Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
Hapa kwa kweli nilichemka muzee!Wewe huna data bora ukae kimya. Umeniacha hoi kwamba kwasababu mwakalinga ni engineer basi ndiye mimi engineer.
Engineer, hapa hujaweka hamira na chumvi? endelea kutuhabarisha tutakuwa tunachangua mchele na pumba ......hii Kyela inaelekea ni balaa 2010, asiye na mwana atafute jiwe bado mapema!Balaa lingine lilitokea jana, vile vyakula vya misaada vilivyotolewa kwa ajili ya mafuriko Kyela jana vilimwagwa na wafuga nguruwe kujizolea. Inasemekana hiyo misaada ilifichwa na hiyo NGO ya jamaa zake Mwakyembe ambao alikuwa anawatumia kugawa misaada. Badala yake walikuwa wanatumia chakula hicho kuwalisha wafanyakazi wanaofanya kwenye kampuni yao binafsi ya ujenzi. Matokeo yake wameshindwa kumaliza mpaka unga umeoza huku wananchi wengi walilalamika wakati ule kwamba hawakupata chakula cha misaada. Mwulizeni Dr wenu vipi alikuwa busy na Richmond mpaka wajanja wana abuse misaada?