Ney wa Barca
JF-Expert Member
- Feb 14, 2011
- 310
- 36
kumbe ndio mana hawajachukua tangu jana nilifikiri wamesahau kufanya mambo
Wakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa Dowans aina ya LM6000 PD 40MW uliopo site A nyuma ya ghorofa la Tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37MW. Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa Songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.
Habari kamili baadae.
Yani tusianze kulalamika leo. Tokea November mwaka jana walitukamata, wakatupiga ngwara, wakatulaza chali, wakatuvua, miguu wakaitawanya, K.Y waka-apply, kote huko tumeshindwa kufurukuta, leo wanaanza mambo tunataka kupiga yowe! Tutulie tushughulikiwe, tujiulize tena 2015...
Yani tusianze kulalamika leo. Tokea November mwaka jana walitukamata, wakatupiga ngwara, wakatulaza chali, wakatuvua, miguu wakaitawanya, K.Y waka-apply, kote huko tumeshindwa kufurukuta, leo wanaanza mambo tunataka kupiga yowe! Tutulie tushughulikiwe, tujiulize tena 2015...
Sasa hizo trilion 2 si inabidi tuuzwe na sisi ili kuzilipa ?hahahaha...... nchi hii kwa usanii tu hawajambo...........kuna siku mtadaiwa trilion 2
ni haki yao waarabu kuwanyonya na kuwanyanyasa watumwa waowakuu hivi ninavyoandika ni kuwa mtambo mmoja wa dowans aina ya lm6000 pd 40mw uliopo site a nyuma ya ghorofa la tanesco umewashwa na hadi sasa unazalisha 37mw. Nitawaletea habari zaidi lakini nina uhakika kuwa hawataweza kutembeza mitambo yao yote kutokana na sababu ambazo nitazieleza hapo baadae. Kiufundi mtambo huo kwa sasa ume-substitute mtambo wa songas ambao kwa sasa upo down kutokana na kupata ajali ya moto hapo jana.
Habari kamili baadae.
lenyewe lililalamika kuwa haliwajui wamiliki....wamiliki wamelete kanyaboya lenyewe limeondoka sijui kwenda mauritania......
hapo hapo mitambo imeanza kuwashwa likirudi litauliza, watalidanganya na wala halitahoji zaidi...jitu hili pumbavu sana
Hawana uwezo wa kufanya hivyo.. You are demanding too much from them Babu...
Ni bora wamewasha. I dont care how much they will pay them. Let them pay 100 trillions, I don't care. What I care ni kama kuwasha huko kutapunguza makali ya mgao wa umeme, basi. Tulipiga kelele wakavunja mkataba wa awali, tukaokoa mamilioni yaliyokuwa yanalipwa kila siku, then what.. maisha yalikuwa mazuri zaidi? Dawa ziliongezeka hospitali?, barabara zilijengwa zaidi? Mboga nyumbani nilibadilisha, au idadi ya bia ninazokunywa pale grocery kwa mama Manka ziliongezeka? Nimeendelea kuishi katika matatizo yale yale, yet umeme ukapungua na mgao ukaanza.
Wacha wawashe. Hii nchi ni ya kifisadi, na hata wasipowalipa Dowans, hizo fedha hawashindwa kuzila. Hii nchi inaongozwa na vilaza, na hata wasipowalipa Dowans hawataweza kuwa na njia mbadala ya ktupatia umeme. What we are demanding from them is beyond their thinking and operating capacity.
Njia ya kuepuka haya matatizo ilikuwa ni kuwaondoa madarakani, na hatukufanya hivyo, then let them do what they are capable to deliver, otherwise they will do nothing. Dowans isiwashwe, umeme ukosekane na bado hela zinaliwa. Kuliko kula hizo hela bure, bora ziliwe na Dowans angalau umeme kidogo tupate.
Wacha wawashe... sasa kesho watupe ratiba mpya inayoonyesha kupungua kwa mgao... Kudadadadadeki.
tukiendelea kuruhusu mediocre performance toka kwa hizi serikali za ccm miaka nenda miaka rudi nchi yetu itabaki nyuma sana kimaendeleo huku hao wanaojiita viongozi wakijiendelea kujilimbikizia mali wao, familia zao na marafiki wao wa karibu. Rwanda waliuana kwa mamilioni mwaka 1994 lakini sasa hivi nchi hiyo katika maendeleo inafanya vizuri sana ukilinganisha na sisi "wenye amani" ya miaka nenda miaka rudi. I am not demanding too much ninachotaka kuwe na kuwajibika pale hawa wanaojiita viongozi wanaposhindwa kutimiza wajibu wao kama viongozi wa nchi au wizara mbali mbali. Tumeona kwa mfano mabomu ya mbagala miaka miwili iliyopita hakuna aliyewajibika kwa kujiuzulu au kufukuzwa kazi, miaka miwili baadaye mabomu ya gongo la mboto wamekuwa na kiburi cha kuweza hata kutamka kwamba "sijiuzulu" si ajabu miaka miwili mingine mabomu hayo yatalipuka tena katika moja ya sehemu hizo au inaweza kuwa lugalo.
Rais anasimama na kuwadanganya watanzania kwamba hawajui wamiliki wa dowans wakati ni uongo wa hali ya juu. Hivi wewe kama rais wa nchi baada ya sakata lote hili la dowans hata kama huwajui wamiliki wa dowans huwezi kuwauliza wasaidizi wako toka wizara ya nishati wakupe briefing kuhusu dowans na hatimaye uwajue wamiliki wa dowans? Iweje ngeleja awajue wamiliki wa dowans wakati kikwete anadai hawajui? Kama wewe unaruhusu uzembe na ufisadi wa hali ya juu unaofanywa na hii serikali iliyopo madarakani kila la heri lakini wengine hatukubaliani na hali hiyo na hivyo tuna haki ya kujadili hapa bila wewe kutaka kuonyesha kwamba...we're demanding too much from them.