DOWANS yaibwaga TANESCO; TZ kulipa gharama na adhabu Bil. 185!

Valambia hajalipwa, kesi inaendelea, ilianzia kwa wakili Mkono, sasa inashikwa na Dr. Tenga. Malipo ya mawakili yameshapitiliza gharama za deni!, mind well supply ilifanyika 1978 wakati wa vita vya Kagera, more than twenty years now!, mawakili wanaendelea kulipwa!.

Kwa Dowans tutumie mkakati huo huo wa Valambia kuibakiza kesi mahakamani kwa muda mrefu mpaka jamaa wanyooshe mikoni kuwa hilo deni halilipiki. Tuache maamuzi yafanyike zaidi ya miaka 20 ijayo na kiukweli baada ya miaka 20 Tanzania itakuwa na watu wengi wanaoelewa zaidi tofauti na ilivyo sasa.
 
Hivi ni nani aliyeishtaki TANESCO? Nakumbuka kuna wakati kampuni hiyo DOWANS ilikuwa kama haina mwenyewe. Yule Valambhia (Not sure of spelling) aliyekuwa anaidai serikali baada ya kusuply vifaa vya jeshi alilipwa????? Just curious?
Mkuu usishangae kama malipo yakifanywa before January 2011
Yaani wizi wanaufanya kama dini
 
ingetumika sharia yoyote atakaethibitika kushiriki ufisadi na kuligharimu taifa apigwe mawe mpk afe kila cku watu wanatutenda tunabaki tukilialia kabla hatujanyamaza wanatutenda tena sasa tupaze sauti zetu hivi haiwezekani siku ya kusheherekea uhuru wa Tanganyika tukabeba mabango maeneo yote ya nchi kupinga ufisadi?

MASHEHE NA MAASKOFU MPO HAYA NDIYO MAMBO YA KUYAPIGANIA NA KUHAMASISHA WAUMINI tusibakie tu acha uovu bali tamkeni wazi hadharani toka rohoni dowans/fulani ni muovu na adui no1 acha uovu nchi ipone la sivyo tupelekeni waumini wote barabarani kabla MUNGU HAJATULANI KWA UOVU HUO,....NAAMINI KWA ASILIMIA 100% YESU/MOHAMAD SAW Ingekuwa wapo hai wasingevumilia kuona uovu huu unafanyika kwenye ardhi hii.......
 
Hilo lawezakana pia hapo ndipo utashangaa hizo hela zimetoka wapi

Na ndo maana nitaisapoti CDM daima -- ndo chama cha upinzani halisi huku bara kinachoitetemesha CCM, baada ya CUF kukubali kutiwa kitanzi. Sikumbuki popote iwapo CUF waliwahi hata kuzungumzia Richmond, sana sana Profesa aliitaka serikali ivunje kanuni ya manunuzi na inunue mitambo ya Dowans.
 
Kwa mara nyingine tena mafisadi wametupiga bao la mkono. Ilikuwaje?

Baada ya serikali kushinikizwa kuuvunja mkataba kwa pressure za wananchi, mafisadi kwa kutumia watendaji wao ambao wana nyadhifa serikalini walikubaliana nao kuwa wao mafisadi (wakitumia Dowans kama vehicle yao) watafungua kesi mahakama ya usuluhishi wa migogoro ya biashara ya kimataifa ambapo serikali itapeleka utetezi wa "kipuuzi" ili ishindwe na wao waweze kuchota mlungula wao, na walikubaliana kuwa uamuzi wa kesi hii ufanyike baada ya uchaguzi ili usije ukaathiri matokeo ya uchaguzi.

Wadanganyika mpo hapo?
 
Kwa mara nyingine tena mafisadi wametupiga bao la mkono. Ilikuwaje?

Baada ya serikali kushinikizwa kuuvunja mkataba kwa pressure za wananchi, mafisadi kwa kutumia watendaji wao ambao wana nyadhifa serikalini walikubaliana nao kuwa wao mafisadi (wakitumia Dowans kama vehicle yao) watafungua kesi mahakama ya usuluhishi wa migogoro ya biashara ya kimataifa ambapo serikali itapeleka utetezi wa "kipuuzi" ili ishindwe na wao waweze kuchota mlungula wao, na walikubaliana kuwa uamuzi wa kesi hii ufanyike baada ya uchaguzi ili usije ukaathiri matokeo ya uchaguzi.

Wadanganyika mpo hapo?


hebu dadvua mboona hiyo tittle ya thread na content havina uwiano
 
Kwa maamuzi kama haya ndiyo unaona kuwa ZITTO aliona mbali ingawa wengi tulimpinga.

Kwa nchi ya kawaida, Zitto alikuwa anachemsha ila labda mwenzetu alijua hili linakuja.

Sasa mbona TRA hawaji na wao kudai hela na faini kubwa tu?

Pesa za watu lazima zirudi. CCM kweli ni Chama na Tanzania ina wenyewe............... Yanamwisho.

mwanangu achana na zito aliona mbali wapi huko mbali alikoona? kwa kushauri kuvunjwa sheria ndio kuona mbali kama mbunge alikuwa na haki kupeleka muswada binafsi kufutwa sheria husika ndipo aseme we msitutoe nje ya mjadala huu mzito unahusu hatima yetu kama taifa na kizazi kijacho mwanangu! niliwahi kusema kuwa kizazi kijacho watafukua makaburi yetu kupima mafuu ya vichwa vetu ili wathibitishe kama kweli tulikuwa wanadamu au mithili ya masokwe fulani pale watakapo shindwa buku(1000)ya kufukia mashimo ambayo wageni wamefisadi na kuondoka na kuacha athari nyingi.....
 
Zitto is part of the problem but not the solution.....................Haiwezekani wezi wakatulazimisha kununua vifaa vibovu kwa bei ya waitakayo kwa sababu hakuna ushindani......................sasa hivi hiyo mitambo ingelikuwa imekufa kama ile ya IPTL na SONGAS......................hakuna majibu mepesi hapo..................

Ruta,
lakini hiyo mitambo mpaka sasa infanya kazi? Halafu huyo zitto alipokuwa akishauri hiyo mitambo inunuliwe ilikuwa inauzwa shilingi ngapi ili tuipime na kiasi ambacho sasa tunatakiwa kuilipa Dowans halafu tuone kama ilikuwa vema au la kuzingatia ushauri wa zitto au kuiachia mitambo iende zake kwa kuvunja mkataba ambao sas unaanza kutugharimu kuliko tungeinunua hiyo mitambo?
 
Watu wanavunja sheria afu wanapitia mlango wa nyuma wanatoa hukumu in their favour...mamlaka za kusimamia hizo sheria zinafahamu kwa makusudi kabisa wanaamua kukaa kimya..

Baadaye kidogo unaskia waziri akisema hatuhitaji mabadiliko ya katiba ,manake anajua hizi ishu za kulindana zitafikia ukomo..

Jamii itaamka muda si mrefu...
 
International Chamber of Commerce, imetoa hukumu yake katika kesi iliyoletwa na Dowans (T) Ltd kupinga uamuzi wa Tanesco kuzuia mitambo ya Dowans.. Hukumu hiyo inaonesha kuwa Tanesco imebwagwa vibaya na kutakiwa kulipa mabilioni ya shilingi kama adhabu pamoja na gharama ya kesi kwa Dowans.. Hesabu za kwangu zinaonesha gharama mbalimbali za kesi na adhabu zinazidi Dola milioni 120! Mtu mwingine kanipigia hesabu anasema Dola milioni 180 ngoja wakija public sijui itakuwa figure ipi..

More info to come..

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)

Hakuna cha kumlipa mtu wala nini, hapa ni kukata rufaa mbele kwa mbele!
 
Nadhani wametumia ujanja kuiuza mitambo kwa njia ya mlango wanyuma hivi ni nani hasa mmiliki wa Dowans? Swali hili serikali haijaliweka wazi bado?
 
Sitaki kumuhusisha Zitto na matatizo haya kivyovyote kwasababu alichopendekeza yeye ilikuwa kuvunja sheria ili kununua mitambo ya Dowans, na kama sivyo itaifishwe! Hawakuinunua na wala haikutaifishwa.

Tujiulize yule aliyezuia isiondolewe ( Ndiye ameleteleza hii hasara) alikuwa na sababu gani. Kwa sababu kama TRA ndiye alizuia basi angeshitakiwa yeye na si Tanesco. Isije ikawa baada ya kuwatilia kitumbua mchanga kwa kuvunja mkataba wao wakacollude na Tanesco waizuie mitambo ili mbeleni waweze kwenda mahakamani na kurudisha hela waliyo invest. Hii inawezekana kabisa kabisa ukichukulia zile kauli tata walizokuwa wanatoa wanasiasa juu ya hii Dowans baada ya mkataba kuvunjwa.

Taifa ni bora lifanye uchunguzi makini ili kuwawajibisha waliohusika na udhaifu huu! Ikumbukwe kosa si kuvunja mkataba ni kukatalia mitambo yao......! Mungu ibariki Tanzania
 
Hakuna cha kumlipa mtu wala nini, hapa ni kukata rufaa mbele kwa mbele!

Article 28 (6) ya Rules of Arbitration of the international chamber of commerce hailazimishi kulipa inachosema ni kuwa:

Every Award shall be binding on the parties. By submitting the dispute to arbitration under these Rules, the parties undertake to carry out any Award without delay and shall be deemed to have waived their right to any form of recourse insofar as such waiver can validly be made.
Hakuna mahali ambapo kuna coercive nature endapo unakataa kulipa. Kama ipo kimya inamaana sio lazima hata kidogo.

Tusikubali kuwa mazuzu
 
Kwa maamuzi kama haya ndiyo unaona kuwa ZITTO aliona mbali ingawa wengi tulimpinga.

Kwa nchi ya kawaida, Zitto alikuwa anachemsha ila labda mwenzetu alijua hili linakuja.

Sasa mbona TRA hawaji na wao kudai hela na faini kubwa tu?

Pesa za watu lazima zirudi. CCM kweli ni Chama na Tanzania ina wenyewe............... Yanamwisho.

Mungu ibariki Tanzania
 
Bila shida si nchi yetu ina mapesa ya kumwaga yasiyokuwa na kazi? acha tu tutawalipa na tutaendelea na mkakati wa kubboresha maisha ya kila mtz kwa kazi zaidi, nguvu zaidi na ari zaidi. Hii nchi sijui tunaipeleka wapi huku ndo kujiingiza kichwakichwa kwenye kesi zinazokula kwetu!

JK akilipa hizi hela nitaamii kwamba na yeye anakula na wenye DOWANS.
 
Hili ni jambo ambalo nililiona kabla, rejea post zangu za zamani. Nilijuwa watashinda kwani Dowans hawana kosa walilofanya.

Makosa ni wehu waliokuwa wanashabikia mitambo ile isinunuliwe na serikali Dowans walipotowa offer. Hata Mh. Zitto Kabwe alipigania sana mitambo hii inunuliwe ili kuepusha kesi, gharama na mgao wa umeme.

Leo kikowapi? Mashine tumezikosa, umeme tumekosa, gharama tutazilipia kwa upuuzi wa watu wachache ambao huwa wanajisemea tu bila kuwa na mantiki.

Sasa ndio mtajuwa kuwa Dr. Rashid ni kichwa.

Ah Dr Rashid ni fisadi kwa maono ya baadhi watu JF ona nchi iko katika giza mikoa 7 na kulipa tutawalipa Dowans tukitaka tusitake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom