwa kuunganisha Bunge.
Bunge linayumba, limepoteza heshima na nguvu kama mhimili unaojitegemea
Serikalini hali nayo inasikitisha, Rais akitueleza vilaza, waziri akisema ni wahadhiri
Hakuna kuheshimu taratibu za ngazi za serikali.
Hatuoni mantiki za Rais kuelekeza ujenzi wa barabara ndani ya Jiji, ili hali kuna serikali ya mkoa, Jiji n.k. Na tangazo la ujenzi huo likitolewa sehemu ya kiroho
Baada ya uchaguzi, tuliandika katika safu hii Taifa limegawanyika, na kazi ya awali ya Rais Magufuli ni kuliunganisha. Hakuna taifa linalofanikiwa likiwa katika vipande.
Kwasasa Taifa limegawanyika Zaidi kuliko hapo awali
Yapo mambo yanayosumbua wananchi wajiulize, nini hasa kinafichwa na serikali hii kwa kutumia nguvu za dola?
Kuna kitu gani serikali ya awamo ya tano inaogopa kisiwekwe wazi?
Wananchi wanajiuliza, nguvu za kuzuia mikutano ya kisiasa zimelenga kuficha nini?
Kwavile serikali imekuwa inatenda 'mambo' kwa uwazi utumbuaji na uwajibikaji, nini inahofia hadi kuzuia mikutano ya wapinzani, ya kawaida kabisa?
Kwa hali ya ilivyo, kila kitu kipo kipo, hakuna anayejua nini kinafanyika Zaidi ya shamra shamra za majipu, ukurupukaji na maamuzi yanayoumiza wananchi kama la sukari
Tunabomoa misingi ya demokrasia tuliyojenga kwa gharama kubwa na kutupa heshima
Tunarudi enzi za Polisi kukimbizana na wapinzani bila sababu za maana.
Tunaishi kwa hofu ya kuzuia wananchi wasijadili hatma zao eti watachonganishwa.
Serikali inayojiamini haigopi tuhuma au uzushi, hii ya 5 inaogopa hata kivuli chake
Tusemezane