Malunde-Malundi
JF-Expert Member
- Jan 10, 2008
- 1,288
- 130
Nimeangalia uchaguzi huu tangu uanze, siku 20 zimeshakatika; bado siku kama 50 hivi kufika siku ya uchaguzi; tofauti na changuzi zingine; CCM mwaka huu wako defensive zaidi; tafiti zao za Redet, Synovate ambazo huwa zinawapa na kuwaongezea makelele, Mwaka huu Dr Slaa anaongoza sasa wanazichakachua ili walau walete kitu fulani waweze kuongeza kelele; tumeona online polls ambazo zote Kikwete aliongoza zote 2005; sasa ameachwa mbali ukianza na hii ya jamii; nenda kule ile ya Daily news (ilifungwa maana Dr Slaa alikuwa na 80%; kikwete 17% bila mabadiliko kwa muda hatimaye wakaitoa). Wagombea wao majimboni ni dalili kuwa upinzani wa mwaka huu una nguvu sana na ndio maana wamezuia kuhudhuria midahalo; Tumeshuhudia midahalo ambayo kwa siku za karibuni wapiga kura wanaziangalia sana; tumeshuhudia mipango ya wapinzani mwaka huu;ni mikali tofauti na kabla Dr Slaa hadi sasa hajafika mji wowote sijui akifika na huko itakuwaje;bado anachukua kura za wakulima na wafugaji kwanza kabla ya kurudi mijini; Kura zinatengeneza UK; inanipa imani hawawezi kutengeneza Radar ingine; hakutakuwa na kura za mchina mwaka huu; so yote hayo yananipa imani kubwa kabisa; watu kimya ila utashangaa sana mwaka huu; nimetembea vijiwe kadha watu wakimuona mtu wa CCM wanakaa kimya akiondoka wanasema; Mwenye kumdharau Dr Slaa labda hana akili; sasa hizo ni dalili za kumwadhibu mtu kimya kimya;maono yangu hayo
Haya yote yananipa imani kuwa Dr Slaa ataweza kushinda kwa asilimia kama 53% na wengine atawabakizia; na hii ni kwa sababu tu watajaribu kumkashifu pamoja na kumpelekea ving'amuzi kama vya dodoma pamoja na kufanya umafia dakika za mwisho kama ule wa CUF-2005(Chadema watch out this 2010 maana bado wanatafuta pa kutokea) na hawatazipunguza kura hizo;Dr Slaa atashinda ila Bunge litakuwa chini ya CCM kwa asilimia kadhaa; coountry firts sio tatizo; hao hao watakimbizwa mchakamchaka mpaka watasema basi; na kazi itafanyika na baada ya hapo nchi itarudi ktk mstari wa Mwalimu; na huko aliko Mwalimu Nyerere atashangilia tena baada ya kuhuzunika karibu miaka 10.
Mhimu: 1. Mawakala imara 2. Kuna uhuni wa kizushi utatengenezwa hapo mbeleni kumchafua zaidi Dr Slaa 3. Kuhamasishana zaidi jinsi muda unavyokwenda; watachanganyikiwa na kukubali kushindwa; Jeshi halina shida linajua umhimu wa haya mageuzi ya fikra yanayokuja; hicho ndiocho kizuri
Haya yote yananipa imani kuwa Dr Slaa ataweza kushinda kwa asilimia kama 53% na wengine atawabakizia; na hii ni kwa sababu tu watajaribu kumkashifu pamoja na kumpelekea ving'amuzi kama vya dodoma pamoja na kufanya umafia dakika za mwisho kama ule wa CUF-2005(Chadema watch out this 2010 maana bado wanatafuta pa kutokea) na hawatazipunguza kura hizo;Dr Slaa atashinda ila Bunge litakuwa chini ya CCM kwa asilimia kadhaa; coountry firts sio tatizo; hao hao watakimbizwa mchakamchaka mpaka watasema basi; na kazi itafanyika na baada ya hapo nchi itarudi ktk mstari wa Mwalimu; na huko aliko Mwalimu Nyerere atashangilia tena baada ya kuhuzunika karibu miaka 10.
Mhimu: 1. Mawakala imara 2. Kuna uhuni wa kizushi utatengenezwa hapo mbeleni kumchafua zaidi Dr Slaa 3. Kuhamasishana zaidi jinsi muda unavyokwenda; watachanganyikiwa na kukubali kushindwa; Jeshi halina shida linajua umhimu wa haya mageuzi ya fikra yanayokuja; hicho ndiocho kizuri