Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 153,250
- 454,848
- Thread starter
- #41
SEHEMU YA 09
Godwin hakujibu kitu, akanyamaza, akakiinamisha kichwa chake chini, alipokiinua, macho yake yalikuwa mekundu na baada ya sekunde kadhaa machozi yakaanza kumtiririka mashavuni mwake kuonyesha kuchomwa na swali alilouliza Winfrida.
“What has happened to you?” (nini kimetokea?) aliuliza msichana huyo.
“I will tell you!” (nitakwambia)
“When?” (lini?)
Godwin hakujibu kitu, alichomwambia Winfrida ni kumuacha kwani alitakiwa kuendelea na kazi yake kama kawaida. Msichana huyo alikuwa na maswali mengi, akahisi kulikuwa na kitu kikubwa kilichotokea kwa mwanaume huyo.
Alitaka kufahamu, kila alipokutana naye swali lake lilikuwa lilelile kwamba ni kitu gani kilitokea mpaka kuishi maisha aliyokuwa akiishi. Godwin hakumjibu kitu, kila siku alimwambia kwamba angemwambia japokuwa hakumwambia siku ambayo angemueleza ukweli kuhusu maisha yake.
Baada ya kuwa karibu kwa miezi miwili huku kila siku msichana huyo akimuuliza swali hilohilo, hatimaye akamwambia kwamba alikuwa tayari kumuhadithia kila kitu ambacho kilitokea kwenye maisha yake.
Akamchukua na kumpeleka katika kibanda kimoja chakavu, akakaa naye mahali hapo. Winfrida alikuwa na kiu ya kutaka kusikia kile kilichokuwa kimetokea katika maisha ya mwanaume huyo.
“Godwin! Niambie ukweli! Nini kimetokea mpaka kuwa mpiga debe na masikini hivyo?” aliuliza Winfrida huku akimwangalia Godwin ambaye hapohapo akaanza kufungua vifungo vya shati lake na kisha kumuonyeshea maneno yaliyoandikwa kwa tattoo ya korosho, maneno yaliyosomeka ‘I WANT TO KNOW WHO KILLED MY DAD, MOM AND SISTER’ (ninataka kumjua aliyemuua baba, mama na dada yangu)
Winfrida alipoyasoma maneno hayo, akashtuka, akahisi kabisa kwamba kulikuwa na simulizi ndefu juu ya maisha ya mwanaume huyo. Akajiweka vizuri na kumuuliza kama alikuwa tayari kumwambia kuhusu kile kilichotokea katika maisha yake.
“Nitakwambia! Nitakuhadithia kila kitu,” alisema Godwin, akaingiza mkono mfukoni na kutoa kitambaa kichafu na kuanza kuyafuta machozi yake. Akajiweka sawa kwa lengo la kumuhadithia msichana huyo kila kitu kilichotokea, historia kali iliyomchoma moyo wake kila siku.
Godwin hakujibu kitu, akanyamaza, akakiinamisha kichwa chake chini, alipokiinua, macho yake yalikuwa mekundu na baada ya sekunde kadhaa machozi yakaanza kumtiririka mashavuni mwake kuonyesha kuchomwa na swali alilouliza Winfrida.
“What has happened to you?” (nini kimetokea?) aliuliza msichana huyo.
“I will tell you!” (nitakwambia)
“When?” (lini?)
Godwin hakujibu kitu, alichomwambia Winfrida ni kumuacha kwani alitakiwa kuendelea na kazi yake kama kawaida. Msichana huyo alikuwa na maswali mengi, akahisi kulikuwa na kitu kikubwa kilichotokea kwa mwanaume huyo.
Alitaka kufahamu, kila alipokutana naye swali lake lilikuwa lilelile kwamba ni kitu gani kilitokea mpaka kuishi maisha aliyokuwa akiishi. Godwin hakumjibu kitu, kila siku alimwambia kwamba angemwambia japokuwa hakumwambia siku ambayo angemueleza ukweli kuhusu maisha yake.
Baada ya kuwa karibu kwa miezi miwili huku kila siku msichana huyo akimuuliza swali hilohilo, hatimaye akamwambia kwamba alikuwa tayari kumuhadithia kila kitu ambacho kilitokea kwenye maisha yake.
Akamchukua na kumpeleka katika kibanda kimoja chakavu, akakaa naye mahali hapo. Winfrida alikuwa na kiu ya kutaka kusikia kile kilichokuwa kimetokea katika maisha ya mwanaume huyo.
“Godwin! Niambie ukweli! Nini kimetokea mpaka kuwa mpiga debe na masikini hivyo?” aliuliza Winfrida huku akimwangalia Godwin ambaye hapohapo akaanza kufungua vifungo vya shati lake na kisha kumuonyeshea maneno yaliyoandikwa kwa tattoo ya korosho, maneno yaliyosomeka ‘I WANT TO KNOW WHO KILLED MY DAD, MOM AND SISTER’ (ninataka kumjua aliyemuua baba, mama na dada yangu)
Winfrida alipoyasoma maneno hayo, akashtuka, akahisi kabisa kwamba kulikuwa na simulizi ndefu juu ya maisha ya mwanaume huyo. Akajiweka vizuri na kumuuliza kama alikuwa tayari kumwambia kuhusu kile kilichotokea katika maisha yake.
“Nitakwambia! Nitakuhadithia kila kitu,” alisema Godwin, akaingiza mkono mfukoni na kutoa kitambaa kichafu na kuanza kuyafuta machozi yake. Akajiweka sawa kwa lengo la kumuhadithia msichana huyo kila kitu kilichotokea, historia kali iliyomchoma moyo wake kila siku.