Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

Eng. Y. Bihagaze

JF-Expert Member
Sep 8, 2011
1,488
908
Kauli aliyoitoa Dr Slaa wakati wa vuguvugu la kampeni za kisiasa kwamba mfuko wa sement utakuwa Tshs 5,000, badala ya Tshs16,500 kwa sasa kwa wakazi wa DSM na zaidi ya Tshs18,000 kwa wakazi wa nje ya mji huu, nimekuwa nikizitafakari kwa kina sana kwa muda mrefu. Kutokana na Uzoefu wangu wa masuala machache alonijalia mola, nilioona kama ni sentensi ya kisiasa zaidi ya kimatendo, lakini sasa nakiri ni sentensi makini na ya kweli. Na si 5000 tu bali pia 2,500 au 3000 kwa mfuko wa 50kgs.

Hivi majuzi, nilikuwa namsikiliza Waziri Viwanda na Biashara Dr. Kigoda akizungumzia masuala ya Kiuchumi kwenye kipindi cha TBC asubuhi. Kauli aliyotoa Abdala Kigoda ilinifanya kile kisifa cha kuitwa Dr nikiondoe haraka na natamani nikiingia ofisini kwake nimwite Mr Abdala. Mkongwe Huyu adui mkubwa wa mabango ya sigara ni hatari kwa Afya yako alisema , AMESIKIA wafanya biashara wa hapa wakimweleza kwamba bei ya mfuko wa sement inayouzwa hapa ni ghali sana kulinganisha na bei ya mfuko utaouagiza kutoka India.

Nikawaza kama mzee huyu, waziri wetu amesikia tu, ameshindwa kufanya tathimini kutumia ziada kidogo ya akili yake iliyompelekea kuitwa DR, kwamba kama hali iko hivyo kwa India km 4,600 tu kutoka TZ, sawa na kwenda kigoma na kurudi dsm mara mbili, ana mipango gani mbadala ya kuhakikisha na hapa kwetu unafuu wa neema unaonekana kwenye gharama ya mifuko ya cement, watu tukajenga?

Sentensi yake hiyo ilinisukumia na kuamsha mawazo yale niliyokuwa nayo awali aliyoyasema Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CHADEMA Dr Wilbroad Slaa-2010, kwamba Bei ya sement ni ghali sana, Serikali yake itaipunguza hadi kufikia Tsh5,000. Na hapo ndipo nilipoona nifanye kauchunguzi kadogo sana ambako mdau wa jamvi unaweza kunikosoa lakini uwezo wa kuchunguza kwangu ndipo ulipofikia..

Cha kwanza nikawapigia madalali wa wagonjwa (india kuna watu kazi yao ni udalali wa wagonjwa, wanatengeneza dili zao kwa kuwasaka wagonjwa kutoka kwenye nchi zao kama Africa na hata penginepo kupitia mashirika mengi kama LIONS CLUB na mengineyo na kuwa connect na daktari husika na kufanya protocal zote za maandalizi na ndivyo nao wanavyopata kula ..anyway that is not ma topic)..nikawauliza wanitajie bei ya mfuko wa sement kwenye soko la kawaida .. baada ya muda wakaniambia ni Rupia 230. Rupia moja ni sawa na Tsh28.

Kwa hiyo mfuko mmoja wa Kg 50 wa sement kule India ni sawa na Tsh 6,440 (28 x 230). Kwa Kontena la 20ft lina uwezo wa kuchukua tani 35-40, lakini meli nyingi zina standard ya kujaza 40ft kwa tani 20 tu. Sasa tani 20 ni mifuko 400 a cement. Kwa bei ya meli zinazosafirisha 40ft kwa 20ton ni dolar 400 (sawa na tzs 632,000 (1,580 x 400).. tukiacha vikodi vidogo vidogo vya asilimia 2.

Hivyo mzigo utafika TZ kwa gharama ya (400[20ton] x 6,440[mfuko] + 632,000[Usafiri] =3,208,000 so Mifuko 400 utaifikisha Tz kwa gharama ya Tshs 3,208,000 na Mifuko 400 utainunua Tz kwenye soko letu kwa gramama ya (400 x 16,500) = 6,600,000 tofauti ya zaidi ya (6,600,000 -3,208,000) = 3,392,000 .. he he he!

Mifuko 400, ukiinunua India na kuiuza TZ kwa Tsh 10,000 tu kwa mfuko utapata Tshs (10,000 x 400)= 4,000,000 na kutengeneza faida chap ya (4,000,000-3,208,000)=792,000.

Biashara ya haraka sana na mifuko itagombaniwa kama njugu na wewe unaifanya biashara yako yote ukiwa nyumbani nyuma ya laptop yako tu na simu ya mkononi basi.

Nikaenda mbali kidogo na kujiuliza kwanini India cement ni bei rahisi. Nikagundua kwamba, kasheshe kubwa ya kutengenza sement iko kwenye maandalizi yake hasa hasa uzalishaji wa vijiwe vidoho vigumu sana vinavyoitwa Clinker. Mchakato wa Kutengeneza malighafi hii clinker ndio mgumu na ghali zaidi. Kwa utafiti mfupi nilioufanya nimegundua utengenezaji wa Clinker Kule India Ni Ghali sana Kulinganisha na hapa kwetu TZ. Nilibahatika kutembelea kiwanda cha Lafarge Mbeya Cement maarufu kwa kutengeneza Cement ya Mnyama (TEMBO CEMENT). --Simba ni Tanga na Twiga ni DSM.

Mchakato wa Kutengeneza Clinker unaanzia kwenye machimbo ya miamba geu yenye vichambuzi (ingredients na Ore mbalimbali) miamba hii hutoka machimboni na kuingizwa kwenye ngome ya mapondo (Crushers) ambapo hupondwa na kuwa miamba midogo mithili ya kokoto na kuzukumizwa kwenye mkanda, na vile vile huchimbwa udongo wa mfinyanzi nao hukimbizwa kwenye mkanda wake mwingine kwa viwango vyao.

Mikanda hii miwili huingizwa kwenye ngome kubwa ya mapondo na kusagwa kwa kuchanganywa kiasi cha kuwa vumbi, hapa ndipo kiasi kikubwa cha Vumbi huzalishwa, kutokana na shughuli pevu inayofanyika. Vumbi hili hudhibitiwa sana ila kiasi kidogo hutolewa nje na kuwa wingu zito sana la Vumbi hatari kwa mazingira. Vumbi hukusanywa kwenye Kiwiko kikubwa na kirefu sana nadhani ndio point ndefu kuliko zote kwenye kiwanda cha simenti, kinachoitwa Cyclone. Cyclone Hili hupokea vumbi hilo na kulisafirisha likahifadhiwe kweye maghala makubwa (Silos) Sasa Vumbi hili laini ndio malighafi ya kutengenezea hizo Clinker.

Vumbi hili hukimbizwa kwenye kinu kikubwa (KILN). Na huko huchomwa kwenye jotoridi la takriban nyuzijoyo 1400. Udongo huyeyushwa na kuchangamana. Chanzo cha moto huwa ni makaa ya mawe ambayo hupondwa na kuwa vumbi kisha husukumwa kwa upepo wenye gandamizo kubwa na kuzalisha moto kama jehanam ya ajabu sana ndani ya jiko hilo. Moto ule (Carbon) na udongo huo ukijumlisha na mzunguko wa jiko lenyewe, manake linachoma huku linazunguka basi huzaa vijiwe vidogo vyeusi vinavyoitwa Clinker.

Clinker hizo hupozwa kwenye ghala (hydrous)na baadae hukimbizwa kwenye mpipa mkubwa unaozunguka wenye magololi ya chuma na vikwazo ndani yake, huko clinker hugongwagongwa na kuwa vumbi laini sana ambalo huchanganywa na vumbi jingine linaloitwa gypsum (udongo unaochimbwa Tanga) na hapo kutoa vumbi ambalo likipata maji hukauka na kuwa jiwe linaloitwa CEMENT.

Baada ya chochezi hilo nikapeleleza na utengenezji wa Clinker kule India, ambapo mawe hununuliwa, mfinyanzi hununuliwa na zaidi ya hayo wao huchoma kwa kutumia mafuta ambapo ni gharama sana sisi tunatumia makaa ya mawe ambayo kusini ni mengi tu..

Ukiangalia mchakato huo HAPA KWETU, Miamba geu iko mingi na bure kabisa, Makaa ya Mawe Tunayo Kusini ya Kumwaga tu, Gypsum ni udongo unaopatikana Tanga mwingi sana na Bure tu. Sasa nani katuroga mpaka Cement isiwe na bei ya Tsh 2500 au 3000 tu????!!!????

Nikagundua gharama Kubwa za Cement ni Unyonyaji tu, Viwanda vingi vinaendesha mataifa ya nje na si Tanzania. Mfano waholanzi hawa Lafarge wanamlipa MZUNGU Technician tu mwenye certificate ya ufundi karibia Dola 8,500 sawa na (8500 x 2580) = Tshs 13,400,000/=kama mshahara wake mwezi, wakati Mhandisi Mtanzania mwenye Jiwe lake moja au mawili, aliyekokotoa shule ngumu ya FoE na term system that time, na kuvivuka vikwazo vyote vya kina Prop Chambega, Luhanga , Masuha Nk ambaye ndiye mkuu wa sekta mojawapo labda project manager, au Chief Electrical, mechanical, Civil nk kiasi cha Tsh 820,000 kwa mwezi. Usawa uko wapi?. Wakati huyu fundi wa kizungu maelekezo na miongozo ya kazi anaipata kwa Mtanzania huyu ambaye ni meneja wa kitengo husika. Hivi usawa uko .. kama Fundi tu anakula madolali yote hayo je Eng wa kizungu, je Chief of DPt je manager je CO wa kizungu anajichotea mangapi.. kama hiyo haitoshi je wanajilipia kwenye serikali yao kiasi gani kwa External security, BIMA, INSUARANCE nk (maana huduma hizi zote wanajitegemezea huko kwao) na kiasi gani wanarundika kwenye mabenki yao na kuimarisha uchumi wao?

Fedha nyingi na Utajiri Mwingi wazawa hawafaidi, tunanyonywa na kukubali kunyonyeka. Kiwanda sio Inshu kubwa, Serikali ikiamua kujenga Kiwanda hiki ni kazi nyepesi na laini sana. Kama Hawa wazungu wanaleta makandamizi haya basi tuwaalike Wajerumani waliowajengea hawa waholanzi na wengineo viwanda waijengee serikali kupitia vichwa makini chini ya PSRC ikaendesha kiwanda hiki kwa ukombozi wa wananchi wake. INAWEZEKANA..

Alamsik..!!


NB: Kwa muda wako jisomee:
Tanzania: Cement sh 5,000 yawezekana!
&k
Maisha BORA: Songea mfuko wa cement sh 20, 000 per bag!
...

you are real brialiant,uchambuzi safi kabisa,mbeya cement kiwanda cha songwe Injinia mwandamizi Maro ni alikuwa injinia mkuu toka kiwanda kinajengwa mpaka kinaanza uzalishaji,aliacha kazi kwa ajili ya mzungu asiyejua kazi kulipwa Milioni 13 ili hali yeye akipokea milioni 1.5,alipatwa na uchungu akaacha kazi.meneja mkuu Diyami alimshauri Mkapa kutobinafisisha kiwanda cha Songwe ila mkapa hakusikia,kwa hiyo bei ya saruji ingeweza kuwa nafuu tatizo ni ufisadi toka kwa hawa wageni tuliowapa viwanda kwa bei ya kutupa,lengo ni kupata super profit,so THE MISSION OF CAPITALIST WHEREVER THEY ARE IS EXPLOITATION by any means,hivyo saruji kuuzwa 5000 kama alivyosema Dr slaa ni kweli,kweli tupu.

dr-slaa.jpg
 
Umechambua vizuri wa Tz tunajitakia umasikini kwa kutompigia kura mtu anayejali maisha yetu. Baadaye tutamlaumu nani?
Hakuna wa kumlaumu wacha tuteseke dhambi hii inatumaliza wenyewe
 
wewe naona unataka kunitoa machozi tu, mpaka sasa pesa yangu nyingi sana imelala kwenye kiwanja nilichonunua nikitegemea kuanza ujenzi baada ya uchaguzi. I wish ningeizungusha pesa yangu saa hizi ningekuwa safi sana.
 
umechambua vizuri sema sasa mada kama hizi ndio zinanifanya nizidi kupata hasira na hii serikali yetu bora usiwe unaziweka hapa tutakuja kuuana bure
 
umechambua vizuri. Inatia hasira sana kuona viongozi wanashindwa kufikiri kwa ajili ya wananchi zaidi wanafikiria matumbo yao tu.!
 
Nimeukubali uchambuzi wako mkuu SALMA2015 na hasa shule ya uzalishaji wa sementi. Si kwamba watawala hawayajui haya bali ni kama wanafanya makusudi tu kwa sababu zao binafsi. Achana na tumbo ndugu yangu!
 
Aisee nimeipenda sana hii makala, haichoshi kusoma!

Unafaa sana kuwa Mwandishi Baby lol!!

Kwa kweli Dr Slaa alikuwa na point kubwa sana katika hili ila magamba walivyo wavivu kufikiri huwa wanageuza hii hoja kama comedy! shauri wako tunaomba viongozi makini wapite hapa na wausome!
 
Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pempeni,DR SLAA aliwaambia mkabisha sasa ukweli umejidhihirisha kuwa mfuko wa saruji unaweza kushuka hadi sh 5000.Nakumbuka wakati wa uchaguzi TBC wakitumiwa na CCM walisema haiwezekani kumbe uongo mtupu hakuna lisilowezekana.
 
umenitia hasira sana,yaan viongozi wa nchi yetu kwani nabni aliyeloga?,walianza vema chini ya mwalimu,mwalimu alipoondoka 1985 taratibu yule mwovu akaanza kupanda magugu,hakika nimepatwa na hasira sana,Mungu akubariki mleta mada hii
 
Mimi nimependa ulivyochambua na ulivyotafiti ,ila nakuapia kwa jina la Mungu kwa sirikali hii ya magamba huo mpango hautafanikiwa.
 
laana na ziwatembelee wale wote wanaoshndwa kung'amua utamu ulioko kwenye uchambuzi huu. Vidole vinawakereketa kukatsha tamaa wengne sababu ya uvivu wao wa kuchambua mambo na kuyaelewa... SALMA2015 nimekuelewa mkuu. Naomba kama kuna mwandsh wa habar apewe ruhusa ya kuuchapisha uchambuzi wako lakini atumie JF kama ndie mwandsh na sio ajiweke yeye tafadhali
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom