Dunia haina usawa

nimeikuta kwenye new post,nolifikiri ni kuhusu damasca
s,ghouta na syria,
nimesamehe story nzuri sana.
 
SEHEMU YA 06

Mapigo ya moyo wa Winfrida yalikuwa yakidunda kwa nguvu, hakuamini kama siku hiyo ndiyo ilikuwa maalum kwake kuzungumza na Godwin, mpiga debe ambaye kila siku aliuendesha moyo wake puta.

Hapo kwa mama ntilie alipokuwa, Winfrida hakuzungumza kitu, mapigo yake ya moyo yalikuwa yakidunda kwa nguvu, alitetemeka huku akiwa na hofu, alimpenda mwanaume huyo na alikuwa mahali hapo kwa ajili ya kuzungumza naye lakini kitu cha ajabu kabisa, maneno yote aliyokuwa ameyapanga yalipotea na hivyo kubaki kama bubu.

“Dah! Wewe dada mzuri kinoma,” alisema mwanaume mmoja, hakutaka kunyamaza, uzuri wa Winfrida ulimchanganya kila mtu aliyekuwa mahali hapo.
Winfrida hakusema kitu, akaachia tabasamu tu na kumwangalia mwanaume huo aliyemsifia. Tabasamu lake lilimchanganya kila mtu aliyekuwa mahali hapo, si wanaume hao tu bali hata mama ntilie aliyekuwa akiwauzia chakula alichanganywa na uzuri wa Winfrida.

“Halafu msichana bomba kama huyu, anakuja kuchukuliwa na boya fulani hivi! Mapenzi yanakera sana, wewe unafikiri atachukuliwa na mshikaji fulani wa kishua, anachukuliwa na mtu asiyejielewa,” aliingilia mwanaume mwingine huku naye akimwangalia Winfrida.

Mpaka dakika hiyo Godwin hakuzungumza kitu, aliyatuliza macho yake usoni mwa msichana huyo. Aliudadisi uzuri wake, alikuwa msichana mwenye uzuri wa ajabu kiasi kwamba hakukumbuka kama aliwahi kumuona msichana wa namna hiyo maishani mwake.

Wenzake waliendelea kumsifia lakini macho yake hatakutoka usoni mwa Winfrida, msichana huyo kila alipokuwa akimwangalia Godwin, aligonganisha macho naye kitu kilichomfanya kuangalia chini huku aibu ya kikekike ikimuingia.
“Kuna siku nitampata msichana kama huyu,” alisema Godwin maneno yaliyomfanya Winfrida kushtuka.

“Hahah! Mzee wa Tandale umpate mtoto kama huyo! Utarogwa! Demu mkali kama huyu unafikiri ataweza kukanyaga Tandale, kwanza kwa ardhi gani? Labda mmuwekee kapeti la kukanyagia,” alisema jamaa mwingine kwa utani na wote kuanza kucheka.

Walizidi kuongea mambo mengi huku yote ikiwa ni kumsifia Winfrida kwa uzuri aliokuwa nao. Msichana huyo hakuzungumza kitu, alibaki kimya huku muda mwingi akiangalia chini.
 
Hii inaenda too slow dear, i hope baada ya bibi nyanjige wa 'huwezi kuua maiti' sasa hii itaongezewa kasi ya kuwaUpdated, i can't wait dear
Cc. Shunie
Kama unakumbuka mwanzo nilivyoweka nilisema namalizia ya Bibi halafu tutaendelea na hii
 
  • Thanks
Reactions: BAK
SEHEMU YA 07

Winfrida hakutaka kula, hata alipoambiwa chakula kipi alichohitaji alimwambia mama ntilie kwamba hakuhitaji chakula, alihitaji kupumzika mahali hapo ila kama malipo, alitaka kuwalipia wateja wote waliokuwa katika kibanda hicho.

“Hayo ndiyo maneno! Tungekuwa na madada wanne kama hawa hapa kituoni, mwezi tu tungetoka vitambi!” alisema Godwin huku akionekana kuwa na furaha tele.
Japokuwa kabla ya kufika mahali hapo alikuwa na maneno mengi ya kumwambia Godwin lakini hakuzungumza kitu, kila alichokuwa amepanga kumwambia mwanaume huyo kilipotea kichwani mwake.

Hakujua sababu iliyoufanya moyo wake kuwa mzito namna hiyo. Baada ya kukaa kwa dakika thelathini, wanaume hao wakaaga na kuondoka, kama kawaida, Godwin akaenda kuendelea na shughuli zake.

Macho ya Winfrida hayakutoka kwake, alibaki akimwangalia. Alimpenda jinsi alivyo, japokuwa alionekana kuwa mchafumchafu lakini moyo wake ulimpenda hivyohivyo. Hakujua jina lake, aligundua kwamba kama angelifahamu jina lake basi isingekuwa kazi kubwa kumpata, na mtu pekee ambaye angemwambia jina hilo hakuuwa mwingine, alikuwa huyohuyo mama ntilie.
“Yule anaitwa nani?” aliuliza Winfrida.
“Yupi?”

“Mwenye jezi ya Manchester?”
“Anaitwa Godwin! Mwanaume mtata sana! Ana hasira za karibu mno,ukimzingua kakuzingua,” alijibu mwanamke huyo, alimuongezea na majibu mengine ambayo maswali yake hakuulizwa.

“Mmh! Mbona anaonekana mpole sana?”
“Ndivyo alivyo! Kama angekuwa anavaa suti na kushika Biblia, kesho tu ungependa kwenda kanisani kwake kuombewa! Ila ndiye mtata kuliko wote. Hapa wanamuogopa mno,” alisema mwanamke huyo.

Hilo halikumtisha Winfrida, aliwafahamu wanaume, wengi walikuwa wakorofi lakini kwa wanawake walishindwa kufanya kitu. Wao ndiyo walikuwa udhaifu wao, hata kama mwanaume alikuwa mkorofi kiasi gani kwa mwanamke angekuwa mpole na kufanyiwa kitu chochote kile.

Siku hiyo akaondoka, ilikuwa ni siku ya mateso mno moyoni mwake. Hakukuwa na siku ambayo alimfikiria sana Godwin kama siku hiyo. Alikaa kitandani, moyo wake ulikuwa ukijilaumu sana, alijipanga kwa mwezi mzima lakini siku ambayo alitakiwa kuzungumza na mwanaume huyo hakufanya hivyo japokuwa alipata nafasi kubwa ya kufanya hivyo.
 
SEHEMU YA 08

Alitamani kupafahamu mahali alipokuwa akiishi, amfuate usiku huohuo na kuzungumza naye. Alikumbuka kwamba aliambiwa ni Tandale, hakufahamu vizuri mtaa huo hivyo alishindwa kwenda.
Alivumilia kwa usiku huo, hakutaka kuwa na haraka kwa kuamini kwamba angefanikiwa kwa kile alichokuwa akikihitaji. Siku iliyofuata hakutaka kwenda chuo, kitu cha kwanza kilikuwa ni kwenda katika Kituo cha Daladala cha Makumbusho kwa ajili ya kuonana na Godwin ambaye aliutesa moyo wake na kumfanya kutokuishi kwa furaha.

Alipofika huko, akamuona akiendelea kuita abiria. Siku hiyo alipiga moyo konde, huku akiwa na hofu kubwa moyoni mwake, akaanza kumsogelea, alipomfikia tu, akamsalimia.
Godwin akamwangalia Winfrida, alimkumbuka, alikuwa msichana yule aliyekuwa amemuona jana yake na ndiye ambaye aliwalipia chakula. Akamchangamkia, wakazungumza kwa muda mchache na kuagana.

Huo ndiyo ukawa mwanzo wa wawili hao kuzungumza, Winfrida hakutaka kuacha kwenda Makumbusho, na kila alipokuwa akielekea huko, kitu cha kwanza kilikuwa ni kumtafuta mwanaume huyo na kuanza kuzungumza naye.

Wakati wakiwa wamezoeana na kuzungumza kwa kipindi kirefu, ndipo Winfrida akagundua kitu cha tofauti kwa mwanaume huyo. Kila alipokuwa akiongea, aliingizia maneno mengi ya Kiingereza na hata wakati mwingine kuzungumza sentensi zaidi ya tano kwa Kiingereza tu.

Winfrida alishangaa, hali hiyo ilimpa maswali mengi kwani mbele yake, mwanaume huyo alionekana kuwa mtu wa tofauti. Alikuwa mpiga debe ambaye aliamini kwamba hakuwa ameingia darasani, sasa ilikuwaje azungumze Kiingereza kizuri kama alivyokuwa akizungumza?

“Wewe ni mpiga debe kweli?” aliuliza Winfrida huku akimwangalia Godwin kwa macho ya mshangao.
“Ndiyo! Kila siku unanikuta napiga debe! Inakuwaje unaniuliza kama mimi ni mpiga debe?” aliuliza Godwin huku akimwangalia Winfrida.
“Unaonekana tofauti!”
“Kivipi?”

“Unazungumza Kiingereza kizuri sana, kunishinda mimi! Inakuwaje uwe mpiga debe tena ukionekana kuwa na maisha ya kimasikini sana?” aliuliza Winfrida huku akiendelea kushangaa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom